Elections 2015 Mgombea Urais CCM 2015: Ni Bernard Membe au January Makamba

Elections 2015 Mgombea Urais CCM 2015: Ni Bernard Membe au January Makamba

Nguruvi3,

Asante sana kwa mchango wako; Migiro binafsi namuweka kwenye top 5 lakini sioni akipita kwani kufikia 2015, nchi itakuwa imeyumba sana na yenye kuhitaji utatuzi wa masuala mengine mengi ya msingi na muhimu kuliko suala la gender equity; Urais wa mwanamke unaendana na perception ya udhaifu, na sidhani kama watanzania wapo tayari kutoka kwenye hali ya sasa na kuingia katika hali nyingine ambayo itafanania na hii ya sasa, kama sio kuizidi; Kutakuwa na agenda kuu tano kuelekea 2015:


  • Ufisadi - membe akiwa mgombea
  • Vijana - January akiwa mgombea
  • Kuokoa Muungano, zamu yetu wazanzibari - Karume
  • Jinsia - Migiro
  • Mtu asiye na makundi - hatumjui bado ingawa tayari jina lake sio geni masikioni mwetu; Migiro katika hili la tano hatoshi kwani inajulikana wazi kwamba karibikia katika kipindi chote chaa wamu ya nne, nafasi zake za uongozi mara nyingi hazijawa za kupigiwa kura bali kuteuliwa;

Migiro atasukumwa sukumwa weee, na hatimaye kukutana na Meghji's Syndrome kwani kwa hoja hiyo hiyo ya gender n.k. Meghji inasemekana ndiye aliyekuwa chaguo la mwenyekiti kama mgombea mwenza mpaka dakika ya mwisho; To put it in a better perspective, hakuna mgombea atakayepita kwa kubebwa na mwenyekiti kwa asilimia 100; Atakayepita ni yule atakayejisaidia mwenyewe, na baadae kupigiwa krosi, assuming chama kitabakia intact mpaka uchaguzi 2015;

All in all, i still believe kwa hoja nilizojenga kwamba agenda kuu itakayotawala ni aidha Ufisadi au Kura za Vijana; Vinginevyo suala la kuwa na mgombea wa kuvunja makundi litakuja kwa kuchechemea sana kwani ili mtu huyu afanikiwe, atahitaji kuungwa mkono kwa fedha na kundi fulani...; Hata 1995, licha ya makundi kuvunjwa, watu fulani fulani bado walihitajika kifedha kusaidia kampeni na ndio maana mpaka leo wana nguvu; kwahiyo tatizo la makundi litajirudia tu hata ateuliwe nani kwani kwenye maamuzi muhimu ya Chama, watawala wa CCM hawapishani kihoja au itikadi bali maslahi; Vita hivi vitakuwa very interesting, tuombee uzima tuvishuhudie;

Pia kwa mtazamo wako, jukumu kubwa la Mangula na Kinana litakuwa ni nini hasa katika yote haya;
 
Mchambuzi,
Pamoja na matatizo tuliyo nayo, watanzania wengi bado hawajafikia kiwango cha kujiuliza kwanini fulani awe kiongozi.
Nadhani utakuwa shahidi kwani hapa Jamvini kila mtu anaibuka na jina lake, wengine wakisema fulani ni mchapa kazi. Ukiuliza kivipi hawana jibu. Nina maana kuwa jinsia inaweza kupigiwa debe ikaonekana kama ndilo tatizo letu kubwa.
Unakumbuka udini na ukabila ulivuovumishwa na watu wakasahau kuwa inflation rate imefikia 19% kutoka 7%.

Kuhusu Meghji sidhani kuwa anaweza kuwa kikwazo kwa yoyote endapo atajitokeza.
Meghji tayari amedhihirisha kusindwa kazi na udhaifu wa hali ya juu sana ambao ukianikwa hata NEC jina haliingii.

Karata ya ujana ya January haina nguvu kwasababu vijana walioaminiwa wote wamevurunda hadi kurejea kwa akina Mangula. Tatizo lingine ni kuwa January ana mizigo inayoambatana naye. Hata kama ni msafi kiasi gani, hatuwezi kumtenga na mnyororo wa Yusufu Makamba, Rostam na Lowasa.
Ikumbukwe kuwa Sitta ni majeruhi mkubwa wa siasa za kundi hilo la January, hivyo ''hujuma'' ni kitu kisichoepukika.

Hili la Mangula na Kinana linahusu nidhamu ndani ya chama. Inavyooenakana Mwenyekiti ameshindwa kusimamia nidhamu ndani ya CC, NEC na Bunge. Kinachofanyika ni kurudisha watu wenye misimamo wanaoweza kuchukua hatua dhidi ya ''waasi''. Wakati wa Mkapa hakukuwa na mambo yanayoonekana sasa hivi.

Katika siku za karibuni Kinana atateuliwa kuwa mbunge wa kuteuliwa katika wale 10 ili aweze kumsaidia Pinda kukabiliana na uasi ndani ya bunge. Kichama linaweza kuwasaidia sana lakini waangalie historia inasemaje pia.

Kuwabana wabunge wa CCM ni kuwapa nafasi wabunge wa upinzani. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Dr Slaa. Kwamba Mkapa aliwabana Wabunge wa CCM akiwa na akina Mangula na hapo kufungua nafasi za akina Slaa na Zitto kuonekana mashujaa. Hilo nalo liangaliwe kwa upande huo.

Kikubwa zaidi ni kutaka Mangula na Kinana wavunje makundi ndani ya chama.
Ni kitu kigumu sana kwasababu udhaifu wa Mwenyekiti ndio chanzo cha udhaifu wa structure nzima.
Watakachokifanya ni kupunguza kasi ya mmomonyoko lakini hawatazuia uharibifu uliotokea.

Kurejeshwa kwa Mangula na Kinana ni kwasababu ya kumsaidia Mwenyekiti ambaye ni dhaifu sana na anayezongwa na habari nyingi za siri ambazo zinaweza kumweka katika wakati mgumu sana. Ni kwasababu hizo Mwenyekiti hana nguvu za kukabiliana na makundi wala ujasiri wa kuteta na Makundi. Tunakumbuka kisa cha Lowasa na Mswekwa Lumumba.

Msekwa hakushindwa kazi. Ukimlinganisha na Mangula, Msekwa ana uzoefu wa chama na amefanya kazi na viongozi wote na anakihamu chama vizuri sana. Kilichomshinda ni udhaifu wa Mwenyekiti aliyekuwa kikwazo kwa maamuzi mazito.
Hicho ndicho kimemshinda Mukama na Nape Nnauye pia.
Nabaki kujiuliza kwanini Mangula na Kinana wameamua kubeba mzigo huo wakijua kuwa kuna kamba zitawavuta miguuni!!
 
Nabaki kujiuliza kwanini Mangula na Kinana wameamua kubeba mzigo huo wakijua kuwa kuna kamba zitawavuta miguuni!!

