Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Vikiwa bure wengine hawatavithamini. Wanaweza wakavichukua wakaishia kwenda kufungia "mandazi"Wanauza au unajichukulia tu ?
Vyombo vya habari havijatoa nafasi ya kutangaza sana ujio wa meli hii. Wamezoea kutangaza meli zile kubwa mfano meli ndefu au meli zenye gari nyingi ziingiapo Nchini.
Agent wa meli ndio anaratibu, hii meli dhumuni lake kuu ni kufanya kazi za kijamii kwa kujitolea na kusaidia wahitaji. Wana akaunti za kuchangia na unaponunua vitu unakuwa umechangia wahitajiMamlaka gani inaratibu shughuli zake iwapo nchini.
Kunywa maji mengi pia zingatia milo mitatu kwa siku.. Inasaidia kuondoa makasiriko ya kipumbavuNi duka la vitabu, sio maktaba. Kwa mujibu wa hilo tangazo hapo juu. Sasa sijui wewe ni mwandishi wa habari au raia tu wa kawaida unajiandikia tu kihole holela kama hukusoma
Akina Patel na Charan!Ni elfu 1 kaka, vitabu vipo vya kila aina, sehemu za kupiga picha za mandhari tofauti. Ice cream kuanzia elfu 1.
Walete watoto wacheze na wenzao wakina Patel na Charan maana leo ndio wamejaa
Ni ya dini walokole,mambo hayo kwao ni haramuWasilete Mambo yao ya ushoga
Punguza stress mazee...ukisoma ndio unaandika Hukusoma?Ni duka la vitabu, sio maktaba. Kwa mujibu wa hilo tangazo hapo juu. Sasa sijui wewe ni mwandishi wa habari au raia tu wa kawaida unajiandikia tu kihole holela kama hukusoma
Sisi watu weusi kwenye vitabu hatuna muamko sana. Hata kujenga tamaduni kwa watoto wasome vitabuAkina Patel na Charan!
Kwa hiyo akina baba Masanaja na akina mama Bahati hawajui umuhimu wa kuwapeleka watoto wao "dukani?"
Kwanini wasiviupload kwenye mtandao halafu waipaki kwao tuMv Logos Hope ni meli ya vitabu yenye library kubwa yenye vitabu mbalimbali inayozunguka kwenye mataifa na bandari mbalimbali duniani.
View attachment 2774301
Meli hii ya kihistoria ilijengwa mwaka 1973 huko Randsburg, kaskazini mwa Ujerumani kisha ikapita mikononi mwa kampuni tofauti mpaka 2004 ilipochukuliwa na GBA Ship na kufanyiwa marekebisho na kuwekewa library ya vitabu, mwaka 2005 ikaanza kuzunguka bandari tofauti Duniani.
View attachment 2774298View attachment 2774299
Meli hii ina urefu wa mita 132.50,upana 21.06 wafanyakazi 442 na imesajiliwa Nchini Malta. Wastani hutembelea nchi 70 na bandari zipatazo 140 duniani kote.
Mara ya mwisho meli hii ilikuja Tanzania 25/01/2016 na kuondoka tarehe 18/02/2016. Mwaka huu tena Tanzania imepata Bahati ya kutembelewa na meli hii imeingia tarehe 05/10/2023 na itakuwa Nchini kwa wiki 2, mpaka tarehe 22/10/2023.
Hii ni fursa kwa sekta ya utalii,elimu na wadau mbalimbali kwenda kutembelea na kujifunza kiingilio ni Shilingi 1000 ya Kitanzania.Tiketi za kuingilia melini zinapatikana geti namba 2 la Bandari ya Dar es Saalam njia ya Kituo kikuu cha Central Police au Stesheni kwa wageni.
View attachment 2774293
Picha baadhi za sehemu za ndani za meli ya Logos Hope.Wenye familia,watoto,mashule kuna vitabu sehemu za kupiga picha,ice cream,kahawa na kumbi za kuonyesha matamasha ya watu mataifa mbalimbali.
View attachment 2774296
Ratiba ya kutembelea siku ya Jumatatu kuna mapumziko. Hivyo ni kuanzia Jumanne mpaka Jumapili.
Kuna watu wanahitaji kuingia melini na kufanya utalii. Waone mazingira ya meli, wajifunze vitu tofautiKwanini wasiviupload kwenye mtandao halafu waipaki kwao tu
Iko gati namba ngapi
Mkuu, nahisi ukisema mtu mweusi, unaweza ukawa unakosea. Pamoja na kuwa usomaji vitabu si tabia iliyozoeleka Tanzania, kuna baadhi ya Watanzania wanaopenda kusoma vitabu, mimi nikiwemo.Sisi watu weusi kwenye vitabu hatuna muamko sana. Hata kujenga tamaduni kwa watoto wasome vitabu
📌Nimeona, ni nzuri sana aisee...kesho basi twende mapema