Elections 2015 Mgombea Urais CCM 2015: Ni Bernard Membe au January Makamba

Elections 2015 Mgombea Urais CCM 2015: Ni Bernard Membe au January Makamba

Mchambuzi

Uchambuzi wako nimeukubali kwa kiasi fulani ila kama mchangiaji mwingine aliyesema uliharibu kidogo kwa kumpigia debe Tundu Lissu mwishoni.

Kwa manufaa ya wasomaji ungeandika sifa chanya na hasi za wajumbe wote wa NEC Taifa. Wajumbe wa bara na Visiwani maana wajumbe hawako kumi tu wako kumi toka bara na kumi toka visiwani. Labda uanze kuandika mjumbe mmoja baada ya mwingine kwa kutumia vigezo vitano ulivyoambatanisha hapo juu. Mfano katika kumi bora Mjumbe namba moja ana vigezo hivi hapa 1,2 3 hana vigezo 1,2,3 then u go down the line. Start with Wassira, Makamba, Nchemba mpaka Mukangara. Vivyo hivyo kwa upande wa Visiwani Dr. Mwinyi, Prof. Mbarawa, Samia Hassan mpaka wa kumi Khadija Aboud.

Swali jingine kati ya Dr. Mwinyi na Wassira nani amepata kura nyingi zaidi. Maana nimeona kura zote za bara lakini kwa visiwani naona yamebandikwa majina tu bila idadi ya kura
 
Last edited by a moderator:
Uchambuzi wako nimeukubali kwa kiasi fulani ila kama mchangiaji mwingine aliyesema uliharibu kidogo kwa kumpigia debe Tundu Lissu mwishoni.

Kwa manufaa ya wasomaji ungeandika sifa chanya na hasi za wajumbe wote wa NEC Taifa. Wajumbe wa bara na Visiwani maana wajumbe hawako kumi tu wako kumi toka bara na kumi toka visiwani. Labda uanze kuandika mjumbe mmoja baada ya mwingine kwa kutumia vigezo vitano ulivyoambatanisha hapo juu. Mfano katika kumi bora Mjumbe namba moja ana vigezo hivi hapa 1,2 3 hana vigezo 1,2,3 then u go down the line. Start with Wassira, Makamba, Nchemba mpaka Mukangara. Vivyo hivyo kwa upande wa Visiwani Dr. Mwinyi, Prof. Mbarawa, Samia Hassan mpaka wa kumi Khadija Aboud.

Swali jingine kati ya Dr. Mwinyi na Wassira nani amepata kura nyingi zaidi. Maana nimeona kura zote za bara lakini kwa visiwani naona yamebandikwa majina tu bila idadi ya kura

Hivi ni kwanini mnasema nimeharibu kwa kumtaja Lissu mwishoni wakati ukweli ulio wazi ni kwamba hii ni timu ya CCM inayojipanga kuingia katika ushindani na chadema 2015? Ni dhahiri mgombea wa Chadema 2015 atakuwa ni mtu makini kama vile Dr. Slaa au Lissu, na ni muhimu CCM ikajipima kwa mtazamo huo, kwani hawa wawili ni viongozi bora kwa vigezo vingi na itaendelea kuwa hivyo mpaka pale CCM itakapokuja na jina ambalo nalo over time lita convince umma kwamba na yeye pia ni kiongozi Bora; Ni muhimu mkaelewa kwamba Chadema wao ni kama wapo tayari in terms of candidates wenye sifa, kinachosubiriwa ni upande wa CCM tu, na ni kwa maana hii, katika maandalizi hayo, ni vyema CCM ikajipima kwa majina kama LISSU, otherwise mchakato wao wa huko Dodoma kujipanga 2015 utakuwa ni kupoteza tu muda;

Bila ya CCM kuja na mkakati ambao utazaa mgombea mwenye kuweza kuwathibiti Lissu au Dr. Slaa 2015, zoezi zima la Dodoma litakuwa limepoteza tu muda na fedha za chama; Na iwapo mjadala wangu ungepuuzia hili, mjadala huu ungekuwa na mapungufu makubwa sana, kwani Membe na January wakipitishwa wataenda kushindanishwa na nini, JIWE?

