Mfanyakazi wa TRA akutwa amehifadhi pesa taslimu Tsh. Bilioni 7 nyumbani

Mfanyakazi wa TRA akutwa amehifadhi pesa taslimu Tsh. Bilioni 7 nyumbani

Uanze kumfundisha mtoto gani kulinda rasilimali wakati anaona unavyobadilisha mipira hapo uwani kwako. Leo Range kesho Discovery keshokutwa Benz. Mtoto gani atakuelewa umwambie uzalendo ni kushika bomba kwenye Eicher
Uzalendo umebeba vitu vingi sana. Tukianza kuwafundisha uzalendo wa kuheshimu Mali za ndani nadhani hata za nje pia wataziheshimu vile vile
 
Uanze kumfundisha mtoto gani kulinda rasilimali wakati anaona unavyobadilisha mipira hapo uwani kwako. Leo Range kesho Discovery keshokutwa Benz. Mtoto gani atakuelewa umwambie uzalendo ni kushika bomba kwenye Eicher
Mfano halisi ni yule chipukizi wa singida fc, utamfundisha nini na anaona sajili mpya tu kila uchwao wa magari na wachezaji.
 
Kama mtu amepata nafasi kwa kuhonga unategemea anarudishaje? nchi ya kijinga sn hii wewe iba kwa nafasi yako maswala sijui ya uzalendo achana nayo kabisa vinginevyo utakuwa ni mjinga sn wenzako wanatajirika wewe unawaza uzalendo
Hahahahhaha kibaya zaidi wanaweza kukuua kabisa kama utakuwa mtu wa gozigozi
 
Kama anafanya biashara zingine mfano madini hizo ni pesa ndogo sana
Nyerere ndo maana alikataa hawa watumishi wa serikali kuwa wafanya biashara sababu aliona loopholes ambazo wangezitumia kujitajirisha kwa kivuli cha uofisa serikalini.

He was too smart in that idea ila mbaya zaidi wamepuuzwa. Nadhani katiba ijayo izingatie hilo. Mtu achague biashara au siasa na utumishi wa umma. Huwezi kuwa mwanasiasa na mfanyabiashara at the same time. Hili ndilo linachochea ubadhirifu wa mali za umma.
 
Sema kwa kuwa mifumo ya nchi yetu ni mibovu,hatafanywa kitu.

Shida wakubwa wake huenda wameiba matilioni na yeye ndie aliyefanikisha ukwapuaji huo.Hivyo ana watetezi wa kuzima hilo sooo.

Hawezi kuwa alikula peke yake.Nchi imeoza sana hii.

Hakuna uzalendo,mwananchi anaongezewa tozo bila taarifa halafu kuna watumishi wa umma wanamiliki pesa ndefu kuliko vipato vyao huku gharama ya maumivu ikirudi kwa mnyonge wa chini.

Mtu analipwa mshahara mzuri na bado anatuibia kummqe.Hii haikubaliki.Ndio maana nchi nyingine zisizotaka upuuzi huu wakikukuta wanakufilisi na wanakunyongelea mbali ili iwe fundisho kwa wengine.

Tunapigwa sana.

Naongeakwa uchungu sana kummqe.
 
Kuna mtu mmoja mpuuzi nilisoma bandiko lake Jana anadai eti, "Unaandamana mwisho uumie Kwa faida ya nani?"

Nilishangaa sana nikaona hapa mabadiliko itakuwa kitendawili.

Mimi nilifanya mageuzi kwenye chuo nilichokuwa nasoma ilinigharimu ila kizazi nilichoacha kilifurahia mabadiliko ya ghafla. Imagine chuo kikuu hakina facilities za kutosha mnahama na viti kwenye venues. Wifi Hamna mnahangaika na ma bundles na system ya usajili hakuna mnapanga foleni siku nzima mnasota kwenye mabenchi.

Yote haya yalifanyiwa changes kabla hata sijamaliza third year ila ni matatizo ambayo yalikuwepo toka naanza certificate management ikawa inaona sawa tu.
Hongera sana Mkuu Extrovert ni wachache sana hapa Tz wenye moyo kama huo. Wengi wabinafsi, anaona yeye anajitosheleza, wengine watajijua wenyewe.

watu wanaogopa sijui kuumia, kufa. Na hiyo ndiyo hofu walishaiweka hawa serikali. Kwamba atakayekaidi, atakutana na kipigo cha mbwa mwizi. Wataua Taifa zima? Pia ujiulize, mtu anayeng'ang'ania madaraka, mpaka anaua je ni madaraka tu au kuna kingine ndani ya hayo madaraka?

Acha tuendelee kuwa keyboard warrior. Iko siku kila mtu, ataamka kwake ajikute barabarani mwenyewe, yakiwafika shingoni.
 
Kuna mtu mmoja mpuuzi nilisoma bandiko lake Jana anadai eti, "Unaandamana mwisho uumie Kwa faida ya nani?"

Nilishangaa sana nikaona hapa mabadiliko itakuwa kitendawili.

Mimi nilifanya mageuzi kwenye chuo nilichokuwa nasoma ilinigharimu ila kizazi nilichoacha kilifurahia mabadiliko ya ghafla. Imagine chuo kikuu hakina facilities za kutosha mnahama na viti kwenye venues. Wifi Hamna mnahangaika na ma bundles na system ya usajili hakuna mnapanga foleni siku nzima mnasota kwenye mabenchi.

Yote haya yalifanyiwa changes kabla hata sijamaliza third year ila ni matatizo ambayo yalikuwepo toka naanza certificate management ikawa inaona sawa tu.
Sawa Fanya mageuzi Kwa nchi Sasa Ili ufe wengine wale pesa sio unaongelea kwenye shuka unataka nani akupambanie
 
Nyerere ndo maana alikataa hawa watumishi wa serikali kuwa wafanya biashara sababu aliona loopholes ambazo wangezitumia kujitajirisha kwa kivuli cha uofisa serikalini.

He was too smart in that idea ila mbaya zaidi wamepuuzwa. Nadhani katiba ijayo izingatie hilo. Mtu achague biashara au siasa na utumishi wa umma. Huwezi kuwa mwanasiasa na mfanyabiashara at the same time. Hili ndilo linachochea ubadhirifu wa mali za umma.
Madhara yake ndio yamezaa huu ufisadi wale watumishi waliokuwa waaminifu na wazalendo serikali iliwatupa wakawa na maisha magumu zaidi ya mbwa wengi walikufa kwa stress za kubezwa na kuchekwa si ulijifanya mnoko kipo watu hata sh elf 2 huna, matokeo yake wakajaa sana chuki na kuwapandikiza watoto wao roho za wizi na upigaji ili watoto wao wasijeishi maisha mabovu kama wao.
 
Back
Top Bottom