Miaka 63 baba mdogo hajawahi kurudi nyumbani

Miaka 63 baba mdogo hajawahi kurudi nyumbani

mama yangu alikuwaga na mjomba wake sasa ni marehemu akiondoka kwao kijijini mikese morogoro, mama akiwa bado mtoto mdogo, alienda tanga ila hakuwa na mawasiliano na kwao, hadi mama akakua na sisi tukazaliwa alirudi kwa kurudishwa mimi nikiwa niko sekondari tayari

tena kurudishwa kwenyewe ni kuwa alikuwa anaumwa sasa watu wa huko wakaona huyu mtu atatufia wakatafuta ndugu zake , wakampata kakaake wakamtumia nauli kaka ke akaenda huko tanga akakabidhiwa ndugu yake akamrudisha morogoro.
hakukaa sana akafariki,

imagine aliondoka miaka ya 1980s mwanzoni, akajakurudi miaka ya 2000 mwishoni
Hii habari yako ni questionable! Mjombake mama aliondoka 1980's mama akiwa mdogo akaja kurudishwa 2000's wewe umshamaliza sekondari. Hebu eleza vizuri.
 
Very sad ....pole sana ndugu yangu ...huenda kuna siku tutamwona tena.
Unyanyasaji na unyanyapaa wa aina hii upo sana kwa kweli .
... aliondoka 1963 baada ya kujifungua; let's assume she was 20. Today she would be 77. Ngumu sana kuonana naye tena Mkuu; tuombe basi japo katika Ufalme wa Mbinguni.
 
Babu yangu hata kabla hajamzaa baba, kaka zake wanne,waliondoka kwenda Zambia (Kitwe kwenye machimbo ya shaba, baadae watatu wakaenda ''KuJhoni''(Joharnesburg) Africa kusini kwenye machimbo ya dhahabu, mpaka leo hawajawahi kuonekana, Ni zaidi ya miaka 70 iliyopita...hii ni kutoka Mbeya Rungwe Tukuyu...........
 
Inauma Sana. Hata sisi shangazi yetu alijifungua mwaka 1963! Naskia akawa anatoka kinyesi. Jamii ikamtenga, akaona isiwe kesi. Ndo hii sasa tunaita "fistula!

Tunajiulizaga sijui alipona au alikufa! Aliondoka na mwanaye😭😭
Nimesikitika sana. Miaka ya zamani kuna watu walipata shida sana na wengine kufa vifo vya mateso makubwa kwa sababu tu ya ujinga, mila na desturi zilizokuwepo kwenye jamii. Hasa wanawake waliathirika sana. Mimi nimezaliwa kwenye jamii ambayo miaka ya nyuma mfumo dume ulikuwa umetamalaki na mwanamke alikuwa anaonekana kama mtumwa wa kufanya kazi. Sitaacha kuwaheshimu kinamama katika maisha yangu nikikumbuka wengi walivyonyanyaswa kwa sababu ambazo ziko nje yauwezo wao.
 
Anko...
Alizamia miaka 18 kwenda kuchimba madini, walikua wawili na Jirani ambaye walikua marafiki sana tangu utoto.
Mwenzake alikaa miaka 12 akarudi kusalimia kwao, akaulizwa mwenzako vipi? Akaseme yupo hataki kuja mpka Afikie malengo yake, japo mpka hapo alikua tayari ameshayapatia maisha vizuri ila kwa malengo yake akaona bado..

Yule Rafiki yake akawa hivyo hivyo anakuja na kuondoka, akimsisitiza mjomba aje, anakataa,
Upepo ukabadilika, mali zikaanza kupukutikaa, Mwenzake yeye alikua na maisha tu ya chini, akaamua kabisa kurudi kwao, Mjomba ndio mambo yakazidi kua magumuu, mama yake(bibi) akawa anaumwa yule rafiki yake akatafuta marafiki wengine kule mgodini ili wamuunganishe na mjomba, ikafanikiwa akamwambia Mama yako Anaumwa sana, furaha yake akuone,

Mjomba akakubali kurudi, alikua hana hata simuu, Ilibidi mawasiliano ya maendeleo ya safari yafaywe baina yetu na konda, watu wakaenda ubungo kumpokea(ilibidi yule rafiki yake naye awepo maana alisema ikitokea mkapotezana na konda hamwezi kumkumbuka) ...

Waliooenda ubungo kumpokea hawakuamini Jamaa alivyochokaa,

Hana simu, nauli alitumiwa, Nguo kaweka kwenya rambo, Yaani kwa ufupi hana hili wala lile,

Safari ya kuja kaskazini ikaanza, huo mpango wa kumrudisha ulifanywa kimya kimya bila mama yake kujua, Maana usije ukabuma sababu ilishatokea hivyo akaumia sanaa, na kati ya wanae huyo alikua akimpenda sanaa, Miaka yote amekua akiota ujio wake na kumsubiria, basi watu wakaona awamu hii wafanye kimya kimya.

Hakuna mtu ambaye alimtambua,
Mama ni mama tuuu, Bibi kusikia tuu sauti ya Hodi Akahamaki kilunga "......... Huyu ni....."
Kuingia ndani, watu hawakuelewa zile nguvu bibi aliziapata wapi za kuamka na kumkumbatia mwanae,
Yeye hakujali amedhoofu wala nini alichofurahi ni kumwona mwanae.....

