Messi Vs Pele

Umejaribu kueleza. Goals 1000 kwenye game nyingine za mchangani. Ndio maana hata Romario naye kafikisha magoli 1000.
Na alisema wazi atacheza mpira mpaka afikishe 1000 goals.

Akaenda kucheza na ile mipira ya ufukweni nadhani timu inakuwa na wachezaji 6 kama sio wa5.
Kwanza kwa nini huu mjadala mmeutoa kwa cr na kuuhamishia kwa pele?
 
Pele ana magoli ya mchongo [emoji23]
 
From the day Piers Morgan made an interview with him (Ronaldo) his life haven’t been the same. I’m mad at Piers Morgan because sometimes you need to think before asking questions. And Ronaldo is that kind of person who can’t hold certain things in his heart. Media destroyed a beautiful game and people reputations. Piers Morgan you have to learn more about moral
 

Wewe unamchukia messi ndio maana unang'ang'ana na babu yako pele mtu ambae era yake hapakua na sheria ngumu kama ilivyo sasa.. Diego Armando alishamfunika huyo babu, kwa messi ndio ataweza!
 

Yani mtu anaanzisha thread ya pele na King Messi kweli! Ni kama ufananishe ukubwa wa bahari na bwawa lipi kubwa while inaeleweka kabisa ni bahari 😃
😃😃
 
Hahaha heri tumbo lililokuzaa msemakweli

Mimi nilipotazama kakomaa eti messi kacheza zama mpira ukiwa rahisi nikaona huyu ni team CR tu [emoji23][emoji23]
Nnavyojua kipindi cha babu hapakua na sheria kali kama ilivyo sasa, na hata kipindi cha diego sidhani kama mpira ulikua rahisi...hawa mashabiki wa ronaldo wanatabu..wametoka kwa ronaldo wamehamia kwa pele..ni kwamba wameishiwa hoja.. Messi ndie mchezaji bora kuwahi kutokea akifuatiwa na mwamba Diego Armando Maradona..
 
Haters wa Messi mmeamua kujifariji kivingine , ungeweka na data za vikombe recently ,na bado Messi anazidi kuvikusanya, mpak aje kustafu watetezi wa legacy za babu mtakuwa mmetera na club zake za mchangani ,ukweli ni kwamba Messi amewapiga gap hao wazee , kizazi kijacho kitakuja kudhibitisha , kizazi cha sa hv bado mna ego , so sad
 

Wanatia huruma sana.. hivi kweli King Messi wakumlinganisha na babu!
 
Zitaje hizo game za mchangani alicheza na timu gani ili tujue maana mkipewa takwimu mnaishia kuleta porojo zitaje hizo mechi za mchangani alicheza kota mwaka gani hadi mwaka Gani na alifunga magoli mangapi swali lako hukuliza Romario uliuliza Kitu ambacho Pele kafanya kweny soka na Messi kashindwa kufanya Romario anaingiaje hapa
 
Vikombe Ata kina Sergio Ramos wameshindwa mjomba kwanin mkipewa takwimu hamtaki kukubali shida yenu mnalazimisha Messi awe GOAT ila takwimu zinamgomea
 
Toa sababu kwanin
 
Embu tuheshimu nafasi za hawa watu. Pele/Maradona. Kuna sababu ni kwann kabla yao hakuna anayetajwa tajwa kwa kiwango chao.

Messi ni wa kizazi hichi, alinganishwe na wa kizazi hichi ambao tayari ameshawaburuza na kuchukua nafasi yake, kumrudisha kwa babu zake na kutaka wavue nafasi zao wampe yeye ni kujidanganya. Tutajadili mpaka mwisho wa JF ila nafasi ya kina Pele itabaki kuwa ya kipekee.
 
Vikombe Ata kina Sergio Ramos wameshindwa mjomba kwanin mkipewa takwimu hamtaki kukubali shida yenu mnalazimisha Messi awe GOAT ila takwimu zinamgomea
Tunaangalia main key kwenye hvyo vikombe husika, sasa tukihesabu hayo magoli kuna ligi za mchangani watu Wana magoli kibao , kuna makombe na vikombe, makombe aliyobeba Pele ya maana ni world cup tuuu , na hajawahi cheza kwenye ligi shindani ulaya ,Messi kabeba makombe yote shindani tena akiwa mchezaji tegemewa , narudia tena makombe yoteeee...na bado anaendelea kuyanyanyua mana hajastaaaf , usipomkubali kama mchezaji Bora kuwahi kutokea kuliko wote basi wajukuu zako watamkubali .....
Tuzo alizobeba Messi , Pele hata nusu hafiki , Pele Hana hata Balon d'Or Moja , Messi anazo Saba na anaenda beba ya nane ..... Tuache unafiki na data za mchongo .... Baada ya hyo ndoo kupelekwa kabatini , mjadala ulifungwa rasmi Nani ni Real 🐐

 
Uyo Diego maradona na Messi wanamzidi kitu Gani Pele viseme apa tusikie
Wote wana world cup, wawili wamecheza ulaya na pia Messi ana Ballon d'Or na mazagazaga.. vile vile wamechezea timu kubwa na haswaa wakiwa ndio tegemezi na kuzisaidia timu hizo kunyanyua ubingwa...

Mbali na world cup, hebu niambie huyo babu alichowazidi Messi na Maradona!
 
Kwa kukuonyesha kwamba mpira sasa hivi umekuwa rahisi kwa Striker ngoja uone jinsi freak of Nature Striker Erling Braut Haaland atakavyopangua rekodi za magoli...., sio kwamba ni mchovu jamaa ana nguvu na ana pace (mbio ) na ukizingatia kiatu hapigwi kutokana na sheria za sasa wewe ngoja uone mambo yatakavyokuwa..., Unless Sheria zibadilike tena au kitokee kitu cha kusitisha career yake..., ila bado ukiangalia ratio nadhani atapata ratio kubwa ambayo itakuwa shida kuivunja....

Tatizo wewe ni mpenzi kwahio macho yako yanatingwa unashindwa kufanya uchambuzi...., ungefanya uchambuzi kidogo tu ungegundua hata huko spain alikocheza kwenye his peak ingawa ana mabao mengi ila ratio yake sio kubwa (yaani sio clinical) goals per match ingawa sio mbaya ila kuna zaidi yake (na hapo tunachambua like for like)

Tukija world cup conversion rate yake kutokana ni kwamba ni kati ya watu waliocheza mechi nyingi kwenye Kombe la dunia lakini ana Kombe moja...., tofauti na Pele ambaye amecheza world cup nne, mbili kati ya hizo moja alipigwa kiatu mpaka mechi ya pili akashindwa kuendelea na kuamua kujiuzulu, nyingine alipigwa kiatu mechi ya pili akatoka wakati ya kwanza alishatupia goli...., Ya kwanza kucheza mechi za mwanzo hakucheza mpaka alivyoingia na kufanya mambo akaendelea mpaka kuchukua kombe 1958, na 1970 akafanya yake pia (baada ya introduction ya red and yellow cards) World Cup Nne - Makombe 3 that's what I call excellent conversion rate....

Unaona hapo juu ni tofauti kati yangu mimi na wewe, mimi nachambua kulingana na happenstances wewe unachambua kutokana na mapenzi yako kwa mtu.... hufanyi comparable analysis....
 
Wote wana world cup,
Messi ana World Cup Moja; na hapo ni baada ya kuingia Fainali mara mbili na ku-bottle it, Messi amecheza mechi nyingi World Cup kuliko wote hao Yaani ni mmoja kati ya wanaoongoza kwa kucheza hili Kombe - Na ameshinda Kombe moja courtesy of heroics za kipa na hapo kwa kukosa penalty kadhaa na timu yake mabao kurudishwa huku wakiwa wanaongeza....

Pele kacheza world cup nne kati ya hizo mbili alipigwa kiatu moja yeye na timu yake hata group la makundi hawakuvuka nyingine baada ya kufunga mechi ya kwanza ya pili kiatu hadi hakuendelea..., na ana World Cup Tatu (I repeat Tatu from Four)
wawili wamecheza ulaya na pia wana Ballon d'Or na mazagazaga..
Tafuta History moja Ulaya walikuja Politics zikakataa asiuzwe pia kipindi hicho cultural differences unless angecheza portugal na language barrier ingekuwa ngumu kwa kijana wa miaka 17 na kipindi hicho wachezaji walikuwa wanacheza makwao hio ndio ilikuwa formula sio kipindi hiki cha mercenaries...., by the way sababu Ballon d'Or ni ya ulaya pekee watoa TUZO walikuja kufanya tena uchambuzi kama lingetoka kwa non European Clubs basi Pele angeshinda same number as Messi na hapo ni kwa yeye kuwa na a shorter career
vile vile wamechezea timu kubwa na haswaa wakiwa ndio tegemezi na kuzisaidia timu hizo kunyanyua ubingwa...

Mbali na world cup, hebu niambie huyo babu alichowazidi Messi na Maradona!
Hivi unajua kitu kilikuwa kinaitwa Intercontinental Cup Hili lilikuwa Kombe la Timu za Ulaya na South America, katafute Pele na Santos walishindwa mara ngapi na hapo ni against na kina AC Milan alafu rudi tuendelee na mjadala ulioshiba (yaani ukiwa na Data zinazoeleweka)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…