DOKEZO Mfumo wa Mtandao kuomba uhamisho Serikalini ni tatizo, unatakiwa kuboreshwa

DOKEZO Mfumo wa Mtandao kuomba uhamisho Serikalini ni tatizo, unatakiwa kuboreshwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Kuna changamoto ya Mfumo wa Employee Self Service (ESS), Watumishi wa Serikali tunateseka.

Nimeanza kutumia Mfumo kwa ajili ya kuomba Uhamisho wa kuhama kutoka ‘Taasisi A’ kwenda ‘Taasisi B’ kwa takribani miezi sita sasa tangu kuanza kwa Mfumo huo rasmi bila ya mafanikio huku nikikumbana na changamoto zifuatazo:

1. Mfumo unaonekana hautambui Professional za Watu (Sifa za Kielemu), badala yake unatambua Vyeo tu vya Kimuundo kwa Taasisi husika.

Hali hiyo inaleta ugumu kwa Watu wenye sifa za Kielemu kuingia kutumia Mfumo kuomba uhamisho kutoka Taasisi moja kwenda nyingine ambako pia sifa za Kielemu anazo za kufanyakazi Taasisi anayotaka kwenda.

Kwenye kipengele hiki Mtumishi akiingia kwa ajili ya kuanzisha maomba tu kwenye Mfumo katika zile menu zinazohusu Uhamisho Mfano:

i. Request Vacancy

ii. Transfer Request zinamletea message inayosomeka: "Designation not found on Destination Organization"

Hivyo, inatuwia vigumu Watumishi kuhama kwenda kutafuta changamoto nyingine nje ya taasisi tulizopo, pia kuongeza hali na kuufanya ubongo uchangamke zaidi na kujifuza vitu vipya.

Screenshot 2024-04-02 075151.jpg

Huu ni mfano ninapokuwa nafanya mchakato wa uhamisho
2. Baadhi ya Watumishi imeonekana wakifuatilia mara kwa mara katika Ofisi za Utumishi bila ya Mafanikio.

Ombi letu ni waweze kutatua Mfumo kuwa imara kama ilivyo kwa matumizi mengine ya kimfumo, vinginevyo itakuwa haina maana kwa hiki walichofanya kuhamishia shughuli katika njia ya Mtandao.

Kingine mfumo unatambua elimu uliyoingia nayo tu wakati taarifa zako zinaingizwa, ukijiendeleza ukataka kuboresha taarifa za ziada hilo haliwezekani, mfumo unakataa.

Malalamiko yalikuwa mengi wakati mfumo wa analojia ulipokuwa unatumia, sasa hii solution nayo imekuwa ni sehemu ya tatizo.

Kuna baadhi ya nafasi ukiomba kwa ajili ya uhamisho unajibiwa “Vacancy is not Available” yaani hakuna nafasi, hata uombe kwenye taasisi ambayo unajua ina uhaba wa Watumishi majibu yatakuwa ni hayohayo.

Just imagine Mwalim au nurse anaambiwa Vacancy is not available? Ni wapi huko ambako hakuna mahitaji ya hao Watumishi.

Pia soma:
 
Mkuu, Toka huu mfumo umezinduliwa Mnamo 2023 mwishoni ni ukweli kuwa haukuwahi kufanya kazi Kwa matakwa ya WATUMISHI wengi hasa kipengele Cha Transfer kutoka taasisi moja kwenda nyingine.

But Kuna barua hii inaeleza kuwa mfumo itaanza kazi tarehe 01/04/2024.
Soma hapa kujiridhisha
 

Attachments

  • IMG-20240331-WA0000.jpg
    IMG-20240331-WA0000.jpg
    147.1 KB · Views: 83
  • IMG-20240331-WA0007.jpg
    IMG-20240331-WA0007.jpg
    93.4 KB · Views: 87
Mkoa wa Mara, Wilaya ya Rorya zaidi ya watumishi wengi wa umma hasa walimu wamenyimwa mshahara wa mwezi wa tatu mpaka leo hii sababu ya huu mdumo kuwa hawakuweka task na subtask na hata baada ya kuweka mpaka leo hii hawajapesa stahiki zao pia hakuna madunzo waliyotolewa na maafisa tehama kwa warumishi hawa. Mfano kuna shule Z naifahamu kwa jina ipo karibu ya kufika mji mdogo wa Shirati karibi shule nzima ya sekondari walimu wake hawajaripwa mshahara na bado wanataka wanafunzi wafundishwe kwa ufanisi?

