Mei Mosi: Dkt. Mpango asema Serikali imepokea hoja ya kuboresha kikokotoo kwakuwa wafanyakazi hawaridhishwi na kanuni zake

Mei Mosi: Dkt. Mpango asema Serikali imepokea hoja ya kuboresha kikokotoo kwakuwa wafanyakazi hawaridhishwi na kanuni zake

Fuatilia kinachojiri kwenye Maadhimisho ya siku ya Mei Mosi Kitaifa, Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha, leo Mei 1, 2024


Maadhimisho haya yamehudhuriwa na Makamu wa Rais, Philip Mpango, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge Tulia Ackson, Mawaziri pamoja na viongozi wengine wa Serikali.

KATIBU MKUU TUCTA, HERI MKUNDA
Akizungumza kwenye Sherehe hizo, Katibu Mkuu TUCTA Heri Mkunda amesema maboresho ya mishahara iliyofanyika bado haijakidhi mahitaji ya wafanyakazi, hivyo vinapaswa kuboresha kwani gharama za maisha zimepanda sana.
View attachment 2978185
Amesema wanatambua uwepo wa nyongeza ya 23.3% ya kima cha chini cha mshahara iliyofanyika, lakini inafaa ongezeko hili lizingatie pia wafanyakazi wengine.

Aidha, wafanyakazi wanaolipwa kwa mapato ya ndani ya halmashauri wanalalamika kutokulipwa maslahi yao kwa wakati kwani uwezo wa halmashauri unatofautiana. TUCTA inapendekeza wafanyakazi wote wa halmashauri kulipwa kutoka Serikali kuu ili kuondoa ubaguzi.

Kuhusu kikokotoo, wafanyakazi hawaridhishwi na namna kinavyofanyika na kimeleta malalamiko mingi. TUCTA inashauri kanuni za ukokotoaji mafao ziboreshwe ili kuleta manufaa kwa wafanyakazi.

Mambo mengine aliyozungumza ni kuongezewa likio ya miezi 3 kwa wanawake waliojifungua watoto njiti pamoja na kupitishwa kwa kitita kipya cha bima ya NHIF bila kushirikisha wafanyakazi kupitia vyama vyao hivyo kuzua taharuki. TUCTA inapendekeza wafanyakazi washirikishwe kwenye maboresho haya ya kitita.

Kikokotoo ni haramu, Wizi na uonevu, Nimestaafu Nina miaka 60, Halafu makadirio ya kuishi ni miaka 72, Halafu mtu anakwambia utapewa kidogo kidogo, hivi hiyo ni akili kweli? Hiyo Hela nitumie nikiwa kaburini? Imebaki miaka 12, Sasa kidogo kidogo hiyo sijui iweje? Huu ni unyonyaji, uonevu, ukiukwaji wa haki ONDOA KIKOKOTOO
 
KIKOKOTOO CHA KOKOTWA HADI MWAKANI MARA OOOH KAMATI ICHUNGUZE UPYA MPAKA LINI SERIKALI HAIJAJIPANGA KWA KULIPA MAFAO HII INAIPA SERIKALI MUDA WA KUJIPANGA NA KUTAFUTA FEDHA , MAANA KULIPA WASTAAFU 1400 KWA MARA MOJA MILIONI 230 KILA MMOJA HASARA SAAAANA SUBIRINI WAFANYAKAZI
 
PM anasemaje mama yupo K'koo au Migomigo anakula kachori,?
 
"Uwezo wa kiuchumi na kibajeti, ujuzi na utendaji wa waajiriwa"..
.........................................
Hii kauli siyo ya kuchukuliwa harakaharaka.
 
Hebu Jifanye Kama Unajikuna Tu Uone!
By Agrey Mwanri
 
Huku tunaambiwa mama atasema Jambo hivi karibuni.
Hahah...
Catastrophes zikipungua, sijui zikiisha.
😆🤣😅 Ndo imeshatoka hiyo.

Halafu mwakani kuna catastrophe ya ukame (sever drought), ambalo serikali nyingi zitalazimika kuwanunulia wananchi wake vyakula.

Likiisha janga la asili hili, linaibuka jingine kivingine. Lini yataisha ili watumishi wapewe stahiki zao?
 
Oooh! Mama atakuja kutoa tamko siku za baadaye!! Yaani watumishi wameshapigwa na kitu kizito kichwani.
Siyo siku za baadae tu ila ni siku za baadae kama nchi itaendelea kuwa kwenye status iliyopo sasa ya ustaimilivu wa wa hali ya sasa ya kushake kwa uchumi unaosababishwa na vita ya urus vs Ukraine na ile ya mashariki ya kati.
 
Back
Top Bottom