Mfahanu Williams Shakespeare na utata wa kazi zake

Mfahanu Williams Shakespeare na utata wa kazi zake

elmagnifico

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2011
Posts
8,261
Reaction score
9,733
Kama ambavyo ukitaja majina ya wanasayansi wakubwa huwezi kukosa kumtaja Newton, hivyo hivyo huwezi kutaja waandishi wa vitabu vya lugha ya Kingereza bila kumtaja William Shakespear.

Huyu ni mwandishi wa michezo ya kuigiza ambaye anashika namba moja katika waandishi wa Kingereza kutokana na uwezo mkubwa aliyokuwa nao katika kazi zake.
Uwezo huo umefanya kuwepo kwa mabishani baina ya wanazuoni baadhi wakipinga ya kwamba Shakespear hakuwa na uwezo wala elimu ya kuandika hizo kazi zinazodaiwa kuwa aliandika yeye.

Ukisoma vitabu vya shakespear kama Julius ceaser, Romeo and Julieth, The merchant of Venice, Hamlet, Macbeth, Othello, The tempest, King Lear, Twelfth Night na kazi zake nyingine nyingi, utagundua huyu mwandishi alikuwa amebobea katika sheria, biasha, saikolojia, utwala, elimu ya tiba na mfumo wa mwili, elimu ya jeshi, lugha ya Kingereza, uchumi, siasa, ametembea sana sehemu mbalimbali duniani na nyanja nyingine.
Jambo hili huleta utata kwakuwa Shakespear hakuwa amesoma sana alikuwa na elimu ya kawaida na kazi yake ikiwa ufundi seremala.

Uwezo huo ndiyo unaowafanya wanazuoni wengi kuhisi ya kwamba siyo yeye aliyeandika kazi hizo bali kuna watu kadhaa ambao walikuwa katika utawala ndiyo waliandika hizo kazi kwa kutumia jina la Shakespear ili wasijulikane.

Katika kazi zake Shakespear alitumia maneno ya Kingereza 31,534 ambapo 14,376 aliyatumia mara moja tu na maneno 846 aliyatumia kwa kuyarudia zaidi ya mara 100.
Inakisiwa Shakespear alikuwa anajua maneno ya Kingereza yapatayo 66,534 wakati mtumiaji wa kawaida wa kingereza anajua kati ya maneno 10,000-20,000.

Na zaidi ni kwamba alitengeneza maneno mapya 1,653 ambayo yanatumika kwenye lugha ya Kingereza.

VITU AMBAVYO WANAZUONI WANAKUBARIANA KUHUSU SHAKESPEAR
William Shakespear alizaliwa Stratfor-upon-Avon, akahamia London alipoanza kujihusisha na kazi ya uigizaji kabla ya kurudi Stratford na kuishi hapo mpaka mwaka 1616 umauti ulipomchukua.

Lakini kupata kumbukumbuku za maisha yake imekuwa vigumu tu ni habari chache zenye ushahidi kama ndoa yake na Anne Hathaway, na vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wao watatu.

Kutokana na kukosekana kwa nakala zozote za maana inayomhusu kunaleta maswali mengi na watu kujiuliza inawezekanaje mtu aliyeonekana kuwa na uelewa mkubwa wa mambo mengi na uwezo mkubwa ambaye kazi alizoandika zinaonekana na ziko wazi ila yeye hakuna nakala zozote za maana zinazomhusu?

Mwandishi T.J Looney yeye anadai ya kwamba anahisi aliyeandika kazi za Shakespear ni Edward de Vere wa Oxford.

Vere alikuwa ana elimu kubwa na alikuwa kasomea sheria, pia alikuwa amesafiri sana na sehemu nyingi alizoaafiri ndizo zinazotajwa kwenye kazi za Shakespear.

Inadaiwa kwamba aliamua kuficha uhalisia wake kwakuwa kazi zake nyingi zilihusisha siasa, jambo ambalo alihisi linaweza kumletea matatizo iwapo atajiweka wazi kama mwandishi.

Lakini hakuba ushahidi wowote ambao unaweza kumuunga Vere na kazi za Shakespear hivyo basi bado Shakespears mwenyewe anabakinkuwa ndiye mwandishi.

Kwa wale ambao wamebahatika kusoma vitabu vya huyu bwana watakubariana na mimi kwamba, huyu jamaa alikuwa ni mwandishi wa kipekee aliyewahi kutokea.
4fe5fbd9fb37be2bccfc86a2f035831a.jpg
 
Ok nitakitafuta kimoja kati ya vitabu vyake tajwa harafu nitarudi tena hapa kwa mchango zaidi.
 
Inasemekana kua Amelia Bassano ni mwanamke aliye andika kazi zote za Shakespear ila kutokana alikua ni mtu Mweusi Jina lake halikuandikwa..
Alifariki akiwa Masikini.

Ukiwa unajua Kuongea na kusoma English basi ujue Huyu mtu amechangia sana Kukua kwa kingereza (msamiati)..
 
Inasemekana kua Amelia Bassano ni mwanamke aliye andika kazi zote za Shakespear ila kutokana alikua ni mtu Mweusi Jina lake halikuandikwa..
Alifariki akiwa Masikini.

