Mgombea binafsi Tanzania: Tatizo ni nini?

Mgombea binafsi Tanzania: Tatizo ni nini?

Mgombea binafsi alisharuhusiwa na mahakama ya afrika ambayo Mch. Mtikila alifungua kesi na akashinda kwa sababu hiyo serikali ilitakiwa ianze mchakato wa kurekebisha vifungu vya katiba ila serikali ilifanya ujanja kwa kisingizio cha kuwepo rasimu ya katiba ambayo ilikuwa imeingiza na kipengele cha wagombea binafsi baada ya mchakato wa katiba kuvurugwa serikali imekaa kimya.

Tatizo sio CCM wala vyama vya upinzani wanaotaka wagombea binafsi ndio maana tumeona hakuna kelele yoyote toka kwa vyama vyote kwani mgombea binafsi akiruhusiwa ndio mwanzo wa vyama vingi kufa kwani karibia vyote vinaendeshwa kwa njia zinazofanana na mtu akitaka kugombea hata kama hakubaliani na vyama hivyo inabidi ajiunge navyo
 
Hivi tuna Katiba inayotufaa kama SHERIA mama au ngrundnorm?Sheria yoyote isiyotenda au isiyosimamia haki au isiyo ya haki siyo sheria.LEX INJUSTIA NON EST LEX
 
Flash back 2008. Je serikali iliheshimu maamuzi ya mahakama kuhusu mgombea binafsi? Fast forward now. je serikali itaheshimu maamuzi ya mahakama kuhusu mchakato haram wa katiba ?
Swali lako ni gumu sana.
 
rodrick alexander,

Lakini nchi nyingi hata jirani zetu Kenya Katiba yao inaruhusu mgombea binafsi,nadhani uwepo wa mgombea binafsi itasaidia kutoa uwanja mpana wa wale wenye nia ya kugombea lakini nia hiyo inafungwa kupitia vyama ambavyo yawezekana vikashindwa kumpa haki ya kugombea kutokana na urasimu na hata uwingi wa wagombea kwa nafasi moja ktk chama.

Pia ili kupunguza gharama,ni vyema ktk katiba kuwe na kipengere kinacho ongelea uhamaji wa vyama na nafasi ya ubunge au udiwani,yaani yaweza kuwa "endapo mbunge au diwani atahama chama chake cha awali kwa sababu zozote zile,nafasi yake ya uwakilishi kwa wananchi itabaki kama ilivyo hadi hapo uchaguzi mkuu utakapofanyika" hii itasaidia kupunguza gharama za chaguzi za marudio,ambazo pesa zake zingeweza kutumika kufanya kazi nyingine za kimaendeleo
 
engmtolera,
Nakubaliana na wewe 100%. Hebu ona hali ya kifedha Kenya inavyoitesa serikali kwa sababu ya kura za marudio. Kura za marudio ni hatari sana kwa uchumi (causing economical instability) na kuweka usalama wa nchi rehani.

Tujitafakari!
 
Hili la mgombea binafsi si CCM wala UPINZANI wote hawalitaki,kwani vyama siku hizi vimekuwa vijiwe vya watu wenye maslai yanayo fanana na ndio maana hata ukikosea unatetewa mf CHENGE na LOWASA na wote wakiingia bungeni wanahakikisha maslai ya chama kwanza na si Tanzania kwanza na hata hizi movement zinazoanzishwa kwangu naziona hazina maslai kwa taifa.

Mimi mwenyewe napenda tuwe na katiba mpya itakayo ruhusu mgombea binafsi ,tatizo katiba mpya inapitishwa na hawa hawa wanasiasa kwa hiyo ,tunaweza pata katiba mpya isiyomtambua mgombea binafsi.
 
Kwa sasa Tanzania inakabiliwa na wimbi la viongozi hasa wabunge na madiwani kuhama vyama vyao licha ya kuchaguliwa na wananchi kwa njia ya sanduku la kura

Moja ya sababu ambazo zinatajwa na wanaohama ni matatizo yaliyomo katika vyama hivyo au kuunga mkono juhudi za Rais

Napendekeza kabla ya 2020 serikali ibadilishe sheria awepo mgombea binafsi, wananchi wenye uwezo wa kuongoza waweze kuchaguliwa na wananchi bila kuzingatia chama anachotoka ili kuepuka gharama za kurudia uchaguzi wa mara kwa mara kwa kile kinachoitwa hama hama kwenye vyama vya siasa

Itaondoa ukiritimba wa watu kuchaguana kwenye vyama vya siasa kwa kujuana na kupitishwa bila kupingwa

Itaondoa chuki ya kivyama,watu kwa sasa wanabaguana hadharani na kuonyesha chuki kwa wananchi wanaoshabikia chama Fulani

Na mwisho itawapa mwanya vijana wengi kujitokeza kugombea nafasi hizo bila vipingamizi ikizingatia kipindi hiki ambacho ajira ni ndogo sana

Nchi nyingi kwa sasa wameruhusu mgombea binafsi kwa hivyo kwa pamoja naomba tuungane kupigania mgombea binafsi ili tuachane na ushabiki wa vyama vya siasa hata hivyo yawezekana bila kutarajia ukawa mbunge au diwani kupitia mgombea binafsi kama Kijana huyu

Screenshot_20180813-131623.jpg
 
Jiwe kaikanyaga KATIBA na anatamani kama siyo kujiongezea muda wa kutawala milele..halafu asikie masuala ya mgombea binafsi?

Unaota wewe.
 
Hatupandishi mishahara TUNABANA matumizi

Tunatoa ajira kiduchu BADO TUNABANA matumizi.

Kujenga shule,vituo vya afya,nyumba za polisi(wafanyakazi) bado TUNABANA MATUMIZI

Ila MABILIONI ya chaguzi za marudio YAPO ya bule ya kuwafurahisha wanasiasa

Hivi kuna awamu imewai kufanya siasa za dizaini za kugarimu taifa?
 
wanajamvi habari za mda huu? mimi naenda moja kwa moja kwenye mada je tunapataje mgombea binafsi maana mimi naona mambo ya vyama ni vurugu tupu mpaka sina hata matumaini yeyote kwa nchi yangu kupata watu wanaoweza kutufikisha mahali pazuri yaani naona watu wamekata tamaa sana.

CCM hawapambani na umaskini wa watanzania bali wanapambana na cdm namna ya kuimaliza ili kusiwe na kelele. lakini ingekuwa inajitahidi sawa badala yake ni uporaji na ufisadi kwa kwenda mbele.

mwaka huu tumeshuhudia mpaka ukaguzi wa CAG umeshindikana kusomwa bungeni kisa tumepigwa na wajanja mpaka aibu tri.1.6 haionekani. kwa awamu hii ni aibu sana maana wamejinasibu wanatokomeza ufisadi lakini ndo wamepigwa vibaya sana.

Sisi tunaowajua ccm tulijua mambo ni mbele kwa mbele ndo maana tunawaza sana sana labda mgombea binafsi atakuwa suluhisho.
 
"WENYE NCHI" hawatakuja kuruhusu kitu kama hicho

Labda yatokee mapinduzi
 
Hata Mwalimu Nyerere alisema Mtanzania yeyote ana haki ya kugombea awe mwanachama wa chama cha kisiasa au asiwe.

Je ni kwanini Watanzania walazimishwe kujiunga na vyama vya kisiasa ili tu kugombea kuwakilisha wananchi. Kuna Watanzania wengi tu hawana vyama sasa kwanini walazimishwe. Inawezekana sikubaliani na chama chochote inakuwaje hapo.
 
Back
Top Bottom