Hoja yako juu ya haja ya kuchambua sifa za wajumbe wote wa NEC ni nzuri lakini maudhui ya uzi huu haikuwa hiyo; Kama kuna umuhimu wa kufana hivyo, hata wewe ungekuja tu na uchambuzi huo kwani tungechangia kwa wingi tu kwa hoja, na kwa kujenga, sio kubomoa;

Kuhusu kura za Mwinyi na Wassira, nadhani Wassira amepata kura nyingi zaidi, kwani kama vile niliona sehemu kwamba Mwinyi kapata kura around 1,800, ila nita confirm nikipata taarifa kamili;
 
Sidhani kama ni rahisirahisi ccm kupata 50% kwa uchaguzi wa 2015 kulingana na hali ya maisha ilivyo sasa kwa wananchi[kiuchumi] na kijamii. Wao wateuane tu ila siku itafika,tanzania ya leo sio kama ya enzi hizo,Ukiwaimbia,ukiwanyanyasa na ukiwagandamiza watanzania, wanajua.Watakemea,wataonya na watachambua pumba na mchele ifikapo 2015 kupitia kura yao.

Kipimo kizuri juu ya kura za CCM kufikia 50% au zaidi ni matokeo ya ubunge katika mikoa yote ya bara uchaguzi wa 2010.

Kwa mfano, katika mikoa yote ambayo kwa juu juu mtu unaweza kudhania ni ngome za Chadema, ukiangalia jumla ya Kura za ubunge kwa kila mkoa, CCM iliishinda chadema kwa at least 55%; hata Arusha ambayo inadhaniwa kuwa ni ngome ya Chadema, jumla ya kura za ubunge katika majimbo yote saba ya mkoa, baina ya CCM na Chadema, CCM ilipata wingi wa kura kwa asilimia at least 55%; Ukichanganya kura zote zilizopigwa for chadema na CCM katika majimbo haya, CCM won (in total katika majimbo yote saba) by at least 55%, i.e:

  • Longido (CCM)
  • Monduli (CCM)
  • Ngorongoro (CCM)
  • Arumeru Magharibi (CCM)
  • Arumeru Mashariki (Chadema)
  • Arusha Mjini (Chadema)
Ni muhimu Chadema wakatumia takwimu hizi kama changamoto yao kuelekea 2015; Vinginevyo kutumia takwimu za kura za Urais 2010 kidogo kuna tatizo kutokana na hoja kwamba kura katika ngazi ya Urais zilichakachuliwa; Tofauti na kura za Urais, kura za Ubunge kwa kiasi kikubwa ziliakisi uhalisia wa mambo on the ground;
 
Nashauri tuachane na siasa za watu (personalities/individuals), twende kwenye siasa za masuala (issues). Mimi kwangu atawale LISSU au MEMBE au MAKAMBA au MHINDI KUMAR au YELLOWMAN au yeyote, haina maana yeyote kwangu. Cha maana kwangu ni mwanangu aende shule bora na aelimike kwa viwango vya kimataifa; mama yangu akienda zahanati yetu ya kijiji apate dawa za maumivu yake ya mgongo; nkilima nyanya zangu nipate kwa kuuza; siment ipungue bei nijenge nyumba bora; nisiombwe rushwa nitaka huduma za serikali ninazozilipia kodi; nisibambikwe kesi na polisi; bima yangu ya afya iniwezeshe kupata tiba ya magonjwa yote nk - na yeyote atakayenihakikishia hayo, hata kama ni MKARA, mimi ntampa kura yangu.

KINGINE: Vyama vipunguze u-vyama, kwa sababu sasa hivi watu ambao ni wanachama wao ni wachache mno, TUJENGE UTAIFA ZAIDI kuliko u-vyama unaotugawanya

Naomba utembelee uzi wangu mwingine ufuatao:
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/350624-wagombea-urais-tiketi-ya-ccm-tunawapimaje.html
 
Unayoyasema yanawezekana ,ila ulitakiwa uende deep zaidi kwa sababu kuna uvumi kwamba January , Mwigulu na Shigella walitumia nguvu kubwa sana A.k.a mijihela , sasa kwenye kigezo chako namba 4 January hawezi ku fit, hata hivyo Urais siyo rahisi kiasi cha mtu kama January kuuweza , sijui kwa nini umejaribu kumpromot mtu huyu ! Ukizingatia tathmini yako , kumbuka kigezo cha 4 .
Ukisoma mstari kwa mstari na kuelewa maudhui yangu ambayo hasa ililenga kuelezea utamaduni wa CCM katika nyakazi hizi, ungeelewa kwamba mimi sipo hapa kumpigia kampeni January; Lakini nashukuru wapo wengi walioelewa maudhui yangu ilikuwa ni nini;
 
Mleta uzi kaamua kumhujumu makusudi Dk SLAA kwa maslahi ya ccm. Hata hivyo GT wameshamwelewa kusudio lake la ndani nalo sio hao Membe na Makamba bali kupima upepo juu ya Dk Slaa baada ya chaguzi hizi za ccm.

