Mhe. Rais Magufuli Kufufua Mmoja wa Mradi Mkubwa wa Kufua Umeme Afrika wa Stiegler's Gorge

Mungu mjalie Rais wetu atekeleze yote
Kwa hapa tulipofikia tumebaki nyuma,yatupasa kukimbia
Viwanda kwa kutegemea chanzo kimoja cha mapato ni shida
Mnaompinga Rais wenu kazi mnayo
 
Shein ashitukia Mikataba ya Mafuta na gesi... ampongeza Magufuli...
 
Fungeni vibwebwe tujenge ujamaa!
Sijui kwanini nimekumbuka huu wimbo.
 
Alishasema Tanzania ni tajiri we unawaza expensive tena
 
Tabia ninayo iona hapa ipo hata mitaani kwetu....... ukiwauliza wasanii hata muulize Diamond platnumz atakwambia wakati naanza kunawatu walisema siwezi kuimba siwezi kufika mbali.......hii tabia ni yakiasili zaidi kwa wa Tanzania, na baadhi ya binadamu wengi duniani......... Hawawezi kuappriciate wakati una hustle, watakubeza tu,.....
 
Kwa wasio fuatilia mambo hawawezi kugundua uwezo wa Rais Magufuli pale anapo amua kufanya mambo makubwa hasa yaliyo washinda walio tutangulia. Ktk hili la umeme ni na thubutu kusema Magufuli atafanya, Iwe kwa mradi huu au mradi mwingine wowote wenye lengo la kuzalisha umeme Tanzania.
Rais Magufuli analipa kipaumbele swala hili la umeme akijua kwamba mambo mengi aliyo yaanzisha na anayotaka kuyaanzisha yana tegemea nishati hii ya umeme ambayo imekuwa adimu na yenye kutumiwa vibaya na wala rushwa.

Mungu amsimamie ili aweze kulitimiza hili kwa maendeleo ya nchi yetu. Penye kustahili pongezi ni vema tuka pongeza tu kwani ameweza kufika katika eneo la mradi na kufanya mazungumzo na wahusika na tumesikia kauli zake. Nina Imani ATAFANYA.
 
Najua right inside your heart you know that Stieglers Gorge is not a dream, ila una jikaza tu.Pole mkuu.Bwawa litajengwa mkuu, take my word. JPM is a man of action,not of empty words.

Ile 50m kila kijiji huko kwenu mmeipata? Maana mwaka jana ilikuwa kwenye bajeti, ila mwaka huu hata kuongolewa haijaongelewa. Sasa sijui ukisema man of action unamaanisha nini.
 
Mkuu Chige nashukuru umeliona hilo na kwa maoni yangu hilo ndiyo tatizo letu. Mradi ni mzuri sana lakini turudi kwenye planning kwanza kule tufanye prioritization ili miradi kama hii ndiyo ipewe kipaumbele in terms of resources allocation hata kama ni kidogo kidogo kila mwaka. Kuna nchi za wenzetu wana miradi kama hii lakini ilikuwa planned miaka 30 iliyopita. Why can't we borrow a leaf from them?
 
Hizo pesa za viongozi kuzurura nje akizibana atajenga mradi wa Umeme , chezea Magufuri wewe ngoja anyoroshe nchi
 
Toka tulipoaminishwa kuwa Gesi asili ya Mtwara ikifika Dar tatizo la umeme litabaki kuwa historia sina imani na hawa jamaa

Maana bomba limetafuna ma bilioni ya Shiling sasa tunaambiwa na CAG linafanya kazi 4% tu.
 

Hakuna asiyependa kuona maendeleo shida ni pale ambapounajiuliza atapata wapi fedha za utekelezaji?

Kukopa tayari deni letu lipo kwenye taa ya njano very soon tutakuwa hatukopeshiki. Vyanzo vya ndani havitoshi labda kwa miaka mitano. Je mradi huo upo kwenye mpango wa miaka 5?

Lakini tuangalie pia kwenye gas ambapo baado tunaweza kuweka mitambo mingine kwa gharama (kulingana na uwezo wetu) na tukaongeza uzalishaji.

Huo mradi ubakie tu tukiwa tayari tuufanye. Ni kweli hydropower is the cheapest of all. Lakini tunaafanyaje wakati uwezo wetu kifedha ni mdogo
 
Ile 50m kila kijiji huko kwenu mmeipata? Maana mwaka jana ilikuwa kwenye bajeti, ila mwaka huu hata kuongolewa haijaongelewa. Sasa sijui ukisema man of action unamaanisha nini.
Ahadi ya 50 million hakutoa JPM, ilikuwa ya Vasco Da Gama.Nadhani unalijua hili.
 
Universe umeme bongo ni hatari upo ghari sana ndio maana unakuta watu wenye umeme hata wewe una jiko la gesi ndani ili kupunguza makali ya gharama sitakiwi kujua wamefungua kinyerezi au la ntakapoona umeme haukatiki hovyo na gharama zimepungua ntajua wamemaliza walichoahidi...
 
Kwa hela msiyoiona mtaani utaiona kwenye miradi.Subiri,ikikamilika tafuteni namna ya kukosoa.
Pesa kutoonekana mtaani ni sababu ya kutokuwepo miradi inayotekelezwa .sasa wewe unakuja kinyume chake.miradi ingekuwa hipo ndio ingeleta pesa mtaani .umesahau pia Mwaka Wa fedha 16/17 miradi imetekelezwa kidogo 38% ndio maana hakuna mzunguko mkubwa pesa .[emoji12] [emoji12] [emoji12]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…