Miaka 97 ya Mzee Mwinyi na amani ya moyoni pasipo nongwa na visasi

Miaka 97 ya Mzee Mwinyi na amani ya moyoni pasipo nongwa na visasi

Mzee ana ukwasi wa kutosha
1960 alikuwa Mkuu wa Chuo cha Ualimu Znz cha Lumumba tangu hapo akaanza kuwa na mshahara mkubwa

1966 Balozi, kaja kuwa Waziri wa Jamhuri tangu 1972

kaja kuwa Rais wa Znz

kaja kuwa Rais wa Muungano

binti yake mmoja kaolewa na mtoto wa Mfalme wa Abudhabi

Mtoto wake Rais wa Znz

mtoto wake mwingine Mbunge wa Bunge la Jamhuri

Ma binti zake ni Wafanyabiashara wakubwa wanaoshiriki kwny kandarasi kubwa kubwa za nje na ndani ya nchi

Vijana wake wa kiume ni ma Tycoon kwny biashara ta Utalii Afrika mashariki

wengine ni Wafanyakazi wa Taasisi kubwa kubwa za kimataifa

sasa hapo akiwa na Ukwasi ni jambo la kushangaa kweli ?

mwenzangu na mie kamshara ka TGSD hata shangazi akidondoka kwny bodaboda kijijini lazima utafutwe utume elf 5 ya kumbeba kwny bodaboda utachomokaje kwny lindi la umskini?
 
Sahihi kabisa

umri na Afya havina uhusiano na dini wala uchamungu

Kauli yako sio sahihi.

Kumbuka kiongozi mbora wa waislamu alikuwa mtume muhammad sala na salamu ziwe kwake.

Mtume alikufa na miaka 63 huku akiwa ni mtu muungwana zaidi kuliko mzee mwinyi.

Kuishi maisha marefu hakuambatani na uislamu na wala hakuambatani na uungwana.

Unaweza kuwa mtu mshenzi na ukaishi maisha marefu,naomba usihusianishe baina ya maisha marefu na uislamu au baina ya maisha marefu na uungwana,havina uhusiano.

BTW nayaheshimu maoni yako mkuu.
 
1960 alikuwa Mkuu wa Chuo cha Ualimu Znz cha Lumumba tangu hapo akaanza kuwa na mshahara mkubwa

1966 Balozi, kaja kuwa Waziri wa Jamhuri tangu 1972

kaja kuwa Rais wa Znz

kaja kuwa Rais wa Muungano

binti yake mmoja kaolewa na mtoto wa Mfalme wa Abudhabi

Mtoto wake Rais wa Znz

mtoto wake mwingine Mbunge wa Bunge la Jamhuri

Ma binti zake ni Wafanyabiashara wakubwa wanaoshiriki kwny kandarasi kubwa kubwa za nje na ndani ya nchi

Vijana wake wa kiume ni ma Tycoon kwny biashara ta Utalii Afrika mashariki

wengine ni Wafanyakazi wa Taasisi kubwa kubwa za kimataifa

sasa hapo akiwa na Ukwasi ni jambo la kushangaa kweli ?

mwenzangu na mie kamshara ka TGSD hata shangazi akidondoka kwny bodaboda kijijini lazima utafutwe utume elf 5 ya kumbeba kwny bodaboda utachomokaje kwny lindi la umskini?
😄😄😄😄😄😁
 
HV mzee huyu kashakabidhiwa ile nyumba ambayo jiwe amemjengea pale kawe huku akiwa Bado Ana nyumba pale mikocheni
 
1960 alikuwa Mkuu wa Chuo cha Ualimu Znz cha Lumumba tangu hapo akaanza kuwa na mshahara mkubwa

1966 Balozi, kaja kuwa Waziri wa Jamhuri tangu 1972

kaja kuwa Rais wa Znz

kaja kuwa Rais wa Muungano

binti yake mmoja kaolewa na mtoto wa Mfalme wa Abudhabi

Mtoto wake Rais wa Znz

mtoto wake mwingine Mbunge wa Bunge la Jamhuri

Ma binti zake ni Wafanyabiashara wakubwa wanaoshiriki kwny kandarasi kubwa kubwa za nje na ndani ya nchi

Vijana wake wa kiume ni ma Tycoon kwny biashara ta Utalii Afrika mashariki

wengine ni Wafanyakazi wa Taasisi kubwa kubwa za kimataifa

sasa hapo akiwa na Ukwasi ni jambo la kushangaa kweli ?

mwenzangu na mie kamshara ka TGSD hata shangazi akidondoka kwny bodaboda kijijini lazima utafutwe utume elf 5 ya kumbeba kwny bodaboda utachomokaje kwny lindi la umskini?
na mtoto wake mwingine ni rais wa JMT ila sijaandika mie
 
Nikiri kwamba sijaisoma makala yote ! Lakini Ali Hassan Mwinyi ndio anakula capacity charges za IPTL ! Hana usafi wowote ule babu yule!!