Aliondoka kwa malengo ya kuja kufunika ukoo kwa utajiri, akarudi akiwa ndio maskini zaidi, akatafutiwa kijimtaji akaanza upya ila kwa shart, lazima abaki kijijini amuangalie mama na mali nyingine mana hakuna mtu, Mama yake alipona wakaishi pamoja kwa furaha miaka mitatu zaidi, Bibi akafariki, yule rafiki yake naye akafariki, ndani ya siku mbili Anko naye akafariki, ilikua mwaka huu, Alinipenda Sana mpaka nikawa najiuliza kwa nini, hata wakati wanawasiliana na yeye kuja alikua ananiulizia, na mimi nilikua simfahamu mana nilikua mdogo na sikua kijijini.. na rafiki yake mkubwa kwenye familia yake alikua mama...

Anko Amefariki na umaskini wake na hata bila mtoto, Japo ameacha kiwanja kikubwa tuu kule.

Kama kuna Ndugu, jirani au rafiki anayejua huu mkasa, Basi tunafahamiana.
 
Kaka yangu ambaye ni mzaliwa wa kwanza aliondoka nyumbani tarehe 22/9/1970 akiwa na umri wa miaka 20 akakaa Mwanza mjini kwa muda wa miaka 18 mfululizo bila kurudi nyumbani Geita vijijini. Hata baba alipofariki mwaka 1979 hakuhudhuria mazishi. Tarehe 1/9/1988 ndipo akaja nyumbani kwangu na kuniomba nimpeleke nyumbani. Nikampeleka tarehe 3/9/1988 akuwa na umri wa miaka 38. Hadi leo hajaondoka nyumbani.

Mkuu unawezaje kukumbuka hadi tarehe na mwezi.?
Na wewe hiyo ‘wizakale’ ni ‘umekuja zamani’, usharudi ulikotoka.?
 
Ila Mkali umetisha wale watumwa ndio tunaowambia Black lives matter ...hao walilazimishwa bana
Ha ha ha; warudi basi. Afrika ardhi imejaa tele. Kwa Tanzania under special arrangements hekta kadhaa zinaweza kutengwa maeneo ya Bahi na Manyoni kwa ajili ya Black Lives walio tayari kurudi ila ndio hawataki kurudi home.
 
Siwajui ndugu wa upande wa mama,sujawahi hata kuona

mama ni mzaliwa Wa shinyanga,aliolewa na baba miaka ya 1986. Walitengena na family baada ya kuolewa wakahama na mkoa

Tangu 1986 hadi Leo 2020 mama hakuwahi kurudi nyumbani kwao

Natamani sana siku moja niwaone ndugu zangu upande Wa mama angalau hata mmoja tu lakini ilishashindika kabisa

Tafadhali kama kuna msaada mnaweza nisaidia niwapate hata mmoja

Muda mwingine nikikutana na mtu alitokea shinyanya huwa namchulia kama ndugu yangu.
Mama jina lake anaitwa Modesta misalaba, aliolewa kwenye ukoo Wa maganiko

Mkuu unakwama wapi.?

Mama yako yupo hai, na unajua kwao ni Shinyanga... ukimuuliza uende hataki kukuelekeza au unasubiri akupeleke.!
 
Babu yangu hata kabla hajamzaa baba, kaka zake wanne,waliondoka kwenda Zambia (Kitwe kwenye machimbo ya shaba, baadae watatu wakaenda ''KuJhoni''(Joharnesburg) Africa kusini kwenye machimbo ya dhahabu, mpaka leo hawajawahi kuonekana, Ni zaidi ya miaka 70 iliyopita...hii ni kutoka Mbeya Rungwe Tukuyu...........
Hiyo ndio basi tena
 
Kaka yangu ambaye ni mzaliwa wa kwanza aliondoka nyumbani tarehe 22/9/1970 akiwa na umri wa miaka 20 akakaa Mwanza mjini kwa muda wa miaka 18 mfululizo bila kurudi nyumbani Geita vijijini. Hata baba alipofariki mwaka 1979 hakuhudhuria mazishi. Tarehe 1/9/1988 ndipo akaja nyumbani kwangu na kuniomba nimpeleke nyumbani. Nikampeleka tarehe 3/9/1988 akuwa na umri wa miaka 38. Hadi leo hajaondoka nyumbani.
Pole ndugu. Wazaliwa wa kwanza sometimes wanakuwa na issues sijui kwanini. Anyway, hata maandiko yanasema ni malango shetani huwachezea kweli kweli. Mvumilie tu kaka mkubwa Bwana atakulipa.
 
Nimesikitika sana. Miaka ya zamani kuna watu walipata shida sana na wengine kufa vifo vya mateso makubwa kwa sababu tu ya ujinga, mila na desturi zilizokuwepo kwenye jamii. Hasa wanawake waliathirika sana. Mimi nimezaliwa kwenye jamii ambayo miaka ya nyuma mfumo dume ulikuwa umetamalaki na mwanamke alikuwa anaonekana kama mtumwa wa kufanya kazi. Sitaacha kuwaheshimu kinamama katika maisha yangu nikikumbuka wengi walivyonyanyaswa kwa sababu ambazo ziko nje yauwezo wao.
Yaani hata Babu akawa anamwambia wewe ushakuwa mkosi...hapo dingi yuko bwiru anasoma..anarudi hom hakumkuta sisy ake ...Kuna makabila mpk leo wanaendekeza hizo mila za ajabu na mamfumo dime....nikibarikiwa kupata mtoto wa kike sitaruhusu aolewe kabila langu... Sitaki kbs
 
Back
Top Bottom