‘Mfalme Zumaridi’, wenzake wafikishwa Mahakamani, akwama kupata dhamana

‘Mfalme Zumaridi’, wenzake wafikishwa Mahakamani, akwama kupata dhamana

Ninyi waandishi wa habari na makamera yenu, mnapiga picha popote ili mpate udaku wa kuuza magazeti yenu
🙆‍♂️ Mtu aliwa hoi hospitali anapbania uhai wake

🙆‍♂️Mtu akishafariki yupo kwenye jeneza

🙆‍♂️Mtu akipata ajali ya kutisha

🙆‍♂️Mtu akiwa kwenye mimbari ya mahakama akipigania haki na uhuru wake

KAMWE KAMA UMELELEWA MELEZI YA BABA NA MAMA USIWAPIGE PICHA
 
Mfme HV nilwaza tu ikiwa huyu Ni bint wangu careen ndio awe anafanya shughuki hz za kukusanya watu na kusafirisha watu kinyume na sheria mban nitaona aibu Kama mzaz
 

Diana Bundala maarufu kama 'Mfalme Zumaridi' na wenzake 83 leo wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali ya mashtaka yanayowakabili.

Zumaridi na wenzake wanakabiliwa na makosa matatu ikiwamo ya usafirishaji haramu wa binadamu, shambulio la kudhuru mwili na kuzuia maofisa wa Serikali kutimiza wajibu wao.

Wakati wa kuwasili ndani ya chumba cha Mahakama Zumaridi ameonekana akiwa amejifunika na kitenge wakati wote kisha akalazimika kukiondoa baada ya kupanda kizimbani kusomewa maelezo hayo.

Hata hivyo, washtakiwa hao hawakusomewa maelezo ya awali ya mashtaka yanayowakabili kutokana na Hakimu Mkazi mwandamizi, Monica Ndyekobora ambaye ndiyo mwenye mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo kutokuwepo leo mahakamani jambo lililosababisha mashauri hayo kusikilizwa na Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza, Stela Kiama.

Washtakiwa baada ya kufikishwa mahakamani wamesomewa mashtaka yanayowakabili na wakili wa Serikali Mwandamizi anayeendesha mashtaka hayo, Emmanuel Luvinga akishirikina na Gisela Bantulaki.

Katika shauri hilo, kuna mashtaka matatu yanayowakabili washtakiwa hao ambayo ni kesi ya jinai namba 11/2022 ambayo ni usafirishaji haramu wa binadamu inayomkabili mfalme Zumaridi peke yake, kesi ya jinai namba 10/2022 ambayo ni kufanya shambulio la kudhuru mwili kwa lengo la kuzuia maofisa wa serikali kutimiza wajibu wao linalomkabili Zumaridi na wenzake 8.

Nyingine ni kesi ya jinai namba 12/2022 inayomkabili mhubiri huyo na wenzake 83 ambayo ni kufanya kusanyiko lisilo rasmi.

Baada ya Washtakiwa kusomewa mashtaka hayo, wakili wa utetezi, Erick Mutta aliwasilisha maombi ya dhamana kwa washtakiwa wanane wanaoendelea kusota rumande na mhubiri huyo ambayo yalikubaliwa na mahakama hiyo baada ya washtakiwa kukidhiri vigezo na masharti ya dhamana.

Kwa upande wake, Mfalme Zumaridi kutokana na kukabiliwa na kesi ya usafirishaji haramu wa binadamu isiyo na dhamana anaendelea kusota rumande na washtakiwa wenzake nane ambao hawajakidhi vigezo vya kupewa dhamana.

Shauri hilo limeahirishwa hadi Aprili 4, mwaka huu litakapoitwa kwa ajili ya kusomwa maelezo ya awali kwa washtakiwa.

Katika hatua nyingine, wakili wa utetezi Erick Mutta ameiambia mahakama hiyo kwamba, mshtakiwa namba 67 (Elias Joseph) ameshindwa kufika mahakamani hapo kutokana na maofisa kutoka Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) kufika ofisi kwake kwa ajili ya kumfanyia ukaguzi.

