Mfumo wa masaa Afrika Mashariki

Mfumo wa masaa Afrika Mashariki

Sijui kama ilishawahi kujadiliwa humu lakini nimekuwa najiuliza sana na kukosa majibu, kwanini mfumo wa masaa wa Afrika Mashariki upo tofauti na sehemu zingine duniani? Sehemu zote siku inaanza saa 6 (0000) usiku lakini kwetu inaanza saa 1 (0700) asubuhi. Kuna sababu ya hii tofauti mahali?

Na tulipatia wapi huu mfumo na kwa nini? Tujiulize wanabodi na tunafaidika nini au tunapata hasara gani kwa hii? Karibuni kwa tafakuri.
Sababu ni mtazamo wa kifalsafa kuhusu siku inaanza wakati gani na kwa sababu gani?
Kwa falsafa za kizungu siku uanza midnight sijui ndio "usiku wa manane"!!!
Kwa falsafa za kiafrika siku inaanza kwa mwonekano wa jua ndio maana hiyo 7:00 a.m tunasema saa 1 maana yake ni saa 1 tokea jua limeonekana, tokea siku imeanza.
Wenzetu wanavyosema 7 o'clock wanamaanisha masaa 7 tokea siku imeanza!
Tatizo ya falsafa yetu ni kwamba pamoja na kusema saa 1 lkn bado tunaandika 7! Kwanini kama ni saa 1 mshale wa saa usionyeshe hiyo 1! Tunaonekana wajinga unaona 7 lkn unasema saa 1!!!!!!
 
Sijui kama ilishawahi kujadiliwa humu lakini nimekuwa najiuliza sana na kukosa majibu, kwanini mfumo wa masaa wa Afrika Mashariki upo tofauti na sehemu zingine duniani? Sehemu zote siku inaanza saa 6 (0000) usiku lakini kwetu inaanza saa 1 (0700) asubuhi. Kuna sababu ya hii tofauti mahali?

Na tulipatia wapi huu mfumo na kwa nini? Tujiulize wanabodi na tunafaidika nini au tunapata hasara gani kwa hii? Karibuni kwa tafakuri.
Watanzania kukipambazuka tu tunaanza kulalamika

Naona unalalamikia masaa🤣
 
Sijui kama ilishawahi kujadiliwa humu lakini nimekuwa najiuliza sana na kukosa majibu, kwanini mfumo wa masaa wa Afrika Mashariki upo tofauti na sehemu zingine duniani? Sehemu zote siku inaanza saa 6 (0000) usiku lakini kwetu inaanza saa 1 (0700) asubuhi. Kuna sababu ya hii tofauti mahali?

Na tulipatia wapi huu mfumo na kwa nini? Tujiulize wanabodi na tunafaidika nini au tunapata hasara gani kwa hii? Karibuni kwa tafakuri.
Umeandika ukiwa umelewa?
 
Muda ni dhana ya kufikirika, hivyo jamii mbalimbali zilidevelop concept ya muda inayofit mazingira na mahitaji yao.

Wabongo siku yetu inaanza asubuhi, wengine siku zao zinaanza usiku, jioni n.k

Kuanza na kuisha kwa siku kumekuwa influenced na mawio na machweo ya jua, maamuzi ya kisiasa (wafalme wa zamani).

Kwetu, asubuhi ni muda wa kuamka. Kuna nchi jua linawaka mpaka masaa 18.
Kuna sehemu za dunia, zinakuwa na giza kwa miezi kadhaa mfululizo hawaoni jua, kisha kunakuwa na mchana kwa miezi kadhaa bila Giza wala nini.

Kimsingi, dhana ya muda ni sahihi kwa kila jamii kulingana na mahitaji yake, hakuna anayekosea, ila tu Kuna standardization iliyofanywa kimataifa ili dunia ielewane kuhusu muda.
 
Muda ni dhana ya kufikirika, hivyo jamii mbalimbali zilidevelop concept ya muda inayofit mazingira na mahitaji yao.

Wabongo siku yetu inaanza asubuhi, wengine siku zao zinaanza usiku, jioni n.k

Kuanza na kuisha kwa siku kumekuwa influenced na mawio na machweo ya jua, maamuzi ya kisiasa (wafalme wa zamani).

Kwetu, asubuhi ni muda wa kuamka. Kuna nchi jua linawaka mpaka masaa 18.
Kuna sehemu za dunia, zinakuwa na giza kwa miezi kadhaa mfululizo hawaoni jua, kisha kunakuwa na mchana kwa miezi kadhaa bila Giza wala nini.