Tufikishieni kwa wenye mamlaka
 
Hiyo changamoto hata mimi nilikutana nayo.
 
Mfumo huu majanga sana,mbaya zaidi hao utumishi hawapokei wala kufanyia kazi changamoto ni kama wameacha mfumo ujiendee wenyewe.
 
Mkuu, Toka huu mfumo umezinduliwa Mnamo 2023 mwishoni ni ukweli kuwa haukuwahi kufanya kazi Kwa matakwa ya WATUMISHI wengi hasa kipengele Cha Transfer kutoka taasisi moja kwenda nyingine.

But Kuna barua hii inaeleza kuwa mfumo itaanza kazi tarehe 01/04/2024.
Soma hapa kujiridhisha
Swali ni kwa nini walizindua mfumo na kuwataka watumishi wanaohitaji kuhama waombe kupitia mfumo huo toka mwaka jana huku wakijua mfumo utaanza kufanya kazi rasmi April, 2024? Kwa nini watumishi wasingeendelea tu kuomba uhamisho kupitia makaratasi wakisubiri hiyo April, 2024?
 
sio tuu vyeo wanadai masomo yoote yafanane je walimu wenye somo la UCHUMI na physical education atapata wapi wa SONGEA mwenye masomo UCHUMI na physical education aliyepo halimashauri aliyetayari kwenda korogwe tanga???? So ni ngumu kuhama kwa mfumo huu bora wangeweka kipengele cha current teaching subject yaani kwa wakati uliopo mwl huyu anafundisha somo gani katika shule hiyo Kati ya masomo mawili mfano physics and mathematics... Mwl anafundisha physics basi wabadilishane na wa physics sio lazima physics and mathematics
 
WARUDIAHE BARUA TUU HADI PALE MFUMO UTAKAPO ELEWEKA AU KUTENGEMAA VIZURI KIUKWELI NI SOURCE KUBWA YA RUSHWAA HUU MFUMO
 
Swali ni kwa nini walizindua mfumo na kuwataka watumishi wanaohitaji kuhama waombe kupitia mfumo huo toka mwaka jana huku wakijua mfumo utaanza kufanya kazi rasmi April, 2024? Kwa nini watumishi wasingeendelea tu kuomba uhamisho kupitia makaratasi wakisubiri hiyo April, 2024?
Utumishi Wana mambo ya ajabu sana, pamoja na kusema kuanzia terehe 1, September 2023 uhamisho utumie mfumo,bado walipokea kisiri maombi ya uhamisho bila kupitia mfumo,kuna watu walipeleka barua zao na washapata vibali tayari,kwahiyo uozo upo pale utumishi,hili Nina uhakika nalo 100%
Ushauri kwa utumishi,ofisi hii imebeba neno ofisi ya raisi,kwa kifupi tulitegemea iwe ni sehemu ya watu kopona majeraha yao na kupata usaidizi wa haraka zaidi
Sasa jiulize,kwanini inachukua miezi yote hii mfumo haujatoa kibali hata kimoja Cha uhamisho,mpaka inafikia hatua wanasema mfumo unaanza rsmi Apri 1 ,2024,wakti walisema ukianza septemba mosi 2023?
Ushauri
Utumishi wawaige watu wa benki,ombi likawafikia ndani ya siku moja mpaka 2 mtu anapata mikopo,sasa utumishi inakuwaje mnakuwa na utaratibu kandamizi kwa watumishi?
Nashauri online permit letter,msisubiri typist wachape Kila barua wakti mnao wachache hapo ofisini
Make mfumo ulivyo,status ikishasoma utumishi manake nafasi IPO,hakuna kikwazo Cha Habari za ikama na kanuni na taratibu,maana kukubali kunaonyesha ikama imekubali,nafasi imetengewa budget na IPO kwahiyo mtoe vibali ndani ya mda mfupi kama mlivoahidi
Nawasilisha
 