Ndio maana nilisema awali kwamba hili lijitu linaloitwa CCM limebadilishwa kichwa kwa kiasi fulani lakini shingo inabakia kuwa ni ile ile, na kama tujuavyo, shingo ndio hugeuza kichwa kulia na kushoto;
 
Chadema hakuna mtu mwenye uwezo wa kuwa rais wala kuchaguliwa na watanzania kuiongoza nchi hii. Wengi historia zao ni tata. Tukijaribu kuwaelimisha watanzania haraka sana mada kama hizo huwa zinafutwa kwenye hii jamii forum au mtu kufungiwa kwa kisingizio eti umetoa kauli isiyo faa. Lakini kama tunataka uhakika wa viongozi basi tuvumilie tu wapigwe kritiki siyo kuwaumiza wa ccm na kuwatetea wa chadema kama ambavyo baadhi ya watu wamefikia atua ya kusema hii jamii forum ni ya watu fulani sina hakika na hili ni suala la kubadidi mtazamo na kuvumilia kritiki kama unazowapa wenzako. Utajidanganya saana kuwatetea watu kwa kufuta mambo yanayowachoma wana chadema
 
Chadema hakuna mtu mwenye uwezo wa kuwa rais wala kuchaguliwa na watanzania kuiongoza nchi hii. Wengi historia zao ni tata. Tukijaribu kuwaelimisha watanzania haraka sana mada kama hizo huwa zinafutwa kwenye hii jamii forum au mtu kufungiwa kwa kisingizio eti umetoa kauli isiyo faa. Lakini kama tunataka uhakika wa viongozi basi tuvumilie tu wapigwe kritiki siyo kuwaumiza wa ccm na kuwatetea wa chadema kama ambavyo baadhi ya watu wamefikia atua ya kusema hii jamii forum ni ya watu fulani sina hakika na hili ni suala la kubadidi mtazamo na kuvumilia kritiki kama unazowapa wenzako. Utajidanganya saana kuwatetea watu kwa kufuta mambo yanayowachoma wana chadema

Unazungumza na nani?
 
Nasikitika kusema kuwa hawa wote ulio wataja ndani ya CCM na hata CHADEMA sioni mwenye uwezo wa kuwa Rais na kuiongoza nchi hii na kufanya mageuzi ya kweli ya kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Anyway, kama hawa ndio watakuwa wagombea wetu nitatumia kigezo cha dini ya mgombea kupiga kura yangu.
 
Nasikitika kusema kuwa hawa wote ulio wataja ndani ya CCM na hata CHADEMA sioni mwenye uwezo wa kuwa Rais na kuiongoza nchi hii na kufanya mageuzi ya kweli ya kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Hoja hii ni ya msingi sana kwani hatuna utamaduni wa kuchagua viongozi wenye uwezo au kwa vigezo nje ya personalities za wagombea - sura, fedha n.k; Kwa vile majority ya watanzania ni illiterate, utamaduni huu utaendelea kwa muda mrefu sana;

Anyway, kama hawa ndio watakuwa wagombea wetu nitatumia kigezo cha dini ya mgombea kupiga kura yangu.
Kwangu binafsi, ni mara kumi nisiende kupiga kura yangu kwa mgombea Udiwani, Ubunge au Urais, kuliko kwenda kutumia haki yangu ya msingi ya kiraia kwenda kufanya maamuzi ya kidini;
 
Chadema hakuna mtu mwenye uwezo wa kuwa rais wala kuchaguliwa na watanzania kuiongoza nchi hii. Wengi historia zao ni tata. Tukijaribu kuwaelimisha watanzania haraka sana mada kama hizo huwa zinafutwa kwenye hii jamii forum au mtu kufungiwa kwa kisingizio eti umetoa kauli isiyo faa. Lakini kama tunataka uhakika wa viongozi basi tuvumilie tu wapigwe kritiki siyo kuwaumiza wa ccm na kuwatetea wa chadema kama ambavyo baadhi ya watu wamefikia atua ya kusema hii jamii forum ni ya watu fulani sina hakika na hili ni suala la kubadidi mtazamo na kuvumilia kritiki kama unazowapa wenzako. Utajidanganya saana kuwatetea watu kwa kufuta mambo yanayowachoma wana chadema
Kinachofanyika hapa ni kujadili kila kitu kwa upana na maoni ya kila mmoja wetu.
Nadhani utakumbuka mara baada ya uchaguzi wa vitongoji na madiwani tulisamama hapa jamvini na kufanya mjadala wa yotakanayo. Chadema walipata critic kikamilifu na CCM credit zake fair without fear

Labda ungetuonyesha wapi unadhani Chadema imeingia kutokana na mada ya Mchambuzi.
Tunaomba uache spinning na ujikite katika mada. Utamaduni wa kila jambo kuligeuza hautusaidii.
 
Mchambuzi, ni kweli mkuu!

Kwa upande wa CCM anayeandaliwa kuwa Rais ni Waziri Membe na hili lipo wazi kabisa,kuhusu J. Makamba ni mtu ambae hana nafasi kwani umri tu nao utambana la sivyo umri ubadilishwe wa kugombea urais ndio utaweza mpa nafasi,si kwamba waliobaki hawatarusiwa kugombea la hasha kwa kuwa ni haki ya kila mtu kugombea nafasi hiyo watapewa nafasi lakini Membe ndio chaguo la CCM kwa sasa labda itokee kuwe na mabadiliko ya kisiasa huko mbele tuendako.
January atakuwa na umri wa miaka 41 ifikapo 2015; nimezingatia kigezo hiki kabla ya kuja na mjadala huu; Kuhusu membe, ni kweli hata mimi naona hivyo; Lakini ningependa ijulikane kwamba nia yangu kuja na uzi hu haikuwa kuwapigia debe hawa wawili bali uchambuzi wangu wa mazingira yanayozaa mgombea Urais. Mjadala kuhusu uwezo na sifa zao kushika madaraka ya nchi ni mjadala mpya kabisa, na binafsi bado sina chaguo langu la mgombea urais CCM kwani zaidi ya sura zao, sijui wanasimiamia yepi kwa taifa letu, kwa msukumo gani, kwanini, na nia yao ni kupeleka wapi nchi yetu; Bado hawajafunguka; Angalau mtu unaweza kuotea kidogo kwa upande wa Lissu na Slaa kwamba watasimimia nini, mfano suala la muungano, ufisadi, utawala wa sheria n.k;
kwa upande wa vyama vingine sina hakika sana nani anaweza shika bendera hiyo ya urais ukimwondoa mzee slaa lakini waliobaki wote bado nafasi zao ktk mioyo wa watanzania ni ndogo sana,kwani umejionea mwenyewe ktk chaguzi ndogo zilizopita bado mageuzi makubwa yanahitajika ili kuweza kuwabadili watanzania watakao kuwa na mgombea kwapani kipindi hico 2015,Kama hata kuwa Slaa basi CCM bado itakuwa na kazi ndogo sana ktk kunyakuwa ushindi kwa uchaguzi wa urais ujao 2015 maana siasa za nchi hii bado zinawategemea wapiga kura wa vijijini ambao ndio wapiga kura wa kweli kuliko mijini.Bado kuna kazi kubwa ya kufanywa.

