Elections 2010 Mheshimiwa John Pombe Magufuli awe Rais wetu

Elections 2010 Mheshimiwa John Pombe Magufuli awe Rais wetu

Hahahaa, ngoja kwanza nikamuulize Sundi, ile nyumba aliyohongwa na kuwanyima haki walioitumikia serikali kwa miaka lukuki aliirejesha?

Lile swaga linatafasiriwa vibaya nasikia pale Sundi alipangishwa kama mwanafunzi wa Chuo kikuu cha Dsm, so ilipogundulika Mzee anapumzika pale ikawa pia kamuuzia lakini hakuna kitu kama hicho nilidokezwa na Jamaa yangu walifuatilia sakata hilo wakakuta ni uvumi na uzushi ndo maana JK kamurudisha Magufuli Ujenzi!!
 
A very poor and most incompetent manager I ever worked with! Kwa taarifa yako (wewe na wengine mnaodhani Magufuli ni mchapa kazi) 99% ya "amri" anazotoa huwa zimefanyiwa kazi na mamlaka husika (mostly donors) yeye hurukia kutangaza ili kupata popularity.

Kiini cha watu kudhani Magufuli anaiwezea wizara anayoongoza in ujenzi wa barabara (ambazo practically zote ni donor-funded). Kwa taarifa yenu; donors wana-direct kila kitu, kuanzia procurement za consultants na contractors hadi malipo ambayo donor country hulipa directly kwenye account ya consultant/contractor. Serikali ina-manage 10% contribution (ambayo nayo mostly ni administration and local taxes). Ni sawa na mtu aje akujengee nyumba halafu wewe ujisifu kuwa umejenge nyumba!

Unaonekana ulizaliwa kabla ya siku zako hazijatimia - kwa akili ya kawaida tu tembelea tovuti ya TANROADS utaona barabara zinazofadhiliwa na donors na zile zinazotumia hela za serikali, utagundua zaidi ya asilimia 70 ya barabara zote zinajengwa kwa hela za serikali, serikali ilishaacha ule mtindo wa kusubiria wafadhiri ndo ijenge barabara na CNN juzi juzi wametangaza Tanzania ni moja Kati ya nchi tano zinzoinvest heavily kwenye infrastructure za barabara na ni ya kwanza kwa Africa Mashariki!

Umeniboa sana uliposema tuna asilimia kumi tu katika kuchangia Ujenzi wa barabara, ni uongo na upotoshaji wa kutupa! Tena huyo Magufuli ndo alilazimisha kwanza kujanga barabara kwa kutumia fedha zetu za ndani iweje leo unalazimisha kusahau historia au umetumwa?
 
Mgombea urais mwaka 2015 kupitia ccm ni kitendawilin kilichokosa mteguzi, kikija kuteguliwa basi ccm itagawanyika makundi makundi.
 
Piga ua! sasa ni zamu ya Zanzibar na Salim Ahmed Salim ndio Rais wetu take msitake! Nyerere alikuja Moshi mwaka 1995 ktk uwanja wa Mashujaa akimnadi Mkapa na Wachagga wakasema hawamtaki Mkapa! bali Mrema Lyatonga na majibu ya Nyerere yalikuwa Mkapa ni Rais wenu mtake msitake!
 
Afadhali ya Magufuli kaomba maboresho ya hospitali ambayo itasaidia na Watanzania wengine, kuna wengine wanapewa fedha na vitu vingine kwa matumizi yao binafsi.
 
Kwanza nadini ya CCM hawezi kukubarika kwa sababu wanajua kuwa atawasumgua kwa kutaka kwake sifa anaweza kufanya kitu cha ajabu bila hata ya kufikiria. Wanaojua vizuri mwanza watakumbuka vituko alivyofanya wakati wa uvunjaji wa kituo cha mafuta cha MOIL, alilazimisha kuvunja matokeo yake serikali iliwalipa pesa nyingi sana wale wahindi wa CCM! Kwa kupenda kujipendekeza JP alipongeza safari za raisi JK pamoja na kujua fika zinaliingiza taifa kwenye ghalama zisizo za lazima hii yote ni kwa sababu huyu mheshiwa anapenda sifa sana so alijipendekeza kwa JK kwa kumpa sifa zisizo na tija kwa watanzania of which watanzania sidhani kama tunahitaji raisi wa style hii. Kwa visasi ndo mwenyewe kumbukeni issue ya fast ferry za Azam alozileta lake Victoria, JP alitaka kumkomoa Mwandosya kwa vile alikuwa amekula karamu ya ujio wa meli hizo hivyo JP akajua kumkomoa ni kugoma kusaini boti hizo kupitishwa kwenye barabara zake kwa kisingizio ni nzito wakati kuna mitambo ya migodini ni mizito mara mbili ya boti hizo kila siku inapitishwa kwenye barabara zake na sisi watz tukishuhudia. Kwa kifupi JP hafai hata kidogo kuwa raisi, ikumbukwe tena aliwahi kupigiwa kelele na wananchi wa Buziku kwenye moja ya mikutano yake jimboni chato,alichokifanya ni kuwaambia kwa kisukuma " Buta baba gete mtalaibona ilami maisha ging'we pyee!" kilichotokea ni kuipindisha barabara ya lami ilotakiwa kupita Buziku akalazimisha ipite Chato ili kuwakomoa wananchi hao....sasa jamani tunamjadiri kuwa raisi wa nchi mtu wa aina hii? Labda kwa vile ni demokrasia acha tumuweke tena raisi wa majaribio kama tulivyofanya 2005 & 2010.

mkuu hapo kwenye red naomba nikurekebishe Magufuli alikuwa sahihi ni kwamba wale wahindi walipata title kwa njia ya rushwa na kikubwa ambacho magufuli alifanya ni kufata ramani ya barabara ila kwa kuwa manispaa ya mwanza walikuwa wamekula rushwa na kutoa hati basi ikabidi waingie hasara ya kulipa fidia kwa hiyo ilikuwa matokeo ya rushwa kwa viongozi wa serikali pale magufuli alistahiri sifa kwa kufichua uozo. hata hapa dar kuna viwanja vingi vya wazi vilivamiwa na watu wamepewa hati akija waziri ambaye anataka virudi basi serikali lazima ilipe fidia kwa uzembe wake. angalia sehemu za mbezi viwanja vyote vya wazi vimejengwa hakuna sehemu za kucheza watoto wala sehemu za shule mpya na hata sehemu za dispensari au hospitali na hivi vyote viliuzwa wakati Lowasa akiwa waziri nenda umuulize kama hajainama chini kwani anajua watu walishasahau.

Kuhusu suala la boti kwanza mmiliki si azam kama unavyosema alikuwa azim dewji alikuwa mfadhili wa simba zamani ila rejea majibu ya magufuli katika lile suala. uzito wa mzigo unaotakiwa kupita kwenye barabara zetu si zaidi ya tani 30 na zile boti ni zaidi ya hizo tani nashangaa waziri mwandosya tena profesa hakuangalia hicho kitu. na hili lazima uangalie kwa makini kwa sababu kuna culvert ndogo ndogo karibu zingefunjika zote. ila kingine zile boti ilikuwa zimechakaa sana ndio maana walivyoambiwa wanatakiwa kuzifungua na kwenda kuzifunga tena ilishindikana. hadi leo hazifanyi kazi zimepaki pale mwanza.
wachukue mwandosya na magufuli ukawaonyeshe zile boti zilipo uone nani ataficha uso kwa aibu.
 
Mmmmmmmmmmmm absolutely true waulize wananchi wa jimbo la Biharamulo alichowafanyia alipindisha barabara ya lami ipite nyumbani kwao kisa eti yeye ni waziri wa ujenzi na wananchi wa Biharamulo walikataa kumchagua kuwa mbunge 1990 huyu jamaa ni mbinafsi sana: Rockon:

barabara ya biharamulo ina lami na ile ya magufuli ina lami nimepita mwezi wa kumi na moja sasa sijui una maana gani kwani zote zina lami.
 
katika CCM ukianza kusema suala la usafi na kutokuwa na kashfa hutapata mgombea zaidi ya mwanangu Dr. Emmanuel Nchimbi na mzazi wangu Dr. Salim A. Salim. Wema wengine CCM wapo ila wapo mbali sana na meza ya maamuzi. Najua wengi mtakuwa mnashangaa ninapomsema Nchimbi but wait and you will see. Ni mtaalam wa siasa ndani ya CCM kuliko mnavyomdhania.
Wapiga kazi CCM wanajulikana ila nao sio malaika ni sawa na wengine.

Hapo wala sikubishii mkuu. Huyu Comrade ni mwanasiasana anajua fitina za kisiasa. Yuko kama kobe anangalia chini huku akitunga sheria.

Ila ikotokea Magufuli amesimama kwenye Urais basi CCM watakuwa wamemaliza uchaguzi kama mwaka 2005. Ila ndani ya CCM wenyewe wanamuogopa.
 
Magufuli hafai, mtu wa visasi sana na pia akikujia juu ujue hujatoa cha juu. Bara bara nyingi zipo chini ya viwango lakini hawarudii kuna nini hapo.
Wewe ndo unamjua vizuri. Visasi vyake na nongwa ni balaa. Pia fanya naye kazi ndo utamjua. Mwulize yule mkurugenzi wa zamani TBA nadhani anaitwa Kimweri.

Baada ya Magufuli kuondoka ujenzi mara ya kwanza yule mkurugenzi wa TBA alimchongea kwa waziri mpya Mramba kwamba magufuli aliwagawia nyumba mpenzi wake wa chuo kikuu na mdogo wake ambao wote hawakuwa wafanyakazi wa serikali, Mramba akawanyang'anya nyumba hizo hao watu wa magufuli. Loo! Magufuli kitu cha kwanza aliporudi ujenzi mwaka 2010 kazi ya kwanza ilikuwa kumfukuza kimweri. Huyu ni mfano mmoja tu. Amewanyanyasa watu wengi sana kila mahali anapofanya kazi.

Anawahadaa tu watu wasiomjua kenye TV. Pia hakuna anayechukua rushwa toka kwa makandarasi kama huyu, na kesho yake akikutana nao kwenye TV anawafokea utadhani anawafukuza siku hiyo hiyo, aah wapi! Geresha tu!
 
Adui wa kwanza wa Tanzania ni Ujinga unaozaa majungu,umbea,na chuki zisizo na msingi!Wanaume wengi wanaongea kwa mipasho wakiwa wamejaa povu mdomoni hata wanapopaswa kutoa hoja.

Matokeo yake wanashindwa kujipa muda wa kutafakari.Ni kweli hata ukitaka kufuga ngombe ili unaweza tu ukaanza na hoja kama ninazoziona hapo juu!Unajua harufu ya kinyesi cha ng'ombe?Unajua anakojoa lita ngapi kwa siku?alafu zile pembe zake zimewahi kutoboa mtu utumbo!

Usipokuwa makini anaweza kuyapiga teke maziwa unayokamua yakamwagika yoote!Baada ya visingizio hivyo mpumbavu yeyote ataziona kama hoja za msingi!Watanzania hatuhitaji malaika kama tulivyodanganywa 2005!Tunataka kiongozi anayejali maslahi ya wengi hata kama ni dictator!Aligawa nyumba za serikali!so what?

hamuwezi kujenga nyingine mnalalamika tuu! Eti wake zetu tuwaweke mbali!hawa wamekuwa bidhaa?kwani unajua sasa hivi nani ana cheat na mkeo?jiamini. Bhana!Mwisho toeni hoja za msingi au sivyo nyamazeni!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
mim binafsi naona mtu ambaye anaweza kuirudisha nchi yetu kwenye msitari ni Don King achilia mbali mapungufu mengine ambayo hata mim na wew tunayo.huu ni mtizamo wangu tu lakin
 
ALIUZA NYUMBA ZA SERIKALI ,YEYE NDO ALIKUWA RAIS?? ETI UNAMJUA MAGUFURI TOKA AKIWA TANROAD MOROGORO ,TANGU LINI MAGUFURI KAFANYA KAZI TANROAD ??? ACHENI ULONGO,HOO KUNA KIPANDE MWANZA KINAJENGWA TOKA 2005,KWANI TOKA 2006 MAGUFURI NI WAZIRI WA UJENZI?? OOH NI MTU WA VISASI,ALIKULIPIZIA KIPI??USIPENDE KUSHUHUDIA BINADAMU WENZIO UWONGO SABABU TU UMEPATA NAFASI YA KUWAJADILI.-To me Namuona Magufuli Kama Mchapakazi wa kuigwa,HAIJALISHI ANATAKA URAIS au lah,KAMA MTU AWEZA MPUUZA MZAZI ALIYE MZAA NA KUMSOMESHA,ITAKUWA MTU KUMPUUZA MAGUFURI ?? ANASTAHILI PONGEZI ZA UTENDAJI SAWA NA MTENDAJI YEYOTE AMBAYE KAZI YAKE INAONEKANA .
 
Ninamkumbuka sana Magufuli kwa haya yafuatayo:

1. Alipokuwa Mifugo na Uvuvi Tanzanzia kwa mara ya kwanza ilikamata maharamia wa kigeni waliokuwa wamezoea kupora samaki wetu - alitoka na msemo wa bahari yetu siyo shamba la bibi. Kikubwa zaidi maharamia hao tena wa kigeni wamehukumiwa kifungo ndani ya ardhi ya Tanzania, waziri gani mwingine kafanya tukio kama hili?? Huyu kwangu ni shujaa!

2. Miaka ya 2000 alikamata magari ya serikali zaidi ya 21,000 ikiwemo mitambo na pikipiki. Magari enzi hizo yalikuwa yakiandikwa mpaka majina binafsi mfano nakumbuka moja liliandikwa Mwakajinga! Isitoshe zoezi hilo limerudiwa juzi kati ambapo magari zaidi ya 1000 yamealikuwa yanatumika vibaya kwa kuwa yalikuwa na namba za kiraia - kwangu mimi huyu ni kiongozi anayelinda mali za umma na kuhimiza matumizi sahihi ya mali za umma. Lakini maadui zake walioguswa na zoezi hili wanamshambulia, ni jukumu la wananchi wa kawaida kulijua hili!!

3. Amejenga barabara za lami zaidi ya kilometa 11000 na mpaka CCM wamekuwa vihelele wakimtumia kwenye majukwaa ili afanye presentation kuhusu mafanikio ktk ujenzi wa barabara tangu uhuru, lakini kibaya zaidi humohumo ndani ya CCM kuna kundi lipo kimkakati kumvuruga pengine aonekane si kitu!

4. Kumekuwa na malamiko ya barabara kujengwa chini ya kiwango, Magufuli kawakaba makandarasi wote na sasa barabara ya Singida kwenda Shelui, upande wa Sekenke inarudiwa na Mkandarasi kwa gharama zake zipatazo shilingi bilioni 15 na juzi kati tumeona makamu wa rais akifungua ile ya Mbagala ambapo Mkandarasi alirudia kwa hela zake, leo Magufuli anaoneka mbaya?

5. Alipokuwa wizara ya ardhi alianzisha mradi wa Viwanja 20,000 kule Kigamboni na kurudisha uwajibikaji wa wafanyakazi wa ardhi kiasi cha wananchi kusifia huduma za Wizara, leo hii mtu huyu anaonekana si lolote ndani ya CCM

6. Akiwa Ujenzi alizuia meli kubwa kusafirishwa kwa njia ya barabara ambapo ingeharibu barabara na hata meli hilo lisingeweza kupita ktk madaraja , lakini CCM hawaoni hili??

7. Kuhusu nyumba nakumbuka lilikuwa ni Azimio la Serikali nzima ambapo baraka zilitoka ktk baraza la mawaziri na yeye alikuwa na jukumu la kutekeleza tu! Sasa wana CCM hata siku moja hawatokei kumtetea hata kwa maneno mepesi tu, mtu huyu anaonekana kwao mbaya! Lakini katika hili nakumbuka hata Nyerere aliuza nyumba za serikali mfano pale Magomeni, Mwanza( Ghana Cottage), Tabora etc wana CCM wameshindwa kutumia mfano huu kumlinda kijana wao???

8. Humu jamvini Watu wanaandika Magufuli kawahi kuwa meneja TANROADS Morogoro ? Uvivu wa kufuatilia taarifa sahihi za viongozi - Hebu angalia CV za wabunge ktk tovuti ya bunge kama Magufuli aliwahi ajiliwa na Wizara ya Ujenzi kama mtumishi wa Umma?

9. Aliwahi chafuliwa kwa kuandikwa na gazeti moja kwa kipindi cha Miezi minane mfululizo, na baadae aliyefanya/tekeleza kazi hiyo kazawadiwa ukuu wa wilaya fulani- sisi siyo wajinga, tunajua mambo hayo!

10. Katika chaguzi za mwaka 2000 na 2005 alipita bila kupingwa jimboni kwake Chato na hata chaguzi za 1995 na 2010 ukiangalia matokeo utajua ni jinsi gani wananchi wake wanamhusudu lakini leo hii watu wanataka kuupoteza ukweli!

11. Lakini hata hivyo, mawaziri wenzake wanakubaliana naye jinsi anavyofanya kazi bila kuogopa mtu!

12. Ndiye aliyeanzisha mfumo wa kujenga barabara kwa kutumia hela zetu za ndani bila kutegemea wafadhiri na alianzisha model ya design and build mpaka wenzetu jirani Kenya wakaja kuiga kipindi hicho Raila Odinga akiwa waziri wa barabara wa Kenya!

13. Ni waziri pekee aliyekaa Wizara ya ujenzi kwa muda mrefu penye vishawishi vya rushwa bila shutuma yeyote ile

WITO WANGU KWA MHESHIMIWA MAGUFULI:

1. Wanaokuchafua sio sisi CHADEMA bali ni wana CCM wenzako ambao kila kukicha wanakuogopa kwa vile unakubalika na wananchi walio wengi!

2. Nakushauri jiunge na CHADEMA ili uje kushirikiana na Dr . Slaa tayari kwa ukombozi wa taifa hili

3. NAKUSISITIZA MHESHIMIWA MAGUFULI NI WAKATI WAKO SASA KUHAMIA CHADEMA

pamoja na hayo yote bado hana sina za kuwa rraisi wa tanzania
 
Wewe ndo unamjua vizuri. Visasi vyake na nongwa ni balaa. Pia fanya naye kazi ndo utamjua. Mwulize yule mkurugenzi wa zamani TBA nadhani anaitwa Kimweri.

Baada ya Magufuli kuondoka ujenzi mara ya kwanza yule mkurugenzi wa TBA alimchongea kwa waziri mpya Mramba kwamba magufuli aliwagawia nyumba mpenzi wake wa chuo kikuu na mdogo wake ambao wote hawakuwa wafanyakazi wa serikali, Mramba akawanyang'anya nyumba hizo hao watu wa magufuli. Loo! Magufuli kitu cha kwanza aliporudi ujenzi mwaka 2010 kazi ya kwanza ilikuwa kumfukuza kimweri. Huyu ni mfano mmoja tu. Amewanyanyasa watu wengi sana kila mahali anapofanya kazi.

Anawahadaa tu watu wasiomjua kenye TV. Pia hakuna anayechukua rushwa toka kwa makandarasi kama huyu, na kesho yake akikutana nao kwenye TV anawafokea utadhani anawafukuza siku hiyo hiyo, aah wapi! Geresha tu!

Mkuu ninavyojua kuhusu Kimweri:

1. Kimweri aliteuliwa na Magufuli mwenyewe kuwa Chief Executive wa Kwanza wa TBA mnamo mwaka 2002 kama sikosei

2. Sheria ya mwaka 1997 namba 30 ya wakala zote za Serikali ikiwamo TBA natamka kuwa mtendaji wa wakala atateuliwa kwa vipindi viwili tu na si vinginevyo, so Kimweri kateuliwa mara mbili na amekaa pale nadhani kwa miaka kumi na kipindi chake kimkatab kilikoma.

3. Alichokifanya Magufuli baada ya mkataba wa Kimweri kuisha na kutoruhusiwa kuendelea na kazi pale TBA kama sheria inavyosema Magufuli alimurudisha Kimweri pale Holland House, Wizarani na anaendelea kufanya/kuchapa kazi.

4. Nachokumbuka ni yule Chief wa TANROADS (Mrema) ndiye aliyefukuzwa baada ya kukutwa na makosa kibao hata ya kimkataba na pia likuwa mwizi mkubwa

5. Nachomlaumu Magufuli ni kwa nini anaendelea kumkumbati Kimwei pale Wizarani wakati vijan wengi wanamaliza hawana kazi, yule pia alitakiwa kufukuzwa tu
 
Hapo wala sikubishii mkuu. Huyu Comrade ni mwanasiasana anajua fitina za kisiasa. Yuko kama kobe anangalia chini huku akitunga sheria.

Ila ikotokea Magufuli amesimama kwenye Urais basi CCM watakuwa wamemaliza uchaguzi kama mwaka 2005. Ila ndani ya CCM wenyewe wanamuogopa.

Nakubaliana na wewe ni ngumu sana kuona waziri wa kawaida tu anaalikwa na mwaziri wakuu wa nchi za Kenya na Zimbabwe kwenye midaharo mikubwa ya siasa, huyu tayari ana mtaji wa uraisi angalia hii picha:

View attachment 85085
 
ha ha aha waulize wananchi wa jimbo la Biharamulo alichowafanyia kupitisha barabara ya lami nyumbani kwao chato kisa yeye alikuwa waziri wa ujenzi na walikataa kumchagua kuwa mbunge uchaguzi wa 1990

Hoja yako ni dhaifu sana:

Tumia akili yako vizuri kukumbuka vitu, nakumbuka mwaka 1990 Magufuli ni kweli alishindwa ubunge an marehemu Kabuye kipindi hicho Biharamulo ni jimbo moja na baade huyu jamaa alienda kusoma masters yake pale UDSM.

Sasa angejengaje barabara ya lami mwaka 1990 kipindi ni mwananchi wa kawaida tena mwanafunzi wa UD?

Na hata alipokuja kuwa Waziri alianza kujenga barabara hiyo unayosema na hata ile ya Kagoma -Lusahunga inayopita Biharamulo so wewe ulitaka kumpangia aanze ujenzi wapi??

Na bado kaenda mbali kwa kujenga ile inayotoka Bwanga mpaka Biharamulo na hapo Biharamulo watakuwa bna kilomita nyingi za lami kuizidi hata Chato kwa Magufuli! tafiti utaona ukweli nilioandika.

Hata hivyo huyu huyu Magufuli alipotoka Wizara ya Ujenzi gharama ya ujenzi ilipanda juu (ili wakubwa wale 10% zao) mfano mzuri - mwaka 2000 mpaka 2005 barabara zilikuwa zikijengwa kilomita moja kwa milioni 350, alipotoa mwaka 2005 mpaka 2010 barabara zilijengwa kilomita moja kwa bilioni 1.9 (ile ya Dodoma - Manyoni 30km)

Magufuli aliporudi Wizara ya Ujenzi kuanzi mwaka 2010 mpaka sasa kilomita moja inajengwa kwa kati ya milioni 700 mpaka 730 na tenda zote zipo chini ya milioni 800 kwa kilomita. Mfano mzuri wa barabara hizo ni Same-Mkumbara na ile ya Iringa - Dodoma!

Utaona ni jinsi gani yule Mrema aliyrfukuzwa na Magufuri mwenyewe alivyokuwa anakula hela za wananchi bila huruma.

Nachomshauri Magufuli ni kuhamia CHADEMA huko aliko siko!!
 
Hapo wala sikubishii mkuu. Huyu Comrade ni mwanasiasana anajua fitina za kisiasa. Yuko kama kobe anangalia chini huku akitunga sheria.

Ila ikotokea Magufuli amesimama kwenye Urais basi CCM watakuwa wamemaliza uchaguzi kama mwaka 2005. Ila ndani ya CCM wenyewe wanamuogopa.

Hahaaa, naona Mpitagwa anamtetea Nchimbi kwa nguvu zooote, Gaidi, Mzee wa Visasi, huyuhuyu ambaye DVD za uchaguzi Meya Songea zinamwonesha anaengeneer kura za kufichwa kwenye chupi? AMA KWELI WATANZANIA TUNA MTINDIO WA UONO!
 
Last edited by a moderator:
Hoja yako ni dhaifu sana:

Tumia akili yako vizuri kukumbuka vitu, nakumbuka mwaka 1990 Magufuli ni kweli alishindwa ubunge an marehemu Kabuye kipindi hicho Biharamulo ni jimbo moja na baade huyu jamaa alienda kusoma masters yake pale UDSM.

Sasa angejengaje barabara ya lami mwaka 1990 kipindi ni mwananchi wa kawaida tena mwanafunzi wa UD?

Na hata alipokuja kuwa Waziri alianza kujenga barabara hiyo unayosema na hata ile ya Kagoma -Lusahunga inayopita Biharamulo so wewe ulitaka kumpangia aanze ujenzi wapi??

Na bado kaenda mbali kwa kujenga ile inayotoka Bwanga mpaka Biharamulo na hapo Biharamulo watakuwa bna kilomita nyingi za lami kuizidi hata Chato kwa Magufuli! tafiti utaona ukweli nilioandika.

Hata hivyo huyu huyu Magufuli alipotoka Wizara ya Ujenzi gharama ya ujenzi ilipanda juu (ili wakubwa wale 10% zao) mfano mzuri - mwaka 2000 mpaka 2005 barabara zilikuwa zikijengwa kilomita moja kwa milioni 350, alipotoa mwaka 2005 mpaka 2010 barabara zilijengwa kilomita moja kwa bilioni 1.9 (ile ya Dodoma - Manyoni 30km)

Magufuli aliporudi Wizara ya Ujenzi kuanzi mwaka 2010 mpaka sasa kilomita moja inajengwa kwa kati ya milioni 700 mpaka 730 na tenda zote zipo chini ya milioni 800 kwa kilomita. Mfano mzuri wa barabara hizo ni Same-Mkumbara na ile ya Iringa - Dodoma!

Utaona ni jinsi gani yule Mrema aliyrfukuzwa na Magufuri mwenyewe alivyokuwa anakula hela za wananchi bila huruma.

Nachomshauri Magufuli ni kuhamia CHADEMA huko aliko siko!!

hahahaaaa ni kweli angalia hii clip:
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom