Miaka 18 ya upotevu wa maisha ya Yesu Kristo. Je, nini hasa siri yake na wanaficha nini?

Miaka 18 ya upotevu wa maisha ya Yesu Kristo. Je, nini hasa siri yake na wanaficha nini?

History ya ujanani ya yesu, haikupotea, bali iliachwa makusudi, tafuta,, "The infant gospel of Jesus"
Mkuu kwema,
infants=mtoto chini ya mwaka mmoja
the infants gospel of jesus
injili ya mtoto yesu....
mkuu nimeisoma yote mpaka akivyokuwa anafukuzwa na wenzake kwwnye kucheza kote nimesoma mkuu shukrani sana...
mpaka kipindi anawafundisha walimu wake kuhusu herufi za kihebrania na maana yake alef,Bet na zingine....ila iliishia pale pale kwenye miaka 10 kama sikosei
 
Habari za Mida hii Ndugu Zangu Naomba kuanza kwa kuwatakia Sikukuu njema ya Kuzaliwa kwa Yesu kwa wale wote wafuasi wa imani ya Kikristo na hope mnaenjoy sana Happy noela

Kabla ya yote ningependa kurejea Luka 1:1-3 Kama inavyosema;
..."Kwa kuwa watu wengi wametia mikono kutunga kwa taratibu habari za mambo yale yaliyotimizwa katikati yetu,kama walivyotuhadithia wale waliokuwa mashahidi wenye kuyaona, na watumishi wa lile neno tokea mwanzo,nimeona vema mimi nami, kwa kuwa nimejitafutia usahihi wa mambo hayo yote tangu mwanzo, kukuandikia kwa taratibu,.........,"


Miaka 2000 iliyopita katika Mji wa bathelehem ya Uyahudi Alizaliwa Mtoto Aliyepewa Jina la Yeshua/Yehoshua ama yesu au Issa unaweza kumuita utakavyoweza kuita kwa lugha yako ilimradi imani ibaki kuwa alizaliwa Mtoto Ambaye ni Mtu muhimu sana katika historia ya ukombozi wa Wakristo duniani,

Na maandiko yote Yameandika kuhusu yesu kuzaliwa kwake,Miujiza yake mafundisho yake kuishi kwake ,Kusulubiwa kwake na kufufuka kwake na hata kupaa kwake kwenda mbinguni.

Maandiko yote ya biblia yaliyopo yanaanza kuzungumzia yesu kuanzia alipokuwa anazaliwa mpaka akiwa na umri wa miaka 12 (Soma luka 2 yote,pia soma mathayo 2)

Lakini baada ya miaka hiyo 12 Biblia ikawa kimya mpaka tena pale ambapo yesu anatimiza miaka 30 ya maisha yake ndo tunaona yesu anaanza kutajwa tena,kipindi anabatizwa na yohana Mbatizaji..(luka 3:23,Marco 1;9 ,Mathayo 3 kuanzia aya ya 14 na kuendelea)

Lakini miaka yake yote kuanzia umri wa miaka 13 mpaka 29 hakuna sehemu yoyote ya biblia inayotaja maisha yake alikuwa wapi? Alifanya nini? Aliishi wapi? na ilikuwaje?
basi nitajaribu kupitia baadhi ya theory na nakala za vitabu ili tuende sawa katika kujibu haya

HOJA KWA UFUPI

Maisha ya yesu kipindi Akiwa hai hakuna aliyekuwa anayanakili ama kuandika maisha yake kwakuwa Maisha yake na injili hii imekuja kuandikwa Miaka 70 mpaka 140 baada ya kifo chake.
Japo inasemekana historia ya yesu ilikuwa inaelezwa kuwa Masimulizi kumhusu yesu yalikuwa yakifahamika kwa watu wengi Sana kwa muda mchache.
kulingana na Injili ya yohana Yesu alifanya kazi kwa muda wa mwaka mmoja tu na kulingana na injili za ki"synoptikia" (synoptic gospels) Yaani Luka matayo na marko alifanya kazi kwa muda wa miaka 2 mpaka mitatu kabla ya kifo chake...
Japo kuliandikwa Vitabu vingi sana zaidi ya 100 kuhusu maisha ya Yesu lakini vitabu 4 tu vya injili ndiyo vilivyokubaliwa kuingia katika biblia rasmi iliyoamriwa kutumika...

Mengi tunayoyajua kuhusu yesu Tunayatoa katika vitabu vinne tu vya injili yaani marko,mathayo luka na yohana,japo vitabu vingine ambavyo havikuingizwa kwenye biblia bado vipo na vingi viko maktaba vimehifadhiwa kwa na unaweza ukaviita APOKRIFA GOSPELS na vina mambo mengi sana ambayo huwezi kuyakuta kwenye biblia na mara nyingi huwa hayaruhusiwi kuzungumzwa kwa uwazi na mengine utayakuta kwenye biblia..
Kwanini hawakutaka kuviingiiza kwa kisingizio cha KUVUVIWA ama canonical views ?.....
Baadhi ya Vitabu Hivyo vingine huzungumzia Maisha ya yesu akiwa na umri wa miaka 13 mpaka 29 kama kitabu cha The Gospel of Mary, Injili ya mtoto yesu na vinginevyo....