Kimsingi nakubaliana na wewe lakini kama nilivyojadili hapo juu, angalau wapo viongozi wa Chadema ambao wanajaribu kutenganisha masuala na personalities katika kutafuta ridhaa ya wananchi; Chadema imeweka ilani yake ya uchaguzi 2010 pembeni na kufanyia kazi mambo mengine muhimu; Lakini CCM bado wanapima mafanikio yao kupitia ilani badala ya kujikita pia kwenye mambo mengine endelevu; Kama ilani yao ni mtaji wa kisiasa, kwanini basi M4C inazidi kushika kasi? Hivi hawana akili ya kujiuliza hili? Kinachotekelezwa kwenye ilani so far ni kumsaidia mtanzania to survive the nexy day, sio kumjengea capabilities za kuweka kupata prosperity into the future, hasa kwa kumweka maskini at the centre of development policy, na kumzungushia resources zote muhimu za taifa lake;

Kushinda kwa mzee Wasira kwa kishindo bado ni changamoto pia kwa vyama pinzani kwani kura zake zinaonyesha jinsi wajumbe wa nec walivyo na imani naye na ikitokea akatoka na mtu wake kwapani basi ndio atakae teuliwa kukimbiza bendera ya uraisi kwa upande wa CCM .
Wassira ana advantage kuu tatu: kwanza ni waziri ofisi ya Rais (ambae pia ni mwenyekiti wa CCM), pili, amekuwa ni mzungumzaji mkuu wa Chama katika matukio yanayohusiana na mifarakano baina ya Chama tawala na Chadema, na tatu, ni mmoja wa vijana wa Nyerere tangia akiwa kijana mdogo; Haya matatu yanampa nguvu kubwa sana miongoni mwa wanachama wa CCM bila ya kujalisha kama hoja zake ni pumba au mchele;

Sioni qualities za wassira kuwa Rais, na hawezi kwenda huko, hasa ikizingatiwa kwamba anatokea kwa Mwalimu; Madaraka ya nchi yanahitaji kuwa diversified ili kila kona ya nchi ijihisi inawakilishwa; Nje ya hapo, tusisahau kwamba Wassira alihamia Chadema kwa muda, which means uwepo wake CCM ni kimadaraka zaidi, kwani wapo wengi ambao walianguka ubunge na wakabakia CCM na kustaafia huko huko ingawa they had nothing to lose kwa kuhamia upinzani; Akigombea atakumbwa na fitina nyingi sana kutoka kwa wenzake na nyingi ya hizo zitakuwa ni legit kabisa;

Na kwa upande wangu naona B. Membe ndio litakuwa chaguo lao na hata kama itashindikana basi watafanya kama ilivyotokea kwa uspika na kuamuwa kumpa mama Roze Migiro ili kuiendesha nchi. Na hapo watanzania ndio watachanganyikiwa kabisa kwani itakuwa ni maswala ya jinsia na kauli mbio ya kipindi hicho itakuwa mwanamke anaweza kama akipewa nafasi na hapo ndipo kura nyingi za kina mama zitakimbilia huko na tuelewe ktk nchi hii wapiga kura wengi ni akina mama na wale watu waishio vijijini na hii itafanya mgawanyo mdogo ubaki kwa akinababa na vijana ambao bado pia kutakuwa na mgawanyiko baada ya waliowengi kuona ni vyema tujaribu kwa mama kwani tulisha jaribu kwa akina baba na hakuna mafanikio makubwa.
Nashindwa kuelewa kwanini watanzania wanazidi kuaminishwa kwamba kuwa waziri wa mambo ya nje maanayake una uwezo zaidi ya wenzako kuongoza nchi; Hii formula inajengwa na variable gani, can someone break it down for us? Membe anaweza kuwa na qualities za Urais lakini sio kwa kipimo cha kuwa waziri wa mambo ya nje; Akigombea kwa kuegemea sana kwenye gear hii, inaweza kumuangusha;Anazo qualities kadhaa za kuwa Rais lakini kwa mtazamo wangu, nyingi ya hizo hazina uhusiano wa moja kwa moja na uwaziri wake wa mambo ya nje;

Kuhusu Rose Migiro, mimi naona huyu anakuwa over hyped or over rated; Na Tanzania ina mambo mengi sana ya msingi ya kushugulikia na yenye uzito mkubwa zaidi kwa manufaa ya watanzania kuliko suala la usawa wa kijinsia; Kabla ya usawa wa kijinsia, tuanze na usawa wa kipato basi; Kama agenda ya jinsia itakuwa na uzito na umma kupitia reliable opinion polls useme hilo, basi afikiriwe; Vinginevyo binafsi sijaona qualities za Migiro za kumwezesha kuwa Rais wa nchi yetu; Kwanza hana experience ya kupigiwa kura, kwani mara nyingi huteuliwa; na pili, kama ni suala la kiongozi mwanamke, wapo wengine wengi wenye kumzidi kiutendaji na kiuzoefu kama kina Tibaijuka;
 
Nguruvi3,

Katika bandiko lako namba 142 umejadili mambo kadhaa ambayo ni ya msingi sana; kwa mfano, umeeleza kwamba moja ya sababu kubwa zilizopelekea uteuzi wa Mangula na Kinana ni kurudisha Nidhamu nani ya Chama; Kwa mtazamo wako, utovu wa nidhamu unaoendelea ni upi? Kwa mujibu wa katiba ya CCM, ibara ya 8 (1 hadi 7), masharti ya mwanachama ni haya - ambayo nadhani kama yanavunjwa ndio utovu wa nidhamu:

1. Kuwa mtu anayeheshimu watu;
2. Kuwa mtu anayefanya juhudi kuelewa, kuieleza, kuitetea na kuitekeleza itikadi na siasa ya CCM;
3. Kuwa mtu mwenye kuamini kuwa kazi ni kipimo cha Utu, na kuitekeleza imani hiyo kwa vitendo;
4. Kuwa mtu anayependa kushirikiana na wenzake;
5. Kuwa mtu ambaye siku zote yuko mstari wa mbele katika utekelezaji wa mambo yote ya Umma, kulingana na miongozo ya CCM;
6. Kuwa wakati ni mfano wa tabia nzuri kwa vitendo vyake na kauli yake, kuwa mwaminifu na kutokuwa mlevi au mzururuaji;
7. Kuwa ama MKULIMA, MFANYAKAZI, au mwenye shughuli nyingine yoyote HALALI ya kujitegemea;

Iwapo unakubaliana na mimi kwamba msingi wa nidhamu ndani ya chama unatokana na ibara hii, Mangula na Kinana wanakuja kurudisha nidhamu zipi zilizomomonyoka kati ya hizi? Kwa mfano:

Iwapo sharti namba (4) litajengewa hoja, hao wenzake ni wepi? Wa upande wa Membe? Sitta? Lowassa? Mwenyekiti?

Iwapo sharti namba (6) litajengewa hoja, nani ni mfano bora wa kuigwa ndani ya chama? Kwani by implication, hata wabunge wa CCM, kazi yao kubwa imekuwa ni kuzurura Dar badala ya kukaa majimboni mwao;

Iwapo sharti namba (7) litajengewa hoja, je kati ya viongozi wote wakubwa wakubwa wa nchi hii, nani amejiongezea kipato chake kupitia Ukulima (kuuza mazao au ufugaji) au Ufanyakazi (mshahara)? Na ni yupi ana shughuli halali ambayo ina rekodi zote za ulipaji kodi TRA, utiifu wa sheria za procurement etc?

Unless suala la nidhamu ni arbitrary na linatekelezwa kwa misingi ya huyu mwenzetu, huyu sio mwenzetu, kazi ya kurudisha nidhamu CCM na kufanikiwa is a non - starter;

Nini mtazamo wako katika hili;
 
Nguruvi3, Unless suala la nidhamu ni arbitrary na linatekelezwa kwa misingi ya huyu mwenzetu, huyu sio mwenzetu, kazi ya kurudisha nidhamu CCM na kufanikiwa is a non - starter;
Nini mtazamo wako katika hili;
Huu ndio msingi wa hoja yangu haswaa!
Nikiri kuwa nilipaswa nitumie neno nidhamu kwa kuliweka hivi '' nidhamu''.

Kifungu cha kwanza kinasema 'kuwa mtu anayehishimu watu''. Endapo kingefuatwa leo hii akina Sophia Simba na Lusinde wasingekuwa viongozi. Nimetumia mfano huo kuonyesha kuwa maandiko hayaendani na hali halisi tuijuayo.