Utumishi Wana mambo ya ajabu sana, pamoja na kusema kuanzia terehe 1, September 2023 uhamisho utumie mfumo,bado walipokea kisiri maombi ya uhamisho bila kupitia mfumo,kuna watu walipeleka barua zao na washapata vibali tayari,kwahiyo uozo upo pale utumishi,hili Nina uhakika nalo 100%
Ushauri kwa utumishi,ofisi hii imebeba neno ofisi ya raisi,kwa kifupi tulitegemea iwe ni sehemu ya watu kopona majeraha yao na kupata usaidizi wa haraka zaidi
Sasa jiulize,kwanini inachukua miezi yote hii mfumo haujatoa kibali hata kimoja Cha uhamisho,mpaka inafikia hatua wanasema mfumo unaanza rsmi Apri 1 ,2024,wakti walisema ukianza septemba mosi 2023?
Ushauri
Utumishi wawaige watu wa benki,ombi likawafikia ndani ya siku moja mpaka 2 mtu anapata mikopo,sasa utumishi inakuwaje mnakuwa na utaratibu kandamizi kwa watumishi?
Nashauri online permit letter,msisubiri typist wachape Kila barua wakti mnao wachache hapo ofisini
Make mfumo ulivyo,status ikishasoma utumishi manake nafasi IPO,hakuna kikwazo Cha Habari za ikama na kanuni na taratibu,maana kukubali kunaonyesha ikama imekubali,nafasi imetengewa budget na IPO kwahiyo mtoe vibali ndani ya mda mfupi kama mlivoahidi
Nawasilisha
Mkuuu tuwasiliane tafazari
 
Kuna changamoto ya Mfumo wa Employee Self Service (ESS), Watumishi wa Serikali tunateseka.
Nimeanza kutumia Mfumo kwa ajili ya kuomba Uhamisho wa kuhama kutoka ‘Taasisi A’ kwenda ‘Taasisi B’ kwa takribani miezi sita sasa tangu kuanza kwa Mfumo huo rasmi bila ya mafanikio huku nikikumbana na changamoto zifuatazo:
1. Mfumo unaonekana hautambui Professional za Watu (Sifa za Kielemu), badala yake unatambua Vyeo tu vya Kimuundo kwa Taasisi husika.
Hali hiyo inaleta ugumu kwa Watu wenye sifa za Kielemu kuingia kutumia Mfumo kuomba uhamisho kutoka Taasisi moja kwenda nyingine ambako pia sifa za Kielemu anazo za kufanyakazi Taasisi anayotaka kwenda.
Kwenye kipengele hiki Mtumishi akiingia kwa ajili ya kuanzisha maomba tu kwenye Mfumo katika zile menu zinazohusu Uhamisho Mfano:
i. Request Vacancy
ii. Transfer Request zinamletea message inayosomeka: "Designation not found on Destination Organization"
Hivyo, inatuwia vigumu Watumishi kuhama kwenda kutafuta changamoto nyingine nje ya taasisi tulizopo, pia kuongeza hali na kuufanya ubongo uchangamke zaidi na kujifuza vitu vipya.
View attachment 2951237
Huu ni mfano ninapokuwa nafanya mchakato wa uhamisho
2. Baadhi ya Watumishi imeonekana wakifuatilia mara kwa mara katika Ofisi za Utumishi bila ya Mafanikio.
Ombi letu ni waweze kutatua Mfumo kuwa imara kama ilivyo kwa matumizi mengine ya kimfumo, vinginevyo itakuwa haina maana kwa hiki walichofanya kuhamishia shughuli katika njia ya Mtandao.
Kingine mfumo unatambua elimu uliyoingia nayo tu wakati taarifa zako zinaingizwa, ukijiendeleza ukataka kuboresha taarifa za ziada hilo haliwezekani, mfumo unakataa.
Malalamiko yalikuwa mengi wakati mfumo wa analojia ulipokuwa unatumia, sasa hii solution nayo imekuwa ni sehemu ya tatizo.
Kuna baadhi ya nafasi ukiomba kwa ajili ya uhamisho unajibiwa “Vacancy is not Available” yaani hakuna nafasi, hata uombe kwenye taasisi ambayo unajua ina uhaba wa Watumishi majibu yatakuwa ni hayohayo.
Just imagine Mwalim au nurse anaambiwa Vacancy is not available? Ni wapi huko ambako hakuna mahitaji ya hao Watumishi.
Pia soma:
 
