Mtu anakuja kukuambia eti "enzi hizo mpira ulikua mgumu". Hebu tuheshimiane asee!
Kipindi ambacho akina Maradona walichukua ndoo kwa goli lililofungwa kwa mkono ndio mpira ulikua mgumu? Kipindi ambacho hakuna VAR, wala idadi kubwa ya mashindano ndio mpira ulikua mgumu? Acheni porojo.
Huu ndio wakati bora kabisa wa mchezo wa mpira, kwa sababu probability ya kufanya udanganyifu ni ndogo sana. Teknolojia imeweka mambo mengi sawa, yani hata ukizidi nywele tu watu wanajua hiyo ni offside, na hupewi goli.
Huwezi kufunga goli kwa mkono katika zama hizi za V.A.R alafu likahesabika!
Watu wanacheza ligi ina mechi 30, wanapiga sijui Carrabao cup, wanapiga FA cup, wanapiga UEFA na wengine EUROPA. Hapo bado michezo ya kimataifa inawasubiri, na kote huko teknolojia ipo kuhakikisha hakuna udanganyifu. Hakuna kitu utaniambia kuhusu mpira wa zamani nikakuelewa!
Messi is the GOAT. That's what the numbers say. And last time I checked, numbers didn't lie!