Meli ya Vitabu Bandari ya Dar es Salaam "Mv Logos Hope" yaingia tena baada ya miaka 7

Meli ya Vitabu Bandari ya Dar es Salaam "Mv Logos Hope" yaingia tena baada ya miaka 7

Nafikiri waandishi wetu wameshajua taarifa kama hizi za meli ya vitabu hazina amsha amsha kwa Wabongo wengi.
Vyombo vya habari havijatoa nafasi ya kutangaza sana ujio wa meli hii. Wamezoea kutangaza meli zile kubwa mfano meli ndefu au meli zenye gari nyingi ziingiapo Nchini.
 
Ni elfu 1 kaka, vitabu vipo vya kila aina, sehemu za kupiga picha za mandhari tofauti. Ice cream kuanzia elfu 1.

Walete watoto wacheze na wenzao wakina Patel na Charan maana leo ndio wamejaa
Akina Patel na Charan!

Kwa hiyo akina baba Masanaja na akina mama Bahati hawajui umuhimu wa kuwapeleka watoto wao "dukani?"
 
20231007_183531.jpg
20231007_183731.jpg
20231007_183715.jpg

Alamsiki

Buenas Noches
 
Mv Logos Hope ni meli ya vitabu yenye library kubwa yenye vitabu mbalimbali inayozunguka kwenye mataifa na bandari mbalimbali duniani.

View attachment 2774301

Meli hii ya kihistoria ilijengwa mwaka 1973 huko Randsburg, kaskazini mwa Ujerumani kisha ikapita mikononi mwa kampuni tofauti mpaka 2004 ilipochukuliwa na GBA Ship na kufanyiwa marekebisho na kuwekewa library ya vitabu, mwaka 2005 ikaanza kuzunguka bandari tofauti Duniani.

View attachment 2774298View attachment 2774299

Meli hii ina urefu wa mita 132.50,upana 21.06 wafanyakazi 442 na imesajiliwa Nchini Malta. Wastani hutembelea nchi 70 na bandari zipatazo 140 duniani kote.

Mara ya mwisho meli hii ilikuja Tanzania 25/01/2016 na kuondoka tarehe 18/02/2016. Mwaka huu tena Tanzania imepata Bahati ya kutembelewa na meli hii imeingia tarehe 05/10/2023 na itakuwa Nchini kwa wiki 2, mpaka tarehe 22/10/2023.

Hii ni fursa kwa sekta ya utalii,elimu na wadau mbalimbali kwenda kutembelea na kujifunza kiingilio ni Shilingi 1000 ya Kitanzania.Tiketi za kuingilia melini zinapatikana geti namba 2 la Bandari ya Dar es Saalam njia ya Kituo kikuu cha Central Police au Stesheni kwa wageni.
View attachment 2774293

Picha baadhi za sehemu za ndani za meli ya Logos Hope.Wenye familia,watoto,mashule kuna vitabu sehemu za kupiga picha,ice cream,kahawa na kumbi za kuonyesha matamasha ya watu mataifa mbalimbali.

View attachment 2774296

Ratiba ya kutembelea siku ya Jumatatu kuna mapumziko. Hivyo ni kuanzia Jumanne mpaka Jumapili.
Kwanini wasiviupload kwenye mtandao halafu waipaki kwao tu
 
Sisi watu weusi kwenye vitabu hatuna muamko sana. Hata kujenga tamaduni kwa watoto wasome vitabu
Mkuu, nahisi ukisema mtu mweusi, unaweza ukawa unakosea. Pamoja na kuwa usomaji vitabu si tabia iliyozoeleka Tanzania, kuna baadhi ya Watanzania wanaopenda kusoma vitabu, mimi nikiwemo.

Nafikiri, ningelikuwepo Dar Es Salaam, nisingekosa kwenda na familia yangu.

Hivi lakini, hakuna kinachoweza kufanyika ili kuwaibua watu wengi zaidi Tanzania wanaopenda kusoma vitabu?
 
Back
Top Bottom