Msingi wa kuleta ''nidhamu'' niuzungumziao ni ule wa kutumia mkono wa chuma ''iron fist' hata kama hoja inalindwa na vifungu vyote vya chama. Mathalani, wabunge watalazimika kukubaliana na hoja za serikali ya chama chao hata kama hawazikubali kifikra na kiroho, na hiyo ni toafuti na katiba na muongozo wa CCM kuhusu uhuru wa kujieleza.

Nidhamu ninayoongelea hapa ni kuwa Lowasa hawezi kumnanga Membe bungeni hata kama kuna ukweli wa anachosema.
Unakumbuka EL aliposema ajira ni bomu tarajiwa, serikali ilimshukia. Hapo ndipo akina Kinana na Mangula watakapoingia na tutasikia watu wakiitwa Dodoma kuhojiwa.

Nidhamu ni ile ya chama kumshukia Fikunjombe kwa kusaini karatasi ya Zitto au Mkono kusema nani ataondoa jina langu.
Lakini pia nidhamu ni ile ya kuzuia watu wenye kashfa nzito kuendelea kutumikia chama.

Tutarajie Mangula na Kinana kutumiwa na Mwenyekiti katika kuwatisha na kuwatia adabu viongozi wote iwe wenye nia njema na taifa hili au nia mbaya. Kwamba nidhamu ya woga inaweza kurudi si kwa kutumia vifungu ndani ya katiba bali mkono wa chuma.

All that being said, nakuhakikishia kuwa itakuwa ni tiba ya panadol kupunguza maumivu na homa na si kutibu Malaria. Chama kimeshaharibika kwasababu sehemu kubwa sana ya wanachama wenye nia njema wapo nje ya system kilichobaki ni chama cha makundi.

Makundi ya akina EL, SamSix na Bashe yatapunguza kelele, guess what! undergorund movement zitakuwepo na madhara yake ni makubwa sana. Madhara ni makubwa kwasababu Mangula na Kinana watafanikiwa ku-supress harakati za makundi, hawata eliminate makundi.

Ili CCM kiweze kurudi katika hali yake ya zamani ni lazima kutokee mpasuko by force au naturally.
By force ni Mangula na Kinana kuchukua hatua ngumu sana dhidi ya establishment na interest za waharibifu wa chama.
Kwa bahati mbaya kikwazo kitakuwa Mwenyekiti wa CCM ambaye ni dhaifu lakini mwenye kauli ya mwisho.

Naturally: nisingeshauri chama chako kisubiri.
Si shauri kwasababu KANU na UNIP zimepitia huko, that has proved futile.

Ikifika hapo bado nabaki kuamini kuwa Mangula na Kinana wameamua kuchafua CV kama zilikuwa nzuri.
Sielewi kwanini wamejitwisha zigo hili wakijua wazi kuwa the rift is so huge to fix within 2 years of their tenure.

Na mwisho, nimesoma thread yako nyingine kuhusu CCM. Nakubaliana na mawazo yako kuhusu reform ya chama.
Ukisoma katiba na muongozo wa CCM ni ngumu sana kutoa makosa. Hata hivyo ukweli unabaki kuwa kuna tatizo.
Labda ningeshauri uwaambie watu wa chama chako yafuatayo.
1. CCM must take difficult decision to weed out ring leaders regardless how potential or prominent they're.
2. Restore the recruitment program based on merit and not tech know who (your very valid point)
3. Dissolve the party organs and call for new election (pristine) before 2015.

Otherwise this could be the begining of the end on the hands of Kinana and Mangula.
 
Nguruvi3,

Kifungu cha kwanza kinasema 'kuwa mtu anayehishimu watu''. Endapo kingefuatwa leo hii akina Sophia Simba na Lusinde wasingekuwa viongozi. Nimetumia mfano huo kuonyesha kuwa maandiko hayaendani na hali halisi tuijuayo.

Cha kusikitisha ni kwamba tabia za ovyo ovyo za baadh ya viongozi zinazidi kuwa kama vile ni sifa au vigezo vya kupata kazi au kupandishwa cheo ‘informally' kwani uhuni uhuni ndani ya Chama kwa kweli UNALIPA; Wakati wa Nyerere hata kuachana na mke wako au mume wako kwa legit reasons kabisa ilikuwa ni doa kubwa katika sifa zako kama kiongozi wa chama; leo hii huu uhuni uhuni hivi unatoa mafunzo gani kwa watoto wetu wenye ndoto za kuja kuwa wanasiasa na viongozi? Kwa kweli CCM imeachana kabisa na maadili; Hata ukienda kwenye sherehe za chama, sherehe za mwenge n.k huko vijijini, hizi ni fursa za kufanya ufuksa na uchafu wa kila aina miongoni mwao; Heshima ya chama imeshuka sana;

Msingi wa kuleta ''nidhamu'' niuzungumziao ni ule wa kutumia mkono wa chuma ''iron fist' hata kama hoja inalindwa na vifungu vyote vya chama. Mathalani, wabunge watalazimika kukubaliana na hoja za serikali ya chama chao hata kama hawazikubali kifikra na kiroho, na hiyo ni toafuti na katiba na muongozo wa CCM kuhusu uhuru wa kujieleza.

Nidhamu ninayoongelea hapa ni kuwa Lowasa hawezi kumnanga Membe bungeni hata kama kuna ukweli wa anachosema.

Unakumbuka EL aliposema ajira ni bomu tarajiwa, serikali ilimshukia. Hapo ndipo akina Kinana na Mangula watakapoingia na tutasikia watu wakiitwa Dodoma kuhojiwa.

Nidhamu ni ile ya chama kumshukia Fikunjombe kwa kusaini karatasi ya Zitto au Mkono kusema nani ataondoa jina langu.
Lakini pia nidhamu ni ile ya kuzuia watu wenye kashfa nzito kuendelea kutumikia chama.

Mwaka 1995, Mrema aliwahi kulielezea hili vizuri sana, alisema hivi:

"Sikuwa na njia ya kumpinga mgombea wa CCM aliyepitishwa na ngazi zote zinazotakiwa na chama, hata kama hafai. Ukimpinga watauliza; huyu Mrema vipi, labda si mwenzetu. Mtu kama Kitwana Kondo kwangu mimi kama Mrema, Kitwana Kondo hafai kuwa diwani wa Kariakoo. Lakini mimi Mrema, kama CCM, Kitwana Kondo anafaa kuwa diwani wa Kariakoo."

Tutarajie Mangula na Kinana kutumiwa na Mwenyekiti katika kuwatisha na kuwatia adabu viongozi wote iwe wenye nia njema na taifa hili au nia mbaya. Kwamba nidhamu ya woga inaweza kurudi si kwa kutumia vifungu ndani ya katiba bali mkono wa chuma.

All that being said, nakuhakikishia kuwa itakuwa ni tiba ya panadol kupunguza maumivu na homa na si kutibu Malaria. Chama kimeshaharibika kwasababu sehemu kubwa sana ya wanachama wenye nia njema wapo nje ya system kilichobaki ni chama cha makundi.

Makundi ya akina EL, SamSix na Bashe yatapunguza kelele, guess what! undergorund movement zitakuwepo na madhara yake ni makubwa sana. Madhara ni makubwa kwasababu Mangula na Kinana watafanikiwa ku-supress harakati za makundi, hawata eliminate makundi.

