NYOTE SOMENI HAPA ILI TUTOE UBISHI KIDOGO KUHUSU HII MIJITU
MAJITU katika Agano la Kale
Hawa majitu kama Goliathi na wengine waliojulikana katika Agano la Kale walikuwa kina nani?
Biblia inatuambia kwamba Daudi alimshinda Goliathi.
Goliathi alikuwa jitu lenye urefu wa zaidi ya mita tatu.
Kwa kuongezea Biblia inatutajia majitu mengine kwa majina, kama Ahimani, Sheshai, Talmai, Safu, Lahmi, Ishi-benobu na wengine pia.
Hawa majitu walitoka wapi? Walielewaje Israeli? Waliwaza nini juu ya Israeli?
Na Mungu aliwaelewaje?
Mungu aliwaza nini juu yao?
Mbona siku hizi hatuna majitu?
Au labda bado wako duniani?
Kuna majitu mengi yanaendelea kufanya kazi siku hizi pia.
MAJITU
Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao, wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua. Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini. Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena, baada ya hayo, wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu, wakazaa nao wana; hao ndio waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa. (MWA 6:1-4)
Biblia ya Kiswahili inatumia jina Wanefili. Wanefili maana yake ni majitu. Majitu ni sawasawa na Wanefili.
Tulisoma mambo yaliyotokea kabla ya Gharika. Majitu yaani wanefili walikuwepo kabla na baada ya Gharika. Majitu yale yalioishi kabla ya Gharika yalifia majini, wakati wa Nuhu. Lakini mambo ya majitu hayakuishia wakati wa Gharika, kwani yalizaliwa tena baada ya Gharika pia.
Tukianza kutaja miaka katika Biblia tangu kuzaliwa kwa Adamu tunaona kwamba Gharika ilitokea mwaka wa elfu moja mia sita hamsini na sita (1656) baada ya kuzaliwa kwa Adamu. Wakati huo watu walikuwepo mamilioni. Katika hali nzuri umri ya watu ulikuwa mara kumi zaidi ya siku hizi. Hivyo kuongezeka kwao kulitokea kwa haraka zaidi.
Sasa tunapochunguza swala la majitu, ni vizuri kukumbuke kwamba Biblia inasema: Hatujui neno lo lote bado, kama impasavyo kujua. (1KOR 8:2) Na Biblia inasema pia: Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; (1KOR 13:9)
Labda unafikiri kwamba hakuna umuhimu kuchunguza na kuongea kuhusu mambo ya majitu, mambo ya wanefili. Mimi ninakuuliza kwamba kwenye Biblia kuna jambo ambalo halina umuhimu wa kuchunguza? Mambo ya maajabu yote yaliyoko kwenye Biblia ni vipawa kutoka kwa Mungu na ni vizuri tuyachunguze kwa unyenyekevu, na shukrani na tuyapokee. Ingawa tuna upungufu katika kujua Neno la Mungu, hata hivyo kuna umuhimu wa kuchunguza na kutafuta maarifa tukisaidiwa na Roho Mtakatifu wa Mungu. Roho Mtakatifu asipotufunulia maandiko hatuelewi Biblia. Hivyo tunategemea kabisa Roho Mtakatifu atusaidie katika kufunua maandiko.
Biblia inatupa majina ya majitu kumi hivi. Kwa kuongezea wamekuwepo uzao wa majitu Waanaki na Warefai. Zamani Waamoni waliwaita Warefai kwa jina Wazamzumi. (KUM 2:20) Kwanza tunataka kujua:
�
UKUBWA wa MAJITU
Kwani aliyesalia katika mabaki ya Warefai ni Ogu pekee, mfalme wa Bashani; tazama, kitanda chake kilikuwa kitanda cha chuma; kitanda hicho, je! hakiko Raba kwa wana wa Amoni? urefu wake ulikuwa ni mikono kenda, na upana wake mikono minne, kwa mfano wa mkono wa mtu. (KUM 3:11)
Mkono ni sawa sawa na dhiraa. Urefu wa mkono moja, yaani dhiraa moja ni karibu na nusu mita. Mikono kenda, yaani tisa ni kama mita nne. Mikono nne ni karibu na mita mbili.
Hatuelezwi ukubwa wa Ogu, lakini urefu wa kitanda chake ulikuwa ni mikono tisa, yaani mita nne, na upana wa kitanda ulikuwa ni mikono minne, yaani karibu na mita mbili. Kuna vitanda vichache pamoja. Swala lilimhusu mfalme wa Warefai Ogu. Ni lazima alikuwa ni mtu mwenye mwili mkubwa kwa sababu alihitaji kitanda kikubwa sana.
Ndipo akatoka shujaa katika kambi ya Wafilisti, aliyeitwa Goliathi, wa Gathi, ambaye urefu wake ulikuwa mikono sita na shibiri moja. (1SAM 17:4)
Urefu wake Goliathi ulikuwa kama mita tatu. Mguu wake ulikuwa mkubwa ingemlazimu kuvaa viatu viwili. Viatu viwili kila mguu. Wakati wa kwenda kulala vitanda viwe vikubwa viwili au vitatu vimefuatana. Mstari unaofuatia unahusu silaha zake.
Alikuwa na chapeo ya shaba kichwani, tena amevaa darii ya shaba; na uzani wake ili darii ya shaba ulikuwa shekeli elfu tano za shaba. (1SAM 17:5)
Na ..amevaa darii ya shaba; ... ulikuwa kilo themanini ambao ni nzito zaidi ya uzito wangu. Tunagundua kwamba majitu walikuwa wakubwa na wenye nguvu sana.
NIA ya MAJITU
Naye akasimama, akawapigia kelele majeshi ya Israeli akawaambia, Mbona mmetoka kupanga vita? Je! mimi si Mfilisti, na ninyi si watumishi wa Sauli? Jichagulieni mtu, akanishukie mimi. (1SAM 17:8)
Goliathi alisema kwamba Waisraeli ni watumishi wa Sauli. Roho wa Mungu ilimtoka Sauli. (1SAM 16:14) Hivyo ilikuwa vizuri kwa Goliathi kudhihaki. Ukweli ni kwamba Waisraeli walikuwa watumishi wa Mungu, siyo watumishi wa Sauli tu. Ilitakiwa iwe hivyo.
Katika mstari wa 43 Goliathi aliapa na kulaani kwa jina la miungu yake. Yeye alikuwa amejitoa kuabudu sanamu na alimlaani Mungu wa Israeli. Yesu alisema: Kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake. (MT 12:34) Moyoni mwake wa Goliathi ulijazwa na mambo mabaya. Jitu yeye alidhihaki, alisema uongo, aliapa kwa miungu yake, alijivuna, alikuwa hayawani na katili. Ni mambo yasiyofanana na yale Mungu anavyotaka tuwe.
BASI NITAREJEA DAKIKA CHACHE ZIJAZO ILI TUPATE HISTORIA KIDOGO KUHUSU ISRAEL NA HII MIJITU LAKINI PIA NI NINI KUSUDIO LA MUNGU KWA MIJITU HII
asalaam kudo