Meli ya Vitabu Bandari ya Dar es Salaam "Mv Logos Hope" yaingia tena baada ya miaka 7

Meli ya Vitabu Bandari ya Dar es Salaam "Mv Logos Hope" yaingia tena baada ya miaka 7

Kwa namna hiyo meli inavyo zunguka nchi nyingi duniani ni nafasi nzuri kwa sekta ya utalii nchini kufanya jambo kuhakikisha kila sehemu hiyo meli inako tia nanga wanajua kuhusu utalii wa Tanzania
 
Kwa namna hiyo meli inavyo zunguka nchi nyingi duniani ni nafasi nzuri kwa sekta ya utalii nchini kufanya jambo kuhakikisha kila sehemu hiyo meli inako nanga wanajua kuhusu utalii wa Tanzania
Sekta ya utalii Tanzania tumepata bahati ya meli hii lakini nafasi hatutumii vizuri.

Mwezi wa 8 meli hii ilikuwa Kenya ilitangazwa na wizara yao ya utalii na vyombo vya habari vya kule.

Sisi Wizara ya Maliasili na Utalii, bodi ya Utalii hata hawajatangaza, wanashindwa kuweka hata mabango yao kuonyesha vivutio kwa wafanyakazi wa meli wapatao 400 hata bango la Karibu Tanzania
 
Vyombo vya habari havijatoa nafasi ya kutangaza sana ujio wa meli hii. Wamezoea kutangaza meli zile kubwa mfano meli ndefu au meli zenye gari nyingi ziingiapo Nchini.
 
Mwaka 2016 kulikuwa na Utaratibu wa gari za kupeleka na kurudisha watu, kutoka geti la kuingia mpaka melini. Mwaka huu hakuna Utaratibu huo. Inalazimu baada ya kukata ticket utembee kutoka gate no.2 mpaka melini.

Meli bado ina siku 14 mbele, Bandari na agent wana nafasi ya kuboresha na kufanya vizuri kwa kupata idadi kubwa ya watu watakao tembelea
 
Anaejua bei za vitabu vyao vinaanzia sh ngapi

Sent from my SM-N975U using JamiiForums mobile
20231007_162111.jpg

Unit 25 ni sawa na Tsh 1500. Ukikuta kitabu ni 100units hapo ni sawa na tsh 6000.
20231007_162634.jpg
 
Mv Logos Hope ni meli ya vitabu yenye library kubwa yenye vitabu mbalimbali inayozunguka kwenye mataifa na bandari mbalimbali duniani.

View attachment 2774301

Meli hii ya kihistoria ilijengwa mwaka 1973 huko Randsburg, kaskazini mwa Ujerumani kisha ikapita mikononi mwa kampuni tofauti mpaka 2004 ilipochukuliwa na GBA Ship na kufanyiwa marekebisho na kuwekewa library ya vitabu, mwaka 2005 ikaanza kuzunguka bandari tofauti Duniani.

View attachment 2774298View attachment 2774299

Meli hii ina urefu wa mita 132.50,upana 21.06 wafanyakazi 442 na imesajiliwa Nchini Malta. Wastani hutembelea nchi 70 na bandari zipatazo 140 duniani kote.

Mara ya mwisho meli hii ilikuja Tanzania 25/01/2016 na kuondoka tarehe 18/02/2016. Mwaka huu tena Tanzania imepata Bahati ya kutembelewa na meli hii imeingia tarehe 05/10/2023 na itakuwa Nchini kwa wiki 2, mpaka tarehe 22/10/2023.

Hii ni fursa kwa sekta ya utalii,elimu na wadau mbalimbali kwenda kutembelea na kujifunza kiingilio ni Shilingi 1000 ya Kitanzania.Tiketi za kuingilia melini zinapatikana geti namba 2 la Bandari ya Dar es Saalam njia ya Kituo kikuu cha Central Police au Stesheni kwa wageni.
View attachment 2774293

Picha baadhi za sehemu za ndani za meli ya Logos Hope.Wenye familia,watoto,mashule kuna vitabu sehemu za kupiga picha,ice cream,kahawa na kumbi za kuonyesha matamasha ya watu mataifa mbalimbali.

View attachment 2774296

Ratiba ya kutembelea siku ya Jumatatu kuna mapumziko. Hivyo ni kuanzia Jumanne mpaka Jumapili.
Iliwahi kuja enzi za magu?
 
Nipo hapa melini kweli watanzania tumelala kila Sekta, wanakuja watu wa nchi mbalimbali, kutoka ubalozini na watanzania wengine wanakosa Cash kulipa vitu.

Vodacom ndio wapo nao wameweka huduma ya kulipa. Kuna watu wanataka Cash wanakosa mpaka watoke nje. Meli wana kubali Credit Card. Hakuna taasisi ya kifedha ilikuja kuweka hata tent kutoa huduma na meli itakuwa nchini week 2.
 
Nipo hapa melini kweli watanzania tumelala kila Sekta, wanakuja watu wa nchi mbalimbali, kutoka ubalozini na watanzania wengine wanakosa Cash kulipa vitu.

Vodacom ndio wapo nao wameweka huduma ya kulipa. Kuna watu wanataka Cash wanakosa mpaka watoke nje. Meli wana kubali Credit Card. Hakuna taasisi ya kifedha ilikuja kuweka hata tent kutoa huduma na meli itakuwa nchini week 2.
Bongo tupo nyuma saana kaka.
 
Back
Top Bottom