Ukiwa unajua Kuongea na kusoma English basi ujue Huyu mtu amechangia sana Kukua kwa kingereza (msamiati)..

Kalikua kashoga haka kamtu..
Yah pia huyu anatajaa na kuna wengi tu wanatajwa kuwa ndiyo waandishi.
Lakini hakuna ushahidi wa kujitosheleza kuthibitisha hilo.
 
Karibu sana kasome Julius Ceaser, ila jiandae kukutana na Kingereza cha zamani.
Kazi zake full of quotations,
Hivyo lazima niwe na dictionary pembeni kwa lugha hiyo iliyotumika humo?
 
Macbeth alipoletewa taarifa kuwa mkewe kafariki wakati yuko vitani napenda alivyosema
"she should have died after the battle when there would be time to mourn properly; she should have waited for me, seeing that my death is so near; she would have died at sometime, either now or later; she should have died after the battle for now, with her gone, I know I shall not win."

Na Ceaser alivyosema "Cowards die many times before their deaths; The valiant never taste of death but once. Of all the wonders that I yet have heard, It seems to me most strange that men should fear, Seeing that death, a necessary end, Will come when it will come."
 
Na ile issue kua Sophia Stewart Aliandika kitabu mika ya 70s ila kikaibiwa na Warner Brothers (Warner bross Picture) then Kwa kutumia hicho kitabu wakatengeneza muvi ya Terminator 1-4 na Matrix 1-2.
Alikua Black, Alifuatilia hiyo kesi mpaka miaka 2000s ndo akalipwa 2.1 bil $ zinaukweli..?
Yah pia huyu anatajaa na kuna wengi tu wanatajwa kuwa ndiyo waandishi.
Lakini hakuna ushahidi wa kujitosheleza kuthibitisha hilo.
 
Na ile issue kua Sophia Stewart Aliandika kitabu mika ya 70s ila kikaibiwa na Warner Brothers (Warner bross Picture) then Kwa kutumia hicho kitabu wakatengeneza muvi ya Terminator 1-4 na Matrix 1-2.
Alikua Black, Alifuatilia hiyo kesi mpaka miaka 2000s ndo akalipwa 2.1 bil $ zinaukweli..?
Hii sijaskia mkuu itabidi niifuatilie niisome.
Kama aliandika kitabu cha namna hiyo miaka ya 70 basi alikuwa ana akili sana.
Ngoja niitafute niisome.
Halafu Amelia Bassano Lanyer hakuwa mweusi kabisa maana wazaze wake walikuwa na Origin ya Italy, Jews na Morocco.
 
Itafute mkuu Jhuyu alikua kachanganya rangi..
Kama hutajali weka Picha za Amelia..
Hii sijaskia mkuu itabidi niifuatilie niisome.
Kama aliandika kitabu cha namna hiyo miaka ya 70 basi alikuwa ana akili sana.
Ngoja niitafute niisome.
Halafu Amelia Bassano Lanyer hakuwa mweusi kabisa maana wazaze wake walikuwa na Origin ya Italy, Jews na Morocco.
 
Itafute mkuu Jhuyu alikua kachanganya rangi..
Kama hutajali weka Picha za Amelia..
Mkuu nimesoma ila kumbe hakulipwa kwanza aliacha kwenda mahakamani na pia hakuleta ushahidi wa kujitosheleza kwahiyo kesi ikafutwa.
Habari za kwamba alilipwa zilisambazwa tu na watu mtandaoni.
Ila kuhusu kuandika kitabu kinaitwa the eye ni kweli alikiandika na akawatumia fox na warner bros ila wote walikataa story yake na baadae nashangaa kazi zinatoka zikiqa na idea inayofanana kama yake thou story flow siyo yake.
 
Acha kudanganya watu wewe ni mwandish mkubwa kweli lakin si namba moja
Mimi ni mwandishi mkubwa wa nyimbo kali hapa bongo mkuu.
Kwa wewe nitakuandikia kwa milion tatu kwa single moja na ngoma ita hit utapiga show za mchangani mpaka watu wanaichoka umetengeneza milion 50...
 
Nasikia Shakespeare alikuwa swaga.
Hii sijaskia mkuu walijuaje kama ni shoga wakati historia ya maisha yake ni tatizo hadi haijulikani hata mwaka wake halisi kwa 100% alizaliwa lini.
Hata jina lake hilo Shakespeare spelling zake zina utata
 
Mkuu nimesoma ila kumbe hakulipwa kwanza aliacha kwenda mahakamani na pia hakuleta ushahidi wa kujitosheleza kwahiyo kesi ikafutwa.
Habari za kwamba alilipwa zilisambazwa tu na watu mtandaoni.
Ila kuhusu kuandika kitabu kinaitwa the eye ni kweli alikiandika na akawatumia fox na warner bros ila wote walikataa story yake na baadae nashangaa kazi zinatoka zikiqa na idea inayofanana kama yake thou story flow siyo yake.
Duuu Sikujua aiseee, sema ww unatabia ya kuleta vistory nusu nusu ungeandalia hata Topic yake..?
 
Back
Top Bottom