Nakubaliana na wewe katika hili...; lakini kwa kuongezea, binafsi sidhani kama Mangula na Kinana wanatarajiwa kufuta makundi au kuya supress, kwani tatizo hili sio la upande mmoja, kila mkubwa ndani ya chama ana kambi yake kuelekea 2015, na ni wahusika hawa hawa kwa pamoja ndio waasisi wa hili; Nachoona ni Kinana na Mangula kutarajiwa to heal the wounds, na kuwapatanisha kwa makubaliano mbalimbali ya madaraka kwamba nyinyi mtapewa uwaziri mkuu, nyinyi urais, nyinyi uspika, nyinyi mambo ya nje, nyinyi fedha n.k; Sioni lingine likifanywa na kina kinana kuhusiana na suala la makundi;

Ili CCM kiweze kurudi katika hali yake ya zamani ni lazima kutokee mpasuko by force au naturally. By force ni Mangula na Kinana kuchukua hatua ngumu sana dhidi ya establishment na interest za waharibifu wa chama.

...Naturally: nisingeshauri chama chako kisubiri.
...Si shauri kwasababu KANU na UNIP zimepitia huko, that has proved futile.

Upo sahihi katika hili; Njia pekee ya kukivusha Chama salama 2015 ni aidha kukisafisha (jambo ambalo haliwezekani kutokana na dhambi ya asili) au kukivunja vipande viwili (suala ambalo nalo ni gumu kutekelezeka kwani wale ambao ndio potential dissents hawana agenda nyingine zaidi ya ufisadi, ndio maana wanasita; lakini wakiamua kufikiria na bongo zao badala ya utumbo, agenda zipo nyingi sana, na ni endelevu, kwa mfano masuala niliyoainisha kwenye uzi wangu mwingine:
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/355066-mangula-kinana-na-hatima-ya-taifa-letu.html

Ni lazima kundi litakalojitoa lianze kwa kusema sisi uchaguzi wa 2015 hatuna interest katika ngazi zote – Urais, Ubunge, Udiwani kwani kipindi cha 2012 – 2020 itakuwa ni kipindi cha kujenga chama; Wakianza na msimamo huu, hakika watakaobakia kwenye chama hiki watakuwa wale wasiokuwa na uroho wa madaraka, na waroho hawa watakimbilia Chadema na kwingineko;

Kwa bahati mbaya kikwazo kitakuwa Mwenyekiti wa CCM ambaye ni dhaifu lakini mwenye kauli ya mwisho.

Ikifika hapo bado nabaki kuamini kuwa Mangula na Kinana wameamua kuchafua CV kama zilikuwa nzuri.
Sielewi kwanini wamejitwisha zigo hili wakijua wazi kuwa the rift is so huge to fix within 2 years of their tenure.

Hivi kweli haudhani kwamba uamuzi wa kuwateua mangula na Kinana haujaenda sambamba na makubaliano fulani na Mwenyekiti juu ya utendaji na maamuzi ndani ya chama kuelekea 2015? Hivi kweli Kinana na Mangula wangekubali kuchukua nyadhifa zao kwenda kufanya kazi chini ya mazingira yale yale ya Mukama na Msekwa ambayo ni very predictable? I beg to differ- binafsi nashawishika kuamini kwamba kuna jambo kubwa sana ambalo hatulijui, hasa uwezekano kwamba kutokana na machafuko yanayoendelea na pia kampeni za kumtoa Mwenyekiti ,sitashangaa iwapo ameshauriwa kuachia nyadhifa hii na yeye kukubali in practice, lakini kuendelea na wadhifa husika in theory ili kwanza kutowapa mwanya maadui, lakini muhimu pia ili nchi isitikisike; Sitashangaa many years later kuja kufahamu kupitia different historians kwamba "Mwenyekiti wa wakati ule alishaachia Ngazi Muda mrefu sana"; Mimi nadhani kwa sasa, Mwenyekiti wa Chama in practice ni Mangula, na ni sehemu ya makubaliano vinginevyo haiingii akilini Mangula kukubali wadhifa huu katika kipindi hiki;

Labda ningeshauri uwaambie watu wa chama chako yafuatayo.
1. CCM must take difficult decision to weed out ring leaders regardless how potential or prominent they're.
2. Restore the recruitment program based on merit and not tech know who (your very valid point)
3. Dissolve the party organs and call for new election (pristine) before 2015.

Niwashauri nikiwa kama nani? Sina muda wa kuwashauri watu ambao hata Mwalimu walikuwa wanachukua ushauri wake kwa shingo upande kutokana na nguvu ya umma aliyokuwa nayo, ndio iwe mimi Mchambuzi? Sina muda wala motivation kwa hilo, muda nilionao, tena mwingi sana, ni wa kubadilishana mawazo na watanzania wa vyama vyote kwa HOJA juu ya mapungufu ya chama tawala katika muktadha wa maslahi ya taifa letu kwani CCM ina athiri kila mtanzania kutokana na kuwa chama tawala kwa zaidi ya miaka 50 i.e kutokana na kuwa madarakani miaka 50 mfululizo, kwa kupenda au kutopenda, CCM ina impact maisha ya watanzania walio wengi, katika nyanja zote za maisha yao ya kila siku- kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni;

Then, Natarajia ku achieve kitu gani? Ni mambo mawili ambayo inawezekana yakaonekana hayana maana kwa wengi:

Kwanza, hawa watawala wanaotusumbua vichwa miaka 15 ijayo watakuwa wastaafu wakila pension zao; Kama mtu bado ni kijana na unaingia katika makundi haya, hautakuwa na sehemu ya kujificha au kuongea la maana watanzania wakakuheshimu miaka 15 – 20 tokea sasa; Naangalia mbele, siangalii leo; Na Pili, nina amini mpaka sasa nipo kwenye upande sahihi wa historia ya Chama Chetu; Hivyo natarajia watoto na wajukuu zangu wakija kusikia mawazo ya baba au babu yao miaka 20 au 25 baadae, waje kusema kwamba Baba au Babu hakika Chose the right side of history right from the outset;

Vinginevyo nilishakataa kuwekeza kwa wapita njia;

Otherwise this could be the beginning of the end on the hands of Kinana and Mangula.

I tend to believe so...
 
Je, ni vigezo gani hutumiwa na CCM kumpata mgombea Urais? Najua wengi katika mjadala huu wataleta hoja khanga, kofia, n.k, kwani ukweli ulio wazi ni kwamba Chama kimechafuka; Lakini tukiweka hili pembeni kwa sasa, Vigezo vinavyotumika kuteua jina la mtu kuwa mgombea Urais (CCM) vipo vingi, na vingine ni very arbitrary na pia mchakato wake sio democratic; Lakini huo ni mjadala mwingine, na kwa sasa ningependa kujadili vigezo vifuatavyo:

  1. Awe na Sifa za Kuwa Mbunge Kufikia Kipindi husika
  2. Awe Mjumbe wa NEC Kufikia Kipindi Husika
  3. Jina lake liwe familiar miongoni mwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa
  4. Asiwe amethibitika kwamba ni mla rushwa (tetesi hazitoshi)/Awe na Sifa Za Kukemea Rushwa
  5. Na Awe na Umri utakaovutia Wapiga Kura Vijana
Kwa mtazamo wangu, mgombea Urais kupitia CCM (2015) atateuliwa kwa kigezo aidha namba nne au namba tano, kulingana na upepo wa siasa utakavyokuwa; Kwa upande mmoja, iwapo Chadema utamweka Kijana kwa mfano Zitto au Lissu, CCM itajibu mapigo kwa kumweka Kijana ambae atakuwa ni January Makamba; Kwa upande mwingine, iwapo agenda ya Vita dhidi ya Ufisadi itazidi kushika kasi chini ya Chadema, hasa iwapo CCM haitatoa kafara angalau watu wawili watatu kuonyeshe progress towards that end, na Chadema kumweka Dr. Slaa au Hata Lissu, CCM italazimika kumweka mgombea ambae atatumika kurudisha imani kwa wananchi kwamba Chama kipo tayari kumaliza rushwa nchini, hivyo kumsimamisha Bernard Membe;

Mchambuzi kwanza naomba usisahau kuwa, pamoja na kuwa Kofia, Khanga, pilau, na vingine kama hivyo kwa kiingereza tunaweza kuviita cheap, tupende tusipende vina-play big role kwenye upigaji kura hasa ndani ya CCM. Sina hakika kama hii ina nguvu sana kwenye upigaji kura ndani ya Chama ngazi ya NEC, lakini naamini kuwa kuna kitu kama hicho lakini kwa sura na ukubwa tofauti. Kwa hiyo ni lazima tukubali kuwa kipo, na huenda kitaendelea kuwepo.

Siku hizi ndani ya CCM, usafi, uadilifu, uwezo wako kichwani, utendaji na vitu kama hivyo.... SI vigezo vya kuchaguliwa kuwa kiongozi, you must be naive to believe in those. Watu wengi wa namna hiyo ndani ya CCM wamewekwa pembeni, na wataendelea kuwekwa pembeni kama wanafikiri usafi, uadilifu, umakini, uwezo wa kazi ndio vitawawezesha kuchaguliwa. Wanaopiga hatua ni wale ambao.....wanacheza michezo michafu kama walivyo wachafu, wasio na uwezo kichwani, au wanatumia wafadhili fulani ambao baadaye wanawalipa fadhila kwa kuwasaidia kuchaguliwa. Mfano mzuri kabisa ni wewe mwenyewe [kumbuka kinyang'anyiro cha ubunge, wenye akili walipenda wewe na wengine kama wewe mshinde, lakini kilichotokea unajua] Ukweli huu upo kwenye chaguzi za CCM katika ngazi zote. Kwa hiyo bado naona kuwa khanga, kofia, T shirt, pilau nk vitandelea. Siasa zetu zimekeuwa chafu, hata kama wewe ni msafi, muadilifu...unatakiwa kuingia kwenye uhuni kwa muda ili uweze kupita.

Sababu hii naweza kusema ndio inafanya hata baadhi ya watu wenye uwezo mkubwa wa kuisaidia Tanzania, kuchagua kukaa pembeni kwa kutotaka kujiingiza kwenye mambo machafu.

Tukija kwenye vigezo vya nani anastahili kugombea urais (hata ubunge, ujumbe wa NEC, etc)...kigezo cha asiwe amethibitika kupokea rushwa na awe na uwezo wa kukemea rushwa, naweza kusema kipo akilini, vinywani au kimaandishi tu, kivitendo hakipo kabisa. Kimsingi mazingira yaliypo ndani ya Chama, yanafanya watu wengi wanaogombea nafasi kupitia CCM wawe na lengo kuu la kutaka kukaa kwenye meza wazapoweza kupokea rushwa sana au rushwa kubwa, au kufanikisha mambo yao machafu kwa mwamvuli wa CCM bila kubugudhiwa na serikali. Wanaweza kutumia lugha yoyote ile lakini ukweli unabaki pale pale.

Issue hapa ni kuwa ndani ya CCM kimsingi definition ya rushwa inategemea ni nani anatuhumiwa. Na ni kigezo ambacho naweza kusema ni cha kitoto na kimepitwa na wakati. Sijui kwa kiswahili tunasemaje, lakini kama tunazungumzia rushwa as bribe, [yaani hongo au mlungula] ni kitu kimoja, na corruption (ufisadi) ni kitu kingine. Kwa tafisiri ya CCM Chenge, Lowassa, Mgonja, Mkapa na wengine ni watu safi...ndio maana bado wako ndani ya chama na kwenye vyombo vya juu vya chama. Sijui kama Bernard Membe na January Makamba wanaweza kuqualify kwa vigezo hivyo, yaani they are clean in the sense that they are not somehow touched with kickbacks and corruption.

Lakini let us be realistic..do you see Bernard Membe or January Makamba for that matter, as people who can stand firm and denounce corruption? Au yatakuwa ndio yale yale ya kusimama majukwaani na kuwazuga watanzania kuwa nachukia rushwa wakati mwenyewe ni fisadi mkubwa. Kati ya hao wawili unaamini kuna yeyote anayeweza kudeal na Mboma, Mkapa, JK, Mwang'onda, Mgonja, Balali, Shimbo na wengine wote waliotajwa kwenye kashfa ya ufusadi? Au unaamini kwa uhakika kuwa kati ya hao kuna mwenyewe uwezo wa kuifumua EPA, IPTL, Richmond, Radar etc etc ...I real doubt.

The point i am trying to make here is, ufisadi is order of the day kwa CCM, na itakuwa ni factor ya kushinda kwenye uchaguzi katika ngazi yoyote. Na hata kama CCM watashinda 2015, hawatashinda kwa votes watashinda kwa sababu hiyo. Ndani ya CCM hakuna anayeweza kuitumia kama ni factor ya kumu-disqualaify mtu kugombea nafasi ndani ya chama. Tupende au tusipende. With Mangula as vice chairman or with Kinana GS, kiuhalisia CCM na ufisadi havitatengana.
Kwa maana nyingine noana kama hata wewe unaona kuwa issue ya ufisadi ndio itakayoiondoa CCM madarakani, kwa kuwa hakuna ambaye yuko safi kabisa kwa tetesi au ushahidi, wasafi wako Chadema kwa kuwa wao hawakukaa kwenye meza ambazo ziliwapa ulaji, na hakuna tetesi au ushahidi wa wao kuwa wala rushwa.

Factor ya kusema awe na umri wa kutia vijana, sidhani kama kwa sasa itafanya kazi. Kikwete aliingia kwa namna hiyo, na watanzania tulikuwa na hope kuwa tutapiga hatua sana kutokana na yeye kuwa Rais, lakini angalia disaster iliyopo sasa. Unless kuwe na sababu nyingine, lakini ya ujana na kuvutia vijana ni factor ya hatari sana, na ndiyo hiyo ambayo imetufikisha hapa kwa leo.

Naona ni vizuri tukiendelea kuwa na subira, kuazia mwanzoni mwa mwaka 2014 tutaanza kuwa na picha nzuri kama tutakuwa na rais nduli, msafi, tapeli, mzugaji au myeyushaji, au mtu ambaye anaweza kuiongoza Tanzania kuelekea kunakotakiwa, katika mazingira mapya ya kimataifa na katika realities mpya ndani ya nchi.
 
Bongolander,

Nashukuru kwa mchango wako mzuri wenye hoja za maana sana – kwenye bandiko lako namba 154; Naomba nianze na hili la Kura Za Pilau kutupatia Rais ajaye kupitia CCM; Ulichosema ni sahihi, na hata juu ya NEC ambako ni kama vile hauna uhakika na matumizi ya pilau kutupatia viongozi, huko nako Pilau hutumika – ujue tu kwamba Pilau huja kwa njia nyingi, vipo vitu vingi ambavyo ni synonymous to Pilau in this context;

Wajumbe wengi wa NEC wapo pale sio kujenga chama bali kuboresha mazingira yao ya posho na kickbacks za hapa na pale kwani ajira ya Chama sasa imegeuka kuwa kama vile ni Ajira Vodacom, Barclays n.k, na ndio maana hata vyombo vya habari navyo vimepotoka katika suala zima la utumishi kwa WANANCHI/UMMA, hasa pale vinaposema fulani na fulani WAMEULA kwa kuteuliwa kushika nafasi fulani; Kweli uongozi wa UMMA ni kuula? Kupotoka huku kwa MEDIA kuna athiri sana Uzalendo miongoni mwa watoto wetu wenye ndoto za ku-pursue careers in politics;

Vinginevyo ujumbe wa NEC kwa kweli ni mzigo kwani ni lawama chungu nzima, hasa iwapo tunatazama nyadhifa hizi kama utumishi kwa wanachama milioni tano au wananchi kwa kuzingatia kwamba NEC ni kama Baraza la Mawaziri la CCM ambalo lina influence kubwa sana na maamuzi ya kisera kwa serikali yake; Lakini kwa vile wana-CCM wengi hugombea ujumbe wa NEC kama njia ya kutafuta ajira kama sekta binafsi, wengi wataendelea kutumia muda mwingi zaidi to pursue and maximize private gain, badala ya public gain, hasa nyakazi za chaguzi ambazo wengi huita MSIMU WA MAVUNO; Hili halitabadilika, na tusitarajie mgombea asiye na pesa kupitishwa na CCM 2015 – iwe ni Udiwani, Ubunge au Urais;

Mbaya zaidi ni kwamba tofauti na CCM ya zamani ambapo busara, rationality, elimu na uzoefu zilikuwa miongoni mwa Sifa kuu za mtu kuchaguliwa kiongozi, leo hii ili upate kukubalika ngazi za juu za chama na kwa wanachama kwa ujumla, ni lazima uwe ignorant, dishonest, irrational and stubborn; Hizi ndio qualities za leadership ndani ya CCM ya leo;

Tukija kwa wapiga kura sasa (wananchi), swali linalofuatia ni je, Why Do Good People Accept Bad Government or Leadership? Binafsi nadhani majibu yapo kwenye maeneo mawili: Culture & Corruption;

Tukianza na Culture – kwa kifupi, An average Tanzanian (mpiga kura) ana amini kwamba yeye ni Mtanzania kwa sababu ya Mtanzania mwingine, Sio Kwa Sababu Yeye ni Mtanzania; Vile vile kwa vile watanzania wengi hawana elimu (illiterate), wengi ni fatalistic – kwa maana ya kwamba wana 'a submissive mental attitude' ambapo huishi kwa kuamini kwamba kila kitu kinachotokea in their surroundings kipo ‘predetermined and inevitable.' Kwa mtazamo wa wengi, there is little they can do to control events, na ndio maana wanakuwa submissive kwa CCM kwa miaka zaidi ya 50, licha ya kuishi maisha ya ufukara; Wengi wanamuachia kila kitu mungu, na ni kutokana na such acceptance of a supernatural order, watanzania wengi are less likely to challenge harsh realities in the present life; This acceptance of hardship ni sehemu kubwa sana ya African personality;

Tukija kwenye Corruption – Hili linaeleweka; Mzizi mkubwa wa rushwa Tanzania ni uvivu wa kufanya kazi, strong family ties (extended families) na kupenda maisha ya anasa, na yote haya yanaweka so much pressure katika utafutaji wa pesa, come what may; Hii huchangia sana ufisadi kila kona;

Pia umekuja na swali na kujenga hoja kwamba haudhani Membe na January wataweza kuangamiza ufisadi; Kwanza naomba niseme kwamba hakuna kiongozi au chama ambacho kitaweza maliza Ufisadi Tanzania, sio CCM, Sio Chadema, Sio CUF…; Ni muhimu wananchi wakajua hilo, vinginevyo kuwaambia otherwise ni kuwatapeli kisiasa; Wanachoweza fanya Chadema au baadhi ya viongozi waadilifu ndani ya CCM iwapo watapewa madaraka ya nchi ni kupunguza tatizo, hasa kwa kuweka sheria zenye meno; Muhimu pia ni kwamba wananchi wanachohitaji ni matumaini kwamba maisha yao yataboreshwa, wakishaona hiyo ‘hope', ambayo inaendana na wao kushirikishwa katika maamuzi kisera, matumizi ya kuridhisha ya kodi zao, utawala wa sheria ambapo haki hainunuliwi n.k, nina amini wananchi wengi wataongeza imani yao kwa viongozi na Chama husika; Lakini chini ya CCM kwa sasa, watanzania live in hopelessness and despair;

Sasa nikija kwa hawa Membe na January, katika hoja yangu ya msingi nilisema kwamba hawa wataweza kuwa viongozi wazuri only under certain conditions, na hili la kukemea rushwa nilijadili pia; Vinginevyo nilisema kwamba kwa sasa bado sioni mwana ccm who can earn my support, endorsement or vote, kwani miongoni mwa wanaotajwa tajwa, sielewi wanasimamia nini na kwanini when it comes to our country and the future of her people; Ushabiki unaoendelea ni kama vile tunajiandaa kuchagua kiongozi wa Simba au Yanga; Vinginevyo msingi wa hoja yangu hii haikuwa kuwapigia debe hawa wawili bali kuelezea mtazamo wangu juu ya possibilities za wao kuteuliwa KWA HOJA, hasa kutokana na utamaduni wa CCM na pia jinsi gani things have been unfolding in the recent past; Kwahiyo mpaka tutakaposikia Membe, January, na wengine, kwanza wakitanganza nia, halafu kutuambia their vision of the future, sidhani kama kwa muda huu tunaweza sema fulani kutoka CCM anatufaa;

Angalau kwa Chadema wapo viongozi ambao wamekuwa wanajitahidi kutenganisha Personalities Zao na issues Wanazosimamia; Kwa mfano, when it comes to Dr. Slaa au Tundu Lissu, angalau kuna mwanga kuhusu nini wanataka kuifanyia TANGANYIKA YETU, nini wanapanga kufanya kuhusu UFISADI, nini wanataka kufanya kuhusu uimarishwaji wa UTAWALA WA SHERIA (sio tu utawala bora kama CCM), n.k; Ni kutokana na haya, ndio maana nahimiza tena kwamba Lissu au Slaa so far ni better choice ya Urais kwa nchi yetu, na itabakia hivyo mpaka pale CCM itakapokuja na mgombea au wagombea wa kujipima na hawa kwa maelezo niliyojadili hapa and elsewhere;
 
Bongolander,

Nashukuru kwa mchango wako mzuri wenye hoja za maana sana – kwenye bandiko lako namba 154; Naomba nianze na hili la Kura Za Pilau kutupatia Rais ajaye kupitia CCM; Ulichosema ni sahihi, na hata juu ya NEC ambako ni kama vile hauna uhakika na matumizi ya pilau kutupatia viongozi, huko nako Pilau hutumika – ujue tu kwamba Pilau huja kwa njia nyingi, vipo vitu vingi ambavyo ni synonymous to Pilau in this context;

Wajumbe wengi wa NEC wapo pale sio kujenga chama bali kuboresha mazingira yao ya posho na kickbacks za hapa na pale kwani ajira ya Chama sasa imegeuka kuwa kama vile ni Ajira Vodacom, Barclays n.k, na ndio maana hata vyombo vya habari navyo vimepotoka katika suala zima la utumishi kwa WANANCHI/UMMA, hasa pale vinaposema fulani na fulani WAMEULA kwa kuteuliwa kushika nafasi fulani; Kweli uongozi wa UMMA ni kuula? Kupotoka huku kwa MEDIA kuna athiri sana Uzalendo miongoni mwa watoto wetu wenye ndoto za ku-pursue careers in politics;

