Elections 2010 Mheshimiwa John Pombe Magufuli awe Rais wetu

Hahahaa, ngoja kwanza nikamuulize Sundi, ile nyumba aliyohongwa na kuwanyima haki walioitumikia serikali kwa miaka lukuki aliirejesha?

Lile swaga linatafasiriwa vibaya nasikia pale Sundi alipangishwa kama mwanafunzi wa Chuo kikuu cha Dsm, so ilipogundulika Mzee anapumzika pale ikawa pia kamuuzia lakini hakuna kitu kama hicho nilidokezwa na Jamaa yangu walifuatilia sakata hilo wakakuta ni uvumi na uzushi ndo maana JK kamurudisha Magufuli Ujenzi!!
 

Unaonekana ulizaliwa kabla ya siku zako hazijatimia - kwa akili ya kawaida tu tembelea tovuti ya TANROADS utaona barabara zinazofadhiliwa na donors na zile zinazotumia hela za serikali, utagundua zaidi ya asilimia 70 ya barabara zote zinajengwa kwa hela za serikali, serikali ilishaacha ule mtindo wa kusubiria wafadhiri ndo ijenge barabara na CNN juzi juzi wametangaza Tanzania ni moja Kati ya nchi tano zinzoinvest heavily kwenye infrastructure za barabara na ni ya kwanza kwa Africa Mashariki!

Umeniboa sana uliposema tuna asilimia kumi tu katika kuchangia Ujenzi wa barabara, ni uongo na upotoshaji wa kutupa! Tena huyo Magufuli ndo alilazimisha kwanza kujanga barabara kwa kutumia fedha zetu za ndani iweje leo unalazimisha kusahau historia au umetumwa?
 
Mgombea urais mwaka 2015 kupitia ccm ni kitendawilin kilichokosa mteguzi, kikija kuteguliwa basi ccm itagawanyika makundi makundi.
 
Piga ua! sasa ni zamu ya Zanzibar na Salim Ahmed Salim ndio Rais wetu take msitake! Nyerere alikuja Moshi mwaka 1995 ktk uwanja wa Mashujaa akimnadi Mkapa na Wachagga wakasema hawamtaki Mkapa! bali Mrema Lyatonga na majibu ya Nyerere yalikuwa Mkapa ni Rais wenu mtake msitake!
 
Afadhali ya Magufuli kaomba maboresho ya hospitali ambayo itasaidia na Watanzania wengine, kuna wengine wanapewa fedha na vitu vingine kwa matumizi yao binafsi.
 

mkuu hapo kwenye red naomba nikurekebishe Magufuli alikuwa sahihi ni kwamba wale wahindi walipata title kwa njia ya rushwa na kikubwa ambacho magufuli alifanya ni kufata ramani ya barabara ila kwa kuwa manispaa ya mwanza walikuwa wamekula rushwa na kutoa hati basi ikabidi waingie hasara ya kulipa fidia kwa hiyo ilikuwa matokeo ya rushwa kwa viongozi wa serikali pale magufuli alistahiri sifa kwa kufichua uozo. hata hapa dar kuna viwanja vingi vya wazi vilivamiwa na watu wamepewa hati akija waziri ambaye anataka virudi basi serikali lazima ilipe fidia kwa uzembe wake. angalia sehemu za mbezi viwanja vyote vya wazi vimejengwa hakuna sehemu za kucheza watoto wala sehemu za shule mpya na hata sehemu za dispensari au hospitali na hivi vyote viliuzwa wakati Lowasa akiwa waziri nenda umuulize kama hajainama chini kwani anajua watu walishasahau.

Kuhusu suala la boti kwanza mmiliki si azam kama unavyosema alikuwa azim dewji alikuwa mfadhili wa simba zamani ila rejea majibu ya magufuli katika lile suala. uzito wa mzigo unaotakiwa kupita kwenye barabara zetu si zaidi ya tani 30 na zile boti ni zaidi ya hizo tani nashangaa waziri mwandosya tena profesa hakuangalia hicho kitu. na hili lazima uangalie kwa makini kwa sababu kuna culvert ndogo ndogo karibu zingefunjika zote. ila kingine zile boti ilikuwa zimechakaa sana ndio maana walivyoambiwa wanatakiwa kuzifungua na kwenda kuzifunga tena ilishindikana. hadi leo hazifanyi kazi zimepaki pale mwanza.
wachukue mwandosya na magufuli ukawaonyeshe zile boti zilipo uone nani ataficha uso kwa aibu.
 

barabara ya biharamulo ina lami na ile ya magufuli ina lami nimepita mwezi wa kumi na moja sasa sijui una maana gani kwani zote zina lami.
 

