Mfano siku ikibainika kula bila kumenya kunaongeza umri wa kuishi hadi miaka 200, tutajiona wajinga sana

Mbona ugali wa dona una virutubisho zaidi na watu wengi wanakoboa mahindi?
 
Unataka maisha marefu na hauna pesa, sa utakula nini?[emoji2377]
 
Kwa hiyo hadi sahivi tunaula huo mti au
Swali la kitoto sana hilo.
💥
Mwaka 1892 kuna mwizi wa kuku alifungwa 6miezi au alipe faini elfu50 baada ya kukiri kosa na mwezi uliopita mwaka huu, kuna jamaa kafungwa 6miezi kwa kosa kama lile la 1892.
 
Dunia inahangaika kuhakikisha idadi ya watu inapungua [rejea siri nyuma ya kovidi] na wewe unataka watu wabuni mbinu ya kuishi zaidi?

Hii tu miaka 80 ni mingi mno na inatosha sana, tuacheni tamaa…. wenzetu nao wanataka kuishi.
 
Hivyo virutubisho ni vipi ambavyo aliyekoboa mahindi havipati kwingine?
Kwa nini kuvipata kwingine kuwe ni issue?

Unaokota briefcase la hela, juu lina mabunda ya shilingi elfu kumi, ndani lina mabunda ya shilingi elfu moja.

Halafu unatupa mabunda ya shilingi elfu kumi ya juu yote.

Watu wakiuliza mbona unatupa hayo mabunda ya elfu kumi ya juu? Unauliza mabunda gani ambayo hayawezi kupatikana kwingine?

Ndiyo swali ulilouliza hapa.
 

Mfano wako haulandani.

Kwanza ifahamike tu ukiokota unapaswa kuripoti na si kufurahia kwa maana sio mali yako.

Ukiamua kutumia basi ujue unatumia kuwa kificho, hivyo utalazimika kufungua uchukue mabunda ya ndani kisha utupe hilo briefcase (ganda) ili upoteze ushahidi.

Dona is overrated, ni sawa tu na kubeza chips over ugali ilihali ni starch vile vile…. same wanga same hamirojo.
 
Kuna mdau kauliza kwani yeye nyani anaishi miaka mingapi?
 
Kuna mdau kauliza kwani yeye nyani anaishi miaka mingapi?
Sijui anaishi miaka mingapi ila maisha ni fumbo sana.Leo maeneo ya kibaruani imetokea ajali na kuua wafanyakazi wawili.Ajali imetokea mikumi, Morogoro baada ya lori kufeli breki lilipokuwa linateremsha mlima.

Likahama njia yake na kwenda kuwaparamia hao wafanyakazi mmoja pale pale akawa marehemu mwingine akawa amesagwa miguu kuanzia mapajani, dah, tumempeleka hospitali wakati wakiwa njiani kuelekea hospital kubwa morogoro mjini akawa amefariki. Jana nimefanya nao kazi hao jamaa na leo asubuhi walikuwa vizuri tu lakini ndani ya dakika tano jamaa ni marehemu dah maisha haya ni fumbo sana. Samahani kwa kutoka nje ya maada.
 
Wala kitimoto lost hawawezi kukuelewa Plus makange
 
Watu wa zaman hawakuishi miaka mingi isipokua walikuaga hawajui hata wamezaliwa lini unakuta mtu anamiaka 80 anasema anamiaka 100 muulize kazaliwa mwaka gan hata hajui
 
Kiongozi wangu Mungu mwenyewe ndo alipunguza umri wetu kuishi, inasemekana ni baada ya ulaji wa nyama kuruhusiwa
Wale watu walioishi miaka mingi hadi 900 hawakuwa wakila nyama. Baada ya gharika ndo nyama ikaruhusiwa na ndo ilikuwa mwanzo wa umri kupungua kwa umri.
Na hata wale walioanza kulishwa nyama walielekezwa kuwa kuna nyama safi na najisi, sisi tunasema usipotapika kula chochote

Mwanzo 6:1-8 BHN​

Binadamu walipozidi kuongezeka duniani na kuzaa wasichana, watoto wa kiume wa Mungu waliwaona hao wasichana wa watu kuwa ni wazuri, wakawachukua wale waliowapenda kuwa wake zao. Hapo Mwenyezi-Mungu akasema, “Roho yangu haitakaa ndani ya binadamu milele, maana yeye ni wa kufa tu. Basi, hataishi zaidi ya miaka 120.”

MWANZO 7​

Gharika kuu
1Mwenyezi-Mungu akamwambia Noa, “Ingia ndani ya safina wewe pamoja na jamaa yako yote, kwa maana, kati ya watu wote wanaoishi nyakati hizi zako, nimekuona wewe peke yako kuwa mwadilifu mbele yangu. 2Chukua pamoja nawe wanyama wote walio safi, dume na jike, saba saba; lakini wanyama walio najisi, chukua dume na jike, wawiliwawili. 3Vilevile chukua ndege wa angani dume na jike, saba saba, ili kuzihifadhi hai aina zao duniani. 4Baada ya siku saba, nitanyesha mvua nchini siku arubaini mchana na usiku, na kila kiumbe hai nilichokiumba duniani nitakiangamiza.” 5Noa akafanya yote kama Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru.
6Noa alikuwa na umri wa miaka 600 wakati gharika ilipotokea nchini. 7Noa, mkewe, wanawe na wake zao wakaingia ndani ya safina ili kuiepa gharika. 8Wanyama walio safi, wanyama walio najisi, ndege na viumbe vyote vitambaavyo, 9wawiliwawili, dume na jike, wakaingia ndani ya safina pamoja na Noa kama Mungu alivyomwamuru. 10Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaanza kuifunika nchi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…