Elections 2015 Mgombea Urais CCM 2015: Ni Bernard Membe au January Makamba

Elections 2015 Mgombea Urais CCM 2015: Ni Bernard Membe au January Makamba

Mchambuzi, nakubaliana na wewe kwamba katika wajumbe 10 waliogombea NEC, Membe anaweza kufikiriwa kuwa mgombea wa CCM. Ingawa amepata nafasi ya sita kiuchaguzi, haimanishi hakubaliki sana kwa wajumbe, bali imetokana na vita vya kisiasa ambavyo vilielekezwa kwake kwa vile anajulikana ana malengo ya uraisi, hivyo alifanyiwa kampeni za kinyume kumzuia, hivyo kitendo cha kupata nafasi ya sita ni sifa tosha ya kuwa mpiganaji na kuvutia makundi ambayo hayakupenda kampeni chafu na maneno ambayo yalilenga kumboa na kumharibia sifa ili akose nafasi ya NEC.

Hata hivyo, naamini CCM bado wanaweza kumleta mtu mwingine nje ya wajumbe wa NEC au watu wengine wenye mvuto ambao ni wajumbe wa NEC kupitia wilaya. Kama walivyofanya kumleta Mangula , nafasi ya m/mwenyekiti.

Kwa jinsi ambavyo siasa za makundi zilivyoitesa CCM, si ajabu wakatumia ule mkakati wao maarufu wote wakose na wakaja na mtu mpya.

Swali ni kwamba , je kuna watu ambao wanaweza kuthubutu kuingia kinyang'anyiro cha kuwa mgombea wa CCM, bila kuhofia madhara yanayoweza kukupata endapo, utaonyesha dhamira ya kugombea halafu ukakosa. Hapo ndipo , wengi hukimbilia bora kujiunga na kambi fulani za wagombea, lakini mwisho wa siku ni kupata madhara yale yale endapo kambi uliyoiunga mkono haifanikiwi.

Hatima basi ni nini? Kwa vile mchakato wa CCM una matatizo mengi ya kumpata mgombea, kwani CCM itakuwa imejeruhiwa sana kumpata mgombea, basi upinzani una nafasi nzuri ya kutoa mgombea. Lakini kumbuka, CCM hawataacha mgombea mzuri apatikane kutoka kwa wapinzani. Mkakati wa mapandikizi ndani ya vyama vya upinzani umepata mashiko sana kwa watu wengine.

Mapandikizi ni pamoja na wagombea wenye kauli au msimamo ndumi la kuwili, pandikizi la udini na ukabila, haya yote yatafanya kazi kinyume cha kupata mzuri hasa CDM au atakapopatikana mgombea mzuri.
 
Uchambuzi mzuri ila kwangu January kasimama vizuri kuliko membe.Sitaki kudiscuss chama ambacho na hakika hakita shinda
 
Bahati mbaya Tanzania sio Zanzibar

Siri inafichuka sasa kuwa Rais wa Tanzania kumbe ni lazima atoke Tanganyika? hizo ni itikadi za Wadanganyika.

Nazidi kushauri wa Znz kuhakikisha hilo linawekw wazi katika Katiba yenu ya Muungano aani nafasi ya juu kabisa ya uongozi lazima iwe kwa kupokezana na kama itakataliwa bora Muungano wenu Ufe kwani kutakuwa hakuna maana nyie kila siku kuongozwa tu na mfumo msioutaka.

 
Kati ya hao wawili, My vote goes to January. He is a new generation leader, with a vision. He will run the country with result oriented policies! Nawapenda Chadema, lakini kama CCM ndio itashika hatamu, of those 2, Go January!
Makamba Junior ana lackexposure kulinganisha na lissu.
 
Mchambuzi kuna mtu mwingine umemsahau naye Dr. Hussein Mwinyi!! Huyu naye ni figure ingine CCM wakitaka kurudisha imani kwa wananchi kuwa ni msafi wananweza mleta huyu!!
 
Another smart propaganda , with Silly people...............towards election hata mimi naweza kujitokeza kuwa mgombea urais provided nitakuwa nimeidai Tanganyika ndani na nje ya Bunge...........

Ningekuheshimu sana kama ungetoa hoja zako kumpinga mleta mada, Mchambuzi.
Lakini kwa kuwa umeishia kutoa kashfa badala ya kuleta hoja, NIMEKUDHARAU!
 
Mchambuzi, nashindwa kuelewa na nashangaa kwanini una m-exclude kipenzi chetu Dr. W. P. Slaa!

Nani alisema Dr.Slaa siyo kipenzi cha vijana?

I wonder!

