Kudo900. Nakusubiri ulete nondo.
TUENDELEE TENA NA KAMA KWELI WATAKA JIFUNZA BASI MALI
ZA KUSOMA
Tusome sehemu fupi kuhusu historia ya Israeli. Hii ni wakati wana Waisraeli walitoka utumwani wa Misri kuelekea kwenye nchi ya ahadi.
Nanyi mkanikaribia kila mmoja wenu, mkasema, Na tupeleke watu mbele yetu, ili watupelezee nchi na kutuletea habari za njia itupasayo kuipandia, na za miji mtakayoifikia. (KUM 1:22)
Tungesoma zaidi Biblia (KUM 9:23,24) tungegundua kwamba Mungu alitaka kuwatoa wakati ule na kuwapeleka katika nchi ya ahadi lakini wale watu walileta fujo walikataa. Hivyo waliwaomba wapelelezi na Mungu akasema: �Endeni mkapeleleze. Kwa sababu hamna imani mioyoni mwenu na katika mawazo yenu, piteni katika njia ambayo ni mavuno ya kutokuamini kwenu. Endeni mkaangalie kwani hamwamini yale niliyowaambia."
Basi wakapanda wakaipeleleza nchi toka jangwa la Sinai hata Rehobu, mpaka kuingia Hamathi. Wakapanda katika Negebu, wakafika Hebroni; na Ahimani, na Sheshai, na Talmai, wana wa Anaki, walikuwako huko. Nao Hebroni ulijengwa miaka saba kabla ya Soani wa Misri. (HES 13:21,22)
Hapa tunawaona majitu. Katika uzao wa Anaki wanapatikana Ahimani, Sheshai na Talmai. Wale wapelelezi walikutana na wale majitu ambao Kalebu aliwafukuza baada ya miaka sitini. Waliongea pamoja na majitu. Baada ya hapo walirejea tena kwenye kambi ya Waisraeli kwa Musa. Halafu waliwaeleza kuhusu safari yao.
Lakini watu wanaokaa katika nchi ile ni hodari, na miji yao ina maboma, nayo ni makubwa sana; na pamoja na hayo tuliwaona wana wa Anaki huko. Wakawaletea wana wa Israeli habari mbaya ya ile nchi waliyoipeleleza, wakasema, Ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi inayowala watu wanaoikaa; na watu wote tuliowaona ndani yake ni watu warefu mno.(HES 13:28,32)
Walikutana na majitu watatu tu. Hawa walibaki sana kwenye mawazo yao baadaye waliona watu wote kuwa na wakubwa wale.
Kisha, huko tuliwaona kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi. (HES 13:33)
Wanefili maana yake ni majitu. Wapelelezi walijiona udogo wao, walijiona kuwa kama mapanzi. Halafu walisema: "nao ndivyo walivyotuona sisi." Wapelelezi walijua kwamba majitu wamewaona kama mapanzi. Wao walijuaje? Ni kwa sababu majitu waliwaita: "Ninyi mapanzi."
Wapelelezi wawili kati ya wale kumi na mbili Kalebu na Yoshua walikuwa na roho ingine. Walikuwa na roho ya kuamini. Wale wengine walikuwa na roho kama wale waliobaki kambini, yaani roho ya kutokuamini. Yoshua na Kalebu walisema katika sura ya kumi na nne, mstari wa tisa, kwamba: wao ni chakula kwetu. Wengine wanawaonaje majitu, wengine kama chakula?
Neno hilo wanaweza kuliona kwa njia tofauti? Kutokuamini inawaangalia wanaonekana, imani inaangalia yanayowezekana kwa Mungu! Majitu hawa waliwadhihaki watu wa Mungu na watasababisha watu wakae katika kutokuamini na hofu, na hivi safari yao ilichukua miaka arobaini, kabla hawajafika nchi ya Kanani. Majitu hawakuweza kuzuia kufika kwao, ila walifanya safari ya wana wa Israeli iende pole pole zaidi. Kutokuamini inajaribu kufanya hivi pia katika maisha yetu kwamba tusingeweza kukua upesi na kusafiri upesi bali pole pole tu.
NIA YA MUNGU KUHUSU MAJITU
Sikiliza, Ee Israeli; hivi leo unataka kuvuka Yordani uingie kwa kuwamiliki mataifa yaliyo makubwa, na yenye nguvu kukupita wewe, miji mikubwa iliyojengwa kuta hata mbinguni, watu wakubwa, warefu, wana wa Waanaki, uwajuao, uliokuwa ukisikia wakitajwa hivi, Ni nani awezaye kusimama mbele ya wana wa Anaki? Basi jua siku hii ya leo kuwa Bwana, Mungu wako, ndiye atanguliaye kuvuka mbele yako kama moto uteketezao; atawaangamiza, tena atawaangusha mbele yako; ndivyo utakavyowafukuza na kuwa poteza upesi, kama alivyokuambia Bwana. (KUM 9:1-3)
Mungu alikubali kuwa kama moto uteketezao, ata waangamiza na kuwaangusha majitu. Mungu alisema: watu wakubwa, warefu, wana wa Waanaki. Kwa msaada wa Mungu Waisraeli waliwafukuza na kuwapoteza. Mungu aliwachukia majitu.
Vile vile kama Bwana alivyomwamuru Musa mtumishi wake, ndivyo Musa alivyomwamuru Yoshua; naye Yoshua akafanya vivyo; hakukosa kufanya neno lo lote katika hayo yote Bwana aliyomwamuru Musa. Wakati huo Yoshua akaenda na kuwakatilia mbali hao Waanaki watoke nchi ya vilima, kutoka Hebroni, na kutoka Debiri, na kutoka Anabu, na kutoka katika nchi yote ya vilima vilima ya Yuda, na kutoka katika nchi yote ya vilima vilima ya Israeli; Yoshua akawaangamiza kabisa na miji yao. Hawakusalia Waanaki hata mmoja katika nchi ya wana wa Israeli isipokuwa katika Gaza, na katika Gathi, na katika Ashdodi walisalia. (YOS 11:15, 21, 22)
Waanaki ni uzao wa majitu. Wakati wa kuwaangamiza majitu Yoshua alitekeleza agizo hilo Mungu aliyomwagiza Musa. Na hivi majitu walibaki nje ya maeneo ya Waisraeli.
Kisha alimpa huyo Kalebu mwana wa Yefune sehemu kati ya wana wa Yuda, kama Bwana alivyomwamuru Yoshua, maana ni Kiriath-arba, ni huyo Arba aliyekuwa babaye Anaki (Huo ndio Hebroni). Huyo Kalebu aliwafukuza watoke hapo hao wana watatu wa Anaki, nao ni Sheshai, na Ahimani, na Talmai, wana wa Anaki. (YOS 15:13, 14)
Arba na Anaki walikuwa majitu kama vile vile Sheshai, na Ahimani, na Talmai, wana wa Anaki. Kalebu alikutana na aliyowafahamu zamani. Kalebu amesema kwamba majitu ni chakula tu. Aliwafukuza mbali. Daudi aliambiwa na Biblia, kwamba katika yote alitimiza matakwa ya Mungu. (MDO 13:22) Alifanya mapenzi ya Mungu hata kuhusu majitu.
Tunasoma tena kuhusu Daudi na huyu Goliathi wa Gathi. Goliathi alikuwa jitu, kama unavyokumbuka. Urefu wake ulikuwa mita tatu.
Ikawa, hapo Mfilisti alipojiinua, akaenda akamkaribia Daudi, ndipo Daudi naye akapiga mbio, akalikimbilia jeshi ili akutane na yule Mfilisti. Daudi akatia mkono wake mfukoni, akatwaa humo jiwe moja, akalitupa kwa kombeo lake, akampiga Mfilisti katika kipaji cha uso; jiwe hilo likamwingilia kipajini, akaanguka chini kifudifudi. Hivyo Daudi akamshinda yule Mfilisti kwa kombeo na jiwe, akampiga Mfilisti akamwua; walakini Daudi hakuwa na upanga mkononi mwake. Hivyo Daudi akapiga mbio, akasimama juu ya Mfilisti, akautwaa upanga wake, akaufuta alani mwake, akamwua, akamkata kichwa kwa upanga huo. Nao Wafilisti walipoona ya kuwa shujaa wao amekufa, wakakimbia. (1SAM 17:48-51)
Ndivyo alivyoenenda Daudi aliyependeza moyo wa Mungu. Daudi alimwua jitu Goliathi. Hata watumishi wake pia.
Basi kulikuwa na vita tena kati ya Wafilisti na Israeli; Daudi akashuka mpaka Gobu, na watumishi wake pamoja naye, akapigana na Wafilisti; naye Daudi akaishiwa na nguvu. Naye Ishi-benobu, aliyekuwa mmojawapo wa Waferai, ambaye uzito wa mkuki wake ulikuwa shekeli mia tatu za shaba kwa uzani, naye amejifungia upanga mpya, alijaribu kumwua Daudi. Lakini Abishai, mwana wa Seruya, akamsaidia, akampiga Mfilisti, akamwua. Ndipo watu wa Daudi wakamwapia, wakasema, Wewe hutatoka tena pamoja nasi kwenda vitani, usije ukaizima taa ya Israeli. Ikawa baada ya hayo, kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; ndipo Sibekai, Mhushathi, alipomwua Safu, aliyekuwa mmojawapo wa Warefai. Kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; na Elhanani, mwana wa Yairi, Mbethlehemi, alimwua Goliathi, Mgiti, ambaye mti wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumaji. Kulikuwa na vita tena huko Gathi; ambako kulikuwa na mtu mrefu sana, mwenye vidole sita katika kila mkono, na vidole sita katika kila mguu, jumla yake ishirini na vinne; yeye naye alizaliwa kwa Mrefai. Naye huyo alipowatukana Israeli, ndipo Yonathani, mwana wa Shama, nduguye Daudi, akamwua. Hao wanne walizaliwa kwake huyo Mrefai wa Gahti; wakaanguka kwa mkono wa Daudi, na kwa mikono ya watumishi wake. (2SAM 21:15-22)
Warefai walikuwa kabila la majitu. Tulisoma majina ya majitu: Ishi-benobu, Safu wa Warefai, Goliathi. Katika mistari hii tunaona tabia za hao majitu na jinsi Mungu alivyowafikiria. Ishi-benobu alinuia kumwua Daudi aliyekuwa amechoka, lakini Abishai, mtoto wa dada yake Daudi alimwua yule jitu na hivyo akaokoa maisha ya mjomba wake.
Sibekai alimwua Safu. (1NYA 20:4). Elhanani alimwua Goliathi wa Gathi, aliyeitwa kwa jina jingine, Lahmi katika kitabu cha NYAKATI. (1NYA 20:5). Yeye alikuwa amechukua jina la nduguye Goliathi, aliyeuawa na Daudi. Daudi alimwua Goliathi akiwa kijana kwa jiwe na kombeo. (1SAM 17). Huyu jitu mwenye vidole vya mguuni sita na vidole vya mkononi sita aliuawa na Yonathani kijana wa ndugu yake Daudi. Benaya, mtu hodari wa Daudi, katika vita pia alikuwepo katika kuwaangamiza majitu.
asalaaam kudo