Uchaguzi 2020 Mgombea Urais wa CHADEMA, Lissu kaahidi Bima ya Afya kwa wote

Uchaguzi 2020 Mgombea Urais wa CHADEMA, Lissu kaahidi Bima ya Afya kwa wote

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Kampeni za uchaguzi zishaanza.

Wagombea wanakatiza nyika sehemu mbalimbali za nchi kuzinadi sera zao. Wanatoa kila aina ya ahadi. ‘Mimi nitafanya hivi, nitafanya vile, nitafanya haya, nitafanya yale’.

Sasa mimi ni mmoja wa watu ambao huwa sitegemei mwanasiasa au mtu mwingine kuniboreshea maisha yangu. Naamini hilo jukumu linaanzia na kuishia kwangu mimi mwenyewe. Nimemsikia mgombea wa CHADEMA akitoa ahadi tele. Ahadi zinazowapagawisha misukule wake.

Moja ya ahadi anazotoa ni ile ya bima ya afya kwa wote. Yaani kila mtu, kila raia, eti awe na bima ya afya. Mimi si mtaalamu wa mambo ya bima wala mambo ya afya. Na wala sina ‘usomi’ wowote ule. Nimeishia kidato cha nne tu 🤣😉. Hivyo, huenda nikawa na uwezo mdogo wa kuelewa na kuchanganua mambo.

Katika ahadi zake hizo, sijasikia namna ambayo mgombea huyo wa CHADEMA ataweza kumpatia kila raia hiyo bima.

Hizo hela atazitoa wapi? Ataenda kuziomba kwa nchi hisani? Ataongeza viwango vya kodi ili kuongeza mapato yatayotumika kuileta hiyo bima? Au ataomba kwa Mungu atudondoshee hizo hela toka mbinguni?

Ahadi ni tele. Namna ya kuzifanikisha ahadi hizo, mpaka sasa ni sufuri!

Oh, na jingine ambalo sijamsikia kabisa akilizungumzia ni hili suala la Corona.

Kulikoni wewe mbeba maono wa CHADEMA? Ushakubali sasa kuwa Corona haipo? Au ushakubali kuwa ipo, lakini si hatari kama tulivyolishwa matango pori na Wazungu?

Manake we mwenyewe tokea urudi, zaidi ya mwezi sasa, huvai cha barakoa na wala hujitengi na jamii!

Unajichanganya kama ilivyo ada na sijakuona hata mara moja ukipiga chafya wala kukohoa.

Kwenye suala la Corona, hata kama huwezi kukiri kwa sauti, nahisi kimoyomoyo unakubaliana na jinsi Ngosha alivyoamua kukabiliana nalo😉.

Sisi akina Ngosha hatukutishika. Mfano mimi, hakuna hata siku moja niliyojifungia ndani. Sijawahi kuvaa barakoa. Na bado nipo nadunda nikibeba maboksi tena yale mazito kwelikweli ilhali kuna watu eti mpaka leo hii wamejifungia ndani kama mwali.

Mangosha wa ukweli hawawezi kujifungia ndani wakiogopa mafua na kikohozi💪🏿💪🏿.
 
JPM alipaswa kuwa nyampara wa barabara na madaraja na sio rais wa nchi!Mwaka huu piga chini huyo Mobutu Seseko,kura yangu kwa Lissu!
Nyie Mataga mmebakiza maneno ya kanga,hamna jipya!Jiwe naye anawaza kumuhonga Lissu maana mambo yamebana!
😁😁,mpaka kampeni ziishe jiwe atakuwa amerukwa na akili!
 
CCM hawapendi kabisa kusikia habari ya bima ya afya.

Sasa kama tunajenga zahanati kila kijiji wananchi watatibiwa kwa utaratibu gani?

Je, serikali inaweza kugharamia matibabu bila wananchi kuchangia kwa namna yoyote ile?
 
Afya ni mtihani mkubwa kwa Watanzania, bima ya wote ni suluhu. Majengo afya mengi hakuna madawa na vifaa tiba vingi mgonjwa anapewa orodha akanunue kabla ya huduma, hata gloves, syringe, nk
 
Kwa mujibu wa mapendekezo ya SADC kwa wanachama wake bajeti ya wizara ya afya inapaswa kuwa angalau 15% ya bajeti nzima ya serikali, hivyo bila shaka Lisu atazingatia hilo.
 
Msukule ni baba ako na mama ako walioshindwa kukutunza ukakimbilia marekani kwenda kubeba box.

Wewe mbeba box utawashauri Nini watanzania.? Maisha yako tu mtihani.

Elimu bure ndio nyie wapumbavu mlisema haiwezekani? Leo ni bilion 22 tu kwa mwezi kwa nchi inayokusanya trion 1 kwa mwezi..

Bima wapi Lissu amesema atatoa bima bure? Lissu alisema ataleta bima na atahakikisha zinakuwa zenye ufanisi sio za Sasa za kulipa laki 190

Halafu unaambiwa dawa hakuna upumbavu mtupu kweli ukiwa CCM unakuwa mpumbabu Sana .