Vinginevyo ujumbe wa NEC kwa kweli ni mzigo kwani ni lawama chungu nzima, hasa iwapo tunatazama nyadhifa hizi kama utumishi kwa wanachama milioni tano au wananchi kwa kuzingatia kwamba NEC ni kama Baraza la Mawaziri la CCM ambalo lina influence kubwa sana na maamuzi ya kisera kwa serikali yake; Lakini kwa vile wana-CCM wengi hugombea ujumbe wa NEC kama njia ya kutafuta ajira kama sekta binafsi, wengi wataendelea kutumia muda mwingi zaidi to pursue and maximize private gain, badala ya public gain, hasa nyakazi za chaguzi ambazo wengi huita MSIMU WA MAVUNO; Hili halitabadilika, na tusitarajie mgombea asiye na pesa kupitishwa na CCM 2015 – iwe ni Udiwani, Ubunge au Urais;

Mbaya zaidi ni kwamba tofauti na CCM ya zamani ambapo busara, rationality, elimu na uzoefu zilikuwa miongoni mwa Sifa kuu za mtu kuchaguliwa kiongozi, leo hii ili upate kukubalika ngazi za juu za chama na kwa wanachama kwa ujumla, ni lazima uwe ignorant, dishonest, irrational and stubborn; Hizi ndio qualities za leadership ndani ya CCM ya leo;

Tukija kwa wapiga kura sasa (wananchi), swali linalofuatia ni je, Why Do Good People Accept Bad Government or Leadership? Binafsi nadhani majibu yapo kwenye maeneo mawili: Culture & Corruption;

Tukianza na Culture – kwa kifupi, An average Tanzanian (mpiga kura) ana amini kwamba yeye ni Mtanzania kwa sababu ya Mtanzania mwingine, Sio Kwa Sababu Yeye ni Mtanzania; Vile vile kwa vile watanzania wengi hawana elimu (illiterate), wengi ni fatalistic – kwa maana ya kwamba wana 'a submissive mental attitude' ambapo huishi kwa kuamini kwamba kila kitu kinachotokea in their surroundings kipo ‘predetermined and inevitable.' Kwa mtazamo wa wengi, there is little they can do to control events, na ndio maana wanakuwa submissive kwa CCM kwa miaka zaidi ya 50, licha ya kuishi maisha ya ufukara; Wengi wanamuachia kila kitu mungu, na ni kutokana na such acceptance of a supernatural order, watanzania wengi are less likely to challenge harsh realities in the present life; This acceptance of hardship ni sehemu kubwa sana ya African personality;

Tukija kwenye Corruption – Hili linaeleweka; Mzizi mkubwa wa rushwa Tanzania ni uvivu wa kufanya kazi, strong family ties (extended families) na kupenda maisha ya anasa, na yote haya yanaweka so much pressure katika utafutaji wa pesa, come what may; Hii huchangia sana ufisadi kila kona;

Pia umekuja na swali na kujenga hoja kwamba haudhani Membe na January wataweza kuangamiza ufisadi; Kwanza naomba niseme kwamba hakuna kiongozi au chama ambacho kitaweza maliza Ufisadi Tanzania, sio CCM, Sio Chadema, Sio CUF…; Ni muhimu wananchi wakajua hilo, vinginevyo kuwaambia otherwise ni kuwatapeli kisiasa; Wanachoweza fanya Chadema au baadhi ya viongozi waadilifu ndani ya CCM iwapo watapewa madaraka ya nchi ni kupunguza tatizo, hasa kwa kuweka sheria zenye meno; Muhimu pia ni kwamba wananchi wanachohitaji ni matumaini kwamba maisha yao yataboreshwa, wakishaona hiyo ‘hope', ambayo inaendana na wao kushirikishwa katika maamuzi kisera, matumizi ya kuridhisha ya kodi zao, utawala wa sheria ambapo haki hainunuliwi n.k, nina amini wananchi wengi wataongeza imani yao kwa viongozi na Chama husika; Lakini chini ya CCM kwa sasa, watanzania live in hopelessness and despair;

Sasa nikija kwa hawa Membe na January, katika hoja yangu ya msingi nilisema kwamba hawa wataweza kuwa viongozi wazuri only under certain conditions, na hili la kukemea rushwa nilijadili pia; Vinginevyo nilisema kwamba kwa sasa bado sioni mwana ccm who can earn my support, endorsement or vote, kwani miongoni mwa wanaotajwa tajwa, sielewi wanasimamia nini na kwanini when it comes to our country and the future of her people; Ushabiki unaoendelea ni kama vile tunajiandaa kuchagua kiongozi wa Simba au Yanga; Vinginevyo msingi wa hoja yangu hii haikuwa kuwapigia debe hawa wawili bali kuelezea mtazamo wangu juu ya possibilities za wao kuteuliwa KWA HOJA, hasa kutokana na utamaduni wa CCM na pia jinsi gani things have been unfolding in the recent past; Kwahiyo mpaka tutakaposikia Membe, January, na wengine, kwanza wakitanganza nia, halafu kutuambia their vision of the future, sidhani kama kwa muda huu tunaweza sema fulani kutoka CCM anatufaa;

Angalau kwa Chadema wapo viongozi ambao wamekuwa wanajitahidi kutenganisha Personalities Zao na issues Wanazosimamia; Kwa mfano, when it comes to Dr. Slaa au Tundu Lissu, angalau kuna mwanga kuhusu nini wanataka kuifanyia TANGANYIKA YETU, nini wanapanga kufanya kuhusu UFISADI, nini wanataka kufanya kuhusu uimarishwaji wa UTAWALA WA SHERIA (sio tu utawala bora kama CCM), n.k; Ni kutokana na haya, ndio maana nahimiza tena kwamba Lissu au Slaa so far ni better choice ya Urais kwa nchi yetu, na itabakia hivyo mpaka pale CCM itakapokuja na mgombea au wagombea wa kujipima na hawa kwa maelezo niliyojadili hapa and elsewhere;
Swadakta kama CCM wanasikia Umeongea !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!ebu ngoja uone Mangula na mwenzie wataweza akili ya uliowataja CDM!!!!
 
Ndani ya intarahamwe yupo ila kwa wananchi hamna hata mmoja
 
Ndugu zangu JF , kwanza kabisa nipeleke shukrani zangu za dhati kwenu wana jukwaa hili la muhimu katika kuijenga jamii yetu , Nataka kufahamu Bernard Kamilius Membe anatumia vigezo gani kwa kujipima anaweza kuwa raisi wa tano (5) wa JMT ? Je kwa uzoefu gani alionao katika Nchi hii ? Au anadhani kuwa Waziri wa Mambo ya Nje ndo kigezo tosha kuwa raisi wa JMT ? Kwa kipindi kifupi cha huyu bwana nchi yetu imekuwa dampo la Madawa ya kulevya yakitokea Nje ya Nchi. Sasa kama suala hili limemshinda ndo Nchi utaiweza ? Nitasikitika sana kama chama cha chake kitampitisha kuwania Nafasi hii adhimu hapa Nchini.




Ndugu zangu JF , kwanza kabisa nipeleke shukrani zangu za dhati kwenu wana jukwaa hili la muhimu katika kuijenga jamii yetu , Nataka kufahamu Bernard Kamilius Membe anatumia vigezo gani kwa kujipima anaweza kuwa raisi wa tano (5) wa JMT ? Je kwa uzoefu gani alionao katika Nchi hii ? Au anadhani kuwa Waziri wa Mambo ya Nje ndo kigezo tosha kuwa raisi wa JMT ? Kwa kipindi kifupi cha huyu bwana nchi yetu imekuwa dampo la Madawa ya kulevya yakitokea Nje ya Nchi. Sasa kama suala hili limekushinda ndo Nchi utaiweza ? Nitasikitika sana kama chama cha chako kitakupitisha kuwania Nafasi hii adhimu hapa Nchini ^^
 
Hili sawali sijui anaulizwa membe au tunaulizwa wanajukwaa?
 
Back
Top Bottom