Mfalme Zumaridi, Mama huyu ni nani na kwanini Serikali imemuacha tu?

Mfalme Zumaridi, Mama huyu ni nani na kwanini Serikali imemuacha tu?

Hatumii Biblia mkuu yeye anatumia kitabu chake
yupo wrong from the beginning,Hairuhusiwi mwanamke kuwa mchungaji,muhubiri,muinjiristi wala shemasi hawajawahi kuwepo kwenye biblia,kwa lugha nyingine mwanamke haruhusiwi kusimama madhabahuni na akawafundisha wanaume,wanawake sababu yeye si kichwa,yeye alidanganywa mwanzo
 
siku za mwisho watu watakua wenye kupenda miujiza na ndio itawapoteza wengi
 
Kwa mara ya kwanza nimeona video yake moja YouTube leo ndio nika search kujua zaidi, Mungu awahurumie sana maana hata hatumii akili nyingi kuwapotosha, na yeye anajiita mungu/mfalme etc. alafu waumini wake wanatoa ushuhuda na kukiri kuwa wamesema uongo!! ( eg niliitwa nikawaambia sina nauli na nauli nilikua nayo kwa vile nilikua sitaki kwenda!! Mwingine akasema nilisema mganga ndio aliyeniponya lakini nilikuja kwa mfalme zumaridi akaniponya) Biblia inasema shetani ni baba wa uongo!! That woman is a witch in a high different level, if she do not change she will have a very special place in hell.
Not only in hell

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Agent wa shetani huyooo.. Hapo anakula hela ya bureeeeeeee, serikali ingebidi ithibiti sana hizi dini, Rwanda wameweza, sisi sijui kwanini tunawaachia, tungewadhibiti hawa, wanawapoteza kabisaa wananchi
 
Kuna wawili juzi wametoa ushuhuda wakwanza kakutana na Bob Nestor Marley,the second one amekutana na kanumba live.eti Bob anatambua uwepo wa mungu chini ya jua aitwae zumaridi.🤣🤣🤣🤣kwekwekwe
 
‎Anaandika Mathew Mathayo‎

Kinachoonekana hapa, sio movie wala maigizo.
Hii ni halisi, huyu mama anayejiita mungu Zumaridi, huwa anaingiwa na Pepo mchafu, akishamwingia ndipo anaanza kuweweseka.

Kama uliwahi kuona movie za mazombi ndivyo Kanisani kwake, watu wote mpaka wapambe wake hugeuka mazombi.

Na anapokushika akakugusa kichwa anakuambukiza uzombi, nawe ukimshika mwenzako unamwambukiza uzombi hivyo hivyo mpaka Watu wote muwe mazombi, ndipo Pepo huyu ajiitaye mfalme Zumaridi, akiwa katika mwili wa mama huyu Diana, anaanza kuwahubiria.

Kumbuka mpaka uwe zombie ndipo utaweza kusikilizana naye, kila atachosema utaitikia tu
Utafanya tuu.

Wangapi walishaona ule wimbo wa Mike Jackson
Unaitwa [emoji1733] The Thriller.
Basi wale mazombie ndio huwa hivi.

Na huyu mama, anadai kuwa
Mike Jackson yupo kwake mwanza pamoja na akina
Kanumba
Sharo Milionea
Albert Mangwea
Rais wa kwanza wa Marekani George Washington
Rais wa kwanza wa chini.
Adolf Hitler
Bob Marley
Lucky Dube
2Pac
Ruge Mutahaba
Ephrahim Kibonde
Fanuel Sedekia
Mwalimu Nyerere
Edward Sokoine
Na wengineo wengi
Akina Mez B, aliyeimba kikuku cha mama roda.
Amina Chifupa nk.

Anasema wapo kwake, ipo siku atawadhiririsha katika mwili wa nyama, wataonekana live.

Mpendwa kama waamini hili ni Pepo,
Sambaza video hii ziwafikie Watumishi Wa Mungu wa Kweli ili Kanisa liombe na kufunga kwa ajili ya Pepo huyu, anayepoteza Roho za Watu.

Yuko wapi Eliya wa Leo?
Apambane na Bahari na manabii wake?

Ni huzuni kuona Tapeli huyu anaachiwa uhuru huku akitesa Watu kwa kuwavika mapepo.

Share video hii, mtumie
Mchungaji wako naye pia
Askofu pia
Shemasi pia
Wazee wa kanisa pia
Wainjilisti pia
Na kila Mtu wa Mungu mwenye uchungu na Jina la Mungu wa Mbinguni.

 
Angekuwa mzungu au mwarabu huenda mngeamini. Walau naye kaanzisha dhehebu la waafrika maana waafrika tu ndiyo tulikana madhehebu yetu na kuanza kufuata ya weupe na ndiyo maana ni bara maskini kuliko yote. Waindi wana madhehebu yao, waarabu pia, wachina, wazungu sisi ni wazee wa kucopy na tunajifanya tunaujua Ukristo na Uislam kuliko hata waanzilishi.
Go Zumaridi japo mimi siwezi kuwa muumini wako
 
Back
Top Bottom