zitto junior
JF-Expert Member
- Oct 7, 2013
- 20,537
- 31,729
- Thread starter
-
- #541
Labda ungeandika kifungu kabisa kurahisisha halafu nikujibu
Naona umeshinda!.Kumbukumbu la torati 3:11
11 (Kwani aliyesalia katika mabaki ya Warefai ni Ogu pekee, mfalme wa Bashani
Biblia hapa inasema ogu ni mrefai aliyesalia sasa naomba unisaidie kama wanefili (warefai) wote walifariki kwenye gharika je mfalme ogu alitokea wapi???
Tuanzia hapo kwanza
Nakubaliana na hitimisho lako 100% ila kuna watu wanakataa kabisa kuwa Mungu hawezi muacha mnefili nyuma kama ilikuwa nia yake kuwaangamiza kwenye gharika ndio maana nikajenga hoja hapo kuwa mbona Mungu aliapa kuwafuta wacanaan wote ila mwisho wa siku aliwaacha wengine hakuwaua na aliwakataza hata waisrael wasiawaue??Kiongozi usijaribu kubishana Na watu!.
Mbona hapo juu nishatoa hitimisho!.
Mpango wa Mungu Huwa Na kusudi maalumu!.
Nimesema hapo juu kuwa Mungu alimwacha OG Na waamor for reasons!...
Hahahahaa!..Nakubaliana na hitimisho lako 100% ila kuna watu wanakataa kabisa kuwa Mungu hawezi muacha mnefili nyuma kama ilikuwa nia yake kuwaangamiza kwenye gharika ndio maana nikajenga hoja hapo kuwa mbona Mungu aliapa kuwafuta wacanaan wote ila mwisho wa siku aliwaacha wengine hakuwaua na aliwakataza hata waisrael wasiawaue??
Kama aliweza kuwaacha hao wacanaan ilihali alishaapa kuwamaliza kivp watu wakatae kuwa Mungu asingeweza kumuacha mfalme ogu??
Nmeshaipost mkuu ila kama kawa JF intelligence wanashikilia nyuzi kwa siku kadhaa ndio wanaiachiaHahahahaa!..
Upo vizuri naona!.
Mjadala umekwisha anzisha mwingine!.
Hawa waliobaki wataleta ubishi wa kitoto!..
Mkuu leta maada ingine
Sahihi jana nimepost Uzi but naona Bado upo pending!..Nmeshaipost mkuu ila kama kawa JF intelligence wanashikilia nyuzi kwa siku kadhaa ndio wanaiachia
Hata wangu utakuta unaachiwa jumatatu huko dah yaani hawa mods mkuu wanaudhi sana na hizi kelele hata hawajali kabisa sijui kwaniniSahihi jana nimepost Uzi but naona Bado upo pending!..
Itabidi ni freeze Uzi wangu ili wako utembee
mkuu ...Kumbukumbu la torati 3:11
11 (Kwani aliyesalia katika mabaki ya Warefai ni Ogu pekee, mfalme wa Bashani
Biblia hapa inasema ogu ni mrefai aliyesalia sasa naomba unisaidie kama wanefili (warefai) wote walifariki kwenye gharika je mfalme ogu alitokea wapi???
Tuanzia hapo kwanza
Kabla ya gharika mkuu..... All in all hata kama ingekuwa baada ya gharika bado swali lingekuja whether og alikuwepo au hakuwepo kabla ya gharika je WANEFILI walirudije baada ya gharika??mkuu ...
aliyesalia katika mabaki ya warefai wapi?
1:Kumbukumbu 2:20 (Nchi hiyo nayo yadhaniwa kuwa ni nchi ya Warefai, hapo kale Warefai walikaa humo; lakini Waamoni huwaita Wazamzumi;
21 nao ni watu wengi, wakubwa, warefu, kama Waanaki; lakini Bwana aliwaangamiza mbele yao; wakawafuata wakakaa badala yao;
au
2:Waliobaki baada ya waamori kuchukua eneo hilo kutoka kwa waamoni.
au
kubaki katika gharika?
Mkuu nimeusoma uzi wote taratiibu nimegundua biblia naisomaga juju muda mwingi tu,nikuulize we kwa uelewa wako mbn mi naona ule mstari katk kitabu cha mwanzo unao sema wana wa mungu walijitwalia mabinti wa binadamu wakazaa nao watoto ambao ndo walikuwa hodari kipindi hicho,sasa tatizo language hapa nilidhani mstari unaofuata unaosema nao wanefili walikuwako siku zile ninavyoelewaga Mimi ni kuwa wanefili walikuwako kabla ya wana wa mungu kujitwalia binti za wanadamu,kingine ni kuwa Nina bible Fulani hivi katika mstari wa wana wa mungu wametajwa kama "wana wa mungu wa kweli" sasa hapa neno wakweli linamuhusu Mungu au "wana" yaani Mungu wa kweli au hao wana wa Mungu ni wana wa kweli wa mungu? Pole nimeandika kwa uelewa wangu tu sijanakili kila neno katk mistari ya biblia.Mkuu hii ni biblia mbona ndio nmeongelea kwenye hii post na hata mfalme Ogu pia biblia inamtaja so hatupo mbali sana na vitabu vya dini
Labda udadavue kipi kimekuchanganya ili wajuvi watiririke
Waamori ni uzao wa nimrodi unafikiri nimrodi alikuwa nani ni yale yale majitu soma mwanzo hakunahaja ya kukimbia mbele mwazo 10:8-20Kiongozi usijaribu kubishana Na watu!.
Mbona hapo juu nishatoa hitimisho!.
Mpango wa Mungu Huwa Na kusudi maalumu!.
Nimesema hapo juu kuwa Mungu alimwacha OG Na waamor for reasons!...
Mkuu ambacho nafkiri unaruka ni kwamba sisi hatubishi kuwa Og hakuwepo kabla ya gharika ila tusaidie wwe je wanefili walirudije baada ya gharika??? Maana Mungu alitaka kuwaangamiza wanadamu wote kasoro Nuhu ambaye hakuwa na damu ya kinefili sasa basi kama mnakataa OGU ndio alivusha damu hiyo je nani basi alivusha damu ya wanefili hadi isipotee kwenye gharikaWaamori ni uzao wa nimrodi unafikiri nimrodi alikuwa nani ni yale yale majitu soma mwanzo hakunahaja ya kukimbia mbele mwazo 10:8-20
Je nimrodi si alizaliwa na kushi mwana wa hamu mzao wa nuhu je nuhu hakuwa mabaki ya gharika au nini tena
Mkuu Nuhu alikuwa uzao wa SETH yaani mwana wa Mungu na kitabu cha jasher ambacho kinatambuliwa na waandishi wa biblia yaani Nabii musa.... Kinasema mabinti wa methuselah ndio waliolewa na wana wa Nuhu je hiyo damu ya UNEFILI itoke wapi wakati ilikuja baada ya WANA WA MUNGU kuzaa na WANA ADAMU whatever au SETH kuzaa na CAINNaongeza hivyo wanefili/warefai hawakujishikiza bali walizaliwa tena kwa nimrodi maana hawakuwa watu wa asili bali walitokana na kuingiliana kwa malaika wa shetani(wana WA Mungu) kwa maana hiyo Hoja yako pamoja na vifungu vyote hukuchimba hayo makabila yanayoelezwa hapo jamaa walikuwepo kutoka kwenye uzao wa nimrodi hakuna aliyejishikiza popote
Yaaani
Mwanzo waliosalia ni 8 tu na katika hao warefai walizaliwa
Unaarudi tu mama mno unaijua sifa ya mwamori utaelewa mnefili katoka WapiMkuu Nuhu alikuwa uzao wa SETH yaani mwana wa Mungu na kitabu cha jasher ambacho kinatambuliwa na waandishi wa biblia yaani Nabii musa.... Kinasema mabinti wa methuselah ndio waliolewa na wana wa Nuhu je hiyo damu ya UNEFILI itoke wapi wakati ilikuja baada ya WANA WA MUNGU kuzaa na WANA ADAMU whatever au SETH kuzaa na CAIN
Sioni mahala damu ya cain ilipenya kuendana na official biblical records...... Je wametoka wapi wanefili hao
Mwanzo 6Mkuu nimeusoma uzi wote taratiibu nimegundua biblia naisomaga juju muda mwingi tu,nikuulize we kwa uelewa wako mbn mi naona ule mstari katk kitabu cha mwanzo unao sema wana wa mungu walijitwalia mabinti wa binadamu wakazaa nao watoto ambao ndo walikuwa hodari kipindi hicho,sasa tatizo language hapa nilidhani mstari unaofuata unaosema nao wanefili walikuwako siku zile ninavyoelewaga Mimi ni kuwa wanefili walikuwako kabla ya wana wa mungu kujitwalia binti za wanadamu,kingine ni kuwa Nina bible Fulani hivi katika mstari wa wana wa mungu wametajwa kama "wana wa mungu wa kweli" sasa hapa neno wakweli linamuhusu Mungu au "wana" yaani Mungu wa kweli au hao wana wa Mungu ni wana wa kweli wa mungu? Pole nimeandika kwa uelewa wangu tu sijanakili kila neno katk mistari ya biblia.
Mkuu swali ni hili naona hatuelewaniUnaarudi tu mama mno unaijua sifa ya mwamori utaelewa mnefili katoka Wapi
Aisee umenisaidia kuanza kusoma biblianapata mawazo kadhaa...
1:ni vizuri tujue kusudi la Mungu kumuacha makusudi wakati Lengo lilikuwa ni Kuangamiza dunia yote kwa Maji. Waliopona walipata neema kwa Mungu na Mungu akawaweka wazi. Ingekuwa kuna Mwovu mwingine anapata rehema tungefahamishwa. Na kujua kama hakuwepo, mara baada ya gharika uendelezo wa vizazi haumuonyeshi wala uzao wake.
2:Rahabu alipata rehema, alafu ile adhabu ilikuwa ni regional sio grobal hata ile ya wakaanani. Lengo na hili la nuhu ni tofauti. Mwanzo Mungu anataka kufuta wanadamu wote, hapo case nyingine anataka kufuta baadhi ya watu waovu katika eneo flani tu, huku maeneo mengine ya dunia uovu unaendelea kama kawaida, hivyo muovu mmoja au wachache kupata rehema, au wajumbe wa Mungu kukengeuka na kitotimiza agizo walilopewa kukomesha regional uovu ni tofauti na sidhani kama ni sawa kutumia mifano hiyo.
3: Rahabu ulikuwa mpango wa Mungu. Na kupitia rahabu na Malaya wengine kama Tamari Yesu alizaliwa. na kuna typology nyingi tunapata kwa rahabu na wokovu wa mwanadamu, pamoja na ile kamba nyekundu iliyowaokoa wanadamu. Assumption Mungu aruhusu hybrid ya uovu, ambayo ndiyo ilikuwa lengo lake kuiangamiza hicho kizazi ambacho wewe unataka kiokolewe.
4:Watu sabini kuingia kwenye safina hiyo assumption ni sahihi kwa vitabu na maarifa nje ya bibilia. lkn hiyo hoja tukiijenga kwenye bibilia inaleta ukakasi mwingi.
*Mwanzo 7:7 wanaoingia wanatajwa. Nuhu, wanawe, mke wa nuhu na wake za wanawe. Mungu anawafahamu wana wa wana na huko nyuma kwenye geneology wametajwa lkn hapa hawakutajwa, na imerudiwa zaidi ya mara moja bila kutajwa, sidhani kama kunausahaulifu ila yawezekana ndivyo ilivykuwa.
*Mwanzo 7:13 Wanatajwa hado majina Shemu,hamu na yafethi na wake zao. Nuhu na Mke waku.
*Mwanzo 8:15,16
Wanatoka kwenye safina, Nuhu, mkewe, wanawe na wake za wanawe.
*Mwanzo 9:1 Mungu anawapa amri kama aliyowapa adamu na hawa kabla hawajapata watoto. Zaeni mkaongezeka mkaijaze nchi. Maana yake walikuwa hawana watoto.