Unachosema sio sahihi, iwapo umekuwa unasoma michango yangu mbalimbali, na hata kwenye uzi huu, nathamini sana mchango wa Dr. Slaa katika siasa za nchi yetu, hasa katika kuinyoosha CCM kwani ilidhania wananchi wataendelea kulala; Dr. Slaa au Tundu Lissu - haya ndio majina ambayo nimekuwa nayajadili kwa CDM 2015, lakini kwa mtazamo wangu, Dr. Slaa anaweza kukumbwa na suala la umri, kwahiyo ni muhimu kwa CDM kuangalia CCM inamsimamisha nani; Vinginevyo iwe, isiwe, ni muhimu Dr. Slaa akawa kwenye safu ya uongozi wa juu wa nchi, aidha kama Waziri Mkuu au Makamo wa Rais, iwapo Urais utaenda kwa mtu mwingine ndani ya CDM, hasa Lissu;

Mimi sioni mtu mwingine ndani ya CDM mwenye qualities za Urais nje ya Zitto, Slaa na Lissu; Na ni muhimu CDM ikaendelea na mchakato wa kumpata mgombea ambae atatokana na CDM die hard aliyepo ndani ya CDM sasahivi, wasifanye kosa la kutegea mtu atakayejitoa CCM na kumweka huyo ndio mgombea; Itaharibu ladha na maana yote ya mabadiliko ambayo wananchi wanaounga mkono CDM leo wamekuwa wanayasubiria kwa hamu kubwa;
 
Mchambuzi, nakubaliana na wewe kwamba katika wajumbe 10 waliogombea NEC, Membe anaweza kufikiriwa kuwa mgombea wa CCM. Ingawa amepata nafasi ya sita kiuchaguzi, haimanishi hakubaliki sana kwa wajumbe, bali imetokana na vita vya kisiasa ambavyo vilielekezwa kwake kwa vile anajulikana ana malengo ya uraisi, hivyo alifanyiwa kampeni za kinyume kumzuia, hivyo kitendo cha kupata nafasi ya sita ni sifa tosha ya kuwa mpiganaji na kuvutia makundi ambayo hayakupenda kampeni chafu na maneno ambayo yalilenga kumboa na kumharibia sifa ili akose nafasi ya NEC.

Ndio maana nilisema awali kwamba kitendo cha membe na january kuamua kuingia kutafuta ujumbe wa NEC kupitia nafasi zile kumi za kifo ulikuwa ni uamuzi wa busara sana kwani whether you lose or win, tayari wapiga kura wa mchakato wa kumtafua mgombea urais 2015 watakuwa wameshakuona; Kumbuka kwamba ni hawa hawa waliompa kura January na Membe Dodoma ndio watakaopigia kura jina la mgombea mteule wa ccm 2015 kwani wajumbe hawa watakuwa kwenye nafasi zao hizo mpaka 2017;

Hata hivyo, naamini CCM bado wanaweza kumleta mtu mwingine nje ya wajumbe wa NEC au watu wengine wenye mvuto ambao ni wajumbe wa NEC kupitia wilaya. Kama walivyofanya kumleta Mangula , nafasi ya m/mwenyekiti.

Mtu aliyegombea ujumbe wa NEC kupitia wilaya atakuwa amecheza pata potea iwapo nia yake ilikuwa ni kuwania Urais 2015, partially kwa maelezo hayo juu; Wilay zimezaa wajumbe wa NEC zaidi ya mia moja, na wajumbe wa mkutano mkuu wa Taifa pengine wanajua majina kama 10% ya wajumbe wote waliopita ngazi za wilaya; Exception iliyopo ni kwa majina ya Lowassa, Nchimbi, Mwandosya na wengine wachache, ambao pamoja na kwamba wamepitia wilayani, majina haya yanajulikana na wajumbe wengi wa mkutano mkuu wa taifa, hivyo suala la wajumbe hawa wa NEC kuji - market kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa taifa 2015 iwapo watagombea Urais haitakuwa kubwa sana; lakini kwa mtazamo wangu, it is less likely kwa nchimbi kupita, hivyo mwishoni kuamua kujiunga na kundi la aidha membe au January; Same applies to Lowassa na Mwandosya;

Kwa jinsi ambavyo siasa za makundi zilivyoitesa CCM, si ajabu wakatumia ule mkakati wao maarufu wote wakose na wakaja na mtu mpya.