Hapo wala sikubishii mkuu. Huyu Comrade ni mwanasiasana anajua fitina za kisiasa. Yuko kama kobe anangalia chini huku akitunga sheria.

Ila ikotokea Magufuli amesimama kwenye Urais basi CCM watakuwa wamemaliza uchaguzi kama mwaka 2005. Ila ndani ya CCM wenyewe wanamuogopa.
 
Magufuli hafai, mtu wa visasi sana na pia akikujia juu ujue hujatoa cha juu. Bara bara nyingi zipo chini ya viwango lakini hawarudii kuna nini hapo.
Wewe ndo unamjua vizuri. Visasi vyake na nongwa ni balaa. Pia fanya naye kazi ndo utamjua. Mwulize yule mkurugenzi wa zamani TBA nadhani anaitwa Kimweri.

Baada ya Magufuli kuondoka ujenzi mara ya kwanza yule mkurugenzi wa TBA alimchongea kwa waziri mpya Mramba kwamba magufuli aliwagawia nyumba mpenzi wake wa chuo kikuu na mdogo wake ambao wote hawakuwa wafanyakazi wa serikali, Mramba akawanyang'anya nyumba hizo hao watu wa magufuli. Loo! Magufuli kitu cha kwanza aliporudi ujenzi mwaka 2010 kazi ya kwanza ilikuwa kumfukuza kimweri. Huyu ni mfano mmoja tu. Amewanyanyasa watu wengi sana kila mahali anapofanya kazi.

Anawahadaa tu watu wasiomjua kenye TV. Pia hakuna anayechukua rushwa toka kwa makandarasi kama huyu, na kesho yake akikutana nao kwenye TV anawafokea utadhani anawafukuza siku hiyo hiyo, aah wapi! Geresha tu!
 
Adui wa kwanza wa Tanzania ni Ujinga unaozaa majungu,umbea,na chuki zisizo na msingi!Wanaume wengi wanaongea kwa mipasho wakiwa wamejaa povu mdomoni hata wanapopaswa kutoa hoja.

Matokeo yake wanashindwa kujipa muda wa kutafakari.Ni kweli hata ukitaka kufuga ngombe ili unaweza tu ukaanza na hoja kama ninazoziona hapo juu!Unajua harufu ya kinyesi cha ng'ombe?Unajua anakojoa lita ngapi kwa siku?alafu zile pembe zake zimewahi kutoboa mtu utumbo!

Usipokuwa makini anaweza kuyapiga teke maziwa unayokamua yakamwagika yoote!Baada ya visingizio hivyo mpumbavu yeyote ataziona kama hoja za msingi!Watanzania hatuhitaji malaika kama tulivyodanganywa 2005!Tunataka kiongozi anayejali maslahi ya wengi hata kama ni dictator!Aligawa nyumba za serikali!so what?

hamuwezi kujenga nyingine mnalalamika tuu! Eti wake zetu tuwaweke mbali!hawa wamekuwa bidhaa?kwani unajua sasa hivi nani ana cheat na mkeo?jiamini. Bhana!Mwisho toeni hoja za msingi au sivyo nyamazeni!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
mim binafsi naona mtu ambaye anaweza kuirudisha nchi yetu kwenye msitari ni Don King achilia mbali mapungufu mengine ambayo hata mim na wew tunayo.huu ni mtizamo wangu tu lakin
 
ALIUZA NYUMBA ZA SERIKALI ,YEYE NDO ALIKUWA RAIS?? ETI UNAMJUA MAGUFURI TOKA AKIWA TANROAD MOROGORO ,TANGU LINI MAGUFURI KAFANYA KAZI TANROAD ??? ACHENI ULONGO,HOO KUNA KIPANDE MWANZA KINAJENGWA TOKA 2005,KWANI TOKA 2006 MAGUFURI NI WAZIRI WA UJENZI?? OOH NI MTU WA VISASI,ALIKULIPIZIA KIPI??USIPENDE KUSHUHUDIA BINADAMU WENZIO UWONGO SABABU TU UMEPATA NAFASI YA KUWAJADILI.-To me Namuona Magufuli Kama Mchapakazi wa kuigwa,HAIJALISHI ANATAKA URAIS au lah,KAMA MTU AWEZA MPUUZA MZAZI ALIYE MZAA NA KUMSOMESHA,ITAKUWA MTU KUMPUUZA MAGUFURI ?? ANASTAHILI PONGEZI ZA UTENDAJI SAWA NA MTENDAJI YEYOTE AMBAYE KAZI YAKE INAONEKANA .
 