UCHAMBUZI

Dr.Elizabeth McNamer,Proffesor of theology and religious history wa rocky Mountain college Huko Billings Montana,
ambaye kwa Miaka 14 Amekuwa Mkurugenzi mkuu wa Bethsaida Biblical Archaeological Excavations in Israel ( Machimbo ya Kiakiolojia ya kiblia huko Israel) Pia ni proffesor maarufu kwa ufundishaji wake wa Maandiko huko Asia Na anaposcast yake kuhus Historia ya Biblia.Katika moja ya mahojiano yake aliwahi kunukuliwa akisema
"Ililichukua kanisa miaka isiyopungua 500 kujadili mambo mbalimbali kuhusu Yesu, na kipi kiwemo kwenye biblia na kipi kisiwemo na kipi kiandikwe na kiandikwe vipi na kipi kiachwe kabisa na kisizungumzwe tena Na wengi hawajui kuwa kuandikwa kwa biblia ya sasa kulichukua miaka mingi sana ,Huku pia kanisa likijadili Yesu anatakiwa kuonekana vipi mbele za jamii..."

Hiyo ni wakati akijibu moja ya maswali kuhusu kitabu chake cha Jesus and First-Century Christianity in Jerusalem by Elizabeth McNamer,

View attachment 2457658

Kutokana na kutokuonekana kwa historia ya Yesu Katika miaka 18, hii ni kuanzia miaka 13 mpaka miaka 29 kwenye biblia kumezua mijadala mingi sana katika Jukwaa la wana theolojia na wasomi wa dini wabobezi wa kikristo mpaka ikafika hatua Wakaunda theory zao ama hypothetical Views zao na Wote wakaipa majina miaka hii kama.. The lost years of Jesus Christ "Miaka iliyopotea ya Hostori ya Yesu kristo" na wengine waliita "The unaccounted years of Jesus Christ" Pia huitwa the silent years au the missing years ...

MILA NA DESTULI ZA KIYAHUDI KUHUSU MIAKA ILIYOPOTEA YA YESU NA CHANZO CHA NADHARIA

Hapa tutaangalia mila na desturi za kiyahudi kuhusu miaka hiyo inayosemekana kutokupatikana historia ya yesu Kama wewe ni mfatiliaji wa mila na desturi za kiyahudi na kiAramaiki utakuwa si mgeni wa maneno kama Bar-Mitzvah au Bat-Mitzvah..

Hizi ni mila kama mila za kwetu africa au kwetu huko uziguani,Au huko kwetu uzaramoni au umasaini na kwingineko...
Kwakuwa yesu alikuwa ni mmoja wa Wayahudi katika kabila la kiAramaic hivo alifata Tamaduni zote..

"Bar Mitzvah" maana yake halisi ni "mwana (wa kiume) mwenye amri." "Bar" ni "mwana wa kiume" katika Kiaramu, ambayo ilikuwa ni lugha ya watu wa Kiyahudi.
"Mitzvah" ni "amri" katika Kiebrania na Kiaramu.

"Bat" ni binti katika Kiebrania na Kiaramu. (Matamshi ya Ashkenazic ni "bas").

Kitaalamu,Maneno hayo humaanisha mtoto anayekua, na ni sahihi kabisa kwa mila za kiyahudi kumuita mtu kama "kuwa bar (au bat) mitzvah.

"Hata hivyo, neno hili linatumika zaidi ku sherehe za ukuaji zenyewe, na kuna uwezekano mkubwa wa kusikia kwamba mtu "ana bar mitzvah" au "alialikwa kwenye bar mitzvah."

Sasa sherehe hizi zikuwaje na zilimaanisha nini
Mtoto wa kiyahudi zamani hizo mpaka leo kwa kufata sheria za Musa (zilizopo kwenye talmud) Anapofikisha umri wa miaka 13 (kwa mtoto wa kiume) na miak 12 (kwa mtoto wa kike) huhesabika kama amekuwa na hufanyiwa sherehe hiyo ya Mitzvah ili ayavae majukumu yake mapya na ieleweke kwamba mtoto akishafanyiwa sherehe hii hawi tena chini ya uangalizi wa wazazi hiyo umaanisha kwamba hawi chini ya amri ya wazazi na ndo maana ikaitwa Bar/Bat mitzvah..

Na ni mujibu baba kufurahi na kumpa maneno mazuri ya wosia mtoto huyo kwani Baba amejitoa katika responsibikity za mtoto huyo kwahyo dhambi zake na maamuzi huwa yapo chini ya mtoto (hapo mwanzo kabla ya miaka 13 mtoto huwa chini ya kifungo cha miaka na wazazi wake hivyo dhambi na malezi yote huwa chini ya wazazi wake) sherehe hizi hufanyika siku ya sabato....

Na mtoto huwa na ruksa ya kwenda mahali popote atakapo..

(Rejea ya Tamaduni hii ipo katika kitabu cha Talmud na inafanywa na wayahudi mpaka leo)..

Mila hizi zinahusianaje sasa na upotevu wa maisha ya yesu kuanzia miaka 13-29?

Inasemekana kwamba baada ya yesu kuwa tayari amekuwa Bar-Mitzvah akiamua kwenda sehemu mbalimbali kutafuta Elimu huku akiiacha Yerusalem na kurafuta elimu sehemu mbalimbali za nchi zote duniani na Hatimae kurudi Akiwa na miaka 30
(Ambayo pia ni miaka ya Kuhubiri na utume kwa mujibu wa Talmud)

Katika miaka ya 1800-1900 kuliibuka nadharia "Hypothetical views" nyingi sana kuhusu the lost years of jesus christ,Japo wanatheolojia wengi wa kisasa yaani morden theologists wanasema kuwa Yesu aliishi Nazareth na alikuwa akifanya kazi na baba ake kama fundi selemala Japo hili linakosa ushahidi zaidi wa moja kwa moja wa kimaandiko kwenye biblia zaidi ya ushahidi wa mathayo 13:55 na Marko 6:3 japo ukiangalia vizur utagundua ni andiko moja lenye sentensi moja na lenye maana tofauti huku kwwnye mathayo limetajwa tofauti na kwenye marko limetajwa tofauti labda ni katika zile njama Dr Elizabeth McNamer alizokuwa akitueleza..sasa twende kwwnye nadharia hizo kuhusu miaka iliyopotea .....

