Mgawo mkali wa umeme na maji unaoendelea nchini ni wazi kabisa watendaji wa Serikali mnaihujumu Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan

Mgawo mkali wa umeme na maji unaoendelea nchini ni wazi kabisa watendaji wa Serikali mnaihujumu Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan

Hii comment sio ya kupuuza, hii ndio picha wanayopewa watanzania kuhusu serikali yao, na ujumbe uwafikie
#WaziriMwenyeDhamanaYaUmeme
#WaziriMwenyeDhamanaYaMaji
#IdaraZoteZinazohusika

Sisi wananchi tunasema mama yetu Samia anza kuwashughulika wote wanaoshindwa kuhudumia wananchi. Tumbua mama uteue walio tayari kufanya kazi usiku na mchana kuondoa hizi kero ndogondogo kwa wananchi
Ccm fitna nyingi. Ndiyo ni hapana na hapana ni ndiyo. Majukwaani utafikiri kila kitu ni sawa, mbele ya kamera ni mapambio nyuma ya pazia fitna tupu na hii itawatafuna hadi mifupa
 
Wameshashindwa kabla hata ya kuanza
Huwezi tafuta cheo kwa gharama ya kumuumiza mwananchi

..mambo yakienda vizuri sifa anapewa raisi peke yake.

..mambo yakiharibika wanalaumiwa wasaidizi, raisi hatajwi.

..raisi ndiye anayeteua wasaidizi, hivyo anapaswa kuwasimamia vizuri ili watimize majukumu yao kwa ufanisi.
 
Lile Bwawa la Umeme litatuangalia kwa macho makubwa sana
 
Hiki kinachoendelea kimyakimya ni mchakato wa kuturudisha kuleee miaka ilee ya 2005, 2006, 2007...... miaka ambayo Dar Es Salaam na Tanzania kwa ujumla ilikua imepambwa na mikokoteni ilishosheheni madumu ya korie yaliyobeba maji na magari yenye matank ya maji kila kona.
Kwa kasi ya ajabu tunarudi miaka Ile ambayo mazingira yalikua yamepambwa kwa sauti za majenereta usiku na mchana

Au ndio ule mkakati wa kuutaka urais umeanza!? Acheni mambo yenu buana. Mama Samia yupo sana bado, ndio kwanza kumekucha

Hali ni mbaya sana na hatari kwa afya kwa jiji lenye wakazi wengi zaidi nchini, Dar Es Salaam. Watu tumepona kwenye corona lakini sasa mnataka kutulazimisha tufe kwa kipindupindu

Watendaji mnaohusika kwenye haya maeneo fanyeni kile kilichokua kinafanyika miaka mitano iliyopita hadi tukasahau kabisa kero ya umeme na maji. Kupewa nafasi ya kuhudumia wananchi kwa huduma muhimu kama umeme na maji halafu hao wananchi wakakosa hizo huduma ni wazi kabisa kwamba kufanya imeshindikana. Bora kuiacha office kuliko kukaa kwenye office halafu huduma asipatikane

Tanesco na idara za maji sisi wananchi tunamuamini rais wetu na yeye amewaamini nyie. Mnapopewa dhamana ya kutuhudumia halafu mnaamua kutuhujumu tutapaza sauti kwamba kazi imewashinda. Heri kuteua na kutumbua kuliko wananchi kuteseka kwa kukosa huduma za msingi tena ambazo wanazichangia kwa kodi zao wenyewe

Mungu ibariki Tanzania
Mungu mbariki Rais wetu Samia Suluhu Hasan
Kazi iendelee

Cc Wizara ya Afya Tanzania
Blah blah za kila siku za dizaini ya "tunampenda rais wetu", "tunamwanini rais wetu", "mama anaupiga mwingi", nk. Kwani mlimchagua kwenye sanduku la kura?
 
Any Yet you can See this and She Can't !!!

What needs to happen for the likes of your to place the blame on her ?

Au ni yale Rais hakosei ?!!!!
 
Alijihujumu mwenyewe kwa kuteua wapiga porojo.

Mambo yakiwa bien,sifa na utukufu anapewa yeye ila yakigoma wanalaumiwa wengine.

Tulimwambia Makamba kwamba propaganda zake zitajitenga tu na ukweli,lilikuwa ni suala la muda.

Mara ukarabati haukufanyika kwa miaka mitano mara vile.

Kiko wapi?
 
Hiki kinachoendelea kimyakimya ni mchakato wa kuturudisha kuleee miaka ilee ya 2005, 2006, 2007...... miaka ambayo Dar Es Salaam na Tanzania kwa ujumla ilikua imepambwa na mikokoteni ilishosheheni madumu ya korie yaliyobeba maji na magari yenye matank ya maji kila kona.
Kwa kasi ya ajabu tunarudi miaka Ile ambayo mazingira yalikua yamepambwa kwa sauti za majenereta usiku na mchana

Au ndio ule mkakati wa kuutaka urais umeanza!? Acheni mambo yenu buana. Mama Samia yupo sana bado, ndio kwanza kumekucha

Hali ni mbaya sana na hatari kwa afya kwa jiji lenye wakazi wengi zaidi nchini, Dar Es Salaam. Watu tumepona kwenye corona lakini sasa mnataka kutulazimisha tufe kwa kipindupindu

Watendaji mnaohusika kwenye haya maeneo fanyeni kile kilichokua kinafanyika miaka mitano iliyopita hadi tukasahau kabisa kero ya umeme na maji. Kupewa nafasi ya kuhudumia wananchi kwa huduma muhimu kama umeme na maji halafu hao wananchi wakakosa hizo huduma ni wazi kabisa kwamba kufanya imeshindikana. Bora kuiacha office kuliko kukaa kwenye office halafu huduma asipatikane

Tanesco na idara za maji sisi wananchi tunamuamini rais wetu na yeye amewaamini nyie. Mnapopewa dhamana ya kutuhudumia halafu mnaamua kutuhujumu tutapaza sauti kwamba kazi imewashinda. Heri kuteua na kutumbua kuliko wananchi kuteseka kwa kukosa huduma za msingi tena ambazo wanazichangia kwa kodi zao wenyewe

Mungu ibariki Tanzania
Mungu mbariki Rais wetu Samia Suluhu Hasan
Kazi iendelee

Cc Wizara ya Afya Tanzania
Kina cha maji kimeshuka Ruvu chini na juu, maji yanazalishwa kwa 40% tu, hakuna mvua hii huwezi kuita hujuma.

Issue ya umeme Makamba amewekwa na mama kwahiyo kama ni hujuma basi mama anajihumu mwenyewe, huwezi kuweka wahuni kwenye wizara nyeti kama ya Fedha na ya nishati.
 
Back
Top Bottom