Uchaguzi 2020 Mgombea Urais kupitia CHADEMA, Tundu Lissu afanyiwa mahojiano kwenye kipindi cha ITV dakika 45

Lisu kachemka maeneo makubwa mawili la kwanza ilitakiwa aende na summary iliyoandikwa ya sera

Alipoulizwa kuhusu sera alitakiwa atiririke hasa azitaje zote ndani ya dakika chache. Hakuzitaja. Kakosa kutumia hiyo golden opportunity. Kaenda mahojiano hana hata ki notebook sera zote utakariri kichwani? Ndio maana kachemka hakuweza kuzitaja zote kaenda na over confidence hewa!

Pili kasahau kuomba kura kuwa watanzania naombeni kura zenu! Hajui hata kazi ya mgombea uraisi kuwa kazi yake kubwa ni kuomba kura.Yeye haelewu kilichompeleka ITV kuwa ni kumpa nafasi akaomba kura watanzania. Lisu hakujiandaa kugombea uraisi.utatokaje kwenye TV bila kuomba kura? Chadema mgombea wenu kichwa cheupee Alienda tu kutalii ITV
 
Not quite true. Hydropower ni gharama.
Kuni na mkaa vitaendelea kutumika. Gesi ndio suluhisho bora kwa nishati nafuu.
Cost. In the U.S., hydropower is produced at an average of 0.085 cents per kilowatt-hour (kWh). This is about 50% the cost of nuclear, 40% the cost of fossil fuel, and 25% the cost of using natural gas (WVIC, 2017). ... A high-efficiency rate of 90% is very impressive, along with the low cost to produce.Sep 14, 2017
 
Huyo Crimea ni robot lipo censored unapoteza muda wako bure kutafuta hoja nalo. We litukane achana nalo.
Ona hili taahira nalo!

Akitukana ndio kura za Lisu zinaongezeka?

Hata hivyo ni kawaida yenu mkiishiwa hoja hukimbilia matusi. Yani mtu mzima bila aibu unataka mtu atukane?

Hizi ni akili au matope?
 
Kama hayo mawili ndo unaita kasoro, basi ni wazi hukuona kasoro.
 
Kokote tumeshawakalisha .. chadema 3 ccm 0 ..hiyo inaitwa 3 bila ... mgombea wenu anaongelea madaraja na teuzi wakat October 28 atakuwa kijijini Chatto anaangalia lissu akiapishwa Taifa ...mwaka huu tafuteni kz ya kufanya, shauri yenu
Coment kama hii utakuta hata Lisu nae anaamini hivyo!
 
Ukimtathimini Lisu kupitia hapa JF basi kashakuwa rais
 
Acha fix mzee kaniletee idadi ya wanaotazama kupitia C band, haya madishi makubwa ya 6 feet halafu uje urekebishe takwimu yako
 
ITV haipo DSTV
 
Unajifanya hujui wakati hujui kitu.

Gas haichimbwi na Serikali. Unataka kujua bei ya floatinh rigs, drill roads na pipes za kusafirishia, kwani unachimba wewe?

Qatar ndiyo nchi inayoongoza kwa utajiri kwa kipimo cha per capita. Uchumi wake ni uchumi wa gas. Kama uchimbaji gas na mafuta ni aghali kiasi cha kuufanya uwe wa hasara, kwa nini mataifa yote yanayovuma rasilimali hiyo, uchumi wao kwa kiasi kikubwa hutugemea huo uchimbaji?

Gas haitumiki tu kuzalishia umeme. Gas ingechimbwa kwa lengo la export. Hilo ndilo lengo kuu. Lakini ingetumika pia kuzalishia umeme na kama malighafi ya kwenye viwanda vya mbolea. Rais Magufuli alivurunda sana kwenye sekta ya gas. Wawekezaji wakaamua kuondoka. Leo Serikali inahangaika kuwarudisha, nao wamegoma japo bado wanashikilia vitalu. The earliest wanaweza kurudi ni baada ya miaka mitano.

Dunia inajitahidi kuondoka kwenye umeme wa kuzalisha kwa kutumia maji kutokana na mabadiliko ya kimazingira. Umeme wa kuzalishwa kwa maji hauna sustainability. Nchi nyingi miaka ya karibuni zimekubwa na upungufu wa umeme kutokana na upungufu wa maji kwenye mabwawa. Haikuwa sahihi kwa sasa kuhangaikia umeme wa maji ambao sustainability yake ni ndogo, wakati tuna vyanzo vingine vya umeme ambavyo vinatufanya tupate faida nyingi kwa pamoja.

Fikiria pia ajira na intersectorial business.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nikiri mbele ya mungu, sijawahi kumfikilia kumchagua lisu na upinzani kwa ujumla, ila jana lisu amenifanya niwe na imani nae kwa asilimia 85% kuwa ana maono ya dhati kabisa na tanzania ya kesho yetu, ngoja kwa kipindi iki cha miaka mitano niweke imani kweke nimchague yeye, amenivutia sana sana sana kumsikiliza, mungu ambariki mnoo
 
Safii sanaa mkuu,usiaribu kura yako kwa wanaochukua media zoote nchin kutangaza mambo ambay hayana umuhimu kwa wananchi wa chini
 
Nami nikiri sikuwai kujua kuwa Lissu ana maono makubwa kiasi hiki, uwezo mkubwa kiasi hiki na mipango mizuri na kabambe kiasi hiki.

Lissu kusema kweli ameitumia vizuri hii golden chance aliyopata kwenye kipindi hiki. Na ukweli ni kuwa kaonyesha ni Kwa nini inasemwa kuwa ni Yeye kwenye uchaguzi huu ndo tumuweke atuongoze.

Mungu ambariki na amuwezeshe ashinde nafasi ya uraisi mwaka huu na awe raisi wetu wa Tanzania 2020 - 2025 kwa Jina lake Takatifu Yesu Kristo! Amina.
 
amein
 

Kwa nini unaumia???....Ona sasa umepika data ukashindwa kutambua kwamba ITV haipo DStV!....Na ulaaniwe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…