Uchaguzi 2020 Mgombea Urais kukutana na wasimamizi wa uchaguzi kipindi cha Kampeni inakubalika kisheria?

Uchaguzi 2020 Mgombea Urais kukutana na wasimamizi wa uchaguzi kipindi cha Kampeni inakubalika kisheria?

Status
Not open for further replies.


"Ma DED wote wapo kwenye Vituo Vyao vya Kazi hakuna aliyeitwa Dodoma...
Nimeona Uongo Ukisemwa Sana Huwa Unageuka kuwa Ukweli ' Lissu amewadanganya wana Musoma Katika Mkutano Wake wa Hadhara Tarehe 26/09/2020! " Jimson Mhagama DED wa Nyasa

Huyu Lissu ni mtu hatari Sana kwa nchi yetu...ni kweli Sasa naamini ametumwa...Halafu Sasa anataja The Hague huku akihamasisha vurugu asijue kuwa yeye naye atakuwa mtuhumiwa nambari wani
 
Comrade, "misukule" ukimaanisha wananchi wenye sifa za kupiga kura, waliojiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura na wenye kadi ya mpiga kura basi upo sawa kabisa maana misukule sisi kwa umoja wetu tutamchagua kwa wingi Rais Magufuli ili ashinde kwa kishindo. View attachment 1582152
Nape na Polepole wanawadanganya labda mshinde kwa Roshindo sio kishindo
 
Ukisoma comments ndio utajua watu magufuli hawampend jaman, amezidi dharau na kejeli kwa watanzania
 

Nimefikiri chadema katika baadhi ya maeneo wangekuwa na picha kama hizi zinaprintiwa za kutosha kisha zinagawiwa kwa waliohudhuria kuonesha hali halisi huku mtoa mada akikazia kwa spichi kali.... lengo ni kuwatia machungu tu nina hakika watu wakiondoka nazo nyumbani na kuwaonesha wengine... hawawezi kosa watakaowasapoti
 
Zipo taarifa za Mwenyekiti wa chama tawala kukutana na wakurugenzi Dodoma wakati kampeni zinaendelea huku Hawa wakiwa ndio wasimamizi wa uchaguzi kwenye majimbo. Tume ya uchaguzi inazungumziaje hatua hii?

Je Ni kweli mkutano huu upo au Ni propaganda za majukwaani tu?

View attachment 1582153




Naona silaha iliyobakia ni kutumia hao wakurugenzi tu ili kuokoa jahazi. Jamboambalo kwangu mimi naona halitafanikiwa kwani huko huko wako ambao watatoa siri ya kinachoendelea na wengine wamechoshwa na maagizo hivyo watayafumbia macho maagizo hayo.
 
Keshokutwa atawaida polisi na wanajeshi.
Asubuhi ya Ijumaa ya wiki hii makundi yote ya majeshi (JW, Polisi na Magereza) yalifunga viunga vya mji wa Arusha waki-match barabarani. Wananchi wa mji huu tulipata taharuki mno! Tulidhani nchi ipo chini ya amri ya jeshi.
 
Asubuhi ya Ijumaa ya wiki hii makundi yote ya majeshi (JW, Polisi na Magereza) yalifunga viunga vya mji wa Arusha waki-match barabarani. Wananchi wa mji huu tulipata taharuki mno! Tulidhani nchi ipo chini ya amri ya jeshi.
Hehehe
 
Naona silaha iliyobakia ni kutumia hao wakurugenzi tu ili kuokoa jahazi. Jamboambalo kwangu mimi naona halitafanikiwa kwani huko huko wako ambao watatoa siri ya kinachoendelea na wengine wamechoshwa na maagizo hivyo watayafumbia macho maagizo hayo.
Ofcourse majimboni Magufuli hatakuwepo maana yeye ndiye anawalazikisha lakini watakuwa wanapima upepo kwanza. Tutawahenyesha lazima watangaze tu.
 
Zipo taarifa za Mwenyekiti wa chama tawala kukutana na wakurugenzi Dodoma wakati kampeni zinaendelea huku Hawa wakiwa ndio wasimamizi wa uchaguzi kwenye majimbo. Tume ya uchaguzi inazungumziaje hatua hii?

Je Ni kweli mkutano huu upo au Ni propaganda za majukwaani tu?

View attachment 1582153



Mbona nasikia jiwe yupo Hoi anamatatizo ya moyo?
 
Hiyo lazima ndani ya week ya mwisho wa kampeni lazima Siro na Mabeyo wafanye press conference zinazo tishia raia hivyo upinzani wajipange namna ya kuneutralise.
Kwamba kuneutralise. Nhiiiiiiiiii😃 nimecheka Kama Magu atakavyocheka akisikia hii kitu unayoshauri hapa.
 