Mleta uzi kaamua kumhujumu makusudi Dk SLAA kwa maslahi ya ccm. Hata hivyo GT wameshamwelewa kusudio lake la ndani nalo sio hao Membe na Makamba bali kupima upepo juu ya Dk Slaa baada ya chaguzi hizi za ccm.
 
Last edited by a moderator:
Lazima ujue kwamba mgombea wa CCM atagombea dhidi ya wagombea kutoka vyama vingine halali vya siasa, na kwa sasa, ni chama kimoja tu ambacho kina uwezo wa kuitoa au kuipa tabu CCM 2015, na chama hicho sio kingine bali ni Chadema, kwani hata mwenyekiti wa CCM taifa FINALLY amekiri hili jana kwenye hotuba yake; Ni katika mazingira hayo, ndio nimemtaja Lissu;

Pengine wewe unaishi nyakati za nyuma kidogo ambapo mteule kugombea kupitia CCM ilikuwa ni automatic anakuwa rais ajaye; Walioharibu such a luxury ride sio mwingine bali ni CCM YENYEWE;

Asante Mungu kwa kuwa sasa CCM wameshapata kibali cha kuzikwa rasmi...Eddo njoo weka nguvu huku kwingine tuwamalize CCM
 
Tanzania inahitaji ukombozi wa kweli na wa lazima. Mabadiliko na maendeleo hayaji kwa maneno tupu ndugu zangu watanzania. CCM wamehodhi kila kitu kuanzia njia zote za uchumi na vyombo vya ulinzi na usalama ili kulazimisha ushindi hata wa wizi 2015.

Elimu ya uraia ni muhimu sana kwa watanzania ili tufahamu haki zetu za msingi. tupinge kwa nguvu zetu zote propanganda uchwara zinazojaribu kutugawa kiudini na kiukabila ili tushindwe kudai haki zetu tulizoporwa na majambazi wachache wanaoneemeka na rasilimali zetu ilhali sisi tunataabika hata kupata mlo 1 wa siku!

Ogopa CCM kama ukoma! We need changes GUYZ COME ON!! TS ENOUGH I SAY ITS ENOUGH!!
 
Mchambuzi, nakubaliana na wewe kwamba katika wajumbe 10 waliogombea NEC, Membe anaweza kufikiriwa kuwa mgombea wa CCM. Ingawa amepata nafasi ya sita kiuchaguzi, haimanishi hakubaliki sana kwa wajumbe, bali imetokana na vita vya kisiasa ambavyo vilielekezwa kwake kwa vile anajulikana ana malengo ya uraisi, hivyo alifanyiwa kampeni za kinyume kumzuia, hivyo kitendo cha kupata nafasi ya sita ni sifa tosha ya kuwa mpiganaji na kuvutia makundi ambayo hayakupenda kampeni chafu na maneno ambayo yalilenga kumboa na kumharibia sifa ili akose nafasi ya NEC.

Hata hivyo, naamini CCM bado wanaweza kumleta mtu mwingine nje ya wajumbe wa NEC au watu wengine wenye mvuto ambao ni wajumbe wa NEC kupitia wilaya. Kama walivyofanya kumleta Mangula , nafasi ya m/mwenyekiti.

Kwa jinsi ambavyo siasa za makundi zilivyoitesa CCM, si ajabu wakatumia ule mkakati wao maarufu wote wakose na wakaja na mtu mpya.

Swali ni kwamba , je kuna watu ambao wanaweza kuthubutu kuingia kinyang'anyiro cha kuwa mgombea wa CCM, bila kuhofia madhara yanayoweza kukupata endapo, utaonyesha dhamira ya kugombea halafu ukakosa. Hapo ndipo , wengi hukimbilia bora kujiunga na kambi fulani za wagombea, lakini mwisho wa siku ni kupata madhara yale yale endapo kambi uliyoiunga mkono haifanikiwi.

Hatima basi ni nini? Kwa vile mchakato wa CCM una matatizo mengi ya kumpata mgombea, kwani CCM itakuwa imejeruhiwa sana kumpata mgombea, basi upinzani una nafasi nzuri ya kutoa mgombea. Lakini kumbuka, CCM hawataacha mgombea mzuri apatikane kutoka kwa wapinzani. Mkakati wa mapandikizi ndani ya vyama vya upinzani umepata mashiko sana kwa watu wengine.

Mapandikizi ni pamoja na wagombea wenye kauli au msimamo ndumi la kuwili, pandikizi la udini na ukabila, haya yote yatafanya kazi kinyume cha kupata mzuri hasa CDM au atakapopatikana mgombea mzuri.

Thanks for this...

Hilo la udini halina nguvu tena this time labda next time....Kwani CCM hawana ujanja this time lazima watasimamisha mtu atakaye haribu hii mission yao ya udini hasa kwa makundi yanayotumiwa ku-balance kura....