1.EARLY THORIES (about early as possible as 70-1600 Ad)

Nadharia za awali Kuwa kuna uthibitisho gani unaounga mkono imani kwamba Yesu alisafiri maelfu ya maili kutoka Yudea hadi nchi nyingine?
Vyanzo vya kwanza kabisa vinatoka katika maandiko ya Injili ya Mathayo, Marko, Luka na Yohana. Bethlehemu ni mahali ambapo inaaminika kuwa Kristo alizaliwa, lakini Injili zinasema familia yake iliondoka mara baada ya hapo na kukaa katika mji wa Nazareti, kutimiza yale ambayo manabii katika Biblia walitabiri; kwamba Yesu ataitwa Mnazareti. Nazareti lilikuwa eneo tulivu, la kilimo na la uvuvi ambapo jamii iliishi maisha yasiyofaa, ikidokeza kwamba hadhi ya Yesu ilikuwa ‘Blue collar’ huku yeye na baba yake seremala

Yusufu wakipata riziki zao duni kama mafundi. Huku kukiwa na matarajio machache ya kazi, nadharia moja ni kwamba huenda Yesu alitafuta kazi fulani umbali wa maili tatu katika mji wenye shughuli nyingi wa Sepphoris katika eneo la kati la Galilaya katika Israeli ya leo, mji uliojulikana wakati huo kwa michoro yake maridadi sana iliyotengenezwa na Waruma. Kukiwa na fursa nyingi za kujenga nyumba na kuta,

Huenda mji huu ukawa ndio hatua ya kwanza kuelekea mahali panapoaminika kuwa mahali pa kuanzia kwa jitihada ya Yesu ya kupata nuru ya kiroho. Ikiwa kama vile wasomi fulani Wakristo wanavyoamini kwamba Yesu alitumia muda mwingi wa miaka hii ya kati akifanya kazi ya seremala katika Galilaya, kuna marejezo machache kuhusu hilo katika Biblia. Pengo la miaka kumi na minane katika maandiko limetokeza nadharia kadhaa za kushangaza, lakini hadi sasa hakuna iliyothibitishwa na ushahidi wa kutegemewa.

2.WALKABOUT (MATEMBEZI)

Nadharia nyingine ni kuhusu Yesu na miaka yake iliyopotea ni kwamba alienda ‘kutembea’ kutoka nyumbani kwao Nazareti. Ikiwa tukio hili linatokea Yesu alikuwa mvulana wa miaka 12, kwa hiyo kijana kama huyo anaonekana alikuwa na uwezo upi wa kihisia-moyo na ujuzi gani ili kuchukua safari kubwa na inayoweza kuwa hatari? Sawa endelea
Yaelekea zaidi alipokuwa akiishi Sepphoris, Kijana Yesu anaweza kuwa alipata ujuzi wake wa mapema wa ulimwengu kupitia lugha ya Kiaramu na kujifunza kusoma. Andiko moja linalodokeza hilo linapatikana katika Injili ya Luka, inayosema kwamba Yesu aliingia katika sinagogi na kusoma kitabu cha kukunjwa cha manabii. Wakati huu akiwa kijana, angepitia moja kwa moja unyanyasaji wa kijamii na kiuchumi wa wakulima wa Kiyahudi wa Kipalestina wa wakati wake, ambao alikuwa sehemu yao. Huenda ujuzi huo ndio uliomtia moyo Yesu kutafuta majibu katika ulimwengu wa nje na huenda ukawa na uvutano juu ya uamuzi wenye utata wa kuacha familia yake.

Wasomi wa elimu ya Historia ya kidini wanaamini kwamba
Yosefu baba wa Yesu alikufa alipokuwa na umri wa miaka 12 hivi na kwamba tukio hilo lenye kuhuzunisha ndio lilikuwa kichocheo kwake, akiwa bado mvulana mdogo, kuanza jitihada ya kibinafsi ya kupata nuru ya kiroho. 'Matembezi' haya yaliyodumu kwa takriban miongo miwili yanaweza kuwa yalianza muda mfupi baada ya kuwa na umri wa miaka 13. Ni katika umri huu hatari ambapo madai ya ‘mengi ya miaka 18 uya upotevu wa historia ya yesu’ huanza na nadharia nyingi za mahali ambapo Yesu alitumia miaka yake ya malezi kukua na kuwa mtu mzima ziko wazi kwa tafsiri nyingi.

Haidhuru Kijana yesu alikuwa na jukumu gani kwa mama yake na jamaa zake huko Nazareti,
ulikuwa uamuzi wenye kutatanisha kuwaacha watu wake wa karibu katika umri mdogo kama huo, alipokuwa akianza safari ya ajabu na hatari kwa miguu. Hata hivyo, baadhi ya Wakristo wanaamini kuwa miaka iliyokosekana haina matokeo madogo na ufunuo wowote kuihusu hauwezi kuleta mabadililko yoyote...

3.VATICAN'S SECRETS (Siri za Vatikani)

Kumekuwa na uvumi kwa miaka mingi kwamba Vatican ina ushiikilia ukweli huu kuhusu maisha ya Yesu na miaka kumi na minane iliyopotea,kwa madai kuwa Habari hizo zinaweza kubadilisha sana imani ya dini ya kikristo ya leo,
Hata hivyo hakuna kilichofichuliwa kuhusu kuwepo kwa hati hizo na kile ambacho Yesu alikuwa akifanya na mahali alipokuwa kuanzia umri wa miaka 13 hadi 30. Baadhi ya watafiti wanaamini kwamba alitumia miaka hii isiyo andikwa kusafiri kwenda Uingereza akiwa na 'Yosefu wa Arimathaya', huku wengine wanaamini alisafiri hadi India na Uajemi. Mwishoni mwa karne ya 19 msafiri Mrusi Aitwaye Nicolas Notovitch alidai kwamba aligundua maandishi ya kweli katika nyumba ya watawa huko India ambayo yalithibitisha kwamba Yesu alisafiri na kufundisha huko na kwingineko Mashariki.

