Uchaguzi 2020 Mgombea Urais CCM kuhutubia kwa kisukuma huko Mwanza. Huu ni ukabila. NEC tunasubiri kuona hatua kali dhidi yake

Post Zako ni za Kihisia Sana Dhidi Ya MAGUFULI...ok

Magufuli Anachombeza TU...Mbona kule Mara Aliongea Kikurya na Kijita?!!
 
Kila Watu wanaelezwa masuala ya Eneo lao na ndio maana kampeni ni kila eneo mgombea anaenda kuwaeleza Watu wa eneo husika na wanaelezwa ilani inawagusa vipi.

Kama ishu ni kurushwa na TV basi wangeongea tu mara moja kila mgombea wakarushwa na TV basi tukasubiri kupiga kura lakini si hivyo kila eneo wanaelezwa masuala yao ya eneo lao na ya nchi.

Unajua kuwa kuna watu usukumani hasa wazee Hawajui kiswahili mpaka Leo? Mgombea akiwaambia kwa Lugha wanayoielewa wataelewa tu na sidhani Kama anaongea Kisukuma bali anakazia baadhi ya masuala kwa kisukuma Ili wananchi hata wasiojua kiswahili wamwelewe.
Ukienda baadhi ya maeneo ya wamasai na wasukuma hawajui kiswahili hili ninauhakika nalo .
 
LISS alivyokuwa Singida vp alizungumza kwa Lugha gani!? Au Kinyaturu nayo ni Lugha ya Taifa!?
 
Magufuli ni mbaguzi hilo lipo wazi
Magufuli ni mkabila hilo lipo wazi
Magufuli ni mdini hilo lipo wazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…