Mhadhara wa Uprofesa: Machungu ya MV Bukoba, Dola na soko

Mhadhara wa Uprofesa: Machungu ya MV Bukoba, Dola na soko

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,151
Reaction score
4,277
Katika tukio la kipekee ambalo linakipa Kiswahili nafasi iliyopokwa siku nyingi ni tukio la muhadhara wa uprofesa kuendeshwa Kwa lugha ya Kiswahili.

Mchango mkubwa wa Profesa Mkandala katika hili siyo jambo dogo. Ni dhahiri kuwa ana mchango mkubwa yeye binafsi na kupitia historia yake ya kiuongozi.

Mihadhara ya aina hii ni nafasi adhimu ya lugha na kupitia nafasi hii Kiswahili kinaikanusha methali isemayo "nabii hakubaliki kwao" Kwa mara ya kwanza.

Mhadhara huu unatukumbushia pia machungu ya ajali ya kuzama kwa meli ya M.V Bukoba. Huku ukitoa sababu kadhaa ambazo zilitolewa na wataalam juu ya ajali hiyo. Maelezo hayo aliyoyanukuu Profesa Mukandala yanaonesha bila shaka kuwa lipo jambo la kujifunza mpaka leo. Maswali mengi juu ya ajali hiyo ya meli ya M.V Bukoba bado yaliacha maswali mengine.

Miaka 15 baada ya ajali ya M.V Bukoba meli nyingine aina ya MV. Spice one ilizama, Miaka saba baadae meli ya M.V Nyerere ilipata ajali. Swali ni nini tunajifunza?

Taasisi kubwa Duniani ni dola na soko. Dola na soko havipo sawa Kwa sababu mifumo ya masoko inatengenezwa na nguvu za dola hivyo ipo haja ya kutazama dola na soko kwenye ajali ya M.V Bukoba. Soko linafasiriwa kama njia za uzalishaji mali.

M.V Bukoba ilikufa ila taasisi yake haikufa. Mhadhara huu wa kipekee unatukumbusha historia ya kuvunjika kwa jumuia ya Afrika mashariki na hasara tuliyoipata Tanzania.

Michakato ya manunuzi ya meli haikufuata utaratibu wa manunuzi. Hakuna uhakika kuwa michoro ya meli na uwezo wake kama ilipitiwa.

Mikataba: Hakukuwa na upembuzi yakinifu hivyo hatua za kawaida za ununuzi hazikufuatwa.
 
Katika tukio la kipekee ambalo linakipa Kiswahili nafasi iliyopokwa siku nyingi ni tukio la muhadhara wa uprofesa kuendeshwa Kwa lugha ya Kiswahili...

1. Huyu ni yule wa ile tume ambayo ilipendelea katiba mpya baada ya 2030?

2. Kwamba katika kipindi chote hicho ingekuwa imeweza kujihakikishia ajira ya kudumu?

3. Kumbe katiba mpya ingepatikana vipi kama kupatikana kwake ndiyo ingekuwa kibarua chao kuota nyasi?
 
Kumbe mhadhara wa uprofesa huwa hivi?, basi lazima tuwe vile?

N. B, hapa JamiiForums tuna ma Dr, Maprofesor wengi mno!, the way I listening this, proffesorium!
 
1. Huyu ni yule wa ile tume ambayo ilipendelea katiba mpya baada ya 2030?

2. Kwamba katika kipindi chote hicho ingekuwa imeweza kujihakikishia ajira ya kudumu?

3. Kumbe katiba mpya ingepatikana vipi kama kupatikana kwake ndiyo ingekuwa kibarua chao kuota nyasi?
Mkuu karibu REDET
 
Anapohusisha plate tectonic za kijiografia na za kijamii naona kuna mahali ananigusa hivi.
Prof. Rwekaza Sympho Mukandala" Dola na soko ndiyo plate tectonic za kijamii"
Hili nalichukua nikiamini nimelitoa kutoka kwa Profesa wa sayansi ya siasa.
....................................
Aliposisitiza katiba mpya naona safari mpya inaanza.
 
Rais Mstaafu Mh. Jakaya Mrisho Kikwete nahisi anapata maswali magumu sana kimoyomoyo kwenye hii "magisterial inaugural lecture"...
Ni kama kaburi mojawapo limefunuliwa.

Jenerali ulimwengu anaongezea kamsemo "kujifanya hamnazo"
Daah anaposema "Imperial President ni kama anatonesha zaidi suala la mamlaka ya Rais.

Hii inaonesha hata wasomi wanataka mamlaka ya Rais ipunguzwe kuepusha majanga kupitia dola na soko.
 
Hii inaugural lecture Kadiri watu wanavyouliza maswali inatanuka na kuwa kama mzimu hivi, uhahitaji damu zaidi. Profesa Rwekaza Mukandala anakiri na kushukuru kuwa maswali ni magumu na yanafikirisha...

Hii ni miongoni mwa "inaugural lecture "matata sana kuwahi kusomwa Tanzania tena kwa lugha ya Kiswahili. Ikumbukwe vyanzo vya Taarifa za mhadhara huu kimoja wapo ni Ripoti ya Jaji Kisanga iliyowekwa wazi tofauti na ripoti nyingine.
 
Upekee wa mhadhara wa aina hii ni kuwa, mihadhara ya aina hii hususani kutoka kwenye sayansi ya siasa tangu ufanyike mhadhara wa mwisho ni miaka arobaini na tano 45 iliyopita.
...................................
Utafutaji wa mada ya kusisimua unazidi kutufanya kuwa na moyo wa shukrani na kuangalia zaidi juu ya nini cha kufanya.
...................
 
Back
Top Bottom