Uchaguzi 2020 Membe: Kamati Kuu haina mamlaka ya kunifukuza Uanachama wa CCM bali Halmashauri Kuu ya Taifa. Asema kati ya Juni na Oktoba chochote kinaweza tokea

Uchaguzi 2020 Membe: Kamati Kuu haina mamlaka ya kunifukuza Uanachama wa CCM bali Halmashauri Kuu ya Taifa. Asema kati ya Juni na Oktoba chochote kinaweza tokea

Kwanini unasema hivyo?

Jamaa siyo wa kumpuuza kihivyo.

Chama atakachoshiriki kitapata faida kuliko kumkosa.

Kwanza atakuja na wanachama wapya wengi

Pili itapelekea nguvu ktk kuchagua wabunge na madiwani wa chama husika cha upinzani.

N.k

Chama chochote atakachogombea kitapeleka value addition nakuambia.

Tafakari
Ni faida zaidi kwa act kuliko chadema, chadema hawawezi mpokea moja kwa moja kwa sababu hawataki tudia kisa la 2015. Act hawana cha kupoteza maana mpaka sasa hawana kitu zaidi ya zitto.
chadema wakimchukua ni goli la kujifunga kwao. Wataisapoti act na mgombea wao ila hawatchukua wao kwa tiketi yao agombee.
 
Nimeamini hivi vyama Ni magenge ya watu, kumbe membe kaonewa naye, kamati kuu haina mamlaka ya kumfukuza MTU uwanachama.sasa kina silinde wanakokimbilia ndo kupo vivo duh
 
Mkuu hongereni kwa hayo maono yenu. Hivi kweli tatizo la sasa ni aina ya mgombea wa upinzani au kutokuwepo kwa tume huru ya uchaguzi?

Nisiwe mnafiki, kumchukua Membe kuwa mgombea wa upinzani, ni kosa kubwa kuliko lile kosa walilofanya wapinzani la kumchukua Lowassa 2015. Ni wapi tunakwama, mbona tatizo la msingi lipo wazi kuwa tume kutokuwa huru ndio tatizo la msingi lilipo?

Bila tume huru ya uchaguzi, ni wendawazimu wapinzani kushiriki huo utapeli uitwao uchaguzi.
Kwa act, kwa kumchukua membe wao watapata kitu zaidi ya kupoteza! Kwa sasa hawana kitu. Nothing to lose sio kama chadema wakimchukua membe moja kwa moja kama mgombea wao.

Nami nionavyo ni kama mleta uzi, kuwa lissu ndiye atakuwa mgombea wa chadema ila hatorudi nchini, na kujitoa automatically! Chadema wataisapoti act.

Haina ubishi, membe hawezi gombea kupitia sisiemu ila kauli yake ya chochote chaweza tokea kati ya juni na octoba na alipoongea hapa nilimuangalia mara mbili sura yake iliangalia dawati na kuiinua na kuwa na usitiaz zaidi, niliamini anaenda gombea urais, kwa tiketi ya act...
 
Nimekusoma halafu kama sijakuelewa vizuri, au kama ni hayo maono yenu nadhani hayajakamilika, mmeota ndoto lakini ikaishia njiani, au huko mbele hiyo ndoto imewadanganya/haitekelezeki.

Kama ACT itasimamisha mgombea Urais Zanzibar, something which is very much likely, itawezekana kweli hao ACT wasimamishe tena mgombea Bara wakiwa kwenye coalition na Chadema? kwamba Chadema hawana mtu yeyote wakugombea tofauti na Lissu!, watakuwa hawajiamini, na kwa chama kinachojinasibu kuwa kikuu cha upinzani ku-fall kwa hii simple trap kwangu itanishangaza.

Hivi Membe himself anakubalika kwa kiasi gani kama mwanasiasa nchi hii? anaweza kweli kupewa hiyo nafasi akaitendea haki kwa kiwango kinachohitajika? kwangu Membe ni jina tu lile linatembea, but sioni chochote cha ziada kwake, JK alimbeba wakati ule but now, no more.. he is done.
 
Mkuu mbona msajili kasema muda wa kujiunga ushaisha!!!!!!
Huyu barafuyamoto ni mtu ambae siku zote mimi na yeye huwa tunakinzani kimawazo na kimisimamo hapa JF yeye aikionekana kuwa ni mtu anaeunga mkono CCM na mimi nikiwa ni mtu naeunga mkono upinzani.

Hata hivyo,kwa mshangao mkubwa leo hii mimi na yeye tumewaza kitu kile kile kwa asilimia 100 jambo ambalo linenifanya nijiulize kama hii imetokea tu kwa bahati au vinginevyo ila nimekuja ku-conlude kuwa haya yatakuwa maono na hiki huenda ndio kinaweza kuja kutokea hapo baadae kabla ya Oktoba mwaka huu.

Ni hivi:Baada ya kuisikiliza clip ya Membe,ndani ya muda mfupi tu nikapata wazo kuwa Membe atahamia ACT-Wazalendo na atateuliwa kuwa mgombea na watachofanya CHADEMA ni kutosimamisha mgombe(watacheza mchezo wa kisiasa) alafu waje wamuunge mkono Membe na lengo ni wao kukwepa kurudia kosa kama lile la kumsimamisha Lowassa(hawatataka kuonekana wanachakuwa tena wagombea kutoka CCM hasa kwa ngazi ya uraisi).

Hivyo ndivyo nilivyowaza, ila kwa mshangao mkubwa, nimekuta na huyu member barafuyamoto nae kawaza kama mimi kwa asilimia 100 ingawa mimi nilienda mbali zaidi kwa kuwaza/kuamini watachofanya CHADEMA ni kumsimamisha Lissu alafu baadae Lissu atajitoa kwa kuhofia usalama wake na hatarudi nchini na mchezo huo wa kisiasa utakuwa umekamilika na CHADEMA wataamunga mkono Membe.

Najua yako yanayosemwa kuhusu Lissu kufanyiwa mizengwe kwenye uteuzi ila hizi zote zinaweza kuwa ni siasa tu zenye malengo fulani.

Tusubiri.

Maoni yangu:
Mimi kama mwananchi wa kawaida,nawashauri wapinzani wasirudie kosa la kumsimamisha mgombe yoyote aliekataliwa,kufukuzwa au kujiondoa CCM katika uchaguzi huu, hasa kwa nafasi ya uraisi, kwani wananchi teyari wana majereha katika mioyo yao hivyo kurudia kosa kama hili kupitia chama chochote cha upinzani ni kutonesha vidonda hivi na zaidi ni kukaribisha hatari ya vyama vya upinzani kudharauliwa, kupuuzwa na hata kukataliwa na wapiga kura na madhara mengine ni hali hii kuwakatisha tamaa wananchi wengi na kuwafanya wasijitokeze kwenye kupiga kura.

Hata Nyalandu nawashauri msimpitishe kuwa mgombea kwasababu hizi hizi nilizozitaja.
 
Amesema lkn kuwa hakuna ajuae Mungu kapanga nn juu yake na Magu pia. Oct. mbali tutegemee lolote hapa katikati.
Hawa mambwiga wa Lumumba kila siku nawaambia hawaelewi wanajifanya wao ni miungu watu,wanatukana mamba kabla hawajavuka mto.
 
Wewe umeanza kuchanganikiwa na barafu za moto wako, we unadhani sisi chadema tunaweza kutegemea chama cha hovyo kama Act kukiunga mkono...nakuomba uhamie ccm huko ndo kuna zero brain .
Dah...
Things are Falling apart aisee..
 
Huyu barafuyamoto ni mtu ambae siku zote mimi na yeye huwa tunakinzani kimawazo na kimisimamo hapa JF yeye aikionekana kuwa ni mtu anaeunga mkono CCM na mimi nikiwa ni mtu naeunga mkono upinzani.

Hata hivyo,kwa mshangao mkubwa leo hii mimi na yeye tumewaza kitu kile kile kwa asilimia 100 jambo ambalo linenifanya nijiulize kama hii imetokea tu kwa bahati au vinginevyo ila nimekuja ku-conlude kuwa haya yatakuwa maono na hiki huenda ndio kinaweza kuja kutokea hapo baadae kabla ya Oktoba mwaka huu.

Ni hivi:Baada ya kuisikiliza clip ya Membe,ndani ya muda mfupi tu nikapata wazo kuwa Membe atahamia ACT-Wazalendo na atateuliwa kuwa mgombea na watachofanya CHADEMA ni kutosimamisha mgombe(watacheza mchezo wa kisiasa) alafu waje wamuunge mkono Membe na lengo ni wao kukwepa kurudia kosa kama lile la kumsimamisha Lowassa(hawatataka kuonekana wanachakuwa tena wagombea kutoka CCM hasa kwa ngazi ya uraisi).

Hivyo ndivyo nilivyowaza, ila kwa mshangao mkubwa, nimekuta na huyu member barafuyamoto nae kawaza kama mimi kwa asilimia 100 ingawa mimi nilienda mbali zaidi kwa kuwaza/kuamini watachofanya CHADEMA ni kumsimamisha Lissu alafu baadae Lissu atajitoa kwa kuhofia usalama wake na hatarudi nchini na mchezo huo wa kisiasa utakuwa umekamilika na CHADEMA wataamunga mkono Membe.

Najua yako yanayosemwa kuhusu Lissu kufanyiwa mizengwe kwenye uteuzi ila hizi zote zinaweza kuwa ni siasa tu zenye malengo fulani.

Tusubiri.

Maoni yangu:
Mimi kama mwananchi wa kawaida,nawashauri wapinzani wasirudie kosa la kumsimamisha mgombe yoyote aliekataliwa,kufukuzwa au kujiondoa CCM katika uchaguzi huu, hasa kwa nafasi ya uraisi, kwani wananchi teyari wana majereha katika mioyo yao hivyo kurudia kosa kama hili kupitia chama chochote cha upinzani ni kutonesha vidonda hivi na zaidi ni kukaribisha hatari ya vyama vya upinzani kudharauliwa, kupuuzwa na hata kukataliwa na wapiga kura na madhara mengine ni hali hii kuwakatisha tamaa wananchi wengi na kuwafanya wasijitokeze kwenye kupiga kura.

Hata Nyalandu nawashauri msimpitishe kuwa mgombea kwasababu hizi hizi nilizozitaja.
Membe asizuiwe kuchukua fomu ya kugombea urais kupitia CCM, ili Magufuli ajipime kupitia kwake namna anavyokubalika ndani ya chama chake na pia kuonesha demokrasia kama kweli ipo huko.
 
MSIMAMO WA MEMBE KUHUSU KUGOMBEA URAIS

Aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Bernard Membe amesema kuwa atagombea nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020 endapo tu Chama cha Mapinduzi kitabatilisha adhabu aliyopewa.

Amesema adhabu ya kufukuzwa uanachama ilitolewa kimakosa kwa sababu uamuzi ulitakiwa kufanywa na Halmashauri Kuu lakini badala yake ulifanywa na Kamati Kuu. "Kwa kuwa chombo kinachotoa adhabu ni Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), na kwa kuwa Kamati ya Maadili tayari imeandaa taarifa yake na wameipitisha kwenye Kamati Kuu na kwa bahati mbaya kamati kuu ikatamka kwamba Membe tumemfukuza. Mpaka hapo Halmashauri Kuu [ya CCM] iatakaposema mheshimiwa Membe hana hatia, wakitamka hivyo leo [jana] au wakitamka hivyo kesho [leo] tutajaza kugombea Urais jumatatu asubuhi," amesema Membe.

Chanzo: swahilitimes

Kazi ipo mwaka huu hakyanani!
 
Nakubaliana na wewe kwa asilimia 100 kuwa bila tume huru hakuna uchaguzi unaostahili kuitwa uchaguzi ila tatizo ni kukosekana kwa msimamo wa pamoja wa wapinzani kuhusu jambo hili hivyo najua watashiriki tu mradi kunadi vyama vyao na kuonyesha nguvu ya watu walio nyuma yao kupitia mikutano ya kampeni lakini sio kutangazwa washindi pale watakaposhinda unless wana mipango ya siri ambao labda sisi hatuijui.

Mkuu salary slip hakuna mipango yoyote bali ni kupoteza kujiamini tu. Hapo ccm walipo wanaomba usiku na mchana wapinzani wa kweli wasisusie uchaguzi. Maana wanajua hilo litawaweka kwenye mazingira magumu, kwani wapiga kura watakuwa wachache mno, pia taswira yao itachafuka kimataifa, halafu watakosa uhalali wa wananchi. Lakini wanajua wapinzani wakishiriki, watahalalisha hicho walichopanga kufanya kwa maslahi ya chama chao. Wapinzani wadai tume huru ya uchaguzi, hakuna kisingizio cha muda, kwani madai halali hayana muda, hasa kwa watu wenye nia ovu.

NB: Salary slip ww ni nguli hapa jukwaani, inakuwaje unaandika bila kuweka koma, wala nukta! Unakwama wapi sheikh wangu?
 
Ni faida zaidi kwa act kuliko chadema, chadema hawawezi mpokea moja kwa moja kwa sababu hawataki tudia kisa la 2015. Act hawana cha kupoteza maana mpaka sasa hawana kitu zaidi ya zitto.
chadema wakimchukua ni goli la kujifunga kwao. Wataisapoti act na mgombea wao ila hawatchukua wao kwa tiketi yao agombee.


Pia wanaweza kufikiria kuungana tena kufanya UKAWA nyingine
 
Wewe jamaa unaonekana ni mkabila..umeingza usukuma hapa..ninyi ndy mnamharibia JPM mpaka ndani ya Chama wanaona mnapendelewa..kama ulisoma shule vizuri huwezi kuandika hoja za kibaguzi na kiharamia humu..onyesha elimu aliyokpa mzazi wako thamani yake..onyesha kama mtu mwenye wazazi waliokpika kwa gharama na kujinyima kwingi...Onyesha elimu na hekima sio upupuu unao andika humu!!
Mkuu hawa jamaa ni wazi kuwa wameishiwa hoja nguvu na karata yao ya mwisho iko kwenye UPORAJI na siyo kwingine.
 
Membe asizuiwe kuchukua fomu ya kugombea urais kupitia CCM, ili Magufuli ajipime kupitia kwake namna anavyokubalika ndani ya chama chake na pia kuonesha demokrasia kama kweli ipo huko.
He has never been a threat! Hata akifanya hivyo poa tu.
 
Back
Top Bottom