Mfanyakazi wa TRA akutwa amehifadhi pesa taslimu Tsh. Bilioni 7 nyumbani

Hivi hao wafanyakazi wa tra ni wote wanapesa mbon kuna jamaa yangu namjua hana cha maan au mfagiaji yule!
 
Hasa watumishi wa umma isee!
Kazi ya kubadili tabia za binadamu sio rahisi,, na hakuna kiongozi atakaejikita hayo majukumu akapendwa na wale anaowagusa.

Huko ulaya jaribu kuingilia mambo ambayo unaona investment risks, uone ma-bank, financial institution na hedge funds zitazokuvaa kuaribu uchumi.

Walau wao wamedhibiti everyday finance (za ndani ya serikali) not everywhere when it comes to tenders.

Sio sisi hata kwenye administration practices ni shida, worst huyu mama ndio anawawekea mazingira wezeshiiz.

Kuna mambo kama unaelewa dunia inavyozunguka, kwetu unakubali tuna utani mbaya. Sio shida serikali inavyofanyq mambo mambo tu bali kuendekeza unrealistic expectations zao za nchi inavyotakiwq kuendeshwa.

Kama ni maendeleo, Nagufuli alikuwa soft katika hatua za maendeleo na lazima kama nchi tupitie wakati wa kubadili fikra. Hiyo ni social development fact based on social development thinking, Hakuna njia nyingine wote walioendelea wamepitia hiyo phase na bado vita yso ilipo (na hakuna nchi iliyoweza tabia ya watu wote mpaka leo).

Sisi more than 95.% yetu tunadhani changes just happen, bile ya kubadili fikra za watu. Hiyo kazi ya kubadili fikra za watu sio rahisi nor popular but it has to be done.
 
I wish vijana wangeelewa hivyo. Huwa namshangaa ambaye mpaka leo hajauona umuhimu wa JPM katika dhana ya maendeleo ya TZ
 


Watanzania tunatumikia baadhi ya watawala wasiostahili sababu ya wizi na ubadhilifu wa mali ya umma.
Na hawa wezi hakuna wanachofanywa. Wanatuibia inaishia kuambiwa tumeibiwa. Inasikitisha na kufikirisha sana
 
Labda ameshitushwa na kubainika kwa jambo hilo!
 
Hii Nchi Viongozi wazalendo walikuwa wakina Mwl Nyerere tu, ambao kama ni nyumba ya maana wamekuja kujengewa na Serikali baada ya Kifo chake.

The rest wamebaki kuhubiri Uzalendo wa midomoni pamoja na kuvaa Scarfs za bendera kuonesha wao ni Wazalendo.

Aibu Kwa Mamlaka iliyowateua 🙌
 
Nashangaa takukuru wanafanya nini? Raisi awakumbushe majukumu yao akikaa kimya inaleta ukakasi ukiangalia wanavyokomaa na walipa kodi wadogo na kuua mitaji yao huku wao wakilijimbikizia mali inaleta hasira
Dawa ni ku riot tu hamna namna hawa jamaa wamezidi yani inafikia mahala wengine tunakua kama sio watumishi wa umma vijana wetu andamaneni mtuokoe na huu usenge hali ni mbaya mnooooo
 
Bilioni 7 ni milioni 7000.....tuseme ni noti za elf 10 na kazifunga ktk bunda za milioni 10, Kwa hyo 7000 gawa kwa 10 ni sawa na bunda 700....duh...ni stoo yote imejaa noti
Halafu majitu ya hivi unakuta ndugu kule kijijini wanapitia maisha ya shida sana lenyewe limehifadhi Noti ndani mpaka zinaliwa na panya!
 
Kwa huu mfumo wa kitapeli ni bora uibe tu hakuna namna
Ni bora? Kwahiyo hapo hiyo kauli yako ina msaada gani hata kama mfumo ni mbovu? Akili za wapi hızı mkuu mbona huwa nakuheshimu hapa jukwaani?

Ni bora hata ungetukana tujuwe umechukia au hata uongelee kuhusu solution.

Sasa hii kauli inanishangaza sana mkuu. Ina reflect hopelessness!
 
Nashangaa takukuru wanafanya nini? Raisi awakumbushe majukumu yao akikaa kimya inaleta ukakasi ukiangalia wanavyokomaa na walipa kodi wadogo na kuua mitaji yao huku wao wakilijimbikizia mali inaleta hasira
We nawe jinga jinga tu.....eti takukuru wanafanya kazi gani??? Kwani hujui takukuru ndo wala rushwa namba moja na wateja wao wakiwa hao tra ....
 
Hii ni bajeti ya Tarura mkoa mzima ,kwa zile barabara za changarawe😡😡 huyu ndio mhujumu uchumi sasa, sio zile kesi nyingine zilikuwa za kukomoana kipindi kile🤣🤣 tungetegemea huyu awe kisutu au korti ya mafisadi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…