Ukweli ni kwamba Rais Magufuli yupo kwenye msongo mkubwa wa mawazo, alijiaminisha kila mtu anamuabudu kisa fix zake za kujenga uchumi bila kujua kuwa watu wana hali mbaya.
Rais Magufuli anataka kuwaaminisha watu wavumilie shida ambazo yeye haziishi, huyu mtu haishi kwenye shida ya njaa, afya na kufunga biashara. Yeye anapewa kila kitu na wanaompa wanamuaminisha kuwa hali ni nzuri sana ili walinde vibarua vyao.
Sasa anapita huko akiona watu kibao anajua anapendwa sana, kesho yake anamshuhudia Lisu akiwa na umati ule ule bila uwepo wa Diamond, Kiba, Harmonize na mazombie wengine, hapa Magufuli kama binadamu mwenye akili zake anaona hali sio nzuri huenda napakwa mafuta kwa mgongo wa chupa ila huenda hali ni ngumu na nikisema niende kichwakichwa nikaibe bila mipango yanaweza nikuta kama yalivyowakuta wenzake huko duniani baada ya kuiba kura kijinga na anajua siku watu wakiamua CCM wenzake watamkimbia asubuh na mapema abaki mwenyewe.
Mimi binafsi sina tatizo na Magufuli kuwa Rais ila nina tatizo na hili dhehebu lake jipya aliloanzisha la kusifia na kutukuza.
 
Kwa wanayofanya ccm katika kuhaha kujinasua wanaweza fanya chochote ilimradi kiwavushe! Huko kwa wasimamizi ndiko uliko mpango mzima wa mauzauza, Tukiweza kukaba huko hakuna pengine!
Nakumbuka mwaka flani mgombea wa sasa wa ccm akiwa mbun ge kule chato aliwahi sema ccm itashinda milele sababu wakurugenzi wote ambao ndio wasimamizi wa majimbo ni makada watiifu wa ccm, hivyo uwezekano ni mkubwa wa kuendelea kutumia mazoea hayo! Pia kuna tetesi kuwa ccm imeagiza nafasi zote za usimamizi wa uchaguzi wapewe Umoja wa vija ccm, yawezekana ndipo maagizo hayo yalipenyezwa! Maana hata muda wa kutangaza nafasi hizo kwa mwaka huu unaacha maswali mengi. Uchaguzi ni October 28, lakini nafasi za kusimamia zimeshatangazwa na sehemu nyingine leo ndio deadline ya kupeleka maombi! Tunajiuliza ni kwanini mwaka huu nafasi zimetangazwa mapema kiasi hiki wakati hata mafunzo tu ya semina huwa ni siku moja au mbili??
Je au ndio kusema wanataka kupanga safu ya wasimamizi wa kukiokoa chama flani? Yote katika yote tunashkuru Mungu mwaka huu kila mbinu inayochomekwa taarifa zinzpztikana na hii ni dalili kuwa Mungu yupo kazini anapigania haki!
Washindwe na walegee wote wenye nia ovu ya kuhujumu maamuzi na matakwa ya wananchi!
 
Kama hawa ma DED watakubali maelekezo ya mteuzi wao ambaye ni mgombea na baadaye uchaguzi ukaharibika na kupelekea fujo na upotevu wa uhai wa watu, damu itakuwa juu ya vichwa vya wale majaji wa mahakama ya rufaa waliobadilisha maamuzi ya mahakama kuu na kuwarudisha hawa ma DED kusimamia uchaguzi mkuu.
kazi kufikiria machafuko tu. we na familia yako mtakuwa mnaishi angani hamta athirika. Ina maana hamjui Raisi bado yupo madarakani na anaweza endelea na shughuli za kiserikali.
 
Jiwe atakuwa anawapa wasimamizi masharti na vitisho kuwa "ukimtangaza mpinzani kuwa mshindi na ukurugenzi unaishia hapo..."
Zipo taarifa za Mwenyekiti wa chama tawala kukutana na wakurugenzi Dodoma wakati kampeni zinaendelea huku Hawa wakiwa ndio wasimamizi wa uchaguzi kwenye majimbo. Tume ya uchaguzi inazungumziaje hatua hii?

Je Ni kweli mkutano huu upo au Ni propaganda za majukwaani tu?

View attachment 1582153



Maji yameshazidi unga
Kila tawi analoshika halishikiki!
Anahangaika tu. Anashika hiki anashika kile.

Maji yamezidi unga.😂😂😂
Keshokutwa atawaida polisi na wanajeshi.
maji kushingo!
Kiujumla in uharamu na haikubaliki.Jpm katuangusha sana watanzania kwa kweli....haki huinua taifa
Umezitoa wapi hizo taarifa kama huo siyo umbeya tu. Ikifika asubuhi ndipo utagundua kuwa ulikuwa unaota tu.
Thibitisha basi comrade ili tuache kujadili tetesi na porojo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom