Viongozi wengi wa waAfrika ambao Nyie mliwaita freedom fighters wengi walipigania uhuru kwa manufaa yao na familia pengine na koo zao Mimi Nina hakika na hilo hususani kwa hapa Africa mashariki labda kidogo Patrice lumumba na wengine wengi ila kwa Africa mashariki wengi walipigania kwa maslahi yao.
Kiongozi Amekaa madarakani miaka 24 kilimshinda nini kubadilisha katiba? Na Utafikia watu wanasema aliamua kung'atuka mwenyewe Bila kushurutishwa Huu ni uongo kabisa to be honest mambo yalimshinda Ndipo akaamua kun'gatuka Sasa yeye kilimshinda nini kutuletea katiba inayoendana na post independence?
Sasa Tumlaumu nani? Hawa waliofuata? Kama yeye alingoza miaka 24 hawa wenzake wa miaka 10 wataweza kwa ubinafsi wao? Hii katiba inamfanya Raisi awe na madaraka ya kufuru na ya kufa mtu eti neno la Rais ni sheria,khaaa haiwezekani kabisa
Na ubaya Sasa katiba Ile Ile imemfanya au imefanya can wahodhi kila kitu halafu unasema Hii nchi inaongozwa kwa katiba ya vyama Vingi? Hii katiba ni ya chama kimoja tu kataa au kubadili. Kwa namna Hii kuindoa Ccm ni ndoto ya alinacha tutaendelea kusaga meno kwa katiba Hii ya mkoloni.
" walio kataa utumwa wanajikuta hawako huru"
Uzi usifutwe Huu Haya ni mawazo huru.
Ukitoa mawazo yako ya kuhusu siasa za nchi hii kwanza inabidi uweke pembeni chuki binafsi na ujadili faida na hasara ya jambo unalolizungumzia ?
Lakini Pia baba wa Taifa hili ndiye dira ya Taifa hili milele.
Kila nchi ina shujaa na mwasisi wake na ndiye aliyeongozwa na Mungu ili kutuletea uhuru na maono ya taifa hili lenye Rasilimali nyingi.
Mwalimu aliona mbali sana na hakua mbinafsi wa kujilimbikizia mali.
Angeweza kuungana na wakaoloni na kuleta katiba mpya halafu uhuru wetu ukawa ndio utumwa wetu wa hiyari.
Mwalimu alitumia Katiba ya wakaoloni kuwanyoosha wakoloni.
Unafikiri ilikua rahisi kutaifisha mali zote za Mabepari na ardhi karibu asilimia 70 ya ardhi yenye rutuba ilikua imehodhiwa na wazungu wachache!
Nani asiyenufaika na ardhi aliyokua amewanyanganya wazungu??
Bila ujasiri na kujitoa mhanga kwa Mwalimu ,ni nani angweza kushindana na mabeberu waliokua wamemiliki njia zote za uchumi kwenye nchi yetu?
Mfano Kama umewahi kuzunguka maeneo ya Lindi,Ruvuma na Ntwara utagundua kuwa ardhi karibu yote ilikua ni mali ya Wazungu. Wazungu walilima Korosho karibu kila sehemu ,walilima pamba ,mkonge na minazi. Je, Wamakonde ,wayao,Wangoni na wamatumbi kwa umoja walio nao wangekubali kuendelea kuwa manamba kwenye ardhi yao ya asili .Ukumbuke watu wa kusini walipambana na wakoloni na kuchoma moto mashamba yao na kungia miche ya pamba kabla ya uhuru.
Je, leo hii maeneo hayo yangakua salama au ingekua kama Kongo ya mashariki? Ukizingatia wenyeji wa maeno hayo wanatofauti kubwa ya kimila na kiimani na wakoloni waliokua wanakalia ardhi yao!!
Umewahi kusikia kuwa enzi za Mkoloni Wachaga walitaka kuhamishwa maeneo yote yanayozunguka Mlima Kilimanjaro ili matajiri wa kizungu waishi huko kama Ulaya. Je, Ulitaka Mwalimu Nyerere asitumie katiba yenye meno kuwafukuza mashetani waliojivika ngozi ya kondoo warudi kwao ulaya. Pangekua na vyama vingi miaka hiyo unafikiri ingekua ni salama kwa nchi yetu wakati wakina Kambona, na Mariale walikua wanaungwa mkono na mabeberu waliokua wameizunguka Tanzania kuanzia Kenya, Zimbabwe ,Msumbiji, Afrika kusini na baadae waarabu wakatumiwa na Marekani kuiingiza Uganda kwenye vita ili kumdhoofusha Nyerere ambaye alikua na uchumi mzuri na huduma bora kwa wananchi wake kuliko nchi zote Afrika mashariki .
