Uchaguzi 2020 Membe aenda Tume ya Uchaguzi kuhakiki fomu zake kabla ya kuziwasilisha rasmi kesho

Kwanini NEC isitume fomu za wagombea kwa njia ya "soft copy" kwenye email za vyama za siasa zikiwa na majina ya wagombea waliopitishwa then ijazee kwa njia hiyo hyo ya soft copy nakurudishwa tume kwa njia ya email kuepuka ujinga na upumbavu unaofanywa na wakurungezi wa halmashauri? Na hakuna anayejua original na copy Ni ipi,.
 
Mambe pandikizi la ccm , Yaani ccm b anatengeneza mazingira ionekane Lissu kakosea hapa ndio muelewe na Kauli yake ya juzi kuwa alienda kutafuta wadhamini kimyakimya ili ?
 
Kwan yeye ndo aliyetunga katiba ? C ni nyinyi Ma ccm ndo mlitunga katiba na inasema hivo na mkasaini mikataba ya kimattaifa ? Mbona hatujaona serikali mnayoisifia ikikataa huo ushoga tz zaidi ya kumkana Paul makonda?
 
Zimeandikwa katika lugha gani hizo fomu? Jiwe amekwenda lakini? Kama zimeandikwa kwa Kimombo, namshauri aende kabla hawajafunga ofisi.
Jiwe anajua kiingereza vizuri sana; tatizo hana uzoefu wa kukiongea tu, lakini hakuna document ya kiingereza inayomshinda kusoma na kuelewa. Anajua kuandika na kusoma vizuri lakini siyo fundi wa kuongea.
 
Hii ndiyo sera ya kuchochea fujo bila kuwa na mantiki. Post hiyo ya Mbowe inatoa ultimatum kwa NEC kuwa hata kama CHADEMA itafanya makosa NEC isismamie sheria kwa kuogopa kuvunjika kwa amani. Hizo ni siasa za kijinga sana; ni afadhali Membe aliyekwenda kuhakiki fomu zake kujiridhisha kuwa hakuna makosa ya kisheria. Huyu Mbowe anataka CHADEMA ibebwe tu hata kama fomu zina makosa ya kisheria !!. Kuna makosa mengine yanaweza kuwa ni mdogo tu, lakini sheria ikachukua mkondo wake; huwa wanasema aliyeiba shilingi moja na aliyeiba milioni moja wote ni wezi mbele ya sheria!
 
..hii habari ipo JF tu, sijaiona mahali pengine popote.

..siamini kama act wanaweza kufanya jambo hilo bila waandishi wa habari.
 
Tenga alishindwa kujaza fomu ya Mrema ya kupinga matokeo wakati wa NCCR.Mwanasheia siyo malaika.
 
Kwa sheria ipi? Je babayenu mnayemwabudu meenda au Yuki bize na makongamano uchwara
Sheria inaruhusu kuhakiki fomu zozote kabla ya kuziwakilisha rasmi; siyo za uchaguzi tu bali ni fomu yoyote ya kisheria. Ulaji mmojawapo wa wanasheria ni Commissioner of Oaths and Notaries ambapo jukumu lao ni kukusaidia kuhakiki formu yako na kuithibitisha kwa kuwalipa fee fulani. Lakini unaweza kwenda kwa hakimu moja kama atapatikana akakuhakikia fomu zako na kuzithibitisha bure kabla hujaziwakilisa rasmi.
 
Kuna mwanasheria mmoja wa CHADEMA huko sehemu za Iringa au Mbeya alijaza fomu za ubunge, halafu akajiapisha mwenyewe ambapo ni kinyume cha sheria, na hivyo fomu yake ikatupiliwa mbali. Kuwa mwanasheria siyo kuwa bingwa wa kila kila kitu; uzoefu una matter sana. Lissu sasa hivi amekuwa anaongea maneno yanayoonyesha kuwa uwezo wake wa sheria umepungua sana, kwani hajafanya kazi zake za kutetea kesi za mazingira na haki za binadamu kwa muda mrefu sana tangu aanze siasa. Ndiyo maana mara nyingi amekuwa anaropoka madai kama vile siyo mwanasheria tena. Kumbuka kuwa hata Richard Nixon alikuwa mwanasheria mzuri sana kabla ya kuingia kwenye siasa; baada ya muda mrefu kwenye siasa akawa crook.
 
Unawashwa matter coni?

Membe na Chadema wapi na wapi ?
 
..hii habari ipo JF tu, sijaiona mahali pengine popote.

..siamini kama act wanaweza kufanya jambo hilo bila waandishi wa habari.
Sasa wewe Jf hauiamini bwashee?

Kamsome Nondo huko twitter atakuwa amepost!
 

..kesi ya karibuni ambayo ninaikumbuka ni TL kumtetea Peter Lijualikali.

..hata alipokuwa bungeni, TL alikuwa ni msaada mkubwa ktk kurekebisha makosa ya serikali ktk miswada waliyokuwa wakiwasilisha.

..ukitaka kujua umahiri wa TL ktk sheria waulize wanasheria waliofanya naye kazi wakati wa bunge maalum la katiba.
 
Kama unakuwa mwanasheria halafu unashindwa kujaza form basi wewe ni lofa tu!
Mbona wapo wengi tu,jaribu kutembelea mahakama utaona hakimu au jaji akiwakisoa hata namna ya kuomba bail,au kukosea vifungu katika viapo n.k
 
Kama unakuwa mwanasheria halafu unashindwa kujaza form basi wewe ni lofa tu!

..wakati mwingine wenye mamlaka huamua tu kwamba umekosea kujaza fomu hata kama hujakosea.

..kuna mambo mengi sana ya ajabu na dhuluma yanafanywa na serikali hii dhidi ya wafuasi wa vyama vya upinzani.

..kwa mfano, ktk uchaguzi wa serikali za mitaa, msimamizi wa uchaguzi ktk jimbo la Kigoma Kusini aliamua kuengue wagombea wote[61] wa ACT-wazalendo kwa madai kwamba wote siyo raia wa Tanzania.

..maamuzi mengine yanafanyika kwasababu baadhi ya waTz wako juu ya sheria.
 
Mbona wapo wengi tu,jaribu kutembelea mahakama utaona hakimu au jaji akiwakisoa hata namna ya kuomba bail,au kukosea vifungu katika viapo n.k
Hilo ni suala jingine unalozungumzia na ni technical!Hili la kujaza form hadi darasa la saba anaweza kwa ufasaha kabisa sembuse mwanasheria ambaye yeye ni area of exoperities!Come on bhana!!!!Kama ni makosa ya kibinadamu,mbona hamjahoji kwanini JPM hajaenda kuhakiki?Kama ni uzoefu,basi hata Lissu ni mzoefu na fomu hizo kwani amekuwa mwanasheria wa CDM kwa miaka mingi na hizo form zimekuwa zikipita kwake wakati wagombea wengine wanagombea urais kupitia CDM!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…