Mechi gani ya Watani wa jadi (Simba na Yanga) unaikumbuka zaidi?

Wewe inaelekea ni shabiki wa Simba wa kizazi cha kuanzia miaka ya 2000....inawezekana ulizaliwa miaka ya 2000...waulize wanaojua historia ya timu hizi mbili ni ipi kati ya Simba na Yanga imemfunga mwenzie mara nyingi...
Hivi rekodi ipo vizuri Hadi kwenye makombe ya mapinduzi,kagame,Tusker challenge,Taifa cup? Mtani jembe,ngao ya hisani n.k n.k....kwa ligi yanga imezidi kufunga Simba ila Sina hakika kwa mashindano yote Kama yanga kamzidi Simba....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Historia inaonyesha mechi kali ni ile ya 1987 marehemu Sahau Kambi akiwabeba mikia wasishuke daraja na Fred Felix Minziro akimshushia kipigo cha mbwa mwizi Kambi
Daaah ilikuaje hii Mkuu
 
Mkuu umeiva aisee
 
Mkuu yaani miaka hiyo kijana wako nlikuwa bado chalii
 
Wakuu tujadili hii gemu kesho ndo kinanuka tena. Nani mwanakulipata mwanakulipewa kesho?
 
Mm nakumbuka mechi ya simba na yanga mwaka 1985..
Front line ya simba ilikuwa zamoyoni mogela,..,zuberi magoha..Sunday juma.
Huku beki za yanga kuna Athuman juma chama Jogoo..rasheed IDD chama,,ahmedi amasha..Yusuf bana.
Nakumbuka mogela alirukiwa miguu miwili ya kichwa na athumani chama,,
Watu tulidhani hatorudi uwanjani,, Mogela alirudi kavaa usongo kwa bendeji kichwa kizima..
Uwanja mzima shabiki wa mnyama tulilipuka kwa furaha..
Hizo ndy zilikuwa mechi za ushindani kipindi hicho.
 
Tarehe 16 kinawaka tena.

Safari hii wanakutana wote wakiwa vizuri.

Unampa nani ushindi?
 
Zikiwa zimebaki siku chache mapacha wa Kariakoo (Simba na Yanga) watakutana uwanjani tar 16/4 jumapili kukabana makoo.

Ukiwa Kama shabiki kindakindaki wa timu Kati ya hizo mbili Simba/ Yanga.

Njoo utueleze hapa ni Derby gani ambayo ilikuumiza roho/kukufurahisha?

Ukitaja na mchezaji aliyefunga/kukufunga na siku yako kuwa mbaya/nzuri itapendeza zaidi.


 
Lile goli la Morrison kwa Manula tukiwa na timu ya kuunga unga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…