CCM haiwezi ku-risk na mchezo huu; kwanza itakuwa haina muda wa kutosha kuuza mgombea mpya kwa wapiga kura, na pili haitakuwa na resources za kutosha kufanya hivyo; Suala la time and resources constraints litachangiwa sana na ukweli kwamba CCM ina vita zaidi ya moja na itabakia kuwa hivyo mpaka 2015; Vita ya kwanza ni kuua makundi ndani ya CCM, vita ya pili ni kudhibiti M4C, na vita ya tatu ni kutafuta mgombea anayefaa kusimama 2015; Muda na resources kukamilisha haya yote haupo; Atakayepitishwa itakuwa ni miongoni mwa hawa hawa ambao tayari umma umewasikia, hivyo kuirahisishia CCM kazi kwenye kampeni huko mbeleni; Kilichobania ni CCM mwezi May 2015 kuamua nani ni serpent na nani ni angel, na je, kati ya angel na serpent yupo atafaa zaidi kuithibiti Chadema kweney uchaguzi mkuu?

Pia ni muhimu ukumbuke kwamba mwaka 1995, CCM ilifanya makosa unayoshauri yafanywe tena 2015 ya kuja na a surprise - kwa mfano Mkapa kuwa mgombea 1995; Nyerere alilazimika kufanya kazi ya ziadi kuzunguka nchi nzima na Mkapa lakini aliambulia kumpatia ushindi wa only 62%, lowest in CCM's history; Na huyo alikuwa nyerere, je leo hii au 2015, nani ndani ya CCM atakayekuwa na uwezo wa kumpigia debe mgombea mpya nchi nzima aibwage Chadema kwa kishindo uchaguzi wa 2015????

Hatima basi ni nini? Kwa vile mchakato wa CCM una matatizo mengi ya kumpata mgombea, kwani CCM itakuwa imejeruhiwa sana kumpata mgombea, basi upinzani una nafasi nzuri ya kutoa mgombea. Lakini kumbuka, CCM hawataacha mgombea mzuri apatikane kutoka kwa wapinzani. Mkakati wa mapandikizi ndani ya vyama vya upinzani umepata mashiko sana kwa watu wengine.
Mapandikizi ni pamoja na wagombea wenye kauli au msimamo ndumi la kuwili, pandikizi la udini na ukabila, haya yote yatafanya kazi kinyume cha kupata mzuri hasa CDM au atakapopatikana mgombea mzuri.

Good and valid argument;
 
Mchambuzi kuna mtu mwingine umemsahau naye Dr. Hussein Mwinyi!! Huyu naye ni figure ingine CCM wakitaka kurudisha imani kwa wananchi kuwa ni msafi wananweza mleta huyu!!

Nakubaliana na wewe lakini kwa mtazamo wangu, iwapo Mwinyi ata attempt, basi ataingia kwa gear ya kuwa mgombea wa zamu yetu wazanzibari, na nadhani ndio maana aliamua kuacha ubunge wa mkuranga (Bara)na kwenda kugombani Zanzibar 2000; Kwa bahati mbaya, itakuwa ni vigumu kwa Mwinyi kuwa a preferred choice ya CCM (Zanzibar) ahead of Amani Karume, na pengine Bilal kama atakuwa bado ana nguvu (umri); Nje ya hawa, Mwinyi pia atapata ushindani mkubwa kutoka kwa Nahoda ambae pia ana wafuasi wengi kutoka CCM (Zanzibar);
 
Nilisikia jamaa wakisema kijiweni.....ni ili kushinda kwa wepesi kwa vyama vyote, raisi ajaye lazma awe mkristu! Hata ukiweka jiwe tu ushindi nje nje kwani wakristu wamepotezwa sana katika kipindi hiki cha 2005 kuelekea 2015. Mi simo ila nilikuwa napita tu!
 
Hivi ni kwanini mnasema nimeharibu kwa kumtaja Lissu mwishoni wakati ukweli ulio wazi ni kwamba hii ni timu ya CCM inayojipanga kuingia katika ushindani na chadema 2015? Ni dhahiri mgombea wa Chadema 2015 atakuwa ni mtu makini kama vile Dr. Slaa au Lissu, na ni muhimu CCM ikajipima kwa mtazamo huo, kwani hawa wawili ni viongozi bora kwa vigezo vingi na itaendelea kuwa hivyo mpaka pale CCM itakapokuja na jina ambalo nalo over time lita convince umma kwamba na yeye pia ni kiongozi Bora; Ni muhimu mkaelewa kwamba Chadema wao ni kama wapo tayari in terms of candidates wenye sifa, kinachosubiriwa ni upande wa CCM tu, na ni kwa maana hii, katika maandalizi hayo, ni vyema CCM ikajipima kwa majina kama LISSU, otherwise mchakato wao wa huko Dodoma kujipanga 2015 utakuwa ni kupoteza tu muda;

Bila ya CCM kuja na mkakati ambao utazaa mgombea mwenye kuweza kuwathibiti Lissu au Dr. Slaa 2015, zoezi zima la Dodoma litakuwa limepoteza tu muda na fedha za chama; Na iwapo mjadala wangu ungepuuzia hili, mjadala huu ungekuwa na mapungufu makubwa sana, kwani Membe na January wakipitishwa wataenda kushindanishwa na nini, JIWE?

Hoja yako juu ya haja ya kuchambua sifa za wajumbe wote wa NEC ni nzuri lakini maudhui ya uzi huu haikuwa hiyo; Kama kuna umuhimu wa kufana hivyo, hata wewe ungekuja tu na uchambuzi huo kwani tungechangia kwa wingi tu kwa hoja, na kwa kujenga, sio kubomoa;

Kuhusu kura za Mwinyi na Wassira, nadhani Wassira amepata kura nyingi zaidi, kwani kama vile niliona sehemu kwamba Mwinyi kapata kura around 1,800, ila nita confirm nikipata taarifa kamili;

Kama alivyosema mchambuzi mgombea wa urais ndani ya CCM atatokea kundi la kifo kati ya bara na visiwani. Kwa maoni yangu huyo mgombea atakuwa ni kati ya wale waliokuwa kwenye tano bora kutokea kundi ka kifo. Exception pekee ya haya maoni yangu ni ni wafuatao Edward Lowassa (Mjumbe wa NEC Wilaya ya Monduli), Bernard Membe (Mjumbe wa NEC Taifa kundi la kifo lakini ameshika nafasi ya #6 ) na Asha-Rose Migiro (Mjumbe wa NEC wa kuteuliwa na Mwenyekiti)


Bara
Wassira Stephen - 2,135
January Makamba - 2,093
Mwigulu Nchemba – 2,012
Shigella Martine - 1,824
Lukuvi William - 1,805


Zanzibar
Mbarawa Mnyaa - 1,850
Mohammed Seif Khatib - 1,668
Khadija Hassan Aboud - 1,625
Shamsi Vuai Nahodha - 1,603
Dkt. Hussein Mwinyi - 1,579

Ntakuja kurudi na uzi mpya kuchambua sifa za wajumbe niliowataja hapo juu
 
Umetoa ufafanuzi mzuri sana, ila umeharibu hapo kwenye para ya mwisho na hasa mstari wa mwisho kabisa ulipompa pande Lissu! Kwa maoni yangu nadhani Dr. Salim atatufaa sana uraisi kwa sasa ili kuvunja makundi yanayoiharibu CCM.
 
Haya sasa baada ya kizota kufunga kazi ma agent wamerudi kazini km kawaida, membe membe mara makamba nadhani kambi ya membe ma agent wake sasa active kazini, kaza buti waweza pata hata ubunge wa viti maalum 2015 in case bwana membe atapita
 
Umetoa ufafanuzi mzuri sana, ila umeharibu hapo kwenye para ya mwisho na hasa mstari wa mwisho kabisa ulipompa pande Lissu! Kwa maoni yangu nadhani Dr. Salim atatufaa sana uraisi kwa sasa ili kuvunja makundi yanayoiharibu CCM.

Kwani mwisho wa siku, mgombea wa CCM ataenda kushindana na kivuli au vyama vya upinzani? Sijui kwanini hamuoni mantiki ya kuweka hoja inayopambanisha mgombea CCM na potential candidate wa Chadema, vinginevyo zoezi zima la CCM kule Dodoma ambalo basically ni kujipanga kwa 2015, litakuwa limepoteza tu muda na fedha;

CCM ijipange kwa kumtafuta mtu atakayepambana na Dr. Slaa au Lissu, nje ya hapo, CCM itakuwa na wakati mgumu sana kupita 2015;

Tatizo la CCM sio makundi, tatizo la ccm ni kukosa dira, na pia ufisadi;
 
Can you tell me January ni consistent kiasi gani maana kama katika kugombea ubunge tu dada mtu alienda kuchota mpunga barric sasa huo urais si ndio kabisa tutawekwa rehani au mnataka kuniambia ile barua tuliyowahi kuisoma humu niyakuforge na kama niya ukweli unadhani huyu anafaa hata kuwa katibu kata? Nyerere aliwahi kusema TUNATAKA RAIS ASIWE MLARUSHWA WALA MTOA RUSHWA NA HATA MARAFIKI ZAKE WAMJUE HIVYO! Je anasifa hizo?

Mkuu hapo ndio huwa tunakosea sana, hivi January anahusika kivipi na kazi za dada yake! January ni January na Mwamvita ni Mwamvita.
 
Ingawa hakuna kanuni inayohitaji mgombea Urais (CCM) kuwa mjumbe wa NEC, imekuwa ni utamaduni kwa kigezo hiki kutumika, na itaendelea kuwa hivyo for the next foreseeable future; Hii ndio sababu kubwa kwanini Chaguzi za NEC mara zote huwa na pilika pilika nyingi na ushindani wa hali ya juu; Hapo nyuma niliwahi kuja na mada iliyojadili kwanini bila ujumbe wa NEC, Urais Kupitia CCM haiwezekani, na kila siku zinavyozidi kwenda mbele, hoja hii inazidi kuwa na mashiko;

January na Membe walikuwa ‘Very Smart’ kuamua to take the risk na kugombea Ujumbe wa NEC kupitia zile nafasi kumi za kifo i.e. NEC Ngazi ya taifa; Ingawa uamuzi huu ulikuwa too risky, suala ambalo wengi waliikimbia na kuamua kwenda kujaribu bahati zao huko wilayani, inaonyesha Membe na January walifanya a Cost – benefit Analysis na hatimaye kuona kwamba, it is more of a political asset than a liability, either for 2015 or beyond, hasa iwapo Chadema itachukua nchi 2015; Faida kubwa ya kuchukua uamuzi huu ni kwamba - whether you lose or win, tayari jina lako litakuwa sio geni miongoni mwa waamuzi wa nani awe mgombea Urais kupitia CCM 2015, ambao ni Wajumbe Mkutano Mkuu wa Taifa (CCM);

Wajumbe wa sasa watamaliza muda wao mwaka 2017, kwahiyo, ni wajumbe hawa hawa waliowapitisha Membe, January, Lukuvi, Wassira, Shigela, Mathayo, Msome, Nchemba, Mukama na Mukangara, ndio watakaopigia kura jina la mgombea Urais (CCM) 2015; Nje na Member na January, wengine waliobakia ni aidha sio Presidential Material au umri hautawaruhusu; Suala hili la Presidential Material ni relative na tutalijadili baadae;

Je, ni vigezo gani hutumiwa na CCM kumpata mgombea Urais? Najua wengi katika mjadala huu wataleta hoja khanga, kofia, n.k, kwani ukweli ulio wazi ni kwamba Chama kimechafuka; Lakini tukiweka hili pembeni kwa sasa, Vigezo vinavyotumika kuteua jina la mtu kuwa mgombea Urais (CCM) vipo vingi, na vingine ni very arbitrary na pia mchakato wake sio democratic; Lakini huo ni mjadala mwingine, na kwa sasa ningependa kujadili vigezo vifuatavyo:

  1. Awe na Sifa za Kuwa Mbunge Kufikia Kipindi husika
  2. Awe Mjumbe wa NEC Kufikia Kipindi Husika
  3. Jina lake liwe familiar miongoni mwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa
  4. Asiwe amethibitika kwamba ni mla rushwa (tetesi hazitoshi)/Awe na Sifa Za Kukemea Rushwa
  5. Na Awe na Umri utakaovutia Wapiga Kura Vijana
Kwa mtazamo wangu, mgombea Urais kupitia CCM (2015) atateuliwa kwa kigezo aidha namba nne au namba tano, kulingana na upepo wa siasa utakavyokuwa; Kwa upande mmoja, iwapo Chadema utamweka Kijana kwa mfano Zitto au Lissu, CCM itajibu mapigo kwa kumweka Kijana ambae atakuwa ni January Makamba; Kwa upande mwingine, iwapo agenda ya Vita dhidi ya Ufisadi itazidi kushika kasi chini ya Chadema, hasa iwapo CCM haitatoa kafara angalau watu wawili watatu kuonyeshe progress towards that end, na Chadema kumweka Dr. Slaa au Hata Lissu, CCM italazimika kumweka mgombea ambae atatumika kurudisha imani kwa wananchi kwamba Chama kipo tayari kumaliza rushwa nchini, hivyo kumsimamisha Bernard Membe;

Ifahamike tu kwamba wagombea wa NEC kupitia wilayani hawana prominence kichama kama wale Kumi waliopita ngazi ya Taifa kwani, tofauti na wa wilayani, wa taifa sasa tayari wanajulikana wapiga kura ambao ni Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa 2012-2017, na ni wapiga kura hawa ndio waliompa Membe na January Kura nyingi za NDIO;

Kwahiyo iwapo Membe na January wataamua kugombea 2015, njia yao ni nyeupe, na sana sana wanachohitaji only ‘fine tuning’ za hapa na pale; Iwapo mungu atawajalia Afya na Uzima, kitendo cha hawa wawili kuchukau fomu ya kugombea Urais 2015, automatically kitapelekea majina yao kufikia hatua ya mwisho ya mchakato wa kupata mgombea wa CCM - yani majina yao yatakuwa ni miongoni mwa majina matatu yatakayopelekwa kwenye Mkutano Mkuu wa Taifa May 2015 kupigiwa kura; Kilichobakia kwa sasa ni kujua jina la tatu litakuwa ni la nani, ingawa huyu wa tatu hatokuwa na nguvu kama Membe au January; Nitafafanua hili lidogo hapo chini;

Uchaguzi wa NEC mwaka huu ulikuwa ni tukio pekee lililobakia kutupatia picha halisi jinsi gani mbio za Urais zitakavyo unfold kuelekea 2015, na unless litokee tukio kubwa sana na lisilotarajiwa kama vile CCM kumeguka na kuwa vyama viwili tofauti, hayata kuja majina mengine mapya na yenye kuvuma kuliko ya Membe, January, Lowassa, Mwandosya, Kigoda, Mwakyembe, Sumaye, Sitta, Migiro, Nape na Magufuli; Kutokana na sababu mbalimbali ambazo tutazijadili baadae, iwapo hawa wengine pia watajaribu bahati yao, mwisho wa siku, wote hawa katika hatua mbalimbali, watahamia kwenye kambi kuu mbili: (1) Kambi ya Membe au (2) Kambi ya January;

Utabiri wangu kama mlivyoona haupo biased, bali ni objective na unaotumia hoja, na sio uganga; Kwahiyo nategemea kwamba hoja yangu itakuwa challenged objectively na bila matusi. Pia ningependa kwenda mbali zaidi kidogo na utabiri wangu kwamba, kutokana na Chadema kuendelea kushindwa kupanua agenda yake ya kuingia ikulu nje ya UFISADI, na pia kutokana na Chadema kuendelea ku-ignore kushinikiza mabadiliko ya Kanuni ya ushindi wa chaguzi kuu i.e. kanuni ya mshindi ni mshindi iliyopitishwa na Bunge, Uchaguzi wa 2015, CCM kupata 50.01% ya popular vote dhidi ya Chadema ni kazi ndogo sana, bila hata ya uchakachuaji; Na kupata 50.01% ni rahisi kwa CCM hata ikiweka mgombea yoyote yule; Vinginevyo, iwapo things remain constant until 2015, na Membe na January wakagombea, Basi Ifikapo November 2015, Rais wa TANO wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania atakuwa ni aidha Bernard Membe, au January Makamba;

Na yoyote kati ya hawa wawili ataweza tu kumudu nafasi hii as long as he fulfills conditions such as: Upeo wa masuala ya kiuchumi na kisiasa - kitaifa na kimataifa katika nyakazi za leo, Uzalendo, anajali maslahi ya taifa mbele, Mkali, Ana uelewa wa matatizo ya wananchi, na ana ubunifu na pia moyo wa dhati wa kuyatafutia ufumbuzi matatizo ya wananchi, hasa wa vijijini; Lakini Rais ajaye ataweza kumudu nafasi hii vizuri zaidi iwapo katiba ya nchi itafanyiwa marekebisho ili kuondokana na migogoro inayoendana na nafasi ya Urais; Suala lingine ambalo ni muhimu sana ni kwamba kutakuwa na ulazima wa Rais mteule (CCM) kupewa ushirikiano na kambi zote zilizopo sasa ndani ya CCM, vinginevyo Rais na nchi itayumba/haitatawalika;

Mwisho kabisa niseme tu kwamba nia yangu hapa sio kupigia debe viongozi hawa wawili kwani mbali ya siasa za NEC nilizojadili na pia conditions nilizojadili hapo juu, bado wana kazi kubwa ya kuaminisha watanzania kwamba atakayepita atakuwa Rais Bora na sio Bora Rais; Na mpaka tufikie hatua hiyo, Chadema wakifanyia kazi mapungufu yao, Rais Bora kwa Tanzania 2015 ni Tundu Lissu, na hii ni changamoto kwa Wagombea wa CCM kwamba muda ukifika, waanze kujieleza kwa wananchi kwamba wanasimamia ISSUES gani, kwani suala la PERSONALITY halitakuwa kigezo tosha cha kumpelekea mgombea Urais ikulu 2015; Inawezekana huko mbeleni wagombea wa CCM wataanza kunadi issues wanazosimamia, lakini mpaka tufike huko, mimi binafsi nadhani iwapo kutakuwa na uchaguzi wa Rais leo, Rais bora wa Tanzania ni TUNDU LISSU;

Kwa kuwa tangu uhuru tumekuwa na marais wanaotoka katika makabila madogo nchini, huenda hoja zako zina ukweli ndani yake kama hutumiwi!
 
Kama alivyosema mchambuzi mgombea wa urais ndani ya CCM atatokea kundi la kifo kati ya bara na visiwani. Kwa maoni yangu huyo mgombea atakuwa ni kati ya wale waliokuwa kwenye tano bora kutokea kundi ka kifo. Exception pekee ya haya maoni yangu ni ni wafuatao Edward Lowassa (Mjumbe wa NEC Wilaya ya Monduli), Bernard Membe (Mjumbe wa NEC Taifa kundi la kifo lakini ameshika nafasi ya #6 ) na Asha-Rose Migiro (Mjumbe wa NEC wa kuteuliwa na Mwenyekiti)




Bara
Wassira Stephen - 2,135
January Makamba - 2,093
Mwigulu Nchemba – 2,012
Shigella Martine - 1,824
Lukuvi William - 1,805


Zanzibar
Mbarawa Mnyaa - 1,850
Mohammed Seif Khatib - 1,668
Khadija Hassan Aboud - 1,625
Shamsi Vuai Nahodha - 1,603
Dkt. Hussein Mwinyi - 1,579

Ntakuja kurudi na uzi mpya kuchambua sifa za wajumbe niliowataja hapo juu

Kumbe Mbarawa Mnyaa ni maarufu kuliko hata Dkt
 
Mkuu Mchambuzi,
Asante kwa mchanganuo wako kimantiki.
Nadhani tunaelewa kuwa kura za mkutano mkuu ni za itifaki na haziwezi kutueleza kwa kina kuhusu wagombea watarajiwa.

Pili, mkutano mkuu una influency ndogo sana katika kupatikana kwa mgombea. Ule ni mhuri mkubwaa usio na madhara kama yupo aliyepita kikwazo cha NEC

Kugombea kwa NEC kuna mikiki sana siku hizi si kwa maana ile ya wajumbe kumfahamu mgombea au mgombea kuonyesha umahiri wake. Heka heka za NEC zinatokana na NEC kuipora madaraka CC kama ilivyokuwa siku za nyuma.
Kikwazo cha wagombea ni NEC,ndiyo maana wengi wanapigania sana huko.

Kupigania maana yake ni kuwa na uwezo wa kujenga kundi la kuunga mkono. Ukiwa nje ya NEC kwa utaratibu wa CCM ya sidhani hata jina lako laweza kutajwa.

Kwa mtazamo wangu January na Membe hawakuchukua risk kwa mintaarafu ya kujulikana. Wamefanya hivyo kwa kujua kuwa risk ya Wilayani itawaondoa machoni kabisa kama ilivyomfanya Mzee F.T.Sumaye ambaye keshasahaulika hadi tunaandika haya. Jan na Membe walifahamu kuwa uwepo wao NEC ni muhimu sana na hivyo kuchukua risk was the best option on the Table.Kama italipa au la ni suala la muda.

Mgombea wa CCM anaweza kutoka nje ya ''circle''. Nimeangalia sekretariati naona wameitwa wenye chama kuokoa jahazi. Wengi hatutawasoma majina yao lakini wanafanya kazi nyuma ya pazia.
Angalia link ya Mangula, Kinana, Seif Khatibu kwa kuanzia tu na tujue sekretariati inaunda 1/3 ya CC.

Kuna mtu hatajwi sana lakini amebeba karata muhimu sana ya CCM. Endapo mdodoro wa chama utakuwa kama ulivyo na uwezekano wa kura za itifaki au 50.01% hautakuwepo basi itatumika karata ya mwisho.
Udini na Ukabila unaonekana kutofanya kazi kama walivyotaraji, sasa tutaona JINSIA na hapa ndipo jina la Asha Rose linapoingia.

Jina la Asha Rose halitaletwa kama mwanamke, litaletwa kama mzooefu wa chama, kimataifa, asiye na makundi ataunganisha wanachama na hana kashfa. Kwenda katika mpambano na Chadema tutasikia hii ni zamu ya wanawake. Mtindo huo anaujua Samwel Sitta.

Ahsante
 
Back
Top Bottom