Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

jimmykb197. Mkuu nifafanulie hapa

4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.
Mwanzo 6 :4
 
jimmykb197. Mkuu nifafanulie hapa

4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.
Mwanzo 6 :4
naomba kujuzwa kuwa hao Wana Wa Mungu ndio malaika. Ushahidi wowote wa kimaandiko?
 
Kudo900. Nakusubiri ulete nondo.

TUENDELEE TENA NA KAMA KWELI WATAKA JIFUNZA BASI MALI
ZA KUSOMA


Tusome sehemu fupi kuhusu historia ya Israeli. Hii ni wakati wana Waisraeli walitoka utumwani wa Misri kuelekea kwenye nchi ya ahadi.

Nanyi mkanikaribia kila mmoja wenu, mkasema, Na tupeleke watu mbele yetu, ili watupelezee nchi na kutuletea habari za njia itupasayo kuipandia, na za miji mtakayoifikia. (KUM 1:22)

Tungesoma zaidi Biblia (KUM 9:23,24) tungegundua kwamba Mungu alitaka kuwatoa wakati ule na kuwapeleka katika nchi ya ahadi lakini wale watu walileta fujo walikataa. Hivyo waliwaomba wapelelezi na Mungu akasema: �Endeni mkapeleleze. Kwa sababu hamna imani mioyoni mwenu na katika mawazo yenu, piteni katika njia ambayo ni mavuno ya kutokuamini kwenu. Endeni mkaangalie kwani hamwamini yale niliyowaambia."

Basi wakapanda wakaipeleleza nchi toka jangwa la Sinai hata Rehobu, mpaka kuingia Hamathi. Wakapanda katika Negebu, wakafika Hebroni; na Ahimani, na Sheshai, na Talmai, wana wa Anaki, walikuwako huko. Nao Hebroni ulijengwa miaka saba kabla ya Soani wa Misri. (HES 13:21,22)

Hapa tunawaona majitu. Katika uzao wa Anaki wanapatikana Ahimani, Sheshai na Talmai. Wale wapelelezi walikutana na wale majitu ambao Kalebu aliwafukuza baada ya miaka sitini. Waliongea pamoja na majitu. Baada ya hapo walirejea tena kwenye kambi ya Waisraeli kwa Musa. Halafu waliwaeleza kuhusu safari yao.

Lakini watu wanaokaa katika nchi ile ni hodari, na miji yao ina maboma, nayo ni makubwa sana; na pamoja na hayo tuliwaona wana wa Anaki huko. Wakawaletea wana wa Israeli habari mbaya ya ile nchi waliyoipeleleza, wakasema, Ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi inayowala watu wanaoikaa; na watu wote tuliowaona ndani yake ni watu warefu mno.(HES 13:28,32)

Walikutana na majitu watatu tu. Hawa walibaki sana kwenye mawazo yao baadaye waliona watu wote kuwa na wakubwa wale.

Kisha, huko tuliwaona kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi. (HES 13:33)

Wanefili maana yake ni majitu. Wapelelezi walijiona udogo wao, walijiona kuwa kama mapanzi. Halafu walisema: "nao ndivyo walivyotuona sisi." Wapelelezi walijua kwamba majitu wamewaona kama mapanzi. Wao walijuaje? Ni kwa sababu majitu waliwaita: "Ninyi mapanzi."

Wapelelezi wawili kati ya wale kumi na mbili Kalebu na Yoshua walikuwa na roho ingine. Walikuwa na roho ya kuamini. Wale wengine walikuwa na roho kama wale waliobaki kambini, yaani roho ya kutokuamini. Yoshua na Kalebu walisema katika sura ya kumi na nne, mstari wa tisa, kwamba: wao ni chakula kwetu. Wengine wanawaonaje majitu, wengine kama chakula?

Neno hilo wanaweza kuliona kwa njia tofauti? Kutokuamini inawaangalia wanaonekana, imani inaangalia yanayowezekana kwa Mungu! Majitu hawa waliwadhihaki watu wa Mungu na watasababisha watu wakae katika kutokuamini na hofu, na hivi safari yao ilichukua miaka arobaini, kabla hawajafika nchi ya Kanani. Majitu hawakuweza kuzuia kufika kwao, ila walifanya safari ya wana wa Israeli iende pole pole zaidi. Kutokuamini inajaribu kufanya hivi pia katika maisha yetu kwamba tusingeweza kukua upesi na kusafiri upesi bali pole pole tu.

NIA YA MUNGU KUHUSU MAJITU

Sikiliza, Ee Israeli; hivi leo unataka kuvuka Yordani uingie kwa kuwamiliki mataifa yaliyo makubwa, na yenye nguvu kukupita wewe, miji mikubwa iliyojengwa kuta hata mbinguni, watu wakubwa, warefu, wana wa Waanaki, uwajuao, uliokuwa ukisikia wakitajwa hivi, Ni nani awezaye kusimama mbele ya wana wa Anaki? Basi jua siku hii ya leo kuwa Bwana, Mungu wako, ndiye atanguliaye kuvuka mbele yako kama moto uteketezao; atawaangamiza, tena atawaangusha mbele yako; ndivyo utakavyowafukuza na kuwa poteza upesi, kama alivyokuambia Bwana. (KUM 9:1-3)

Mungu alikubali kuwa kama moto uteketezao, ata waangamiza na kuwaangusha majitu. Mungu alisema: watu wakubwa, warefu, wana wa Waanaki. Kwa msaada wa Mungu Waisraeli waliwafukuza na kuwapoteza. Mungu aliwachukia majitu.

Vile vile kama Bwana alivyomwamuru Musa mtumishi wake, ndivyo Musa alivyomwamuru Yoshua; naye Yoshua akafanya vivyo; hakukosa kufanya neno lo lote katika hayo yote Bwana aliyomwamuru Musa. Wakati huo Yoshua akaenda na kuwakatilia mbali hao Waanaki watoke nchi ya vilima, kutoka Hebroni, na kutoka Debiri, na kutoka Anabu, na kutoka katika nchi yote ya vilima vilima ya Yuda, na kutoka katika nchi yote ya vilima vilima ya Israeli; Yoshua akawaangamiza kabisa na miji yao. Hawakusalia Waanaki hata mmoja katika nchi ya wana wa Israeli isipokuwa katika Gaza, na katika Gathi, na katika Ashdodi walisalia. (YOS 11:15, 21, 22)

Waanaki ni uzao wa majitu. Wakati wa kuwaangamiza majitu Yoshua alitekeleza agizo hilo Mungu aliyomwagiza Musa. Na hivi majitu walibaki nje ya maeneo ya Waisraeli.

Kisha alimpa huyo Kalebu mwana wa Yefune sehemu kati ya wana wa Yuda, kama Bwana alivyomwamuru Yoshua, maana ni Kiriath-arba, ni huyo Arba aliyekuwa babaye Anaki (Huo ndio Hebroni). Huyo Kalebu aliwafukuza watoke hapo hao wana watatu wa Anaki, nao ni Sheshai, na Ahimani, na Talmai, wana wa Anaki. (YOS 15:13, 14)

Arba na Anaki walikuwa majitu kama vile vile Sheshai, na Ahimani, na Talmai, wana wa Anaki. Kalebu alikutana na aliyowafahamu zamani. Kalebu amesema kwamba majitu ni chakula tu. Aliwafukuza mbali. Daudi aliambiwa na Biblia, kwamba katika yote alitimiza matakwa ya Mungu. (MDO 13:22) Alifanya mapenzi ya Mungu hata kuhusu majitu.

Tunasoma tena kuhusu Daudi na huyu Goliathi wa Gathi. Goliathi alikuwa jitu, kama unavyokumbuka. Urefu wake ulikuwa mita tatu.

Ikawa, hapo Mfilisti alipojiinua, akaenda akamkaribia Daudi, ndipo Daudi naye akapiga mbio, akalikimbilia jeshi ili akutane na yule Mfilisti. Daudi akatia mkono wake mfukoni, akatwaa humo jiwe moja, akalitupa kwa kombeo lake, akampiga Mfilisti katika kipaji cha uso; jiwe hilo likamwingilia kipajini, akaanguka chini kifudifudi. Hivyo Daudi akamshinda yule Mfilisti kwa kombeo na jiwe, akampiga Mfilisti akamwua; walakini Daudi hakuwa na upanga mkononi mwake. Hivyo Daudi akapiga mbio, akasimama juu ya Mfilisti, akautwaa upanga wake, akaufuta alani mwake, akamwua, akamkata kichwa kwa upanga huo. Nao Wafilisti walipoona ya kuwa shujaa wao amekufa, wakakimbia. (1SAM 17:48-51)

Ndivyo alivyoenenda Daudi aliyependeza moyo wa Mungu. Daudi alimwua jitu Goliathi. Hata watumishi wake pia.

Basi kulikuwa na vita tena kati ya Wafilisti na Israeli; Daudi akashuka mpaka Gobu, na watumishi wake pamoja naye, akapigana na Wafilisti; naye Daudi akaishiwa na nguvu. Naye Ishi-benobu, aliyekuwa mmojawapo wa Waferai, ambaye uzito wa mkuki wake ulikuwa shekeli mia tatu za shaba kwa uzani, naye amejifungia upanga mpya, alijaribu kumwua Daudi. Lakini Abishai, mwana wa Seruya, akamsaidia, akampiga Mfilisti, akamwua. Ndipo watu wa Daudi wakamwapia, wakasema, Wewe hutatoka tena pamoja nasi kwenda vitani, usije ukaizima taa ya Israeli. Ikawa baada ya hayo, kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; ndipo Sibekai, Mhushathi, alipomwua Safu, aliyekuwa mmojawapo wa Warefai. Kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; na Elhanani, mwana wa Yairi, Mbethlehemi, alimwua Goliathi, Mgiti, ambaye mti wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumaji. Kulikuwa na vita tena huko Gathi; ambako kulikuwa na mtu mrefu sana, mwenye vidole sita katika kila mkono, na vidole sita katika kila mguu, jumla yake ishirini na vinne; yeye naye alizaliwa kwa Mrefai. Naye huyo alipowatukana Israeli, ndipo Yonathani, mwana wa Shama, nduguye Daudi, akamwua. Hao wanne walizaliwa kwake huyo Mrefai wa Gahti; wakaanguka kwa mkono wa Daudi, na kwa mikono ya watumishi wake. (2SAM 21:15-22)

Warefai walikuwa kabila la majitu. Tulisoma majina ya majitu: Ishi-benobu, Safu wa Warefai, Goliathi. Katika mistari hii tunaona tabia za hao majitu na jinsi Mungu alivyowafikiria. Ishi-benobu alinuia kumwua Daudi aliyekuwa amechoka, lakini Abishai, mtoto wa dada yake Daudi alimwua yule jitu na hivyo akaokoa maisha ya mjomba wake.

Sibekai alimwua Safu. (1NYA 20:4). Elhanani alimwua Goliathi wa Gathi, aliyeitwa kwa jina jingine, Lahmi katika kitabu cha NYAKATI. (1NYA 20:5). Yeye alikuwa amechukua jina la nduguye Goliathi, aliyeuawa na Daudi. Daudi alimwua Goliathi akiwa kijana kwa jiwe na kombeo. (1SAM 17). Huyu jitu mwenye vidole vya mguuni sita na vidole vya mkononi sita aliuawa na Yonathani kijana wa ndugu yake Daudi. Benaya, mtu hodari wa Daudi, katika vita pia alikuwepo katika kuwaangamiza majitu.

asalaaam kudo
 
hapo wametajwa kama sons of God not Angeles. sasa naomba kama kuna mtu anaweza kunihakikishia hao sons of God ndio malaika wenyewe?
IMG_20180430_211616_803.JPG
 
Mkuu ww ndio ukasome upya.... Mbona msosi walipiga kama kawaida

Mwanzo 19
3 Akawasihi sana, nao wakaja, wakaingia nyumbani mwake. Akawafanyia karamu, akawapikia mikate isiyochachwa nao wakala

Chief uliniita sasa nisha itika japo naona Kama uzi mmeshauhamisha hivi lakini nimeitika ulichoniitia hebu pitia huku mimi nikimsubiri
Da'vinci nae apite tuone yake
 
Jamani haya yanawezekana maana hata toothpick walizokuwa wanatumie enzi hizo ni kubwa sana kwa sasa unaweza kuzifananisha na nguzo ya umeme.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Hapo kitombeo hakijasimama, basi ata wanifeli wa kike walikuwa na bonge la papuchi haki ya mtume...!
Mkuu,unamaanisha kuwa hawa wanefili wa kike walikuwa na kyuma kama mlango wa container?
 
Kwanza kuna kitu hakileti ukweli katika Biblia maana hapa katika maandiko ya mwanzo kuna mkanganyiko inaonyesha WANEFILI WALIKUWEPO KABLA YA BINADAMU

1 Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,
Mwanzo 6 :1

2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.
Mwanzo 6 :2

4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.
Mwanzo 6 :4
Kweli biblia pana mweh!
 
mitale na midimu. Hiki tunachojadili si maandiko ya biblia?
Mambo mengi tuliyo nayo kwa kiasi kikubwa majibu yake yanapatikana ktk biblia hata kama tukiwa na ufahamu wa namna gani utegemezi wa biblia hatuukwepi kabisa.
 
pia haikusemwa mbele za Bwana kuwa ni mbinguni au kolote kule
Hata wanao enda kwenye masinagogi makanisani misikitini huwa wanajihudhurisha mbele za Mungu nao huitwa wana wa Mungu

prove kama wana wa Mungu ndi malaika?
Mbona biblia iko wazi kabisa kwenye kisa cha nebukadneza !!

Daniel 23
25 Akajibu, akasema, Tazama, mimi naona watu wanne, nao wamefunguliwa, wanatembea katikati ya moto hali hawana dhara; na sura yake yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu.

28 Nebukadreza akanena, akasema, Na ahimidiwe Mungu wa Shadraka, na Meshaki, na Abednego; aliyemtuma malaika wake, akawaokoa watumishi wake waliomtumaini, wakaligeuza neno la mfalme, na kujitoa miili yao ili wasimtumikie mungu mwingine, wala kumwabudu, ila Mungu wao wenyewe
 
911sep11.
Hawa wana wa Mungu siyo malaika kwani biblia haijaficha kitu ilipo paswa kuandika malaika imeandika, ilipopaswa kuandika shetani imeandika na ilipotakiwa kuandika mwana wa Mungu imeandika na ukweli umebaki katika tofauti ya kila andiko na hivi ni vitu tofauti kabisa.
 
mitale na midimu. Hiki tunachojadili si maandiko ya biblia?
Mambo mengi tuliyo nayo kwa kiasi kikubwa majibu yake yanapatikana ktk biblia hata kama tukiwa na ufahamu wa namna gani utegemezi wa biblia hatuukwepi kabisa.
pamoja mkuu nimepita kwa juujuu.
ninaona hoja zimejengwa kwa mafungu ya bibilia baadhi nikashawishika kutoa maoni.
ikiwa msingi ni bibilia basi hakuna kilichopona katika gharika nje ya safina.

nimesema hivyo maana mada inataka tujadili mambo ya bibilia bila kufungwa na bibilia kwa kiasi flani kitu ambacho kwa mtazamo wangu ni contradiction.
ila nimejifunza mambo mapya mengi.

Mungu akubariki mkuu zitto jr
 
Mchawi Mkuu. Mkanganyiko upo kwasababu maandiko yanasema ni wana wa Mungu wewe unasema malaika wengine wanasema shetani hapa ndipo kunako kanganya
@impongo. Hapana!
Wana wa Mungu ni wale fallen angel ambao walishuka duniani katika mlima Fulani hivi!.
Chini ya kiongozi wao!.
Ukisoma katika vitabu vingine vya kale Wana wa Mungu wameelezewa kama! Malaika!
Na Wala siyo binadamu kama unavyodhani!
Kumbuka malaika ana uwezo wa kufanya mengi!
 
Mchawi Mkuu. Binafsi kwa maelezo haya sikubaliani kuwa wanefili ni malaika maana Bible haisemi hivyo
Rejea hapa
1 Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,
Mwanzo 6 :1

2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.
Mwanzo 6 :2

Hapa kusema wanefili ni mashetani siyo sahihi kwa sababu biblia inasema ni wana wa Mungu.
Wanefili ni product ya specis mbili kati ya
Binadamu Na malaika!.
Ni sawa Na nguruwe azae Na mbwa!
Yule mtt atakayetokea!
 
Mbona biblia iko wazi kabisa kwenye kisa cha nebukadneza !!

Daniel 23
25 Akajibu, akasema, Tazama, mimi naona watu wanne, nao wamefunguliwa, wanatembea katikati ya moto hali hawana dhara; na sura yake yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu.

28 Nebukadreza akanena, akasema, Na ahimidiwe Mungu wa Shadraka, na Meshaki, na Abednego; aliyemtuma malaika wake, akawaokoa watumishi wake waliomtumaini, wakaligeuza neno la mfalme, na kujitoa miili yao ili wasimtumikie mungu mwingine, wala kumwabudu, ila Mungu wao wenyewe
na wa nne mfano wa mwana wa Mungu. Ila hakua mwana wa Mungu bali kwa mujibu wa Nebkadneza alimwuta/taja malaika. bado fungu hilo halituoneshi kuwa malaika kwa jina jingine wanaitwa wana wa Mungu
 
Back
Top Bottom