Iddi Amini alikua dikteta lakini ndiye aliyewanufaisha waganda Mpaka leo wanashika uchumi wao wenyewe badala ya kuwa watumwa.
Nyerere alishatukomboa na kupata uhuru na kuweka misingi ya umoja na amani lakini sisi wenyewe ndio tunaoiba mali za umma.
Nchi imewekewa misingi mizuri ya kuiwezesha kuendelea inachohitaji ni siasa safi na uongozi bora peke yake.
Watu wanashindana kuiibia serikali halafu tunamlaumu Nyerere.
Katiba inakwamishwa na wanasiasa wenyewe na sio Nyerere. Yeye alipambana wakati huo wa mkoloni jeuri na asiyekua na huruma lakini vijana wa Leo wanaogopa kupambana na watu wanaoishi nao na kula na kunywa nao mpaka kulala nao halafu tunamlaumu Nyerere.
Yaani woga wetu unahusiana nini na Nyerere. Nchi ina mwaka wa Nane sasa sijawahi kusikia watu wamepelekewa chakula cha msaada halafu mtu anamlalamikia Nyerere aliyewapa watanzania maksini na matajiri haki sawa ya kumiliki ardhi . Leo wakoloni weusi ambao ni ndugu zetu wanauza ardhi yote na misitu yake na wanyama wake na madini yake na gesi yake halafu tunamlaumu Nyerere badala ya kujifunza kuwa yeye aliwezaje kuwangoa wakoloni wakati huo ambao hata mitandao haikuwepo na railimali fedha zikiwa ndogo sana kwenye chama Chake cha TANU.
Mwalimu alifanya makubwa kwa sehemu yake na aliijenga nchi katika mifumo na kitaasisi na palikua na Demokraia kubwa sana ndani ya CCM.
Hivi unategemea CCM wataondoka madarakani kwa kuwachekea chekea wanaobadili matokeo. ?
Tundu Lisu bila shaka atakua mwasisi wa Taifa la Tanganyika na baba wa Tanganyika kwasababu anajua kuwajenga watu kifalsafa na kiujasiri. Yaani Watanzania vijana wenye nguvu wa Kimasai ,Kikurya ,Kisonjo Kisukuma , kinyakyusa , Kimbulu,Kinyamwezi ,Kingoni ,kimakonde n.k Kama wanaona kuwa Katiba iliyopo ni ya mkoloni halafu wanashindwa kumtoa mkoloni wanayeishi naye,kula naye kumywa naye, kusali naye na kwenda naye sokoni basi basi ujue kizazi hiki ndicho cha hovyo na sio Katiba.
Yaani kijana anakaa pembeni anaangalia kura zake kwemye uchaguzi rahisi wa serikali za mitaa usio na askari wa kutosha kila nyumba zinabadilishwa na wazee waliohongwa kofia halafu analalamika na kumlalamikia Nyerere na katiba .
Vijana wa leo wangezaliwa enzi za ukoloni tusingepata uhuru mana ni wepesi kuhongwa na kuporwa haki zao .
Wengine wanashangilia ardhi kuuzwa kwa wakoloni eti waajiriwe kulima mashamba ya Wazungu 😂😂😂😂.
Yaani shamba liliwa la kwake halimi ila akipewa mzungu basi anaariwa kulima na kupalilia na kulinda ngedere alimradi tu anaamka asubuhi halafu anakwenda kwenye kibarua kwa mzungu au mwarabu.
Tuwajenge watanzania katika falsafa ya mwalimu ya kupinga dhulma ,uonevu, ubaguzi ,udini, ukabila ,kuiza mali za umma kwa wageni halafu pesa zinakua nauli ya kwenda kuwaita wageni wengine tena kuwagawia bandari zetu.
Tupinge matumizi mabaya ya mali za umma.