Kwanza nadini ya CCM hawezi kukubarika kwa sababu wanajua kuwa atawasumgua kwa kutaka kwake sifa anaweza kufanya kitu cha ajabu bila hata ya kufikiria. Wanaojua vizuri mwanza watakumbuka vituko alivyofanya wakati wa uvunjaji wa kituo cha mafuta cha MOIL, alilazimisha kuvunja matokeo yake serikali iliwalipa pesa nyingi sana wale wahindi wa CCM! Kwa kupenda kujipendekeza JP alipongeza safari za raisi JK pamoja na kujua fika zinaliingiza taifa kwenye ghalama zisizo za lazima hii yote ni kwa sababu huyu mheshiwa anapenda sifa sana so alijipendekeza kwa JK kwa kumpa sifa zisizo na tija kwa watanzania of which watanzania sidhani kama tunahitaji raisi wa style hii. Kwa visasi ndo mwenyewe kumbukeni issue ya fast ferry za Azam alozileta lake Victoria, JP alitaka kumkomoa Mwandosya kwa vile alikuwa amekula karamu ya ujio wa meli hizo hivyo JP akajua kumkomoa ni kugoma kusaini boti hizo kupitishwa kwenye barabara zake kwa kisingizio ni nzito wakati kuna mitambo ya migodini ni mizito mara mbili ya boti hizo kila siku inapitishwa kwenye barabara zake na sisi watz tukishuhudia. Kwa kifupi JP hafai hata kidogo kuwa raisi, ikumbukwe tena aliwahi kupigiwa kelele na wananchi wa Buziku kwenye moja ya mikutano yake jimboni chato,alichokifanya ni kuwaambia kwa kisukuma " Buta baba gete mtalaibona ilami maisha ging'we pyee!" kilichotokea ni kuipindisha barabara ya lami ilotakiwa kupita Buziku akalazimisha ipite Chato ili kuwakomoa wananchi hao....sasa jamani tunamjadiri kuwa raisi wa nchi mtu wa aina hii? Labda kwa vile ni demokrasia acha tumuweke tena raisi wa majaribio kama tulivyofanya 2005 & 2010.