Uchaguzi 2020 Mgombea Urais kupitia ACT-Wazalendo, Bernard Membe achukua fomu za Kugombea Urais wa Tanzania ofisi za NEC

Mahesabu yako hayako sawa Mh Magufuli alipata 58.46% of total votes. Wapinzania kwa ujumla wao walipata 41.54%
Kumbe. Basi walimwibia Lowassa kura zake. Imebidi nikaangalie kumbe Lowasa alipata asilimia 39😭
 
Kapicha mkuu
 
Kesho ni zamu ya Rais wa Jamhuri anatinga!! Hupendi bac zima data hiyo kesho siku nzima ili usikereke!! Ni ushauri tu kwako tena wa bure!!
 
Naamini Makubaliano kati ya CHADEMA na ACT yameshindwa.

Kuna Ishu ya kuachiana majimbo, nadhani hapo ndo pamekuwa pagumu

Kwangu naona ni sawa tu, waswahili wote ni ngumu kuungana maana maslahi binafsi ndio yako mbele. Ni bora kila mtu ashinde mechi zake, kuliko huko mbele ya safari kuishia kuchafuana kutokana na kurubuniwa na ccm. Mfano wa CUF na NCCR uko wazi.
 

Sasa wanazigawana kura ndo hicho CCM wanakitaka
 
Kwangu naona ni sawa tu, waswahili wote ni ngumu kuungana maana maslahi binafsi ndio yako mbele. Ni bora kila mtu ashinde mechi zake, kuliko huko mbele ya safari kuishia kuchafuana kutokana na kurubuniwa na ccm. Mfano wa CUF na NCCR uko wazi.

Nakuunga mkono.

Huu uchaguzi ndiyo utakaoitangaza ACT nchi nzima na kupata inroads na kujisimika.

Bila vyama vyote kusacrifice, yaani kutaka kutumiana tu kama ngazi ili mmoja anufaike na mwingine awe mbeba viatu vya mwenzie bila shaka kungepelekea mmoja kuja kujuta huko mbeleni.

Mimi ninavyoona, Mwananchi ndiye mwamuzi, kama watampenda mgombea mmoja basi watampa huyohuyo bila kujali mwingine ni nani!

Haifai kumlaumu yeyote kuwa kapunguza kura za mwenzie, wakati kama kweli wananchi wamempenda huyo wanayedhani angeshinda basi wangempa tu bila kujali wengine wote waliopo
 

Absolutely, nimeona NCCR na CUF wakilalamika kuwa cdm iliwaiingiza mjini. Ili kuepuka hilo, ni vyema kila mtu ajitegemee na adui awe ni ccm kwa wote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…