Uchaguzi 2020 Mgombea Urais CCM kuhutubia kwa kisukuma huko Mwanza. Huu ni ukabila. NEC tunasubiri kuona hatua kali dhidi yake

Uchaguzi 2020 Mgombea Urais CCM kuhutubia kwa kisukuma huko Mwanza. Huu ni ukabila. NEC tunasubiri kuona hatua kali dhidi yake

Post Zako ni za Kihisia Sana Dhidi Ya MAGUFULI...ok

Magufuli Anachombeza TU...Mbona kule Mara Aliongea Kikurya na Kijita?!!
 
Kila Watu wanaelezwa masuala ya Eneo lao na ndio maana kampeni ni kila eneo mgombea anaenda kuwaeleza Watu wa eneo husika na wanaelezwa ilani inawagusa vipi.

Kama ishu ni kurushwa na TV basi wangeongea tu mara moja kila mgombea wakarushwa na TV basi tukasubiri kupiga kura lakini si hivyo kila eneo wanaelezwa masuala yao ya eneo lao na ya nchi.

Unajua kuwa kuna watu usukumani hasa wazee Hawajui kiswahili mpaka Leo? Mgombea akiwaambia kwa Lugha wanayoielewa wataelewa tu na sidhani Kama anaongea Kisukuma bali anakazia baadhi ya masuala kwa kisukuma Ili wananchi hata wasiojua kiswahili wamwelewe.
Ukienda baadhi ya maeneo ya wamasai na wasukuma hawajui kiswahili hili ninauhakika nalo .
 
LISS alivyokuwa Singida vp alizungumza kwa Lugha gani!? Au Kinyaturu nayo ni Lugha ya Taifa!?
 
Hii ni aibu aisee, yaani inatia kinyaa sana niko namsikiliza anapiga kampeni Magu kila baada ya maneno matatu ni full kisukuma.

Haileti picha nzuri kabisa, kwa sababu kampeni inarushwa Tanzania nzima, sasa kusema kwamba kama anamwaga sera, mtu wa kule Tanga anamuelewa vip?

Huu ni udhaifu mkubwa, halafu eti ndo anajifananisha na Baba Wa Taifa, shame. Nashangaa hata wanaomtetea, huu ni ukabila wa wazi wazi.

Ingekuwa ni mgombea ubunge sawa ila rais anahutubia kisukuma???

Hivi hawa ndo CCM walikuwa wanasema watu wa kaskazini ni wakabila? Au ni tabia ya Nyani kutokuona Kundule??
Magufuli ni mbaguzi hilo lipo wazi
Magufuli ni mkabila hilo lipo wazi
Magufuli ni mdini hilo lipo wazi.
 
Back
Top Bottom