Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

Grahnman. Sasa mkuu hapo nimechanganya wapi?
Wana wa Mungu waliwaona wana wa binadamu ya kuwa ni wazuri je wana wa Mungu walikuwa wapi?

Rejea hapa 4 Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa,
Mwanzo 3 :4

5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.
Mwanzo 3 :5

Huyu nyoka alitoka wapi?
Je jamii hii ya wanefili si unaona wamekuwa na ustaarabu kabla ya wanadamu
Hapo wewe unachanganya mambo sasa! Wanefili wamekuwako baada ya wana wa Mungu kukutana kimwili na wana wa wanadamu.
 
Mchawi Mkuu. Binafsi kwa maelezo haya sikubaliani kuwa wanefili ni malaika maana Bible haisemi hivyo
Rejea hapa
1 Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,
Mwanzo 6 :1

2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.
Mwanzo 6 :2

Hapa kusema wanefili ni mashetani siyo sahihi kwa sababu biblia inasema ni wana wa Mungu.
 
Mwanzo 7:21 Wakafa wote wenye mwili waendao juu ya nchi, na ndege, na wanyama wa kufugwa, na kila mnyama wa mwitu, na kila kitambaacho chenye kutambaa juu ya nchi, na kila mwanadamu;

mkuu source nyingine sawa, ila bibilia hapana. Vilikufa vyote. labda kama swntensi hiyo niliyoiquote ilimaanisha nini.
Kila kitu kipo kwa mwenye ufahamu anaelewa ila anaueamua kuufunga ufahamu wake atabakia na kitendawili! Umenukuu vema kabisa.
Maji yalikuwa yakitoka chini ya ardhi, na juu mvua kubwa ikinyesha isiyowahi kutokea! Huyo mwenye mwili wa namna gani atakayeweza kuishi hapo?!
 
Mkuu Point yako ipo sahihi kiasi chake maana hatuna ushahidi wa moja kwa moja lakini inasemekana binadamu alikuwepo kabla ya uumbwaji wa Adamu

Nitarudi ili tusaidiane katika kulifahamu hili ningojee kidoogo
Naja
Binadamu ni nani na Adamu ni nani?!
 
Mchawi Mkuu. Mkanganyiko upo kwasababu maandiko yanasema ni wana wa Mungu wewe unasema malaika wengine wanasema shetani hapa ndipo kunako kanganya
 
Nakushauri ukasome tena mkuu kwa maana tunaambiwa malaika ambao walimtembelea Ibrahim walienda tu kwa umbile la mwanadam na waliondoka wakaelekea katika kijiji cha sadum kwa lut na walivyofika walikaribishwa na lut hakujua kama hao wageni wake ni malaika kutoka mbinguni wakakaa na wakatengewa chakula wakakaribishwa kula na walikataa na hapo ndipo walimwambia lut kwamba sisi ni malaika kutoka mbinguni tumetumwa kwako ili kukuokoa hivyo unatakiwa ujiandae ucku huu pamoja na watu wako muondoke zenu katika kijiji hiki cz tunataka kukiangamiza. Hakuna hata sehem moja ya andiko inayosema malaika kazaa na mwanadam acheni kupotosha watu bhana.
Mkuu hakuna anyepotosha kwani kuna mahala nmeandika malaika walizaa na binadamu?? Kwenye mada yangu maana wote tunajua wanefili ni uzao wa cain na seth likowazi kabisa ila Nimeleta hiyo hoja ya MALAIKA baada ya mchangiaji mmoja kusema malaika hawezi kumzalisha mwanadamu ndio nkauliza Yesu aliwezaje kuzaliwa bila maria kulala na mwanaume?? Kama alipata kwa kupandikizwa tu na roho mtakatifu je malaika hawawezi pia..... Ni swali tu kusaidiana hakuna upotoshaji

Kingine nmesema kma hao malaika waliweza kwenda kwa Abraham kwa muonekano wa kibinadamu na walifanya kila kitu ambacho mwanadamu anaweza kufanya kwanni usiamini pia wangeweza hata kulala na mwanamke??

Haya ni maswali ya kujiuliza tu so hakuna haja ya kutoa kashfa kuwa nani mpotoshaji nani sio ni kueleweshana tu
 
NYOTE SOMENI HAPA ILI TUTOE UBISHI KIDOGO KUHUSU HII MIJITU

MAJITU katika Agano la Kale

Hawa majitu kama Goliathi na wengine waliojulikana katika Agano la Kale walikuwa kina nani?