Naunga mkono hoja. Pamoja naye, Mwakyembe & Lowassa wanafaa sana.
 

pamoja na hayo yote bado hana sina za kuwa rraisi wa tanzania
 

Mkuu ninavyojua kuhusu Kimweri:

1. Kimweri aliteuliwa na Magufuli mwenyewe kuwa Chief Executive wa Kwanza wa TBA mnamo mwaka 2002 kama sikosei

2. Sheria ya mwaka 1997 namba 30 ya wakala zote za Serikali ikiwamo TBA natamka kuwa mtendaji wa wakala atateuliwa kwa vipindi viwili tu na si vinginevyo, so Kimweri kateuliwa mara mbili na amekaa pale nadhani kwa miaka kumi na kipindi chake kimkatab kilikoma.

3. Alichokifanya Magufuli baada ya mkataba wa Kimweri kuisha na kutoruhusiwa kuendelea na kazi pale TBA kama sheria inavyosema Magufuli alimurudisha Kimweri pale Holland House, Wizarani na anaendelea kufanya/kuchapa kazi.

4. Nachokumbuka ni yule Chief wa TANROADS (Mrema) ndiye aliyefukuzwa baada ya kukutwa na makosa kibao hata ya kimkataba na pia likuwa mwizi mkubwa

5. Nachomlaumu Magufuli ni kwa nini anaendelea kumkumbati Kimwei pale Wizarani wakati vijan wengi wanamaliza hawana kazi, yule pia alitakiwa kufukuzwa tu
 

Nakubaliana na wewe ni ngumu sana kuona waziri wa kawaida tu anaalikwa na mwaziri wakuu wa nchi za Kenya na Zimbabwe kwenye midaharo mikubwa ya siasa, huyu tayari ana mtaji wa uraisi angalia hii picha:

View attachment 85085
 
ha ha aha waulize wananchi wa jimbo la Biharamulo alichowafanyia kupitisha barabara ya lami nyumbani kwao chato kisa yeye alikuwa waziri wa ujenzi na walikataa kumchagua kuwa mbunge uchaguzi wa 1990

Hoja yako ni dhaifu sana:

Tumia akili yako vizuri kukumbuka vitu, nakumbuka mwaka 1990 Magufuli ni kweli alishindwa ubunge an marehemu Kabuye kipindi hicho Biharamulo ni jimbo moja na baade huyu jamaa alienda kusoma masters yake pale UDSM.

Sasa angejengaje barabara ya lami mwaka 1990 kipindi ni mwananchi wa kawaida tena mwanafunzi wa UD?

Na hata alipokuja kuwa Waziri alianza kujenga barabara hiyo unayosema na hata ile ya Kagoma -Lusahunga inayopita Biharamulo so wewe ulitaka kumpangia aanze ujenzi wapi??

Na bado kaenda mbali kwa kujenga ile inayotoka Bwanga mpaka Biharamulo na hapo Biharamulo watakuwa bna kilomita nyingi za lami kuizidi hata Chato kwa Magufuli! tafiti utaona ukweli nilioandika.

Hata hivyo huyu huyu Magufuli alipotoka Wizara ya Ujenzi gharama ya ujenzi ilipanda juu (ili wakubwa wale 10% zao) mfano mzuri - mwaka 2000 mpaka 2005 barabara zilikuwa zikijengwa kilomita moja kwa milioni 350, alipotoa mwaka 2005 mpaka 2010 barabara zilijengwa kilomita moja kwa bilioni 1.9 (ile ya Dodoma - Manyoni 30km)

Magufuli aliporudi Wizara ya Ujenzi kuanzi mwaka 2010 mpaka sasa kilomita moja inajengwa kwa kati ya milioni 700 mpaka 730 na tenda zote zipo chini ya milioni 800 kwa kilomita. Mfano mzuri wa barabara hizo ni Same-Mkumbara na ile ya Iringa - Dodoma!

Utaona ni jinsi gani yule Mrema aliyrfukuzwa na Magufuri mwenyewe alivyokuwa anakula hela za wananchi bila huruma.

Nachomshauri Magufuli ni kuhamia CHADEMA huko aliko siko!!
 

Hahaaa, naona Mpitagwa anamtetea Nchimbi kwa nguvu zooote, Gaidi, Mzee wa Visasi, huyuhuyu ambaye DVD za uchaguzi Meya Songea zinamwonesha anaengeneer kura za kufichwa kwenye chupi? AMA KWELI WATANZANIA TUNA MTINDIO WA UONO!
 
Last edited by a moderator:

hahahaaaa ni kweli angalia hii clip:
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…