ZIKO THEORY NYINGI SANA NITAENDELEA KUZINDIKA KADRI NIPATAVYO UWEZO

CLARIFICATION
To declare interest "Part of the story was done on wasafi Tv the "storybook"
Kwanza kuna uthibitisho wowote usiokua na shaka kwamba huyu yesu alishawahi kuwepo hapa duniani? Isije ikawa story zake ni habari za kutungwa tu kama robin hood n.k
 
Habari za Mida hii Ndugu Zangu Naomba kuanza kwa kuwatakia Sikukuu njema ya Kuzaliwa kwa Yesu kwa wale wote wafuasi wa imani ya Kikristo na hope mnaenjoy sana Happy noela

Kabla ya yote ningependa kurejea Luka 1:1-3 Kama inavyosema;
..."Kwa kuwa watu wengi wametia mikono kutunga kwa taratibu habari za mambo yale yaliyotimizwa katikati yetu,kama walivyotuhadithia wale waliokuwa mashahidi wenye kuyaona, na watumishi wa lile neno tokea mwanzo,nimeona vema mimi nami, kwa kuwa nimejitafutia usahihi wa mambo hayo yote tangu mwanzo, kukuandikia kwa taratibu,.........,"


Miaka 2000 iliyopita katika Mji wa bathelehem ya Uyahudi Alizaliwa Mtoto Aliyepewa Jina la Yeshua/Yehoshua ama yesu au Issa unaweza kumuita utakavyoweza kuita kwa lugha yako ilimradi imani ibaki kuwa alizaliwa Mtoto Ambaye ni Mtu muhimu sana katika historia ya ukombozi wa Wakristo duniani,

Na maandiko yote Yameandika kuhusu yesu kuzaliwa kwake,Miujiza yake mafundisho yake kuishi kwake ,Kusulubiwa kwake na kufufuka kwake na hata kupaa kwake kwenda mbinguni.

Maandiko yote ya biblia yaliyopo yanaanza kuzungumzia yesu kuanzia alipokuwa anazaliwa mpaka akiwa na umri wa miaka 12 (Soma luka 2 yote,pia soma mathayo 2)

Lakini baada ya miaka hiyo 12 Biblia ikawa kimya mpaka tena pale ambapo yesu anatimiza miaka 30 ya maisha yake ndo tunaona yesu anaanza kutajwa tena,kipindi anabatizwa na yohana Mbatizaji..(luka 3:23,Marco 1;9 ,Mathayo 3 kuanzia aya ya 14 na kuendelea)

Lakini miaka yake yote kuanzia umri wa miaka 13 mpaka 29 hakuna sehemu yoyote ya biblia inayotaja maisha yake alikuwa wapi? Alifanya nini? Aliishi wapi? na ilikuwaje?
basi nitajaribu kupitia baadhi ya theory na nakala za vitabu ili tuende sawa katika kujibu haya

HOJA KWA UFUPI

Maisha ya yesu kipindi Akiwa hai hakuna aliyekuwa anayanakili ama kuandika maisha yake kwakuwa Maisha yake na injili hii imekuja kuandikwa Miaka 70 mpaka 140 baada ya kifo chake.
Japo inasemekana historia ya yesu ilikuwa inaelezwa kuwa Masimulizi kumhusu yesu yalikuwa yakifahamika kwa watu wengi Sana kwa muda mchache.
kulingana na Injili ya yohana Yesu alifanya kazi kwa muda wa mwaka mmoja tu na kulingana na injili za ki"synoptikia" (synoptic gospels) Yaani Luka matayo na marko alifanya kazi kwa muda wa miaka 2 mpaka mitatu kabla ya kifo chake...
Japo kuliandikwa Vitabu vingi sana zaidi ya 100 kuhusu maisha ya Yesu lakini vitabu 4 tu vya injili ndiyo vilivyokubaliwa kuingia katika biblia rasmi iliyoamriwa kutumika...

Mengi tunayoyajua kuhusu yesu Tunayatoa katika vitabu vinne tu vya injili yaani marko,mathayo luka na yohana,japo vitabu vingine ambavyo havikuingizwa kwenye biblia bado vipo na vingi viko maktaba vimehifadhiwa kwa na unaweza ukaviita APOKRIFA GOSPELS na vina mambo mengi sana ambayo huwezi kuyakuta kwenye biblia na mara nyingi huwa hayaruhusiwi kuzungumzwa kwa uwazi na mengine utayakuta kwenye biblia..
Kwanini hawakutaka kuviingiiza kwa kisingizio cha KUVUVIWA ama canonical views ?.....
Baadhi ya Vitabu Hivyo vingine huzungumzia Maisha ya yesu akiwa na umri wa miaka 13 mpaka 29 kama kitabu cha The Gospel of Mary, Injili ya mtoto yesu na vinginevyo....