Swala gani halitekelezeki la TRA kufumuliwa? Na kuanzisha Kodi moja bandalini ambayo Ni 10% ya mzigo unaoagizwa..

Maana ya kupunguza Kodi Ni kuuza Sana kama tulikuwa tunatoza Kodi 50% ya bidhaa zinazoingia nchini ikashushwa mpaka 10% it means tutahakikisha tunaongeza uingizwaji wa mizigo kwa 40% ili kuendana na mapato Yale Yale bila kuwaumiza wafanyabiashara.

CCM mnaona kwamba vitu havitekelezeki kwa sababu mliishi kwa uongo na upumbavu na ndio nyie mnaowafanya watanzania misukule .

Muache kuwa wapumbavu na kuita watu misukule wakati nyie ndio misukule.
 
Selikali ya CCM inadhurumu watanzania.
Bima ya Afya ninayo nakatwa kwenye mshara wangu. Lakini nikienda hospital Hakuna Dawa, hakuna vifaa tiba, hakuna Madaktari, glaves ni aibu sana kwa kweli. Unaelekezwa duka unalopaswa kwenda kununua hivyo fifaa na dawa.

Bila matibabu Bima ya Afya ni mzigo.
 
We ushasikia hizo ahadi atazifanikishaje? Hela za bima ya afya kwa watu wote atazitoa wapi? Atazichapisha labda?


Inawezekana wewe umeshalewa "Bhusega" ndio maana huoni mikakati ya TL ya kupata pesa ya Bima, ni vipi unashindwa kuona namna ambayo serikali hukusanya mapato na kupanga bajeti zake? mkuu kweli wewe ni nyani kama nyani wa Jangwani
 
Mangosha wa ukweli hawawezi kujifungia ndani wakiogopa mafua na kikohozi💪🏿💪🏿.
Nasikia kuna mmoja alikiambia mujini akaenda kujificha hukoo......(LoL) au yeye si ngosha mwenzetu!!!!
 
Watu wenye upeompana wa ufahamu wa mambo wanataka Lissu afafanue fedha za mambo yote anayoahidi anazitoa wapi kama ni kodi basi aseme.

Kama JPM kashindwa kuongeza ajira yeye Lissu ataongeza ajira atazitoa wapi?.sio kupayuka tu kama anakula ugali na mrenda.
 
Naona hoja yako ipo kwenye "hizo hela atatoa wapi"?

Kwani wale wenye bima za afya hususani watumishi wa umma, pesa zinatoka wapi?!

Do you need to be reminded kwamba wapo watu wa kawaida wenye kipato kizuri tu tena pengine kuliko hao watumishi wa umma lakini bado hawana bima ya afya?!

WHY?

Kwa sababu issue hapa sio pesa bali ni mfumo ! Ukishatengeneza mifumo inayoeleweka, hilo suala linawezekana!

Chukulia mfuko wa bima ya afya kwa wale ambao sio watumishi wa serikali... ukienda, unatajiwa figures za ajabu ajabu; kwa mfano mtu na familia yake kwa mwaka zaidi ya TZS 1M

Kama kwa mwaka ni zaidi ya 1M, ina maana kwa mwezi ni almost 80K. Je, unataka kusema watumishi wa umma hata wale wa ngazi za chini wanalipa 80K kwa mwezi?!

Why hawa wa mtaani watakiwe kulipa kiasi kikubwa kiasi hicho?!

Tena kiuchumi, unaweza ku-increase revenue kwa kuongeza sales ambazo nazo zinaweza kuongezeka kwa ku-lower price!

Which means, ukisema say 20K wengi wanaweza kuchukua hiyo bima na bado mfuko usipate hasara kwa sababu sio wote watakaotumia!

Kinyume chake, unaposema 80K, watu wanaamua kukimbia moja kwa moja... ndo kama yale ya kodi yanayosemwa!!

Aidha, wanaposema bima ya afya kwa wote haina maana kwamba kv (say) kuna Watanzania 56M basi each and everyone out 56M people watakuwa na bima bali unaweza kutengeneza mfumo and affordable plan to make each and everyone kuwa na bima ya afya!
 
Ukitaka CCM wahare damu gusia suala la kuwapa wananchi hasa wazee na walemavu bima ya afya na swala la kuwaongezea mishahara wafanyakazi ambao wameteswa na CCM kwa miaka 5 bila kuongezewa mishahara.
 
..CCM hawapendi kabisa kusikia habari ya bima ya afya.

..sasa kama tunajenga zahanati kila kijiji wananchi watatibiwa kwa utaratibu gani?

..je, serikali inaweza kugharamia matibabu bila wananchi kuchangia kwa namna yoyote ile?


Hapa sasa ndio ushangae kauli za kiranja wa mabox huku ugaibuni
 
..CCM hawapendi kabisa kusikia habari ya bima ya afya.

..sasa kama tunajenga zahanati kila kijiji wananchi watatibiwa kwa utaratibu gani?

..je, serikali inaweza kugharamia matibabu bila wananchi kuchangia kwa namna yoyote ile?
Well, hata wao maswali yanawahusu...
 
Back
Top Bottom