Amesema mshtakiwa namba 38 (Maria Joseph) ameshindwa kufika mahakamani hapo kutokana na kulazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando akipatiwa matibabu ya majeraha aliyopata wakati wa ukatamaji uliofanywa na maofisa wa Jeshi la Polisi mkoani humo.

Pia amesema mshtakiwa namba 84 (Kanyangi Mary) na 68 wameshindwa kuhudhuria shauri hilo kutokana na kuhudhuria matibabu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mwanza ya Sekou Toure.

Chanzo: Mwananchi

Tatizo Zumaridi alividharau vyombo vya dola bila kujua Ni mtego.
 

Diana Bundala maarufu kama 'Mfalme Zumaridi' na wenzake 83 leo wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali ya mashtaka yanayowakabili.

Zumaridi na wenzake wanakabiliwa na makosa matatu ikiwamo ya usafirishaji haramu wa binadamu, shambulio la kudhuru mwili na kuzuia maofisa wa Serikali kutimiza wajibu wao.

Wakati wa kuwasili ndani ya chumba cha Mahakama Zumaridi ameonekana akiwa amejifunika na kitenge wakati wote kisha akalazimika kukiondoa baada ya kupanda kizimbani kusomewa maelezo hayo.

Hata hivyo, washtakiwa hao hawakusomewa maelezo ya awali ya mashtaka yanayowakabili kutokana na Hakimu Mkazi mwandamizi, Monica Ndyekobora ambaye ndiyo mwenye mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo kutokuwepo leo mahakamani jambo lililosababisha mashauri hayo kusikilizwa na Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza, Stela Kiama.

Washtakiwa baada ya kufikishwa mahakamani wamesomewa mashtaka yanayowakabili na wakili wa Serikali Mwandamizi anayeendesha mashtaka hayo, Emmanuel Luvinga akishirikina na Gisela Bantulaki.

Katika shauri hilo, kuna mashtaka matatu yanayowakabili washtakiwa hao ambayo ni kesi ya jinai namba 11/2022 ambayo ni usafirishaji haramu wa binadamu inayomkabili mfalme Zumaridi peke yake, kesi ya jinai namba 10/2022 ambayo ni kufanya shambulio la kudhuru mwili kwa lengo la kuzuia maofisa wa serikali kutimiza wajibu wao linalomkabili Zumaridi na wenzake 8.

Nyingine ni kesi ya jinai namba 12/2022 inayomkabili mhubiri huyo na wenzake 83 ambayo ni kufanya kusanyiko lisilo rasmi.

Baada ya Washtakiwa kusomewa mashtaka hayo, wakili wa utetezi, Erick Mutta aliwasilisha maombi ya dhamana kwa washtakiwa wanane wanaoendelea kusota rumande na mhubiri huyo ambayo yalikubaliwa na mahakama hiyo baada ya washtakiwa kukidhiri vigezo na masharti ya dhamana.

Kwa upande wake, Mfalme Zumaridi kutokana na kukabiliwa na kesi ya usafirishaji haramu wa binadamu isiyo na dhamana anaendelea kusota rumande na washtakiwa wenzake nane ambao hawajakidhi vigezo vya kupewa dhamana.

Shauri hilo limeahirishwa hadi Aprili 4, mwaka huu litakapoitwa kwa ajili ya kusomwa maelezo ya awali kwa washtakiwa.

Katika hatua nyingine, wakili wa utetezi Erick Mutta ameiambia mahakama hiyo kwamba, mshtakiwa namba 67 (Elias Joseph) ameshindwa kufika mahakamani hapo kutokana na maofisa kutoka Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) kufika ofisi kwake kwa ajili ya kumfanyia ukaguzi.

Amesema mshtakiwa namba 38 (Maria Joseph) ameshindwa kufika mahakamani hapo kutokana na kulazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando akipatiwa matibabu ya majeraha aliyopata wakati wa ukatamaji uliofanywa na maofisa wa Jeshi la Polisi mkoani humo.