UCHAMBUZI

Dr.Elizabeth McNamer,Proffesor of theology and religious history wa rocky Mountain college Huko Billings Montana,
ambaye kwa Miaka 14 Amekuwa Mkurugenzi mkuu wa Bethsaida Biblical Archaeological Excavations in Israel ( Machimbo ya Kiakiolojia ya kiblia huko Israel) Pia ni proffesor maarufu kwa ufundishaji wake wa Maandiko huko Asia Na anaposcast yake kuhus Historia ya Biblia.Katika moja ya mahojiano yake aliwahi kunukuliwa akisema
"Ililichukua kanisa miaka isiyopungua 500 kujadili mambo mbalimbali kuhusu Yesu, na kipi kiwemo kwenye biblia na kipi kisiwemo na kipi kiandikwe na kiandikwe vipi na kipi kiachwe kabisa na kisizungumzwe tena Na wengi hawajui kuwa kuandikwa kwa biblia ya sasa kulichukua miaka mingi sana ,Huku pia kanisa likijadili Yesu anatakiwa kuonekana vipi mbele za jamii..."

Hiyo ni wakati akijibu moja ya maswali kuhusu kitabu chake cha Jesus and First-Century Christianity in Jerusalem by Elizabeth McNamer,

View attachment 2457658

Kutokana na kutokuonekana kwa historia ya Yesu Katika miaka 18, hii ni kuanzia miaka 13 mpaka miaka 29 kwenye biblia kumezua mijadala mingi sana katika Jukwaa la wana theolojia na wasomi wa dini wabobezi wa kikristo mpaka ikafika hatua Wakaunda theory zao ama hypothetical Views zao na Wote wakaipa majina miaka hii kama.. The lost years of Jesus Christ "Miaka iliyopotea ya Hostori ya Yesu kristo" na wengine waliita "The unaccounted years of Jesus Christ" Pia huitwa the silent years au the missing years ...

MILA NA DESTULI ZA KIYAHUDI KUHUSU MIAKA ILIYOPOTEA YA YESU NA CHANZO CHA NADHARIA

Hapa tutaangalia mila na desturi za kiyahudi kuhusu miaka hiyo inayosemekana kutokupatikana historia ya yesu Kama wewe ni mfatiliaji wa mila na desturi za kiyahudi na kiAramaiki utakuwa si mgeni wa maneno kama Bar-Mitzvah au Bat-Mitzvah..

Hizi ni mila kama mila za kwetu africa au kwetu huko uziguani,Au huko kwetu uzaramoni au umasaini na kwingineko...
Kwakuwa yesu alikuwa ni mmoja wa Wayahudi katika kabila la kiAramaic hivo alifata Tamaduni zote..

"Bar Mitzvah" maana yake halisi ni "mwana (wa kiume) mwenye amri." "Bar" ni "mwana wa kiume" katika Kiaramu, ambayo ilikuwa ni lugha ya watu wa Kiyahudi.
"Mitzvah" ni "amri" katika Kiebrania na Kiaramu.

"Bat" ni binti katika Kiebrania na Kiaramu. (Matamshi ya Ashkenazic ni "bas").

Kitaalamu,Maneno hayo humaanisha mtoto anayekua, na ni sahihi kabisa kwa mila za kiyahudi kumuita mtu kama "kuwa bar (au bat) mitzvah.

"Hata hivyo, neno hili linatumika zaidi ku sherehe za ukuaji zenyewe, na kuna uwezekano mkubwa wa kusikia kwamba mtu "ana bar mitzvah" au "alialikwa kwenye bar mitzvah."

Sasa sherehe hizi zikuwaje na zilimaanisha nini
Mtoto wa kiyahudi zamani hizo mpaka leo kwa kufata sheria za Musa (zilizopo kwenye talmud) Anapofikisha umri wa miaka 13 (kwa mtoto wa kiume) na miak 12 (kwa mtoto wa kike) huhesabika kama amekuwa na hufanyiwa sherehe hiyo ya Mitzvah ili ayavae majukumu yake mapya na ieleweke kwamba mtoto akishafanyiwa sherehe hii hawi tena chini ya uangalizi wa wazazi hiyo umaanisha kwamba hawi chini ya amri ya wazazi na ndo maana ikaitwa Bar/Bat mitzvah..

Na ni mujibu baba kufurahi na kumpa maneno mazuri ya wosia mtoto huyo kwani Baba amejitoa katika responsibikity za mtoto huyo kwahyo dhambi zake na maamuzi huwa yapo chini ya mtoto (hapo mwanzo kabla ya miaka 13 mtoto huwa chini ya kifungo cha miaka na wazazi wake hivyo dhambi na malezi yote huwa chini ya wazazi wake) sherehe hizi hufanyika siku ya sabato....

Na mtoto huwa na ruksa ya kwenda mahali popote atakapo..

(Rejea ya Tamaduni hii ipo katika kitabu cha Talmud na inafanywa na wayahudi mpaka leo)..

Mila hizi zinahusianaje sasa na upotevu wa maisha ya yesu kuanzia miaka 13-29?

Inasemekana kwamba baada ya yesu kuwa tayari amekuwa Bar-Mitzvah akiamua kwenda sehemu mbalimbali kutafuta Elimu huku akiiacha Yerusalem na kurafuta elimu sehemu mbalimbali za nchi zote duniani na Hatimae kurudi Akiwa na miaka 30
(Ambayo pia ni miaka ya Kuhubiri na utume kwa mujibu wa Talmud)

Katika miaka ya 1800-1900 kuliibuka nadharia "Hypothetical views" nyingi sana kuhusu the lost years of jesus christ,Japo wanatheolojia wengi wa kisasa yaani morden theologists wanasema kuwa Yesu aliishi Nazareth na alikuwa akifanya kazi na baba ake kama fundi selemala Japo hili linakosa ushahidi zaidi wa moja kwa moja wa kimaandiko kwenye biblia zaidi ya ushahidi wa mathayo 13:55 na Marko 6:3 japo ukiangalia vizur utagundua ni andiko moja lenye sentensi moja na lenye maana tofauti huku kwwnye mathayo limetajwa tofauti na kwenye marko limetajwa tofauti labda ni katika zile njama Dr Elizabeth McNamer alizokuwa akitueleza..sasa twende kwwnye nadharia hizo kuhusu miaka iliyopotea .....

1.EARLY THORIES (about early as possible as 70-1600 Ad)

Nadharia za awali Kuwa kuna uthibitisho gani unaounga mkono imani kwamba Yesu alisafiri maelfu ya maili kutoka Yudea hadi nchi nyingine?
Vyanzo vya kwanza kabisa vinatoka katika maandiko ya Injili ya Mathayo, Marko, Luka na Yohana. Bethlehemu ni mahali ambapo inaaminika kuwa Kristo alizaliwa, lakini Injili zinasema familia yake iliondoka mara baada ya hapo na kukaa katika mji wa Nazareti, kutimiza yale ambayo manabii katika Biblia walitabiri; kwamba Yesu ataitwa Mnazareti. Nazareti lilikuwa eneo tulivu, la kilimo na la uvuvi ambapo jamii iliishi maisha yasiyofaa, ikidokeza kwamba hadhi ya Yesu ilikuwa ‘Blue collar’ huku yeye na baba yake seremala

Yusufu wakipata riziki zao duni kama mafundi. Huku kukiwa na matarajio machache ya kazi, nadharia moja ni kwamba huenda Yesu alitafuta kazi fulani umbali wa maili tatu katika mji wenye shughuli nyingi wa Sepphoris katika eneo la kati la Galilaya katika Israeli ya leo, mji uliojulikana wakati huo kwa michoro yake maridadi sana iliyotengenezwa na Waruma. Kukiwa na fursa nyingi za kujenga nyumba na kuta,

Huenda mji huu ukawa ndio hatua ya kwanza kuelekea mahali panapoaminika kuwa mahali pa kuanzia kwa jitihada ya Yesu ya kupata nuru ya kiroho. Ikiwa kama vile wasomi fulani Wakristo wanavyoamini kwamba Yesu alitumia muda mwingi wa miaka hii ya kati akifanya kazi ya seremala katika Galilaya, kuna marejezo machache kuhusu hilo katika Biblia. Pengo la miaka kumi na minane katika maandiko limetokeza nadharia kadhaa za kushangaza, lakini hadi sasa hakuna iliyothibitishwa na ushahidi wa kutegemewa.

2.WALKABOUT (MATEMBEZI)

Nadharia nyingine ni kuhusu Yesu na miaka yake iliyopotea ni kwamba alienda ‘kutembea’ kutoka nyumbani kwao Nazareti. Ikiwa tukio hili linatokea Yesu alikuwa mvulana wa miaka 12, kwa hiyo kijana kama huyo anaonekana alikuwa na uwezo upi wa kihisia-moyo na ujuzi gani ili kuchukua safari kubwa na inayoweza kuwa hatari? Sawa endelea
Yaelekea zaidi alipokuwa akiishi Sepphoris, Kijana Yesu anaweza kuwa alipata ujuzi wake wa mapema wa ulimwengu kupitia lugha ya Kiaramu na kujifunza kusoma. Andiko moja linalodokeza hilo linapatikana katika Injili ya Luka, inayosema kwamba Yesu aliingia katika sinagogi na kusoma kitabu cha kukunjwa cha manabii. Wakati huu akiwa kijana, angepitia moja kwa moja unyanyasaji wa kijamii na kiuchumi wa wakulima wa Kiyahudi wa Kipalestina wa wakati wake, ambao alikuwa sehemu yao. Huenda ujuzi huo ndio uliomtia moyo Yesu kutafuta majibu katika ulimwengu wa nje na huenda ukawa na uvutano juu ya uamuzi wenye utata wa kuacha familia yake.

Wasomi wa elimu ya Historia ya kidini wanaamini kwamba
Yosefu baba wa Yesu alikufa alipokuwa na umri wa miaka 12 hivi na kwamba tukio hilo lenye kuhuzunisha ndio lilikuwa kichocheo kwake, akiwa bado mvulana mdogo, kuanza jitihada ya kibinafsi ya kupata nuru ya kiroho. 'Matembezi' haya yaliyodumu kwa takriban miongo miwili yanaweza kuwa yalianza muda mfupi baada ya kuwa na umri wa miaka 13. Ni katika umri huu hatari ambapo madai ya ‘mengi ya miaka 18 uya upotevu wa historia ya yesu’ huanza na nadharia nyingi za mahali ambapo Yesu alitumia miaka yake ya malezi kukua na kuwa mtu mzima ziko wazi kwa tafsiri nyingi.

Haidhuru Kijana yesu alikuwa na jukumu gani kwa mama yake na jamaa zake huko Nazareti,
ulikuwa uamuzi wenye kutatanisha kuwaacha watu wake wa karibu katika umri mdogo kama huo, alipokuwa akianza safari ya ajabu na hatari kwa miguu. Hata hivyo, baadhi ya Wakristo wanaamini kuwa miaka iliyokosekana haina matokeo madogo na ufunuo wowote kuihusu hauwezi kuleta mabadililko yoyote...

3.VATICAN'S SECRETS (Siri za Vatikani)

Kumekuwa na uvumi kwa miaka mingi kwamba Vatican ina ushiikilia ukweli huu kuhusu maisha ya Yesu na miaka kumi na minane iliyopotea,kwa madai kuwa Habari hizo zinaweza kubadilisha sana imani ya dini ya kikristo ya leo,
Hata hivyo hakuna kilichofichuliwa kuhusu kuwepo kwa hati hizo na kile ambacho Yesu alikuwa akifanya na mahali alipokuwa kuanzia umri wa miaka 13 hadi 30. Baadhi ya watafiti wanaamini kwamba alitumia miaka hii isiyo andikwa kusafiri kwenda Uingereza akiwa na 'Yosefu wa Arimathaya', huku wengine wanaamini alisafiri hadi India na Uajemi. Mwishoni mwa karne ya 19 msafiri Mrusi Aitwaye Nicolas Notovitch alidai kwamba aligundua maandishi ya kweli katika nyumba ya watawa huko India ambayo yalithibitisha kwamba Yesu alisafiri na kufundisha huko na kwingineko Mashariki.

ZIKO THEORY NYINGI SANA NITAENDELEA KUZINDIKA KADRI NIPATAVYO UWEZO

CLARIFICATION
To declare interest "Part of the story was done on wasafi Tv the "storybook"
Hii inakusaidia au kutusaidia nini? Hayo mambo ya wabaguzi wa kiyahudi na kiarabu waachie wao wenyewe. Ningekuwa wewe, ningeandika habari za babu yangu badala ya kupoteza muda kwenye ngano koloni na nyemelezi
 
Hii comment sikuiona mkuu ahahahah hebu nielezee hii
Kitabu kinaelezea kulikuwa na ndoa ya siri Kati ya Yesu na maria Magdalena na
pia biblia imeficha vitu vingi ukitaka kumjua Yesu vizuri nenda kasome vitabu vya kiyahudi kwa maana Jews ndio dini iliyekuwepo kipindi hiko kabla ya ukristo
Na mafundisho ya Jews yanaitwa Talmud katafute kitabu cha The Talmud unmasked utaona vingi kuhusu Yesu kuanzia kuzaliwa kwake hadi kusulubiwa
 
Kitabu kinaelezea kulikuwa na ndoa ya siri Kati ya Yesu na maria Magdalena na
pia biblia imeficha vitu vingi ukitaka kumjua Yesu vizuri nenda kasome vitabu vya kiyahudi kwa maana Jews ndio dini iliyekuwepo kipindi hiko kabla ya ukristo
Na mafundisho ya Jews yanaitwa Talmud katafute kitabu cha The Talmud unmasked utaona vingi kuhusu Yesu kuanzia kuzaliwa kwake hadi kusulubiwa
Talmud nishasoma yote babylon pamoja na ya jerusalem
 
"Mungu ni Roho nao wamuabuduo imewapasa kumuabudu katika Roho".

ukimchambua yesu kihistoria au kithiolojia huwez muelewa. Ndio maana hata wanadini (dini ya kiyahudi) walishindwa kumuelewa wakamuua.
Wayahudi waliokua nae hawakumuelewa wewe ndo uje useme unamuelewa?hii kumuabudu ktk roho na kweli bado umeitoa huko huko kwa Wayahudi, sasa wewe unaelewa nini
 
Yesu alienda india somewhere navada ,alienda kuexperience love kwa ma master wa kibuddha,hawakumfundisha chochote,walimwonesha jinsi yakubaki kuwa natural as a human being na kuwa awakened,yesu alikuwa kwenye buddhahood,na dini yake ni the religion of intelligence,religion of no thoughts,no mind,no body,silence,innocence,the religion of herenow and eternal,yesu alivyorudi kwenye mwendelezo kwenye bible alikuwa si somebody alikuwa ni nobody yani presence yake ndo ilikuwa ina exist alishakufa kitambo maana kufa ni kuua knowledge,false identity,ego,mind,thoughts and remain empty hence akiwa tayari keshajiunga na cosmic mirror ambacho ni whole yani kinachoona vyote hence kuwa God,jesus was just a person like you and nothing else na kilichomfanya awe unique ni kwakuwa aliamua kuishi yeye kama yeye bila speciality,natural,love,innocence,with state of not thinking but just knowing kwakuwa all is here and will always be.



Wangejiloga kuandika historia ya yesu jua yafuatayo,kusingekuwa na makanisa,misikiti,juain,jews and other kind of temples or monastery maana wanadamu wangejua wao ni kina nani,wanauwezo gani na nguvu zipi,wanadamu wangejua wao ni miungu katika Mungu,kumbuka yesu alisema kila mtu atabeba msalaba wake maana yake this is my path now face your own.
Mzee kuna jambo la ziada unalifahamu hapa ambalo wengi kama sio wote hatulifahamu, nadhani unatakiwa uandike zaidi
 
Nadhani shida yako ni vitabu vya Apokrifa (apokrifa books) hivyo vitabu vipo na unaruhusiwa kuvisoma na kuacha hivyo unavyodai ni Apographa vilivyo sahihi kwetu na vingine usivyovitaka wewe,,Na zaidi unaruhusiwa kuanzisha version yako pia ya biblia ukaiita kwa jina lako na isio na hayo mapungufu ya kusadikika unayoyadhania.Naamini utapata wafuasi wengi tu (wanaofanana na wa kibwetere) mnaoshare mashaka yanayofanana.
Kibwetere ni levo nyingine kabisa. Kati ka dhama za utandawazi, Kuaamnisha watu hadi kuwatia kiberiti sio mchezo.
 
Usitarajie KUPATA majibu ya uhakika coz,waumini wametishwa kuhoji Mambo HAYO ni dhambi!
Umenena vyema kabisa. Kila dini inalo la nmna hiyo. Kila dini ina imani ambayo haihojiki - nyingine utaambiwa ni maagizo ya Mwenyezi Mungu. Utayahoji vipi maneno yaliyoagizwa na Mwenyezi Mungu?
Masuala ya dini ni masuala ya imani kwa Mwenyezi Mungu ambaye hautuwezi kumhoji - inabaki ni imani, na naona ibaki hivyo hivyo. Kama Maisha fulani ya Yesu yalifichwa ili kujenga watu kiimani na wakawa na amani - hakuna haja ya kuyatafuta eti kuyafichua.
Watu wakianza kufichua nadharia za yanayosemekana kufichwa kwa kila dini kuna wengine hawatstahimili, wanaweza kuanza kushikiana mapanga. Tusifike huko - yamefichwa wana amani, waache wabaki na imani yao inayowapa amani.
(Sisi wenye familia tuna maisha ya namna hiyo. Kama unaishi na mwenzio kwa amani, basi usitake kuchunguza maisha yake ya zamani ambayo wewe hukuyajua kabla, na hata hayo mnanyoishi pamoja lakini anakuficha. As long as hayakuletei madhara yoyote - achana nayo muendelee kuishi kwa amani)
 
Yesu alienda india somewhere navada ,alienda kuexperience love kwa ma master wa kibuddha,hawakumfundisha chochote,walimwonesha jinsi yakubaki kuwa natural as a human being na kuwa awakened,yesu alikuwa kwenye buddhahood,na dini yake ni the religion of intelligence,religion of no thoughts,no mind,no body,silence,innocence,the religion of herenow and eternal,yesu alivyorudi kwenye mwendelezo kwenye bible alikuwa si somebody alikuwa ni nobody yani presence yake ndo ilikuwa ina exist alishakufa kitambo maana kufa ni kuua knowledge,false identity,ego,mind,thoughts and remain empty hence akiwa tayari keshajiunga na cosmic mirror ambacho ni whole yani kinachoona vyote hence kuwa God,jesus was just a person like you and nothing else na kilichomfanya awe unique ni kwakuwa aliamua kuishi yeye kama yeye bila speciality,natural,love,innocence,with state of not thinking but just knowing kwakuwa all is here and will always be.



Wangejiloga kuandika historia ya yesu jua yafuatayo,kusingekuwa na makanisa,misikiti,juain,jews and other kind of temples or monastery maana wanadamu wangejua wao ni kina nani,wanauwezo gani na nguvu zipi,wanadamu wangejua wao ni miungu katika Mungu,kumbuka yesu alisema kila mtu atabeba msalaba wake maana yake this is my path now face your own.
Ebwana eee [emoji1783][emoji1783]

This is my path, find your own fellas.... Hadi leo mnamsubiri
 
Utata unakuja hapo walipoanza kumuita Yesu/jesus mbadala wa jina lake halisi.

Huo uhuni wa kubadiri majina ya manabii na wahusika wa matukio upo ktk biblia tu ni maajabu haya, hata Qur'an na vitabu vingine ama dini zingine na hata historia za kawaida hutoona kubadirika kwa majina ya wahusika kwa visingizio kuwa wametafsiri kutoka ktk lugha fulan,

Kwanini wahindu ama waislam wasimbadiri muhamad ama Allah asiitwe kwa majina ya uswahili ama huko uzunguni wasiwabadiri mitume wa uislamu kwa lugha zao wanazoelewa?

Je inawezekana vipi mtu anaeitwa Juma hapa Tanzania akienda china abadiri jina eti aitwe kichina, na akienda uingereza aitwe kwa lugha wanayoitafsiri jina la Juma? Na akienda uturuki wabadiri tena hamuoni kuwa huo ni mchezo mchafu wa kuficha jambo hapo?

Huyo yesu ni aina ya kiumbe chenye majina meengi hapa dunian na ktk dini kulko kiumbe chochote, maana wanadini wanataka kutuaminisha mambo yasiyowezekana.

Ni kweli maisha ya huyo yesu ni mengi hayajulikani, na sio kujulikana tu bali kutafsirika.

Kikawaida ukiisoma biblia kwa macho ya upembuzi utagundua kuwa kuna wakina yesu zaid ya mmoja humo wamechanganywa,

Kwa mission aliyotumwa hapa dunian haikuwa ya kuja kuishi kwa miaka 33 bali zaidi ya 55, maana kikawaida cheo chake ama mission yake ya Utume ilikuwa aanze baada ya kufikisha miaka 25 na kustaafu miaka55, lkn maajabu ya watafsiri wakaweka maneno yao ya uongo.

Pia kuna mengi hayajawekwa wazi kuhusu wale mitume wake kuwa walikuwa 13 kutoka ktk kabila 13 za waisraeli[emoji23][emoji23].

Ni mengi yamefichwa ktk biblia kwa kujua ama kutokujua sababu kuu ya kutokujua ni kuchakachua kitu walichoshindwa kukichakachua.

Biblia ukiisoma nje ya mahaba ya dini na vifungo vya mashetani ya kidini basi utagundua mengi sana.

Hakukuwa na haja ya kubadiri majina ya huyo mwana wa Mungu na kumuita Yesu sjui jesus mala yeshua, wangeacha tumuite majina yake halali.

Jiulizen kama maandiko yalikataza kubadiri ama kuongeza lolote kwanini hawa wafia dini waliongeza upuuzi wao waliouona ni bora? Kutafsiri maana ya sentensi na historia sio mbaya, lkn kubadiri majina ya wahusika huo ni uhuni na ushenzi kama sio ujambazi.

Yesu ama jesus hajawai kuwepo, hajawai kuwepo maana ilo jina halina muhusika kutoka historia yoyote hapa dunian ndiomaana hata uwepo wake unamikanganyiko kuanzia ktk biblia yenyewe, mpaka kwa walioicopy biblia hao wanaomuita issa bin mariam, wote waongo wakubwa.

Historia za watu wa kale, imechezewa mno, imeharibiwa sana, Yesu hatorudi mtamsubiri sana, maana haiwezekani kitu kilichoundwa kwa kufananisha na mtu mwingine mseme kiumbe hiki kiwepo haiwezekani.

Someni sana maandiko nje ya dini zenu mtaelewa hili jambo, View attachment 2459327
Safi sana
 
Back
Top Bottom