Meli ya thamani inateketea, wanamsaliti Nyerere

Meli ya thamani inateketea, wanamsaliti Nyerere

Pole sana mkuu, lakini maumivu ni yetu sote.

Hebu ngoja nikusononeshe na mifano mingi zaidi ya hiyo uliyoitaja hapo.

Tanzania kuna jua karibu kila siku, mwaka mzima. Kuna sehemu zina upepo wa kutosha sana kuzalisha umeme. Sasa hivi tunao viongozi wanao kesha wakitafuta namna ya kuwaleta wawekezaji hapa, waje watumie jua letu, upepo wetu wazalishe umeme ili watuuzie kwa bei mbaya, na wala viongozi wetu hawaoni uchungu wowote hapo.

Tunayo ardhi nzuri kabisa ya kutuwezesha kuzalisha mazao ya kutupatia mafuta ya kula ya kutosha kwa matumizi yetu na hata kuwauzia wengine nchi za nje. Wananchi wetu, wakulima wanakosa msaada wa serikali yao ili wazalishe mazao haya kwa wingi, lakini viongozi wetu wanajuwa jambo moja tu, la WAWEKEZAJI toka nje!

Huku ni kuwa na kilema cha akili, sijui kilema hiki kitarekebishwa vipi tuanze kujuwa namna ya kutumia raslimali zetu kutunufaisha sisi wenyewe.
 
Unajengaje uwezo wa ndani bila Mwekezaji mzungu? Kwani kabla ya mzungu kuja na vyombo vyake ulijua kuwa kuna gesi Mtwara?

Kabla ya Williamson kununua almasi pale mwadui, kuna mtu alikuwa anajuwa kuwa Ina thamani? Mbona wasukuma walikuwa wanachezea nao la kete?

Tuwe wakweli, mzungu ndiye mwenye teknoloji na ndiye mwenye soko. Mzungu ndiye mwenye elimu na ndiye anatufundisha. Hamna kitu kitakuwa na thamani asiposema yeye.

Akiamua kuwa takataka za dampo ni thamani, bado utajicheka tena kuwa kwa nini mpaka mzungu.
Inasikitisha sana kusoma mawazo kama haya, lakini, heee, mkuu Stxnet, ni haki yako kutamba na mawazo yako uonavyo inafaa.
 
Inasikitisha sana kusoma mawazo kama haya, lakini, heee, mkuu Stxnet, ni haki yako kutamba na mawazo yako uonavyo inafaa.
Tatizo ni kuwa wenye mawazo kama haya ndiyo wengi wameshika hatamu...Hakika tunahitaji substitution ndiyo hapo na mimi nakubali sasa tuwe na katiba mpya...Bila hivi hawa matarishi watatuuza mazima mchana kweupe pasipokujitikisa kwakua wametufunga mikono na miguu kisha wanasema hatuwezi kujisaidia
 
Mama amesikia kilio chako tulia kidogo,kila kitu kitakaa sawa.
#Kazi imeanza,alikuwa anausoma kwanza mchezo.
 
Hivi wewe uko timamu kweli??
South Africa ni mfano mzuri.Ilijengwa na wazungu a.k.a Makaburu,ila kama ingeingia kwa Mandela miaka ya 60 huko,ingekuwa hovyo tu.Sera ya ujamaa nayo kwa nchi yetu iliturudisha nyuma sana.Shukrani kwa Mwinyi kuvunjilia mbali ujamaa.
 
Wameamua Demokrasia huku wanajidai tusi wakwamishe wanajenga uchumi. Mtaani watu wana hasira tena hasira mbaya. Hasira ya kumbambikiwa kesi, hasira ya mzunguko wa fedha kuwa hafifu, hasira wa uhaba wa malisho kwa mifugo wao, uhaba wa demokrasia kuchugua viongozi wanao wataka wao, hasira ya kunyimwa kufanya mikutano ya kisiasa wakati wao wanafanya. Hili la timu kuendelea kucheza uanjani peke ya litaigharimu sana.

Wataendelea kuchukiwa watasusa na hamtajua wamesusa. Hii ni hatari tusiruhusu kuendelea na uhuru aliyetuachia Nyerere, akaukoleza Mwinyi, akaulea Mkapa akaukuza Kikwete, akaunyonga Magufuli watanzania wakalia kasononeka sana.

Akaja mama wanalia zaidi. Tujisahihishe. Tusipofanya hivyo kwa sababu tume beba lawama tutaendelea kufoka moyoni tunajua fika kuwa tunafanya makosa. Tusizibe masikio yatatukuta makubwa ambayo hatukutarajiwa tufike huko.
 
Unajengaje uwezo wa ndani bila Mwekezaji mzungu? Kwani kabla ya mzungu kuja na vyombo vyake ulijua kuwa kuna gesi Mtwara?

Kabla ya Williamson kununua almasi pale mwadui, kuna mtu alikuwa anajuwa kuwa Ina thamani? Mbona wasukuma walikuwa wanachezea nao la kete?

Tuwe wakweli, mzungu ndiye mwenye teknoloji na ndiye mwenye soko. Mzungu ndiye mwenye elimu na ndiye anatufundisha. Hamna kitu kitakuwa na thamani asiposema yeye.

Akiamua kuwa takataka za dampo ni thamani, bado utajicheka tena kuwa kwa nini mpaka mzungu.
South Africa ni mfano mzuri.Angepewa ile nchi Mandela miaka ya 60 huko,nchi ingekuwa hovyo tu.
 
Umemkumbuka sana mwl JK Nyerere kimtindo ingawa kwa kuwaamusha walio vimbiwa na kodi zetu.
 
Wakumlaumu ni huyo huyo Nyerere. Alikuwa na kiherehere cha kuongoza kabla ya nchi kuwa tayari. Matatizo mnayoyaona sasa hivi ni matunda ya kujitawala kabla hatujawa tayari.
Hakuna ushahidi wa hilo
 
Wakumlaumu ni huyo huyo Nyerere. Alikuwa na kiherehere cha kuongoza kabla ya nchi kuwa tayari. Matatizo mnayoyaona sasa hivi ni matunda ya kujitawala kabla hatujawa tayari.
Huu ni ujinga mbaya zaidi.
 
Haya ndio mawazo ya kizalendo, na sio mtu kujiita mzalendo kisa kapewa V8 ya umma. Kulitakiwa kujengwe viwanda ili vitoe ajira kwa vijana, na sio serikalini kujaa magari ya bei kubwa huku wananchi wanateseka kwa kukosa ajira.
Huyu jf member nimemkubali kwa hili bandiko maana kasema ukweeeriiiiiii mtupu.
 
Pole sana mkuu, lakini maumivu ni yetu sote.

Hebu ngoja nikusononeshe na mifano mingi zaidi ya hiyo uliyoitaja hapo.

Tanzania kuna jua karibu kila siku, mwaka mzima. Kuna sehemu zina upepo wa kutosha sana kuzalisha umeme. Sasa hivi tunao viongozi wanao kesha wakitafuta namna ya kuwaleta wawekezaji hapa, waje watumie jua letu, upepo wetu wazalishe umeme ili watuuzie kwa bei mbaya, na wala viongozi wetu hawaoni uchungu wowote hapo.

Tunayo ardhi nzuri kabisa ya kutuwezesha kuzalisha mazao ya kutupatia mafuta ya kula ya kutosha kwa matumizi yetu na hata kuwauzia wengine nchi za nje. Wananchi wetu, wakulima wanakosa msaada wa serikali yao ili wazalishe mazao haya kwa wingi, lakini viongozi wetu wanajuwa jambo moja tu, la WAWEKEZAJI toka nje!

Huku ni kuwa na kilema cha akili, sijui kilema hiki kitarekebishwa vipi tuanze kujuwa namna ya kutumia raslimali zetu kutunufaisha sisi wenyewe.
Hivi unafikiri kuna mtanzania mwenye elimu tosha kufanya hayo?
Hiyo elimu atakuwa kaipata wapi?
Hivi unafikiri kuna mzungu yupo tayari kutoa elimu yenye kukidhi mahitaji ya utafiti na ugunduzi kwa mwafrika?
Tuache kujidanganya kuwa tunawasomi sahihi wa kuyafanya haya kwa elimu nusu waliyopewa na hao hao wazungu.
 
Tatizo ni kuwa wenye mawazo kama haya ndiyo wengi wameshika hatamu...Hakika tunahitaji substitution ndiyo hapo na mimi nakubali sasa tuwe na katiba mpya...Bila hivi hawa matarishi watatuuza mazima mchana kweupe pasipokujitikisa kwakua wametufunga mikono na miguu kisha wanasema hatuwezi kujisaidia
Weka mifano ya nchi za afrika zilizopiga hatua kiteknolojia kwa kutumia wa Afrika wenyewe.
 
Mama ni mzalendo sana. Tumpe muda.
Huko ndani hawataki kumpa muda wanasema ufisadi umezidi, na yeye anasema hajafanya ufisadi bali ni awamu zilizopita, sasa sijui awamu zilizopita yeye hakuwepo
 
Wakumlaumu ni huyo huyo Nyerere. Alikuwa na kiherehere cha kuongoza kabla ya nchi kuwa tayari. Matatizo mnayoyaona sasa hivi ni matunda ya kujitawala kabla hatujawa tayari.
Kwa hilo namtetea Nyerere. Hata tungekaa miaka 10 zaidi Waingereza hawakuwa na mpango wa kuendeleza chochote. Lawama kwa Mwalimu ni kutuachia Katiba ya Kifalme kwenye mfumo wa vyama vingi.
 
Back
Top Bottom