Kimsingi, dhana ya muda ni sahihi kwa kila jamii kulingana na mahitaji yake, hakuna anayekosea, ila tu Kuna standardization iliyofanywa kimataifa ili dunia ielewane kuhusu muda.

Hii inaleta maana sana kiongozi, ila tunabadilisha siku alfajiri lakini tarehe inabadilika midnight??
 
Sio hitimisho ni swali, toa uelewa wako kiongozi! Dunia ina mambo mengi sana hamna mjuvi wa kila kitu. Asubuhi sisi tunasema ni saa moja wenzetu wanasema ni Seven lakini pia saa zetu zinasoma 7 sio 1
Kijana mtafutie dogo yoyote wa dldarasa la 7 aliefaulu vizuri geography. Atakuelewesha hasa hawa waliomaliza juzi.
 
Unamaanisha kwetu tarehe inabadilika saa 1 asubuhi?
Kuna tofauti kubwa ya siku na tarehe! hapa hoja ilikuwa kwanini 7:00 a.m Afrika Mashariki tunasema ni saa 1 asubuhi!! Kwa falsafa ya Kiyahudi kwa mfano siku mpya uanza saa 9 alasiri ingawaje tarehe ni ile ile. Mfano mzuri hapa ni Wasabato kuanzia Ijumaa adhuhuri hawafanyi kazi kuheshimu Sabato, maana yake Sabato imeshaingia ingawaje bado tupo Ijumaa kwa sisi wengine na tarehe haijabadilika. Yesu alikufa Ijumaa saa 9, siku ya kwanza, akashinda kaburini siku 1 tu ya Jumamosi! Wakristu hufundisha kwamba alikaa kaburini siku 3, hiyo haina maana ya masaa 72 ya kizungu! Kwahiyo kuna tofauti kati ya siku na tarehe!
 
Kuna tofauti kubwa ya siku na tarehe! hapa hoja ilikuwa kwanini 7:00 a.m Afrika Mashariki tunasema ni saa 1 asubuhi!! Kwa falsafa ya Kiyahudi kwa mfano siku mpya uanza saa 9 alasiri ingawaje tarehe ni ile ile. Mfano mzuri hapa ni Wasabato kuanzia Ijumaa adhuhuri hawafanyi kazi kuheshimu Sabato, maana yake Sabato imeshaingia ingawaje bado tupo Ijumaa kwa sisi wengine na tarehe haijabadilika. Yesu alikufa Ijumaa saa 9, siku ya kwanza, akashinda kaburini siku 1 tu ya Jumamosi! Wakristu hufundisha kwamba alikaa kaburini siku 3, hiyo haina maana ya masaa 72 ya kizungu! Kwahiyo kuna tofauti kati ya siku na tarehe!
Hujaeleweka umehubiri biblia badala ya kujibu swali
 
Yes ndio kwa nini sisi tuna alfajiri/adhuhuri asubuhi mchana jioni/alasiri usiku wakati dunia ina AM na PM tu? Ndio nachotaka kujifunza au kupata uelewa! Sisi ni special au tuna sababu zingine?
Nadhani ni kutokana na utofauti wa lugha. Ni sawa na ukiuliza kwanini meza wao wanaita table. Kisha tablet kishikwambi na kumeza ni swallow.

Zaidi ya hapo sijui
 
Nadhani ni kutokana na utofauti wa lugha. Ni sawa na ukiuliza kwanini meza wao wanaita table. Kisha tablet kishikwambi na kumeza ni swallow.

Zaidi ya hapo sijui

So siku yetu imekuwa na parts 4 za mataifa mengine parts 2 tu so inaondoa mantiki ya lugha! Ingekuwa Usiku na mchana tu ingemake sense, sasa alfajiri, adhuhuri alasiri/mchana na jioni inakuwa tofauti kidogo!
 
Kijana mtafutie dogo yoyote wa dldarasa la 7 aliefaulu vizuri geography. Atakuelewesha hasa hawa waliomaliza juzi.

Wabongo bana, ndo maana tunafeli sana, sasa hapa nini hiki? Why nikatafute mtu mwingine tena? Kwa kuwa una uelewa finyu? Kuna threads nyingi tu pita kule kwa kulana kimasikhara
 
Tofauti iko kwenye muda kirejea (usiku wa manane au macheo).

Muda wa saa 4 asubuhi katika lugha ya Kiingereza inasemwa zimepita saa 10 baada ya usiku wa manane (ten am), wakati Kiswahili inasemwa zimepita saa 4 baada ya macheo/mapambazuko (saa nne asubuhi).

Utaona wazi kwamba hakuna tofauti yoyote ya muda, ila namna tu ya urejewaji muda husika.
 
Back
Top Bottom