Uchaguzi 2020 Mgombea Urais CCM kuhutubia kwa kisukuma huko Mwanza. Huu ni ukabila. NEC tunasubiri kuona hatua kali dhidi yake

Uchaguzi 2020 Mgombea Urais CCM kuhutubia kwa kisukuma huko Mwanza. Huu ni ukabila. NEC tunasubiri kuona hatua kali dhidi yake

Wasukuma pekee ni Milioni ngapi Chief? Kama umeenda shule njoo na jibu halafu nikulipue
Tabora, Simiyu, Mwanza, Shinyanga na Geita ni mikoa mitano ambayo yote ni ya kabila mmoja la wasukuma.

Ndio kabila kubwa kuliko makabila yote Tanzania kama ulikuwa hufahamu.

Rais kuongea kisukuma sio kosa kumbuka anaongea na kundi kubwa la watu na havunji sheria.
 
Mgombea wa ccm alipokuwa Magu amehutubia kwa kisukuma mwanzo mwisho. Ninakushauri kaeni naye na mumwambie asiiharibu nchi yetu kwa kupanda mbegu ya ukabila.

Wasukuma kwa wingi wao wangeamua kuwa wakabila huyo Nyerere angepata taabu tangu miaka ile ya sitini mwanzoni. Na asingeongoza kwa amani.

Huwa inashangaza kuona makabila madogo yakijitutumua na kutaka kusikika na kutawala makabila makubwa.
 
Hii ni aibu aisee, yaani inatia kinyaa sana niko namsikiliza anapiga kampeni Magu kila baada ya maneno matatu ni full kisukuma.

Haileti picha nzuri kabisa, kwa sababu kampeni inarushwa Tanzania nzima, sasa kusema kwamba kama anamwaga sera, mtu wa kule Tanga anamuelewa vip?

Huu ni udhaifu mkubwa, halafu eti ndo anajifananisha na Baba Wa Taifa, shame. Nashangaa hata wanaomtetea, huu ni ukabila wa wazi wazi.

Ingekuwa ni mgombea ubunge sawa ila rais anahutubia kisukuma???

Hivi hawa ndo CCM walikuwa wanasema watu wa kaskazini ni wakabila? Au ni tabia ya Nyani kutokuona Kundule?

Sheria ya Maadili ya Uchaguzi, kifungu 2.1k kinasema vyama vya siasa na wagombea wana wajibu wa "kuhakikisha kuwa lugha ya Kiswahili itakuwa ndiyo lugha pekee itakayotumika katika kampeni za uchaguzi"

View attachment 1560689
Nec ipi Mkuu? Hii hii au kuna ingine?
 
Tabora, Simiyu, Mwanza, Shinyanga na Geita ni mikoa mitano ambayo yote ni ya kabila mmoja la wasukuma.

Ndio kabila kubwa kuliko makabila yote Tanzania kama ulikuwa hufahamu.

Rais kuongea kisukuma sio kosa kumbuka anaongea na kundi kubwa la watu na havunji sheria.
Wala sio ukabila!!!
 
Wasukuma kwa wingi wao wangeamua kuwa wakabila huyo Nyerere angepata taabu tangu miaka ile ya sitini mwanzoni. Na asingeongoza kwa amani.

Huwa inashangaza kuona makabila madogo yakijitutumua na kutaka kusikika na kutawala makabila makubwa.
Kwa hiyo sasa ni wakati wa makabila makubwa kutawala!!!??
 
Hii ni aibu aisee, yaani inatia kinyaa sana niko namsikiliza anapiga kampeni Magu kila baada ya maneno matatu ni full kisukuma.

Haileti picha nzuri kabisa, kwa sababu kampeni inarushwa Tanzania nzima, sasa kusema kwamba kama anamwaga sera, mtu wa kule Tanga anamuelewa vip?

Huu ni udhaifu mkubwa, halafu eti ndo anajifananisha na Baba Wa Taifa, shame. Nashangaa hata wanaomtetea, huu ni ukabila wa wazi wazi.

Ingekuwa ni mgombea ubunge sawa ila rais anahutubia kisukuma???

Hivi hawa ndo CCM walikuwa wanasema watu wa kaskazini ni wakabila? Au ni tabia ya Nyani kutokuona Kundule?