Biblia inatuambia kwamba Daudi alimshinda Goliathi.

Goliathi alikuwa jitu lenye urefu wa zaidi ya mita tatu.

Kwa kuongezea Biblia inatutajia majitu mengine kwa majina, kama Ahimani, Sheshai, Talmai, Safu, Lahmi, Ishi-benobu na wengine pia.

Hawa majitu walitoka wapi? Walielewaje Israeli? Waliwaza nini juu ya Israeli?

Na Mungu aliwaelewaje?

Mungu aliwaza nini juu yao?

Mbona siku hizi hatuna majitu?

Au labda bado wako duniani?

Kuna majitu mengi yanaendelea kufanya kazi siku hizi pia.

MAJITU

Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao, wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua. Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini. Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena, baada ya hayo, wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu, wakazaa nao wana; hao ndio waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa. (MWA 6:1-4)

Biblia ya Kiswahili inatumia jina Wanefili. Wanefili maana yake ni majitu. Majitu ni sawasawa na Wanefili.

Tulisoma mambo yaliyotokea kabla ya Gharika. Majitu yaani wanefili walikuwepo kabla na baada ya Gharika. Majitu yale yalioishi kabla ya Gharika yalifia majini, wakati wa Nuhu. Lakini mambo ya majitu hayakuishia wakati wa Gharika, kwani yalizaliwa tena baada ya Gharika pia.

Tukianza kutaja miaka katika Biblia tangu kuzaliwa kwa Adamu tunaona kwamba Gharika ilitokea mwaka wa elfu moja mia sita hamsini na sita (1656) baada ya kuzaliwa kwa Adamu. Wakati huo watu walikuwepo mamilioni. Katika hali nzuri umri ya watu ulikuwa mara kumi zaidi ya siku hizi. Hivyo kuongezeka kwao kulitokea kwa haraka zaidi.

Sasa tunapochunguza swala la majitu, ni vizuri kukumbuke kwamba Biblia inasema: Hatujui neno lo lote bado, kama impasavyo kujua. (1KOR 8:2) Na Biblia inasema pia: Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; (1KOR 13:9)

Labda unafikiri kwamba hakuna umuhimu kuchunguza na kuongea kuhusu mambo ya majitu, mambo ya wanefili. Mimi ninakuuliza kwamba kwenye Biblia kuna jambo ambalo halina umuhimu wa kuchunguza? Mambo ya maajabu yote yaliyoko kwenye Biblia ni vipawa kutoka kwa Mungu na ni vizuri tuyachunguze kwa unyenyekevu, na shukrani na tuyapokee. Ingawa tuna upungufu katika kujua Neno la Mungu, hata hivyo kuna umuhimu wa kuchunguza na kutafuta maarifa tukisaidiwa na Roho Mtakatifu wa Mungu. Roho Mtakatifu asipotufunulia maandiko hatuelewi Biblia. Hivyo tunategemea kabisa Roho Mtakatifu atusaidie katika kufunua maandiko.

Biblia inatupa majina ya majitu kumi hivi. Kwa kuongezea wamekuwepo uzao wa majitu Waanaki na Warefai. Zamani Waamoni waliwaita Warefai kwa jina Wazamzumi. (KUM 2:20) Kwanza tunataka kujua:


UKUBWA wa MAJITU

Kwani aliyesalia katika mabaki ya Warefai ni Ogu pekee, mfalme wa Bashani; tazama, kitanda chake kilikuwa kitanda cha chuma; kitanda hicho, je! hakiko Raba kwa wana wa Amoni? urefu wake ulikuwa ni mikono kenda, na upana wake mikono minne, kwa mfano wa mkono wa mtu. (KUM 3:11)

Mkono ni sawa sawa na dhiraa. Urefu wa mkono moja, yaani dhiraa moja ni karibu na nusu mita. Mikono kenda, yaani tisa ni kama mita nne. Mikono nne ni karibu na mita mbili.

Hatuelezwi ukubwa wa Ogu, lakini urefu wa kitanda chake ulikuwa ni mikono tisa, yaani mita nne, na upana wa kitanda ulikuwa ni mikono minne, yaani karibu na mita mbili. Kuna vitanda vichache pamoja. Swala lilimhusu mfalme wa Warefai Ogu. Ni lazima alikuwa ni mtu mwenye mwili mkubwa kwa sababu alihitaji kitanda kikubwa sana.

Ndipo akatoka shujaa katika kambi ya Wafilisti, aliyeitwa Goliathi, wa Gathi, ambaye urefu wake ulikuwa mikono sita na shibiri moja. (1SAM 17:4)

Urefu wake Goliathi ulikuwa kama mita tatu. Mguu wake ulikuwa mkubwa ingemlazimu kuvaa viatu viwili. Viatu viwili kila mguu. Wakati wa kwenda kulala vitanda viwe vikubwa viwili au vitatu vimefuatana. Mstari unaofuatia unahusu silaha zake.

Alikuwa na chapeo ya shaba kichwani, tena amevaa darii ya shaba; na uzani wake ili darii ya shaba ulikuwa shekeli elfu tano za shaba. (1SAM 17:5)

Na ..amevaa darii ya shaba; ... ulikuwa kilo themanini ambao ni nzito zaidi ya uzito wangu. Tunagundua kwamba majitu walikuwa wakubwa na wenye nguvu sana.

NIA ya MAJITU

Naye akasimama, akawapigia kelele majeshi ya Israeli akawaambia, Mbona mmetoka kupanga vita? Je! mimi si Mfilisti, na ninyi si watumishi wa Sauli? Jichagulieni mtu, akanishukie mimi. (1SAM 17:8)

Goliathi alisema kwamba Waisraeli ni watumishi wa Sauli. Roho wa Mungu ilimtoka Sauli. (1SAM 16:14) Hivyo ilikuwa vizuri kwa Goliathi kudhihaki. Ukweli ni kwamba Waisraeli walikuwa watumishi wa Mungu, siyo watumishi wa Sauli tu. Ilitakiwa iwe hivyo.

Katika mstari wa 43 Goliathi aliapa na kulaani kwa jina la miungu yake. Yeye alikuwa amejitoa kuabudu sanamu na alimlaani Mungu wa Israeli. Yesu alisema: Kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake. (MT 12:34) Moyoni mwake wa Goliathi ulijazwa na mambo mabaya. Jitu yeye alidhihaki, alisema uongo, aliapa kwa miungu yake, alijivuna, alikuwa hayawani na katili. Ni mambo yasiyofanana na yale Mungu anavyotaka tuwe.

BASI NITAREJEA DAKIKA CHACHE ZIJAZO ILI TUPATE HISTORIA KIDOGO KUHUSU ISRAEL NA HII MIJITU LAKINI PIA NI NINI KUSUDIO LA MUNGU KWA MIJITU HII

asalaam kudo
 
nyie nao hebu nionesheni katika biblia palipo andikwa malaika wakashuka na kulala na binadamu. Ukisema wana wa Mungu ndio malaika uje na andiko linalothibitisha madai yako kuwa wana wa Mungu walio tajwa ndio malaika senyewe
 
Mkuu hakuna anyepotosha kwani kuna mahala nmeandika malaika walizaa na binadamu?? Kwenye mada yangu maana wote tunajua wanefili ni uzao wa cain na seth likowazi kabisa ila Nimeleta hiyo hoja ya MALAIKA baada ya mchangiaji mmoja kusema malaika hawezi kumzalisha mwanadamu ndio nkauliza Yesu aliwezaje kuzaliwa bila maria kulala na mwanaume?? Kama alipata kwa kupandikizwa tu na roho mtakatifu je malaika hawawezi pia..... Ni swali tu kusaidiana hakuna upotoshaji

Kingine nmesema kma hao malaika waliweza kwenda kwa Abraham kwa muonekano wa kibinadamu na walifanya kila kitu ambacho mwanadamu anaweza kufanya kwanni usiamini pia wangeweza hata kulala na mwanamke??

