GreenStone
Senior Member
- Apr 27, 2015
- 159
- 87
Ok
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mr. Mangi Kuna mtu aliyeongea maswala ya kulipa au kutokulipa kwenye huu uzi??
Kwanza umeisoma mada ukaielewa au umepost tu??
Kwanini una muita mwenzako tapeli? Amekutapeli nini?
Tusipende kujadili mtu jadili idea au mawazo!
Wanao jadili wenzao ni small minded people.
Mkuu embu twende hoja kwa hoja...tuweke mihemko pembeni!
Ni wapi bwana mdogo alishawahi kusema ana software ambayo inakupa faida hata kama umelala? Je unaweza thibitisha beyond reasonable daught kwamba jamaa alisema hiki kitu?
Katika hoja yako ndefu nimefurahishwa na hii line!
Je kama ontario ni "proven scammer" kwanini usimshitaki ili achukuliwe hatua kama kweli unaamini ulichoandika ni "proven" au ni kitu cha uhakika?
Kama huwezi kumshitaki au kuthibithisha ulichoandika, nikisema una chuki na wivu nitakua nimekosea?
Wazungu wamefanya yote hayo ila wameshindwa hiki, sasa kwanini wewe au sisi tusifanye hiki walichoshindwa ili tuwazidi?
Maana nikiangalia kwa umakini ulichoandika hapa ni kama unasema "they did nothing"! tunarudi kule kule kwenye chuki na ubinafsi na wivu uliotujaa watanzania!
Naona unazunguka sana,
Hoja yangu ya msingi ni hii...
Tafadhali naomba majibu ya hoja yangu!
Mi naweza kusema hii chuki imeanzia juu mpaka chini, yaani kuanzia kwa rais anavyochukia waliofanikiwa mpaka kwa members humu JF! inasikitisha sana kwa kweli, badala ya kujadili mada tuko busy kumjadili jamaa mbaya zaidi watu wanamuita tapeli na wakiambiwa wametapeliwa nini hawana majibu!!!
Ni chuki na roho mbaya na wivu!!
Mkuu umeandika vyema sana, na hii ina reflect matatizo tuliyo nayo kama taifa!! its pain!!
Mkuu mimi sio mtu wa matusi, na sifurahishwi kuona mtu anaandika matusi badala ya hoja za msingi!!
Turudi kwenye mada...
Hapo kwenye red;
Kwa hiyo ndugu yangu kwa kusikia maneno ya watu tena unao waita "dumbest people" ndio una muita mwenzako tapeli na mwizi?
Sasa kama ni maneno uliyasikia kutoka kwa "dumbest people" kwanini unasema ni "proven" au kwanini unayaita ni ya uhakika?
Post ya adrenaline ni hii... haya mjibu sasa!
Yes! na badala ya kujifunza kutoka kwao tumebaki kuwaponda utazani sisi tuna hata kiwanda cha baiskeli!!
Kama hoja yako kwamba forex kupigwa marufuku nairaland ni kielelezo cha forex kuwa utapeli , je unajua kwamba kuna nchi facebook, twitter zimepigwa marufuku je kwasababu zimepigwa marufuku ni kielelezo kwamba facebook na twitter ni matapeli?
Sijui kama unaewa, sijui kama unanielewa! hizo facebook na twitter nimekupa mfano tu kwamba kitu kufungiwa marekani haimaanishi tanzania ni haramu au hakiruhusiwi japan au china and vice versa!!
Mkuu unajua maana ya ponzi scheme? kama unajua, je unaweza niambia ina uhusiano upi na forex trading?
Sasa nikasome mara ya ngapi mkuu?
Forex haina uhusiano na ponzi scheme, na niliukuuliza kama unajua maana ya ponzi scheme ukaishia kutoa hoja mfu!
Sasa hebu niambie kwanini unasema forex ni ponzi scheme?
Kama hujaelewa hata nilichoandika basi kuna ukweli kwenye nilichosema (small-minded)!
Hahahaa najipendekeza?
Ukitakata nisiku quote basi na wewe usini quote as simple as that, sawa?