DOKEZO Mfanyabiashara maarufu Arusha aibiwa Tsh. Milioni 100 kwenye akaunti ya Benki ya NMB

DOKEZO Mfanyabiashara maarufu Arusha aibiwa Tsh. Milioni 100 kwenye akaunti ya Benki ya NMB

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2016
Posts
753
Reaction score
1,812
Mfanyabiashara maarufu katika mikoa ya Arusha, Dar na Dodoma Joseph Kalugendo mkazi wa Moshoni jijini Arusha, ameibiwa fedha zake zaidi ya milioni 100 katika benki ya NMB tawi la Clock Tower Arusha na mtumishi wa benki hiyo.

Taarifa ambazo zimethibitishwa na Mfanyabiashara huyo amedai kuwa siku za usoni alienda katika benki hiyo kwa ajili ya kuchukua fedha ndipo alipopigwa na butwaa kukuta kitita hicho hakipo.

Meneja wa benki hiyo Kanda ya Kaskazini Praygod Mphuru alipohojiwa alikiri kuwepo kwa tukio hilo akidai tayari wamemsimamisha kazi mfanyakazi wao Samweli na kwamba suala hilo linafanyiwa kazi na kuomba suala hilo lisitangazwe.

Pia vigogo wa benki hiyo kwa sasa wanahaha kutafuta mchawi aliyetoa taarifa hizo kwa waandishi wa habari na tayari baadhi ya wafanyakazi wameitwa na kuhojiwa juu ya taarifa hizo za ndani kufika kwa wanahabari

Joseph ambaye hufanya biashara za bar na kusambaza vyakula kwenye kambi za jeshi anadaiwa kulundika kiasi hicho cha fedha kwa muda mrefu bila kutoa kiasi, na kwamba mfanyakazi huyo aliona huenda anayeimiliki alishakufa na kuanza kuchomoa kidogo kidogo na kufikia zaidi ya Tsh. Milioni 100.

Hata hivyo baada ya taarifa hizo kubainika uongozi wa benki ulifanya kikao kizito na kubaini kwamba mfanyakazi wao aliyefahamika kwa jina moja la Samweli ndiye aliyehusika na wizi huo kwa kuchomoa fedha hizo kidogo kidogo hadi kufikia hicho cha fedha.

Uongozi wa benki hiyo tayari umemsimamisha kazi lakini suala hilo bado lipo kimya huku Mfanyabiashara huyo akilalamikia hatima ya fedha zake, maana benki hiyo kuwa kimya na haimpi jibu linaloeweka namna ya kurejeshewa.

Screenshot_20230811_105217_WhatsApp.jpg
 
Hela ni zako alaf na bado zikuhangaishe.

Ukiwa mwingi wa Mambo hakun kinacho kushinda. Amtafute kibatala au guru yeyote pesa inarudi tena faida juu
FNB walishawahi mfanyia jamaa yangu hivyo hivyo kumchomolea pesa kibao kwenye account yake ya USD. Jamaa alikuwa kifungoni nje ya nchi. Alipotoka kaibuka kudai mpunga wake, mavi yaliwagonga chupi maana kipindi cha kifungo walimzungusha sana mkewe katika kufuatilia pesa.

Walimpa fidia ya 35% juu ya kile kiasi kilichopigwa kwa ombi kwamba asitangaze wala kwenda kwenye vyombo vya sheria. Baada muamala kusoma tu, jamaa akafunga na account yenyewe.
 
Bank ya NMB sio salama kabisa, matukio na malalamiko ya wizi ni mengi sana. Mimi mwenyewe ni muhanga wa kupigwa na hii Bank.

Serikali fanyeni uchunguzi kwenye hii Bank maana ni hatari sana, anzeni na pale Mbezi Beach Africana.

Ndomana matukio ya vifo vya wafanyakazi wa Bank ni vingi sababu ya haya mambo.

NMB nilihama muda sana.
 
Mfanyabiashara maarufu katika mikoa ya Arusha ,dar na Dodoma Joseph Kalugendo mkazi wa Moshoni jijini Arusha,ameibiwa fedha zake zaidi ya milioni 100 katika benki ya NMB tawi la Clock Tower Arusha na mtumishi wa benki hiyo.

Taarifa ambazo zimethibitishwa na Mfanyabiashara huyo amedai kuwa siku za usoni alienda katika benki hiyo kwa ajili ya kuchukua fedha ndipo alipopigwa na butwaa kukuta kitita hicho hakipo.

Meneja wa benki hiyo kanda ya kaskazini PRAYGOD MPHURU alipohojiwa alikiri kuwepo kwa tukio hilo akidai tayari wamemsimamisha kazi mfanyakazi wao SAMWELI na kwamba suala hilo linafanyiwa kazi na kuomba suala hilo lisitangazwe.

Joseph ambaye hufanya biashara za bar na kusambaza vyakula kwenye kambi za jeshi anadaiwa kulundika kiasi hicho cha fedha kwa muda mrefu bila kutoa kiasi kwamba mfanyakazi huyo aliona huenda anayeimiliki alishakufa na kuanza kuchomoa kidogo kidogo na kufikia zaidi ya sh,milioni 100.

Hata hivyo baada ya taarifa hizo kubainika uongozi wa benki ulifanya kikao kizito na kubaini kwamba mfanyakazi wao aliyefahamika kwa jina moja la SAMWELI ndie aliyehusika na wizi huo kwa kuchomoa fedha hizo kidogo kidogo hadi kufikia hicho cha fedha .

Uongozi wa benki hiyo tayari umemsimamisha kazi lakini suala hilo bado lipo kimya huku Mfanyabiashara huyo akilalamikia hatima ya fedha zake maana benki hiyo kuwa kimya na haimpi jibu linaloeweka namna ya kurejeshewa.View attachment 2714317
Kuchomoa hela kwenye akaunti ya mtu halafu jinai hiyo inafanywa na mtumishi wa bank ni wazi NMB si sehemu salama kuweka akiba
 
Back
Top Bottom