Yanga ni habari nyingine kama huamini waulize TP Mazembe walivyopigwa leo. Yanga ni noma kweli.Mimi kama mdau wa mpira wa miguu nimefuatilia sana mchezo huu wa leo kupitia luninga. Niseme ule ukweli mpira wa YANGA kwa sasa hivi uko juu sana na kwa kweli wamecheza kwa ustadi mkubwa sana licha ya kufungwa. Goli walilofungwa ni goli ambalo timu yeyote inaweza kufungwa na inajulikana mpira ni dakika tisini. Mimi binafsi nimewakubali sana YANGA.
Kwa hiyo unashauri magazeti yangeandika nini labda!?Nadhani Watanzania tufike mahali tuache Siasa kwenye michezo kwani siasa haina nafasi kabisa.Ukisoma magazeti ya Tanzania wiki mbili zilizopita yalikuwa yanatufahamisha watanzania kuwa Yanga imejiandaa vya kutosha kiasi ambacho watanzania wasubiri matokeo tu.Magazeti yaliipamba Yanga mpaka ikabweteka kiasi cha kujiamini kuwa timu ya Tp Mazembe si lolote inafungika kirahisi wakati ukweli timu ya Tp Mazembe no timu Kubwa ktk Afrika.Matokeo tumeyaona uwanja wa Taifa.Viongozi wa Yanga acheni kucheza Mpira magazetini , matokeo mmeyaona.
kijifuraha Fulani amazing....!!!!ujue kuna kijiraha fulani hivi nakipataga wakifungwa yanga,sijui nikisemeje sema nikijifuraha hivi fulani...
Dhaaa kweli la kuvunda halina ubani yaani kila mkiingia ni 1-0 hivi ni kweli wa kimataifa au wasindikizaji wa kimataifa?
KAULI KUTOKA KWA MSEMAJI WA TP MAZEMBE
Anasema mamutu ya hapa mukuje muone mushiba maana mushiba ndio watu wanaendaga bure sasa yanga wamefanya bure watu waje washuhudie mushiba yao
Asiishie kwenye hiyo mechi moja na mechi zingine zinazofuata aendelee na moyo huo!Binadamu tumetofautiana katika fikra. Wapo wenzetu wenye uwezo wa kuona hadi ya kesho yake, akina mshana Jr, pasco wanalijua hili vizuri.
Leo namuweka mwenyekiti mpendwa sana wa yanga, kwa kuona mbali akaamua kupunguza machungu ya mashabiki. Maana kiingilio na kufungwa juu kungeuma zaidi. Mpendwa mwenyekiti akaamua kupunguzia mashabiki na wanachama mojawapo. Waingie bure.
Mwenyekiti ubarikiwe sana.
JECHAAAAAAASio mbaya Yanga tunaongoza