*Mwanzo 9:18,19 wanatajwa wana wa nuhu hao watatu, na anapigilia msurmari mstari wa 19, "HAWA WATATU WALIKUWA WANA WA NUHU NA KWA HAWA WATATU NCHI YOTE IKAENEA WATU"
* Mwanzo 10:1 watoto wa hawa jamaa wanaozungumziwa ni Baada ya Gharika, baada ya kuambiwa na Mungu zaeni mkaongezeke mkaijaze nchi.
5:Katika gharika Umesema Shem Alikuwa na miaka 100. hivyo anatakiwa awe ameshapata watoto.
Mwanzo 7:6, wakati mtoto wa kwanza anaingia na miaka 100, Baba mtu alikiwa na miaka 900.
hapo utaona Nuhu alipata mtoto akiwa na Miaka 800. kwa ratio hiyo tukiihamishia kwenye kizazi chetu au ukitoa sufuri Nuhu aliingia anamiaka 90, mtoto wake akiwa na Miaka 10.
kwa umri wa kabla ya gharika miaka mia ni kama teeneger. Ila kwa ukomavu wao walikuwa wameoa. yawezekana walikiwa hawajaoana muda mrefu au kwa ratio ya baba na watoto, watoto hawakuwa tayari wameshapata watoto.
mkuu nafikili kibibiliabibilia zaidi.
Asante mkuuMkuu ukiwa msomaji wa biblia utaelewa hoja yangu kivipi Mungu anaweza toa hukumu ila akaruhusu masalia wabaki na amefanya hivyo hata kwa wanefili wa baada ya gharika (Waamori)ambayo ni familia ya mfalme Ogu
Twende taratibu
1. Mungu anamuamuru waisraeli waue wakaanani WOTE wasibakize kitu
Kumbukumbu la torati 20
16 Lakini katika miji ya mataifa haya akupayo BWANA, Mungu wako, kuwa urithi, usihifadhi kuwa hai kitu cho chote kipumzikacho;
17 lakini uwaangamize kabisa, Mhiti, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, kama alivyokuamuru BWANA, Mungu wako;
2.Tukisoma kwenye joshua baada ya kuwa wameikamata canaani waliweka makubaliano na hawa wanefili ya kuwaacha hai!!
Joshua 9:15
15 Naye Yoshua akafanya amani pamoja nao, na kufanya agano nao, ili kwamba waachwe hai; na wakuu wa mkutano wakawaapia
3.Kinyume kabisa na maagizo ya Mungu ya kwanza tunaona wagibeoni wakiachwa hai na waliingia agano ambalo Mungu alisupport
Kumbukumbu 7
1 BWANA, Mungu wako, atakapokutia katika nchi uendayo kuimiliki, atakapoyang?oa mataifa mengi watoke mbele yako, Mhiti, na Mgirgashi, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, mataifa saba makubwa yenye nguvu kukupita wewe;
2 wakati BWANA, Mungu wako, atakapowatoa mbele yako, nawe utawapiga; wakati huo ndipo uwaondoe kabisa; usifanye agano nao, wala kuwahurumia; wala usioane nao
4.mpaka hapa unaweza kufikiri waliamua wenyewe waisrael lahasha..... Huko mbeleni tutaona MUNGU akiwaadhibu waisraeli kwa kuvunja agano hilo la kuwaacha waamori/wagieboni hai
2 samuel 21
1 Kulikuwa na njaa siku za Daudi muda wa miaka mitatu, mwaka kwa mwaka; naye Daudi akautafuta uso wa BWANA. BWANA akasema, Ni kwa ajili ya Sauli, na kwa nyumba yake yenye damu, kwa kuwa aliwaua hao Wagibeoni.
Je unataka kusema Mungu ni kigeugeu au utakubaliana na mimi kuwa Mungu aliamua kuwaacha hao wagibeoni kwa kusudi lake???
Na je kama tunaona hapa Mungu aliamrisha waue waamori WOTE ila baadae Mungu alitaka wengine wabakizwe je huoni hoja ya kusema Ogu kuwa mnefili pekee kuachwa kwenye gharika kuwa ina mashiko maana tumeona kumbe Mungu akitoa hukumu ya WOTE huwa anaacha exceptions!!!
Karibu tuelimishane mkuu wangu
Cc SALA NA KAZI Malcom Lumumba Eiyer popbwinyo Kudo900