Meli ya Vitabu Bandari ya Dar es Salaam "Mv Logos Hope" yaingia tena baada ya miaka 7

Meli ya Vitabu Bandari ya Dar es Salaam "Mv Logos Hope" yaingia tena baada ya miaka 7

Offshore Seamen

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2018
Posts
5,489
Reaction score
14,091
Mv Logos Hope ni meli ya vitabu yenye library kubwa yenye vitabu mbalimbali inayozunguka kwenye mataifa na bandari mbalimbali duniani.

Logos_Hope_Kiel2008.jpg


Meli hii ya kihistoria ilijengwa mwaka 1973 huko Randsburg, kaskazini mwa Ujerumani kisha ikapita mikononi mwa kampuni tofauti mpaka 2004 ilipochukuliwa na GBA Ship na kufanyiwa marekebisho na kuwekewa library ya vitabu, mwaka 2005 ikaanza kuzunguka bandari tofauti Duniani.

images (14).jpeg
download.jpeg


Meli hii ina urefu wa mita 132.50,upana 21.06 wafanyakazi 442 na imesajiliwa Nchini Malta. Wastani hutembelea nchi 70 na bandari zipatazo 140 duniani kote.

Mara ya mwisho meli hii ilikuja Tanzania 25/01/2016 na kuondoka tarehe 18/02/2016. Mwaka huu tena Tanzania imepata Bahati ya kutembelewa na meli hii imeingia tarehe 05/10/2023 na itakuwa Nchini kwa wiki 2, mpaka tarehe 22/10/2023.

Hii ni fursa kwa sekta ya utalii,elimu na wadau mbalimbali kwenda kutembelea na kujifunza kiingilio ni Shilingi 1000 ya Kitanzania.Tiketi za kuingilia melini zinapatikana geti namba 2 la Bandari ya Dar es Saalam njia ya Kituo kikuu cha Central Police au Stesheni kwa wageni.
20231007_125957.jpg


Picha baadhi za sehemu za ndani za meli ya Logos Hope.Wenye familia,watoto,mashule kuna vitabu sehemu za kupiga picha,ice cream,kahawa na kumbi za kuonyesha matamasha ya watu mataifa mbalimbali.

r74111.jpg


Ratiba ya kutembelea siku ya Jumatatu kuna mapumziko. Hivyo ni kuanzia Jumanne mpaka Jumapili.
 
Mimi nipo dsm kwa Sasa ningetamani kwenda kuchukua vitabu Kama the power of subconscious mind je Bei zao zinaweza kuwa sh .ngapi? Wakuu .

???? Tutajienu Bei wakuu tujue
 
Ni duka la vitabu, sio maktaba. Kwa mujibu wa hilo tangazo hapo juu. Sasa sijui wewe ni mwandishi wa habari au raia tu wa kawaida unajiandikia tu kihole holela kama hukusoma
Una makasiriko ya nini braza?
Jamaa ametudokeza tu na sio mwandishi wa habari, shida yako nini mkuu wangu?

Hasira za maisha msilete huku mnadhalilisha utu mliokirimiwa bure na Muumba.

Kunywa maji kwanza mkuu
 
Back
Top Bottom