Sheria ya Maadili ya Uchaguzi, kifungu 2.1k kinasema vyama vya siasa na wagombea wana wajibu wa "kuhakikisha kuwa lugha ya Kiswahili itakuwa ndiyo lugha pekee itakayotumika katika kampeni za uchaguzi"

View attachment 1560689
Mtatapatapa kutafuta visingizio mpaka BASI! Nasubiri Lissu naye alivalie njuga hili ingawa naye nilimsikia akiongea kilugha cha kwake pale kwao. Msisumbuke na vitu vidogo vidogo au ndiyo dalili za mfa maji au uhaba wa SERA!?
 
Hujanielewa nilichomaanisha.
Tutaelewana tu. Yawezekana nimekuelewa vile usivyotaka nikuelewe na si lazima nikuelewe utakavyo.
Ndio maana tuna utashi na uwezo wa kutafakari kila mmoja anao wake.
Sentensi moja inatosha kufikisha ujumbe husika
 
Kila Watu wanaelezwa masuala ya Eneo lao na ndio maana kampeni ni kila eneo mgombea anaenda kuwaeleza Watu wa eneo husika na wanaelezwa ilani inawagusa vipi.

Kama ishu ni kurushwa na TV basi wangeongea tu mara moja kila mgombea wakarushwa na TV basi tukasubiri kupiga kura lakini si hivyo kila eneo wanaelezwa masuala yao ya eneo lao na ya nchi.

Unajua kuwa kuna watu usukumani hasa wazee Hawajui kiswahili mpaka Leo? Mgombea akiwaambia kwa Lugha wanayoielewa wataelewa tu na sidhani Kama anaongea Kisukuma bali anakazia baadhi ya masuala kwa kisukuma Ili wananchi hata wasiojua kiswahili wamwelewe.
Ukienda baadhi ya maeneo ya wamasai na wasukuma hawajui kiswahili hili ninauhakika nalo .

Kama hawaelewi kiswahili, kwa hiyo ataongea kote aendako? naona kaanzia Mkoa wa Simiyu, Shinyanga, Mara, Geita na ataendelea kufanya hivyo Tabora, Katavi na Rukwa haya yote ni mikoa yenye idadi ya kutosha ya Wasukuma?
 
Mh. raise anaboa sana kwa hii tabia yake.
kiswahi yenyewe hajui msimlaumu ,hawezi kuongea sentensi moja iliyonyooka kwa kiswahili ,english hajui na kiswahili hajui lia ameamua kuja na kisukuma
 
Yeye anafikiri mwanza wanaishi wasukuma peke yao? Wengi hapo kwenye mkutano hawamwelewi, Tanzania ina makabila zaidi ya 120 na wanaishi mikoa mbalimbali bila kujali kabila gani.
Ina maana jamaa anaomba kura kutoka Kabila lake tu?
 
Tutaelewana tu. Yawezekana nimekuelewa vile usivyotaka nikuelewe na si lazima nikuelewe utakavyo.
Ndio maana tuna utashi na uwezo wa kutafakari kila mmoja anao wake.
Sentensi moja inatosha kufikisha ujumbe husika
Hakuna wakati wa kabila kubwa wala dogo kutawala, ujumbe ni kwamba tuwashukuru kina Nyerere kwani kama wangekuwa hawana maono basi kabila kubwa kama wasukuma wangesumbua tangu miaka ile ya sitini mwanzoni baada tu ya uhuru.

Nigeria na mataifa mengine makubwa yalishindwa kuwadhibiti “wasukuma” wao na mpaka kesho wanasumbuka.
 
Hakuna wakati wa kabila kubwa wala dogo kutawala, ujumbe ni kwamba tuwashukuru kina Nyerere kwani kama wangekuwa hawana maono basi kabila kubwa kama wasukuma wangesumbua tangu miaka ile ya sitini mwanzoni baada tu ya uhuru.

Nigeria na mataifa mengine makubwa yalishindwa kuwadhibiti “wasukuma” wao na mpaka kesho wanasumbuka.
Kwa hiyo ni lugha ipi inapaswa kutumika katika kampeni zinazoendelea?
Haya ni Maadili ya Uchaguzi wa Urais, Wabunge na Madiwani, 2020. Msisitizo kwa kinachofanyika kanda ya Ziwa.