Jambo la hatari ninalo liona ni kuwa kama watafanikiwa kumdanganya mdogo wangu (ambaye amepigwa mawe mengi humu JF) wamtumie kwa malengo ya ku-twist kura za vijana na dini fulani....Huyu mdogo wangu ana ambition sana za kuwa senior leader (akiwa na very sincere heart) lakini kitu kimoja anakikosa hana favour (kutokana na his family background) ya nepotism so wanaotaka kumtumia watamtumia kwa faida yao huku wakitumia ambition zake kama hook naye kwavile anaona kadri siku zinavyoenda chances zinazidi kupungua (kutokana na kukosea katika kujenga trust na viongozi waandamizi ndani ya chama chake) and the future to him seems to be very uncertain...

CDM needs to give this good guy a concreat promise kama walivyofanya kwa Dr. wakati wa uchaguzi uliopita maana hapa ni swala la private/individual costs ambayo bila kupewa incentive ya kutosha ku-define future ya mtu ili awe rational lazima anaweza danganywa alafu akishatumiwa ikifikia sehemu hao wabinafsi waki break through wana m-flash kama toilet paper....I pity him lakini ndiyo nepotism inavyo function....

I wish I could advise him jinsi ya kuwala chenga ya mwili hao watu....Lakini hata hivyo its not too late I know which button I should press to help 'im get out of that snear!
 
1. Dr wa ukweli Wilbrod Slaa ndiye chaguo la wengi, iwe ndani au nje ya Chadema.

2. Kama kuchaguliwa NEC kupitia kapu ndio kigezo, basi CCM Steven Wassira ndiye nambari WANI kwa CCM, ateuliwe yeye basi.

3. Naungana na wanaodhani kuwa jamaa nia yake (na wenzake?) ni kujaribu kuwa-confuse CDM na watanzania kuhusu mgombea urais kupitia CDM.

4. Wajumbe wengi wa Mkutano mkuu wa CCM, na pia NEC ya CCM ni wafuasi wa Lowassa. Kuna uwezekano mkubwa wa yeye au mfuasi wake kuchaguliwa kugombea kupitia CCM.

5. Come 2015, it may be btn Dr Slaa vs Lowassa. Ooh & Prof Lipumba as usual!
 
1. Dr wa ukweli Wilbrod Slaa ndiye chaguo la wengi, iwe ndani au nje ya Chadema.

2. Kama kuchaguliwa NEC kupitia kapu ndio kigezo, basi CCM Steven Wassira ndiye nambari WANI kwa CCM, ateuliwe yeye basi.

3. Naungana na wanaodhani kuwa jamaa nia yake (na wenzake?) ni kujaribu kuwa-confuse CDM na watanzania kuhusu mgombea urais kupitia CDM.

4. Wajumbe wengi wa Mkutano mkuu wa CCM, na pia NEC ya CCM ni wafuasi wa Lowassa. Kuna uwezekano mkubwa wa yeye au mfuasi wake kuchaguliwa kugombea kupitia CCM.

5. Come 2015, it may be btn Dr Slaa vs Lowassa. Ooh & Prof Lipumba as usual!

Hapo ndipo ukombozi wa kweli utakapotimia na Dr Slaa kuiongoza TZ.
 
Sidhani kama ni rahisirahisi ccm kupata 50% kwa uchaguzi wa 2015 kulingana na hali ya maisha ilivyo sasa kwa wananchi[kiuchumi] na kijamii. Wao wateuane tu ila siku itafika,tanzania ya leo sio kama ya enzi hizo,Ukiwaimbia,ukiwanyanyasa na ukiwagandamiza watanzania, wanajua.Watakemea,wataonya na watachambua pumba na mchele ifikapo 2015 kupitia kura yao.
 
Nashauri tuachane na siasa za watu (personalities/individuals), twende kwenye siasa za masuala (issues).

Mimi kwangu atawale LISSU au MEMBE au MAKAMBA au MHINDI KUMAR au YELLOWMAN au yeyote, haina maana yeyote kwangu. Cha maana kwangu ni mwanangu aende shule bora na aelimike kwa viwango vya kimataifa; mama yangu akienda zahanati yetu ya kijiji apate dawa za maumivu yake ya mgongo; nkilima nyanya zangu nipate kwa kuuza; siment ipungue bei nijenge nyumba bora; nisiombwe rushwa nitaka huduma za serikali ninazozilipia kodi; nisibambikwe kesi na polisi; bima yangu ya afya iniwezeshe kupata tiba ya magonjwa yote nk - na yeyote atakayenihakikishia hayo, hata kama ni MKARA, mimi ntampa kura yangu.

