Mema kwa mkulima wa Tanzania... Bashe na Rais Samia wanafanya kweli

Mema kwa mkulima wa Tanzania... Bashe na Rais Samia wanafanya kweli

Mkulima wa Tanzania sasa hivi ana kituo cha kisasa cha huduma kwa mtej (,Customer care).

Bashe kwa mara ya kwanza Tanzania, anaifanya Wizara ya kilimo kuwa ni watoa huduma wa kisasa kwa wakulima. Jionee:



Mengine tutaendelea kuwaletea.

Hongera Bashe, Hongera Rais Samia.

Hicho kituo kiko wapi na kinafikiwa vipi?
 
Kituo cha huduma kwa wateja kinamsaidia nini mkulima anaetegemea mvua na mbolea isiyo na bei ya kueleweka?

Kituo cha huduma kwa wateja kina msaada gani kama mkulima analima kisha anapangiwa bei ya kuuza ama anazuiliwa asiuze mazao yake nje ya nchi?

Ama mkulima anakua anapiga simu anauliza kama shamba lake limejaa magugu, je ayapalilie ama anachome anapewa majibu wa desk officer farmers wa ofisi?
Nyie ndo wale Pinga Pinga wa bawacha?
 
Wakulima tuliopo kwenye kilimo tumenyamaza tu maana yaliyopo hayatufurahishi, ila nyie wadananda mnajifanya yamkulima mnayajuwa.

Mtu hujawahi hata kulima, hujuwi chochote kuhusu kulima ila na wew unazungumzia kilimo. Customer care itanisaidia nin kama nalima mazao ya biashara na bei inakuwa iko chini, sanaa sanaa tu kila mwaka.
Mkuu inaudhi sana. Mijitu inavimbiwa tu Chipsi na Dona mjini hawajui hata Kilimo chake. Yaweza kuwa mimi siyo Farmer lakini Mkulima wa kati, hizi ngonjera za akina Bashe labda ni kwa ajili ya Big Farmers siyo Peasants waliojaa kila kona ya Tanzania.
 
Uzi umesusiwa
Huu uzi siyo wa kuchangiwa, elewa namna ya nyuzi zilizopo, sasa hapa mtu atabisha nini, na kila kitu kipo wazi? Huu uzi umelenga kuelemisha watu. Unabaki hapa kuwa "reference". Tukibishana huko, nakuleta hapa ujionee au nakuvutia post nakubandikia ulipo.

Usifikiri kila uzi ni wa watu kuchangia.
 
Aisee, sijui ni teuzi sijui ni pesa, inatafutwa sana kwa kumshawishi alie juu.
Sijakuelewa. Nani anae tafuta pesa? na nani anaetafuta uteuzi? Labda tuanzie hapo halafu tukupe darsa hayo utayapata wapi na vipi.
 
Kilimo kiko Mashambani. Hizi mbwembwe za kwenye keyboards hazisaidii wakulima.

Inashangaza mno!

Uhalisia wa kilimo na mkulima huku mashambani ni mbingu na ardhi na hizi propaganda.

Wawekezaji na pesa za uwekezaji vinawekwa kwenye mashamba ya viongozi na ndugu na Jamaa zao halafu mtanzania anaekamuliwa kwa double taxation kila kona anapewa nadharia na maneno Kama waimba taarabu.

Inaumiza sana.
 
Sijakuelewa. Nani anae tafuta pesa? na nani anaetafuta uteuzi? Labda tuanzie hapo halafu tukupe darsa hayo utayapata wapi na vipi.
Darsa gani mkuu, maana hali halisi za wakulima tunazijua, siasa za wanasiasa kuwanufaisha wakulima hazijaanza leo.

Na uzuri ni kua watz wengi tumekulia mikononi mwa familia za wakulima.
 
Laiti wakulima wangekuwa wanapiga hesabu za uzalishaji sidhani kama watu wangekima. Ni wachache sana wanafaidika na kilimo kama wakulima hususani wenye uwezo wa kuhifadhi nafaka baada ya mavuno
 
BBT ni NINI?
BBT ni mpango wa kipekee kuwahi kutokea Tanzania ( pengine hata duniani) ulianzoshwa na amama Samia kwa kiwango kikubwa kupitia rasilmali mama ya Tanzania ambayo ni ardhi, kwa sasa kngo kikubwa unasimamiwa na Mheshimiwa Bashe, Waziri wa Kilimo: Jiponee na jisikilizie:


View: https://youtu.be/OTEEoNW2j0M


Naamini, baada ya bandari, huo ni mpango wa kwanza utaopigwa vita na kanisa katoliki. Sababu zipo wazi.
 
Porojo tu hakuna jipya.
BBT ya Samia Suluhu na Hussein Bashe ni mpango kabambe haujawahi kutokea Afrika, hautakiwi ufanikiwe. Tunalijuwa hilo.

Ardhi ya kilimo inahodhiwa na nani?
 
Back
Top Bottom