Hiyo ni aya 2.1 (k) ikieleza wajibu wa Chama cha Siasa. Kwenda kinyume na maadili haya ni kosa linaloweza kufikishwa katika kamati ya Maadili na kutolewa uamuzi ikiwa ni pamoja na Chama kilichokosea kuzuiwa kufanya kampeni.
View attachment 1563528

ADHABU ZINAZOWEZA KUTOLEWA NA KAMATI ZA MAADILI


View attachment 1563529

Uwezo wa mlalamikaji au mlalamikiwa kufungua kesi mahakamani ikiwa hajaridhika na uamuzi wa Kamati ya Maadili (hii ni pamoja na nafasi ya Urais)

View attachment 1563532

Uamuzi wa Jumla kuhusu chama kutotekeleza maadili ya Uchaguzi
View attachment 1563539
Si vibaya baada ya kuona ushahidi huo ambao umetengenezwa na wanaouvunja kujitoa ufahamu kisha kujibaraguza...
Yasipokemewa sasa basi yaachwe ili kila mwenye kutafuta kura kwa kunena kwa lugha na azitafute ili mwisho wa siku tuvune matunda tunayofurahia sasa!!
 
Hii ni aibu aisee, yaani inatia kinyaa sana niko namsikiliza anapiga kampeni Magu kila baada ya maneno matatu ni full kisukuma.

Haileti picha nzuri kabisa, kwa sababu kampeni inarushwa Tanzania nzima, sasa kusema kwamba kama anamwaga sera, mtu wa kule Tanga anamuelewa vip?

Huu ni udhaifu mkubwa, halafu eti ndo anajifananisha na Baba Wa Taifa, shame. Nashangaa hata wanaomtetea, huu ni ukabila wa wazi wazi.

Ingekuwa ni mgombea ubunge sawa ila rais anahutubia kisukuma?

Hivi hawa ndo CCM walikuwa wanasema watu wa kaskazini ni wakabila? Au ni tabia ya Nyani kutokuona Kundule?

Sheria ya Maadili ya Uchaguzi, kifungu 2.1k kinasema vyama vya siasa na wagombea wana wajibu wa "kuhakikisha kuwa lugha ya Kiswahili itakuwa ndiyo lugha pekee itakayotumika katika kampeni za uchaguzi"

View attachment 1560689
Rais Duni kama huyu hivi aliwahi kuwepo nchi gani nyingine ?
 
Kwa hiyo ni lugha ipi inapaswa kutumika katika kampeni zinazoendelea?

Si vibaya baada ya kuona ushahidi huo ambao umetengenezwa na wanaouvunja kujitoa ufahamu kisha kujibaraguza...
Yasipokemewa sasa basi yaachwe ili kila mwenye kutafuta kura kwa kunena kwa lugha na azitafute ili mwisho wa siku tuvune matunda tunayofurahia sasa!!
Asilimia kubwa ya wanaokuwepo katika hiyo mikutano wanaelewa kisukuma na sio kwamba kwa kuongea kisukuma kuna kifungu cha katiba kinavunjwa.

Hili ni jambo dogo sana kulinganisha na yaliyoandikwa kwenye ilani ya kurasa 303 yenye kutakiwa kutekelezwa ndani ya miaka mitano.

Nyerere alikuwa anaongea kizanaki mpaka katika mikutano ya CCM miaka ile na hakuna aliyewahi kumkosoa.

Tuachane na hizi nongwa za kitoto.
 
Asilimia kubwa ya wanaokuwepo katika hiyo mikutano wanaelewa kisukuma na sio kwamba kwa kuongea kisukuma kuna kifungu cha katiba kinavunjwa.

Hili ni jambo dogo sana kulinganisha na yaliyoandikwa kwenye ilani ya kurasa 303 yenye kutakiwa kutekelezwa ndani ya miaka mitano.

Nyerere alikuwa anaongea kizanaki mpaka katika mikutano ya CCM miaka ile na hakuna aliyewahi kumkosoa.

Tuachane na hizi nongwa za kitoto.
Endelea kupamba kaburi lkn ndani mwake ni uvundo mtupu. Swali: Kutumia kilugha kwenye kampeni ni kuendeleza ubaguzi na ukabila. Kweli si Kweli??
 
Back
Top Bottom