KINGINE: Vyama vipunguze u-vyama, kwa sababu sasa hivi watu ambao ni wanachama wao ni wachache mno, TUJENGE UTAIFA ZAIDI kuliko u-vyama unaotugawanya
 
Mkuu Mchambuzi kwanza kabisa Heshima yako, analysis yako ni nzuri, kwa upande wangu naona kwa sasa inatosha tumeshaona udhaifu wa kuwa na Kiongozi asiye na msimamo, mfano Kikwete, Its enough. Tunahitaji Kiongozi atakaye restore Uzalendo, kutokomeza rushwa tunajuwa ni kazi ngumu lakini aonekane yupo serious kwa vitendo katika kupiga vita rushwa, kuzilinda rasilimali zetu za nchi, awe na heshima na unyenyekevu juu ya wananchi na awe anatujali kwa muda wote asiwe Waziri wa mambo ya Nje kama tulienaye kwa sasa.

Sikubaliani na wewe kusema kuwa January na Membe wanaweza kupiga vita ufisadi, hao ni Copy and Paste ya Mr. Kikwete watakuwa wadhaifu kama alivyo Kikwete. I don't trust them to lead my Country. I love my Country more than Kikwete they way he love this Country.

Lowassa he maybe good leader but sidhani kama ataweza kupigania vita ya ufisadi wakati yeye mwenyewe ametajwa sana katika wala na watoaji rushwa. This guy he is disaster if he will become president of my Country, I dont trust him too.

Dr. Slaa, he my be old and if he decide to run for President of my country, he has my vote and i do trust more than any politician in my country right now. And if he wont run, i will see who to trust. Lissu also he si good choice, but he is not popular like Zitto, will Tanzanian people accept him?

Sikusema Membe na January wanawea kupiga vita ufisadi, niliseme kete ya CCM 2015 iwapo Ufisadi bado utakuwa unashika moto kwa kasi kwenye nyika ya siasa, basi atakuwa ni Membe; Kuna tofauti kati ya haya i.e. Membe atamaliza ufisadi na membe atateuliwa iwapo Ufisadi utakuwa bado ni agenda kubwa ifikapo 2015;
 
Mchambuzi, ni kweli mkuu!

Kwa upande wa CCM anayeandaliwa kuwa Rais ni Waziri Membe na hili lipo wazi kabisa,kuhusu J. Makamba ni mtu ambae hana nafasi kwani umri tu nao utambana la sivyo umri ubadilishwe wa kugombea urais ndio utaweza mpa nafasi,si kwamba waliobaki hawatarusiwa kugombea la hasha kwa kuwa ni haki ya kila mtu kugombea nafasi hiyo watapewa nafasi lakini Membe ndio chaguo la CCM kwa sasa labda itokee kuwe na mabadiliko ya kisiasa huko mbele tuendako.

kwa upande wa vyama vingine sina hakika sana nani anaweza shika bendera hiyo ya urais ukimwondoa mzee slaa lakini waliobaki wote bado nafasi zao ktk mioyo wa watanzania ni ndogo sana,kwani umejionea mwenyewe ktk chaguzi ndogo zilizopita bado mageuzi makubwa yanahitajika ili kuweza kuwabadili watanzania watakao kuwa na mgombea kwapani kipindi hico 2015,Kama hata kuwa Slaa basi CCM bado itakuwa na kazi ndogo sana ktk kunyakuwa ushindi kwa uchaguzi wa urais ujao 2015 maana siasa za nchi hii bado zinawategemea wapiga kura wa vijijini ambao ndio wapiga kura wa kweli kuliko mijini.

Bado kuna kazi kubwa ya kufanywa.

Kushinda kwa mzee Wasira kwa kishindo bado ni changamoto pia kwa vyama pinzani kwani kura zake zinaonyesha jinsi wajumbe wa nec walivyo na imani naye na ikitokea akatoka na mtu wake kwapani basi ndio atakae teuliwa kukimbiza bendera ya uraisi kwa upande wa CCM na kwa upande wangu naona B. Membe ndio litakuwa chaguo lao na hata kama itashindikana basi watafanya kama ilivyotokea kwa uspika na kuamuwa kumpa mama Roze Migiro ili kuiendesha nchi. Na hapo watanzania ndio watachanganyikiwa kabisa kwani itakuwa ni maswala ya jinsia na kauli mbio ya kipindi hicho itakuwa mwanamke anaweza kama akipewa nafasi na hapo ndipo kura nyingi za kina mama zitakimbilia huko na tuelewe ktk nchi hii wapiga kura wengi ni akina mama na wale watu waishio vijijini na hii itafanya mgawanyo mdogo ubaki kwa akinababa na vijana ambao bado pia kutakuwa na mgawanyiko baada ya waliowengi kuona ni vyema tujaribu kwa mama kwani tulisha jaribu kwa akina baba na hakuna mafanikio makubwa.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom