Elections 2010 Mheshimiwa John Pombe Magufuli awe Rais wetu

Elections 2010 Mheshimiwa John Pombe Magufuli awe Rais wetu

Kwa muono wangu huyu bwana ndio anafaa kumrithi Kikwete, kwa Nchi yetu ilipofikia tunahitaji Rais mwenye msimamo na mbabe kama huyu jamaa, hatuhitaji tena mtu soft!!!!!

Nakuunga mkono. Tulipofika, hatujui kesho kuna nini!!
 
kwa muono wangu huyu bwana ndio anafaa kumrithi kikwete, kwa nchi yetu ilipofikia tunahitaji rais mwenye msimamo na mbabe kama huyu jamaa, hatuhitaji tena mtu soft!!!!!
kufokafoka hovyo hakumaanishi kwamba yeye ni kiongozi bora na mara nyingi mtu mkali na mfokaji sana nyuma yake kuna kitu anaficha.
 
Acheni ushabiki wa mavyama yenu,semeni kwanini anafaa na kwanini hafai,ili hata wasiomjua wafahamu kiundani uzuri wake na udhaifu wake kiutendaji.
 
Rasmi Magufuli umeingia kwenye Mitandao.........Sooon tutakumbusha zile Series za Rai wakati ule wakina Gen. Ulimwengu:A S 39:
 
Yalikuwa ni maamuzi ya serikali nzima JK kipindi hicho akiwemo iweje umuhukumu yeye binafsi, yeye alitekeleza kama waziri mwenye dhamana! Au nawe ndo wale wanawahukumu kwa kuwaandika majina watendaji wa serikali badala ya kuishitaki serikali?

mkuu usipokubaliana na uamauzi au ukiona uamuzi ni mbaya unajiuzulu,huyu ni mwizi tu hakuna jina jingine
 
Si kila waziri anaweza kuwa raisi wa nchi. Mhe. Magufuli ana uthubuti wa kupewa majukumu na kuyasimamia na si vinginevyo. Kwa misimamo yake bora abaki kuwa waziri kwani zaidi ya hapo anaweza kuongoza nchi kidikteta.

Na tulipofikia tunahitaji kiongozi wa namna hii, vyakula vyote vitashuka bei, mafuta n.k
 
Dr. John Joseph Pombe Magufuli akisimamishwa na CCM basi uchaguzi utakuwa umeisha in favour of CCM. Iwe hafai au anafaa lakini wananchi wana imani naye kiasi cha kutosha kwa hiyo anafaa.
 
Ninamkumbuka sana Magufuli kwa haya yafuatayo:

1. Alipokuwa Mifugo na Uvuvi Tanzanzia kwa mara ya kwanza ilikamata maharamia wa kigeni waliokuwa wamezoea kupora samaki wetu - alitoka na msemo wa bahari yetu siyo shamba la bibi. Kikubwa zaidi maharamia hao tena wa kigeni wamehukumiwa kifungo ndani ya ardhi ya Tanzania, waziri gani mwingine kafanya tukio kama hili?? Huyu kwangu ni shujaa!

2. Miaka ya 2000 alikamata magari ya serikali zaidi ya 21,000 ikiwemo mitambo na pikipiki. Magari enzi hizo yalikuwa yakiandikwa mpaka majina binafsi mfano nakumbuka moja liliandikwa Mwakajinga! Isitoshe zoezi hilo limerudiwa juzi kati ambapo magari zaidi ya 1000 yamealikuwa yanatumika vibaya kwa kuwa yalikuwa na namba za kiraia - kwangu mimi huyu ni kiongozi anayelinda mali za umma na kuhimiza matumizi sahihi ya mali za umma. Lakini maadui zake walioguswa na zoezi hili wanamshambulia, ni jukumu la wananchi wa kawaida kulijua hili!!

3. Amejenga barabara za lami zaidi ya kilometa 11000 na mpaka CCM wamekuwa vihelele wakimtumia kwenye majukwaa ili afanye presentation kuhusu mafanikio ktk ujenzi wa barabara tangu uhuru, lakini kibaya zaidi humohumo ndani ya CCM kuna kundi lipo kimkakati kumvuruga pengine aonekane si kitu!

4. Kumekuwa na malamiko ya barabara kujengwa chini ya kiwango, Magufuli kawakaba makandarasi wote na sasa barabara ya Singida kwenda Shelui, upande wa Sekenke inarudiwa na Mkandarasi kwa gharama zake zipatazo shilingi bilioni 15 na juzi kati tumeona makamu wa rais akifungua ile ya Mbagala ambapo Mkandarasi alirudia kwa hela zake, leo Magufuli anaoneka mbaya?

5. Alipokuwa wizara ya ardhi alianzisha mradi wa Viwanja 20,000 kule Kigamboni na kurudisha uwajibikaji wa wafanyakazi wa ardhi kiasi cha wananchi kusifia huduma za Wizara, leo hii mtu huyu anaonekana si lolote ndani ya CCM

6. Akiwa Ujenzi alizuia meli kubwa kusafirishwa kwa njia ya barabara ambapo ingeharibu barabara na hata meli hilo lisingeweza kupita ktk madaraja , lakini CCM hawaoni hili??

7. Kuhusu nyumba nakumbuka lilikuwa ni Azimio la Serikali nzima ambapo baraka zilitoka ktk baraza la mawaziri na yeye alikuwa na jukumu la kutekeleza tu! Sasa wana CCM hata siku moja hawatokei kumtetea hata kwa maneno mepesi tu, mtu huyu anaonekana kwao mbaya! Lakini katika hili nakumbuka hata Nyerere aliuza nyumba za serikali mfano pale Magomeni, Mwanza( Ghana Cottage), Tabora etc wana CCM wameshindwa kutumia mfano huu kumlinda kijana wao???

8. Humu jamvini Watu wanaandika Magufuli kawahi kuwa meneja TANROADS Morogoro ? Uvivu wa kufuatilia taarifa sahihi za viongozi - Hebu angalia CV za wabunge ktk tovuti ya bunge kama Magufuli aliwahi ajiliwa na Wizara ya Ujenzi kama mtumishi wa Umma?

9. Aliwahi chafuliwa kwa kuandikwa na gazeti moja kwa kipindi cha Miezi minane mfululizo, na baadae aliyefanya/tekeleza kazi hiyo kazawadiwa ukuu wa wilaya fulani- sisi siyo wajinga, tunajua mambo hayo!

10. Katika chaguzi za mwaka 2000 na 2005 alipita bila kupingwa jimboni kwake Chato na hata chaguzi za 1995 na 2010 ukiangalia matokeo utajua ni jinsi gani wananchi wake wanamhusudu lakini leo hii watu wanataka kuupoteza ukweli!

11. Lakini hata hivyo, mawaziri wenzake wanakubaliana naye jinsi anavyofanya kazi bila kuogopa mtu!

12. Ndiye aliyeanzisha mfumo wa kujenga barabara kwa kutumia hela zetu za ndani bila kutegemea wafadhiri na alianzisha model ya design and build mpaka wenzetu jirani Kenya wakaja kuiga kipindi hicho Raila Odinga akiwa waziri wa barabara wa Kenya!

13. Ni waziri pekee aliyekaa Wizara ya ujenzi kwa muda mrefu penye vishawishi vya rushwa bila shutuma yeyote ile

WITO WANGU KWA MHESHIMIWA MAGUFULI:

1. Wanaokuchafua sio sisi CHADEMA bali ni wana CCM wenzako ambao kila kukicha wanakuogopa kwa vile unakubalika na wananchi walio wengi!

2. Nakushauri jiunge na CHADEMA ili uje kushirikiana na Dr . Slaa tayari kwa ukombozi wa taifa hili

3. NAKUSISITIZA MHESHIMIWA MAGUFULI NI WAKATI WAKO SASA KUHAMIA CHADEMA


Kwenye RED; that is precisely kinachosemwa na watu tunaomfahamu Magufuli kwa kufanyakaz nae. Usichokijua wewe (na wenye mtazamo wako kuhusu Magufuli) ni kuwa huyu bwana huwa anafanya mambo bila kufikiri kitakachotokea baadae. Kwa taarifa yako, Mwakajinga alikopeshwa hilo gari (kuna kipindi serikali iliwakopesha maofisa stahili magari ambayo yalikuwa yanamilikiwa na serikali na mkopaji hakurushusiwa kubadilisha namba hadi amalize kulipa). Udhalilishwaji huo kwa Mwakajinga na wengine kuliigharimu serikali maana wote waliochukua hatua walilipwa fidia. Waziri makini angejua hayo kabla hajayatangaza hadharani.

Umem-credit Magufuli na ujenzi wa km 11000 za barabara, ila usichokijua ni kuwa barabara hizo zote zimejengwa kwa fedha za wafadhili au mikopo ya benki ya dunia (na usimamizi wake hufanywa na donors wenyewe). Na process ya kupata fedha za kujenga hizo barabara zilianza na kujadiliwa kwa proposals za serikali ya awamu ya kwanza na ya pili. Unamsifia aliekabidhiwa barabara iliyokamilika wakati aliefanya kazi ya kujenga si yeye!

Kwa kifupi; huo "uchapakazi" wa Magufuli ni wa media tu!
 
Unaonekana ulizaliwa kabla ya siku zako hazijatimia - kwa akili ya kawaida tu tembelea tovuti ya TANROADS utaona barabara zinazofadhiliwa na donors na zile zinazotumia hela za serikali, utagundua zaidi ya asilimia 70 ya barabara zote zinajengwa kwa hela za serikali, serikali ilishaacha ule mtindo wa kusubiria wafadhiri ndo ijenge barabara na CNN juzi juzi wametangaza Tanzania ni moja Kati ya nchi tano zinzoinvest heavily kwenye infrastructure za barabara na ni ya kwanza kwa Africa Mashariki!


Umeniboa sana uliposema tuna asilimia kumi tu katika kuchangia Ujenzi wa barabara, ni uongo na upotoshaji wa kutupa! Tena huyo Magufuli ndo alilazimisha kwanza kujanga barabara kwa kutumia fedha zetu za ndani iweje leo unalazimisha kusahau historia au umetumwa?

Hivi wewe ulielewa nilichokiandika au ulipokuwa unasoma ulikuwa umelewa???? Unajua hesabu wewe?? Hivi miradi 29 kati ya 68 ndio 70%, what have you been drinking sir??

Hebu nionyeshe nilipoandika ulichodai kuwa nimeandika hapo kwenye RED. Uwe unasoma na kuelewa, au na wewe ni "educated illiterate"???
 
Slaa hata akihamia CCM hatakuja kuwa rais wa Tanzania

Hv wewe nani kakudanganya CCM wanaweza kuwa madarakani 2015 mpaka udiriki kusema Slaa hata akihamia CCM hawezi kuwa Rais. CCM imeshakufa.

Kwa upande wa Magufuli ni mtendaji mzuri, sitaki kumbeza kazi anayofanya wote tumeiona, ila kwa nafasi ya Urais bado sana. Jamaa ni mtendaji mzuri ila sioni sifa za urais kwake hasa kwa jinsi ya alivyo na Jazba na kukurupuka sana katika mambo mengi. Namkubali sana tu kama ana mtu juu yake wa ku control decisions zake.


Nisaidien wanajamvi hivi huyu Emmanuel Nchimbi mbona naona Kama CCM wanamkuza sana, ana lipi la kumsafisha hivyo?
 
hebu endeleeni kumchambua maana sie wengine huwa tunamsikia tu kwenye ufunguzi wa ujenzi wa mabarabara.
ni mbabbe asiye na huruma ......huwezi chekelea kuwabomolea maskini katika nchi ambayo hakuna sera /haitekezwi .....asiliamia 90 ya makazi hayajapimwa ni kosa la wamiliki wa nyumba au serikali
 
Kuna kakipande ka barabara fulani kako mwanza palipoishia barabara ya Green Acre. Kila mwezi Nyanza toad wako aple wanajenga toka mwaka 2005. Unajua ni project ya nani? Mi mwenye nisingempa kura yangu bora nipigie jiwe.
Dodoma yote pale mjini ni nyanza, haka kakampuni kana mlio wa mbu, anaekajua atumwagie
 
Watu bana wakiamua kumpaka mtu matope, eti "BUTA BABA GETE MTALEOBONE LAMI"
 
Hivi wewe ulielewa nilichokiandika au ulipokuwa unasoma ulikuwa umelewa???? Unajua hesabu wewe?? Hivi miradi 29 kati ya 68 ndio 70%, what have you been drinking sir??

Hebu nionyeshe nilipoandika ulichodai kuwa nimeandika hapo kwenye RED. Uwe unasoma na kuelewa, au na wewe ni "educated illiterate"???

Nikibishana na wewe nitaonekana pia sina akili, wewe ni wa kukuacha mwenye kuelewa atafuatilia na tajua ukweli upo wapi!
 
Kwenye RED; that is precisely kinachosemwa na watu tunaomfahamu Magufuli kwa kufanyakaz nae. Usichokijua wewe (na wenye mtazamo wako kuhusu Magufuli) ni kuwa huyu bwana huwa anafanya mambo bila kufikiri kitakachotokea baadae. Kwa taarifa yako, Mwakajinga alikopeshwa hilo gari (kuna kipindi serikali iliwakopesha maofisa stahili magari ambayo yalikuwa yanamilikiwa na serikali na mkopaji hakurushusiwa kubadilisha namba hadi amalize kulipa). Udhalilishwaji huo kwa Mwakajinga na wengine kuliigharimu serikali maana wote waliochukua hatua walilipwa fidia. Waziri makini angejua hayo kabla hajayatangaza hadharani.

Umem-credit Magufuli na ujenzi wa km 11000 za barabara, ila usichokijua ni kuwa barabara hizo zote zimejengwa kwa fedha za wafadhili au mikopo ya benki ya dunia (na usimamizi wake hufanywa na donors wenyewe). Na process ya kupata fedha za kujenga hizo barabara zilianza na kujadiliwa kwa proposals za serikali ya awamu ya kwanza na ya pili. Unamsifia aliekabidhiwa barabara iliyokamilika wakati aliefanya kazi ya kujenga si yeye!

Kwa kifupi; huo "uchapakazi" wa Magufuli ni wa media tu!



Una agenda yako ya Siri, Magufuli jembe japo hajastahili kuwa Rais. Au na wewe (Jamaa yako) ni mmoja wa waliokuwa wameregister magari ya umma kwa jina binafsi.
 
Una agenda yako ya Siri, Magufuli jembe japo hajastahili kuwa Rais. Au na wewe (Jamaa yako) ni mmoja wa waliokuwa wameregister magari ya umma kwa jina binafsi.

Maybe una umri mdogo sana (kiasi kwamba yalipokuwa yanafanyika niliyoyasema hapa hukuwa na uwezo wa kuyafuatilia) au uelewa wako wa jinsi serikali inavyofanya kazi ni practically zero. Maana kama miaka ya 90 ulikuwa na angalau miaka 18 ungeshasikia programs nilizozisema hapa, na kama ulikuwa mkubwa na hukuzisikia hilo si kosa langu. It is your loss not mine being ignorant of things that are common and open to the members of the public (who care to know them that is).

As far as Magufuli is concerned, sina ajenda nae, iwe ya siri au isiyo ya siri.
 
Back
Top Bottom