Tetesi: Membe awakatalia Kardinali Pengo na Askofu Malasusa kumsamehe Musiba

Tetesi: Membe awakatalia Kardinali Pengo na Askofu Malasusa kumsamehe Musiba

Wakati dalali wa Mahakama kampuni ya Yono (vijana wa kazi) ikihesabu siku zilizobaki katika 14 (siku za kazi) alizolewa mtukanaji Cyprian Majura Musiba kumlipa fidia Kachero Bernard Membe jumla ya shilingi 9.2 Bilioni, Bwana Musiba amewaangukia viongozi wa dini Askofu Alex Malasusa (KKKT Diyosisi ya Pwani) na Kardinali Porlycarp Pengo kumwombea msamaha kwa Membe asipige mnada mali zake.

Taarifa kutoka ndani ya familia ya Membe nyumbani kwake Mikocheni zinaeleza kwamba Jumatatu ya tarehe 24/4/2023 majira ya saa 10 alasiri mjumbe kutoka kwa Pengo alifika kwa Membe kumpa ujumbe wa Pengo kumsihi amsamehe Musiba.

"Alikuja hapa padre wa moja ya makanisa yetu kuleta ujumbe huo lakini naona Mzee alimkatalia na kumwambia 'namheshimu sana baba Askofu Pengo lakini kwenye hili anisamehe yeye (Pengo) huyu kijana lazima alipe gharama ya matusi yake' " anasema mwanafamilia aliyetajwa kwa jina la Colleta na kuongeza:

"Lakini jioni yake ya saa moja Askofu Malasusa naye alimpigia simu Mzee kuongelea suala hilo hilo lakini naye Mzee alimpa majibu yale yale aliyompa mjumbe wa Pengo." Hata hivyo kwa maelezo ya Colleta ni kwamba si tu ni msimamo wa Mwanadiplomasia huyo Bali ni msimamo pia wa familia.

Hii inakuja baada ya jitihada za Askofu Mwamakula pia kugonga mwamba baada ya kumwandikia barua Membe ya msamaha kwa Musiba.

Wakati hayo yakijiri hapa Mikocheni, tayari kampuni ya Yono imeshatua jijini Dodoma itakapoanzia kazi ya mnada kwa kuanza na apartments za Musiba zilizoko Ihumwa, nyumba yake ya Chamwino, guest house yake ya Msalato na shamba la hekari 10 njia ya Singida.

Baada ya hapo Yono atatimba apartment ya Kigamboni, shamba la hekari 5 Bagamoyo kabla ya kugeukia mitambo yake ya uchapaji iliyoko jengo la Exim ghorofa ya 8 jirani na Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es salaam.

Ikumbukwe kwamba huko nyuma Musiba alichapa magazeti yake kampuni ya Malindi Printing huko Mbweni ambayo ni mali ya TISS. Jambo hili lilileta ukakasi wa kisheria kwani sheria ya vyombo vya habari (2016) inamtaka mlalamikaji kumshitaki Mwandishi, mhariri, mchapaji na msambazaji. Kwa mantiki hiyo DG wa TISS angetakiwa kusimama kortini. Ili kuokoa jahazi Musiba "alinunuliwa" mitambo mingine Mpya kutoka Ujerumani na kwa "huruma" mwana TISS Membe aliridhia. Nayo itanadiwa baada ya siku 14 kutamatika pamoja na nyumba na mashamba yake ya kijijini nakadhalika.

My take: Vijana tujifunze kitu katika sakata hili la Musiba na Membe kwamba tuwe na akiba ya maneno. Lakini pia akili ya kupewa changanya na zako. Waliokuwa wakimpa akili karibia wote wamemkimbia tena ndio wamekuwa jirani na Membe. Amtegemeae mwanadamu mwisho huwa kama hivi. Musiba kwishney!
yamemkuta kama ilivyo jina lake musiba,tulimkanya sana hapa enzi ya mwenda zake akatuona tumekosa uzalendo wacha sasa avune upuuzi wake
 
Kama alitegemea kutoboa kupitia hiyo njia Naona atakwama tu huyo musiba hana kitu.

Kufulia uzeeni kubaya sana kunamfanya mtu afanye mambo ya kumshushia hadhi kabisa.

Sasa kweli waziri wa mambo ya nje mstaafu ni mtu wa kungangania kuuza mali za Musiba??

Anajiabisha kuliko hata vile anavyodai kuaibishwa na musiba.
Unajiabisha wewe kwa kushindwa kumchangia mwenzenu ambaye alikuwa mstari wa mbele kuhamasisha watu wauawe.

Hongera sana Membe kwa kuwa na msimamo thabiti wa kutetea utu wa mwanadamu kwa kuwajibisha wale wote wanaoutweza.

Tungekuwa na watu japo 100 kama Membe nchi hii ingekuwa na mabadiliko fulani hata kwenye maadili.
 
Kwa nini haku appeal mpaka case ifike mahama za EAC, yaani yeye angeenda na mwendo wa ku apeal tu!
Sidhani kama hii case ilifika kwenye Mahakama ya Rufaa!
Well I’m just curious [emoji3166]
Alikuwa anakaidi wito wa mahakama kwa makusudi akijua mahakama isingekuwa na cha kumfanya bahati mbaya Uzi ukakatika/JPM akaondoka na kesi ikiwa imeshaamyliwa kuundelea upande mmoja.
 
Membe ni failure anayetapatapa.

Aliwahadaa ACT wazalendo kwamba ataingia dakika ya 89 na kufunga goli alafu akaishia kufanya kampeni za urais kwenye kijiji cha Rondo
Mkuu

Kufunga goli dakika ya 89. Ni kauli ya kijasusi sana kuliko unavodhani!

Unafikiri kufukuzwa kwake ccm ni Bahati mbaya!!!?

Alipaswa abaki ILI mwendazake amshulikie akiwa NDANI kuliko nje!

Kachero akiwa nje ana uhuru wa kutosha wa kufunga goli na kweli alifunga KWA kwenda Dubai na kurudi nchini dakika za mwisho!

Na ACT kutakua chama kikubwa sana tena chenye ushawishi mkubwa baada ya chadema kufa!!!

Zito anaenda kuwa mwenyekiti wa chama mkuu wa upinzani nchini!!!

Ujio wa Membe ACT haukua wa Bahati mbaya!!
 
Yeye adinde tu, Tunachomwombea ni uzima na uhai.

Kwani siku zinaganda??.

Magufulinists ni lazima tutarudi tu Katika Uongozi, ni lazima !!.
Magufulinists ni watu gani? Ni hao waliokuwa wanahamasisha watu kuuawa kama alivyokuwa anafanya Musiba, au ni wake waliokuwa wanaua, wanateka, kupoteza watu, na kuwabambikia watu kesi?

Kama ni hao, usahau kabisa. Uovu mkubwa hutokea once and forever. Baada ya pale watu huwa wamepata funzo, na hujenga tabia ya kutoruhusu kabisa uovu mkubwa usitokee tena.

Ni miaka mingapi imepita, umewahi kusikia Ujerumani ina kiongozi kama Hitler?

Ni miaka mingapi imepita umewahi kusikia Italy ina kiongozi kama Benito Mussolin?

Ni miaka mingapi imepita umewahi kusikia Chile wana kiongozi kama Augusto Pinochet.

Ni miaka mingapi imepita umewahi kusikia South Afrika ina kiongozi kama P. W. Botha?

Mataifa yote ambayo huwa yamepitia utawala wa kidikteta uliofanya uovu mwingi, baada ya pale huwa yanabadili mifumo ambayo hujenga chuki kubwa dhidi ya udikteta, na ndiyo maana huwa madikteta hawarudi tena na kupata nafasi ya aina yoyote.
 
Namwelewa sana Membe. Musiba ni jeuri kweli kweli. Binafsi sijawahi kumsikia Musiba akiomba msamaha hadharani wala kujuta hadharani kwa yale mambo yote ya hovyo aliyoyafanya badala yake anasubiri maaskofu wamuombee msamaha hadharani. Membe ni binadamu tena muungwana sana na naamini iwapo Musiba angeenda kwenye vyombo vyote vikubwa vya habari akakiri yote yaliyotokea na kumuomba msamaha Membe na wengineo aliowakosea na kuwaomba watanzania wote msamaha lazima Membe angefuta kesi na wala tusingefika huku kwenye hukumu.

Lakini yote kwa yote serikali iliombwa muda mrefu iunde tume ya maridhiano ya kitaifa ili kuondoa hasira zinazowaka ndani kwa ndani kwa watu waliumizwa na utawala uliopita lakini serikali haijalifanyia kazi suala hili. Kwa hiyo tutegemee tu huko mbele ya safari kuona kesi kama hizi za Musiba nyingi tu.

Kwa upande mwingine lazima watu wa hovyo hovyo lazima wajifunze katika kupitia hali ngumu na ikiwezekana nao wapitishwe katika njia zile zile au zinazofanana na walizopitisha wenzao ili wangine waliobaki wajifunze. Hili la Musiba na Sabaya liwafunze wale wote wanaofanya mambo ya hovyo kwa aidha kutumwa au kujipendekeza wajue kuwa itakapofika kusimama mahakaamani watasimama wao wenyewe kama watu wabinafsi na si vingenevyo.
 
Nchi imeoza hii!! TISS inachapa magazeti ya kuchafua raia wa nchi. Yaani taasisi inayotakiwa kuhakikisha nchi iko salama na ina utulivu ndio inashiriki kwenye kampeni za kuwavuruga wananchi?
Mkuu

Kitengo cha propaganda. Hicho mkuu!!

Kina kazi maalum !!

NADHANI. TISS watatafuta namna ya kumsaidia!kuna picha itachezwa tu halafu itamuokoa musiba kwenye hio ishu!!!

Kama alitumika bas ni KWA manufaa ya umma yasiyooonekana tena yenye faida KWA Membe!! Yeye mwenyewe tena kwa kazi yake ya kikachero!!!
 
kiongozi asiyesamehe hafai kuongoza watu membe huyu huyu je angekuwa raisi ingekuwaje ! kipimo cha akili ni karma

Kumsamaehe mtu mwovu anayehamasisha watu kuuawa ni ushetani mkubwa. Ni sawa leo umwambia Samia awatoe wafungwa wote wa makosa ya mauaji, halafu ndiyo useme.ni kiongozi mzuri.

Wauaji na wanaohamasisha mauaji ni mashetani wanaotakiwa kupigwa vita na kuadhibiwa vikali kwa nia ya kuwalinda binadamu wengine.

Ni kwa vile tu jeshi leta la Polisi nalo ni dhaifu sana. Musiba alistahili kukamatwa na kufunguliwa makosa ya jinai kwa kuhamasisha watu kuuawa.
 
Kama alitegemea kutoboa kupitia hiyo njia Naona atakwama tu huyo musiba hana kitu.

Kufulia uzeeni kubaya sana kunamfanya mtu afanye mambo ya kumshushia hadhi kabisa.

Sasa kweli waziri wa mambo ya nje mstaafu ni mtu wa kungangania kuuza mali za Musiba??

Anajiabisha kuliko hata vile anavyodai kuaibishwa na musiba.
Acha hizo, Musiba si WA kuonewa huruma!! Mwanaharakati uchwara
 
Duh..., kama mwandishi huyu, ambaye mimi nilimuona kama ni mwandishi kilaza, kanjanja na kichaa kabisa Kichaa mmoja, anaweweseka sana juu ya Zitto, kamtungia uongo, umebuma, Zitto tuko nae hapa Dodoma, anamiliki mali kama hizo!, then huyu jamaa ni kichwa sana!. Ametuheshimisha sana, hivyo najiunga na Maaskofu, Membe amsamehe tuu!.

Kitendo cha Membe kutowatii maaskofu kitamgharimu sana!. Kuna kiongozi fulani aliwahi kuwadharau maaskofu, najua ni nini kilikuja kumtokea, hivyo sitaki Membe yamkute ya kumkuta!. Amsamehe tuu Musiba!.

P.
Ameshakataa huyo maaskofu, labda Zumaridi akienda atabadili maamuzi.
 
Back
Top Bottom