Husika na mada tajwa hapo juu,

Tunaomba mtu yoyote mwenye ufahamu wa kwamba mtumishi akishaomba uhamisho kwa njia ya mfumo wa ESS inachukua muda gani kupata kibali Cha uhamisho na kwenda kwenye kituo kipya?

NB; Mfumo wa ESS umerahisisha Mambo mengi sana ya kiutumishi
 
Ili kuendana na Teknolojia, Serikali kwa nia na dhamira safi ilianzisha mfumo wa Employee Self Service (ESS). Moja ya kazi ya mfumo wa ESS ni kuwawezesha watumishi kuomba uhamisho kwa njia ya mtandao na kuachana na mazoea ya zamani ya kuandika barua na kupitisha kwa mamlaka husika. Mfumo huu badala ya kuja kuwa msaada umegeuka mwiba mchungu kwa watumishi hasa wanaotaka kubadili kada au kuhama taasisi.

Kwa mfano taasisi fulani ilitangaza nafasi za uhamisho kwa watumishi wa umma na kati ya masharti ya maombi ni kwamba:
1. Muombaji anatakiwa kuambatanisha barua ya maombi itayopitia kwa muajiri
2. Muombaji aambatanishe CV
3. Muombaji aambatanishe vyeti ya taaluma.

Changamoto inayokuja hapa ni kwamba masharti ya tangazo la uhamisho haliendani na mfumo ulivotengenezwa. Mfumo unaruhusu kuambatanisha CV tu peke yake ila tangazo linataka uambatanishe cv, vyeti na barua ya maombi kitu ambacho hakikubali katika mfumo.

Ukiangalia kiambatisho hapo kuna sehemu ya “attachment” ila cha ajabu haikubali kuambatanisha faili lolote lile na ukifungua hapo inaonesha CV tu.

Pili hata kama ukiamua kuviweka vyote hvo katika faili moja kisha uambatanishe mfumo unakataa sababu faili linakua na saizi kubwa wakati faili linatakiwa lisizike ukubwa wa 700KB. Changamoto nyingine ni kwamba kama mfumo unapitishwa na mwajiri au msimamizi wa mtumishi inakuaje tena unaambiwa uandika barua ya kuomba kuhama ambayo nayo inatakiwa kupitia kwa mwajiri?

Hapo ni kama kupoteza muda maana kama mtumishi kapitishiwa maombi yake katika mfumo ina maana mwajiri wake kashamruhusu hakuna mantiki ya yy kuomba tena ruhusu kwa kundika barua za makaratasi.

Naomba wahusika kwamba wahakikishe maelekezo ya maombi ya uhamisho ya taasisi za serikali yaendane na mfumo ulivotengenezwa, pia kwenye mfumo waongeze kipengele cha mtumishi kuambatanisha vielelezo vingine kama vyeti, barua nk tofauti na sasa kuna kiambata cha wasifu pekee.

Tatu nashauri Serikali iwe na data base ya watumishi wake wanaotaka uhamisho hasa wa kubadili kada ili iwe wepesi pale inapotokea nafasi ya hzo kada wanazoomba basi iweze kuwafikia kwa wepesi na kuwahamisha hii inaweza kupunguza changamoto watumishi wanazokutana nazo katika mchakato wa kuomba uhamisho.

46B5BC64-E422-4799-A1CD-E5DFB7F7F701.jpeg
 
Sio uhamisho tu hata likizo me niliomba kwenye mfumo,ila hauko stable at the end of the day tukalazimishwa kujaza form tu za hardcopy maana mfumo Kila saa unacheza
 
Back
Top Bottom