Pia amesema mshtakiwa namba 84 (Kanyangi Mary) na 68 wameshindwa kuhudhuria shauri hilo kutokana na kuhudhuria matibabu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mwanza ya Sekou Toure.

Chanzo: Mwananchi
Hatimaye anayejiita MUNGU mahakamani,hata hivyo huu upuuzi uliachwa muda Sana!
 
mungu kukosa dhamana.. inasikitisha
 
Ni upumbavu pili mtuhumiwa ana mali nyingi tena zisizohamishika kwann zisitumike kama dhamana.
Pili hili la hakimu husika kutokuwepo siku ya kesi husika, kwann asiwepo nani anabeba hii Dhamana ya mtu kupigwa tarehe tena hadi hakimu awepo.
Wabongo tuache ujuaji kidogo, maelezo yanasema kesi yake ya jinai haina dhamana wewe unataka apewe dhamana.

Labda icho unachokiomba ulishawahi kukisikia kinafanyika wapi? Mtu anakesi ya jinai alafu anapewa dhamana.

Sisi kilakitu nikulalamika tu, angepewa dhamana tungelalamika kwanini apewe dhamana kwa kesi ya jinai, amenyiwa bado tunalalamika vilevile
 
Wengi tunaamini mafundisho yake yanapingana na Mungu lakini tuwe waangalifu tusijipe kazi ya Mungu ya kumhukumu kutumia sheria zetu za Duniani.
Kama kumweka mtu rumande kwenye mrundikano wa watu na maisha mabovu kama ya mifugo sio lazima, basi huo ni uonevu ambao hata huyo Mungu hapendi.
 
Wabongo tuache ujuaji kidogo, maelezo yanasema kesi yake ya jinai haina dhamana wewe unataka apewe dhamana.

Labda icho unachokiomba ulishawahi kukisikia kinafanyika wapi? Mtu anakesi ya jinai alafu anapewa dhamana.

Sisi kilakitu nikulalamika tu, angepewa dhamana tungelalamika kwanini apewe dhamana kwa kesi ya jinai, amenyiwa bado tunalalamika vilevile
Sasa wewe unaona hizo kesi tatu zina point za kumtia hatiani?
Hio ya usafirishaji haramu si hadi wapatikane ushahidi
 
Sasa wewe unaona hizo kesi tatu zina point za kumtia hatiani?
Hio ya usafirishaji haramu si hadi wapatikane ushahidi
Kwa uelewa wangu ni kuwa kesi yake itaendelea kusikilizwa akitokea rumande kwa sababu haina dhamana.

Endapo ushahidi usipothibitisha anayo hatia basi ataachiwa huru. Ila kesi kesi yake haitosikilizwa akitokea nyumbani haina dhamana, labda wamfutie ilo shitaka la jinai abaki na hayo mengine
 
Wengi tunaamini mafundisho yake yanapingana na Mungu lakini tuwe waangalifu tusijipe kazi ya Mungu ya kumhukumu kutumia sheria zetu za Duniani.
Kama kumweka mtu rumande kwenye mrundikano wa watu na maisha mabovu kama ya mifugo sio lazima, basi huo ni uonevu ambao hata huyo Mungu hapendi.
Mungu
Kwa uelewa wangu ni kuwa kesi yake itaendelea kusikilizwa akitokea rumande kwa sababu haina dhamana.

Endapo ushahidi usipothibitisha anayo hatia basi ataachiwa huru. Ila kesi kesi yake haitosikilizwa akitokea nyumbani haina dhamana, labda wamfutie ilo shitaka la jinai abaki na hayo mengine
Ni uonevu lakini,mbona waganga wa kienyeji waharibu Sana Maisha ya watu na hata ukienda kwenye majumba yao watu wamekusanyika bila kibali,wao mbona awakamatwi
 
Naona watuhumiwa wapigwa sana sasa hao ni kina mama uwe mwanaume ni kuvunjana miguu kma yule wa mauaji ya msuya.
Wenzako waligeuka makerubi, hawasikii maumivu wala amri walikuwa wanamlinda Mungu wao Zumaridi!! Wajinga ndio waliwao!!
 
Back
Top Bottom