Haya ni maswali ya kujiuliza tu so hakuna haja ya kutoa kashfa kuwa nani mpotoshaji nani sio ni kueleweshana tu
Nimekuelewa mkuu
 
Mchawi Mkuu. Usitake nikubaliane na mawazo yako bila kunipa ukweli leta maandiko nikuelewe yaani uniambie wanefili ni malaika wakati maandiko yanasema hivi

2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.
Mwanzo 6 :2
 
Nakushauri ukasome tena mkuu kwa maana tunaambiwa malaika ambao walimtembelea Ibrahim walienda tu kwa umbile la mwanadam na waliondoka wakaelekea katika kijiji cha sadum kwa lut na walivyofika walikaribishwa na lut hakujua kama hao wageni wake ni malaika kutoka mbinguni wakakaa na wakatengewa chakula wakakaribishwa kula na walikataa na hapo ndipo walimwambia lut kwamba sisi ni malaika kutoka mbinguni tumetumwa kwako ili kukuokoa hivyo unatakiwa ujiandae ucku huu pamoja na watu wako muondoke zenu katika kijiji hiki cz tunataka kukiangamiza. Hakuna hata sehem moja ya andiko inayosema malaika kazaa na mwanadam acheni kupotosha watu bhana.
Mkuu ww ndio ukasome upya.... Mbona msosi walipiga kama kawaida

Mwanzo 19
3 Akawasihi sana, nao wakaja, wakaingia nyumbani mwake. Akawafanyia karamu, akawapikia mikate isiyochachwa nao wakala
 
Mkuu ww ndio ukasome upya.... Mbona msosi walipiga kama kawaida

Mwanzo 19
3 Akawasihi sana, nao wakaja, wakaingia nyumbani mwake. Akawafanyia karamu, akawapikia mikate isiyochachwa nao wakala
Ucjali mkuu nishaajua tofauti yetu mimi naww ni kwamba tumesoma vitabu tofauti. Ila ucjali tukopamoja mkuu
 
Kila kitu kipo kwa mwenye ufahamu anaelewa ila anaueamua kuufunga ufahamu wake atabakia na kitendawili! Umenukuu vema kabisa.
Maji yalikuwa yakitoka chini ya ardhi, na juu mvua kubwa ikinyesha isiyowahi kutokea! Huyo mwenye mwili wa namna gani atakayeweza kuishi hapo?!
mkuu tuliambiwa watu wataachana na neno, wageukie hadithi za kutungwa na philosophical ideas.
ni hatari sana kujadili mambo ya bibilia na kuyapa authority sawa na nadharia nyingine.

Kitendo cha bibilia kusema walikufa viumbe wote nje ya safina. na Yesu akapigilia msumari baadae. mada ya kwamba kuna lijamaa kubwa sana liliponyoka adhabu ya Mungu utadhani Mungu alikuwa anacheza kombolela na viumbe wake ilipaswa ijadiliwe kwa nadhalia nyingine bila kuhusisha bibilia ambayo huo mjadala ilishaufunga. chochote hai chenye ufanano na wanefili si wanefili wa kabla ya gharika.

maoni.
 
Grahnman. Mkuu kwani kuandika malaika kulishindikana nini mbona bible haiandiki vitu kwa kuficha kama bible inaandika wafiraji sembuse kuandika malaika ukweli unabaki wanefili ni wanefili na malaika ni malaika huu ndio ukweli wa maandiko.
Na wanefili walikuwako kabla ya wanadamu

4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.
Mwanzo 6 :4
 
nyie nao hebu nionesheni katika biblia palipo andikwa malaika wakashuka na kulala na binadamu. Ukisema wana wa Mungu ndio malaika uje na andiko linalothibitisha madai yako kuwa wana wa Mungu walio tajwa ndio malaika senyewe
Ayubu 2:
1.Tena kulikuwa na siku hao wana wa Mungu walipokwenda kujihudhurisha mbele za BWANA, Shetani naye akaenda kati yao, ili kujihudhurisha mbele za BWANA.
2 BWANA akamwuliza Shetani, Umetoka wapi? Shetani akamjibu BWANA, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani.....
 
Ayubu 2:
1.Tena kulikuwa na siku hao wana wa Mungu walipokwenda kujihudhurisha mbele za BWANA, Shetani naye akaenda kati yao, ili kujihudhurisha mbele za BWANA.
2 BWANA akamwuliza Shetani, Umetoka wapi? Shetani akamjibu BWANA, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani.....
prove wana wa Mungu ndio malaika
 
pia haikusemwa mbele za Bwana kuwa ni mbinguni au kolote kule
Hata wanao enda kwenye masinagogi makanisani misikitini huwa wanajihudhurisha mbele za Mungu nao huitwa wana wa Mungu

prove kama wana wa Mungu ndi malaika?
 
Back
Top Bottom