Ni kiri kwamba sijaisoma makala yote ! Lakini Ali Hassan Mwinyi ndio anakula capacity charges za IPTL ! Hana usafi wowote ule babu yule!!
Mzee Mwinyi angekuwa na fikra na mawazo kama yako nahisi asingekuwa na afya yenye nguvu alionayo sasa, hapa sizungumzii kuwa na umri mkubwa.

Nachoamimi mimi kufa mapema ni mipango yaungu mwnyewe. Roho mbaya husababisha kudhohofu kwa afya ya mwili pia.
 
Wewe mjinga tu wazee wa kislam wanaokufa mapema wote ni waovu? Vipi wakristo wazee wapo wengi tu! Udini ndo shida yenu wavaa madera! Vipi akina warioba huwaoni?Pia akina Butiku, Samwel Marechera!
Ni Malecela sio Marechera. Ukifika wakati wao watazungumziwa kwa uzoefu wao tofauti na huu wa Mwinyi.
 
Rais Mstaafu wa awamu ya pili leo anatimiza miaka 97, ni mingi kwa kuiandika na kuihisi kichwani ukifanya tafakari ya kina. Ni miongo tisa na miaka saba. Amekula magunia kwa magunia ya chumvi. Ni umri mkubwa sana kuendelea kuwepo hai, akiwaona wajukuu na watoto zao. Mzee Mwinyi kwa sisi tuliokuwepo duniani wakati anaingia na kuondoka ikulu ni heshima na baraka kumuona akiwa hai miaka 27 baada ya kuondoka Ikulu.

Wengi watajiuliza ameweza vipi kuishi miaka mingi namna hii. Wapo watakaosema hana makuu kwa maana ya kutoweka visasi moyoni, wapo watakaosema hanywi pombe akiwa ni muumini mzuri wa dini ya kiislam. Na wapo watakaokwenda mbali zaidi kwa kusema amekuwa akijitunza na siku zote akishiriki matembezi ya hiari na yeye mwenyewe kupenda kutembea. Na anayependa kutembea mazoezi ya asubuhi au kukimbia taratibu (jogging) anakwepa maradhi mengi yakiwepo yale ya moyo yenye kuua haraka na pasipo kutarajiwa.

Mzee Mwinyi ameendelea kuwepo wakati wazee wenzake karibu wote wa miaka ile ya awamu ya kwanza na ya pili wakiwa tayari wameshazikwa. Siku ya msiba wa hayati John Magufuli akasoma pasipo miwani!, na akatembea kwenda na kurudi kwenye kiti chake pasipo msaada wa kushikiliwa na mtu yoyote.

Ni kweli wote tunapita juu ya uso wa dunia, lakini kupita kwa baadhi yetu ni kule kwenye baraka. Unaweza kujiuliza inakuwaje Mzee huyu anazidi kusherehekea siku za kuzaliwa kila mwaka wakati wanasiasa vijana tu wakiaga dunia. Vijana waliozaliwa akiwa tayari ni mwanasiasa wanakufa na kumuacha yeye akiendelea kuishi kwa upole bila ya makuu pale kwake mbele kidogo ya Msasani kwa Mwalimu Nyerere.

Hakuwa na makuu, hakutunza hasira wala visasi. Hakutaka kuibadili dunia (To change the world), hakuamini kuwa kila tatizo anaweza yeye kama yeye akalitatua na hivyo kuumiza walio wengi katika mchakato wa utatuzi wa hilo tatizo. Hata baada ya kukejeliwa na Mwalimu Nyerere pale Kilimanjaro Hotel Simba Grill mwezi March mwaka 1995 aliendelea kuwa mkimya mpaka ilipofika siku akaamua kujibu mapigo.

Na baada ya hapo hakutaka kujikweza au kupandisha mabega, ni kama alisamehe na kuendelea kuwa huru moyoni. Hiyo ni sifa anayotakiwa kuwa nayo kiongozi mkuu wa Taifa. Uwezo wa kunyenyekea kwa kuyaona ni madogo tu baadhi ya mambo yanakukwaza na kukukera ukiwa ofisini. Ni mtihani mgumu sana kwa viongozi wenye madaraka makubwa kwa mujibu wa katiba yetu kuweza kujishusha huku wakiwa na vyombo vyote wanavyoweza kuvitumia katika kumuangamiza mtu anayewakera.

Miaka 27 ya kuishi kama mstaafu ni mingi, wengi wakijitahidi sana wataishi miaka mitano au kumi na kuaga dunia. Amewaona wasaidizi wake watatu wakiingia ikulu na kuondoka akiendelea kula raha pale nyumbani kwake. Huyu ni mwanasiasa ambaye maisha yake ni zaidi ya kitabu alichokizindua mwaka jana. Kwamba ukiwa hai huhitaji kujijazia makorokoro mengi kichwani kwako, yataishia kukuumiza na kukumaliza siku usiyoitarajia.

Pia ni somo la ucha Mungu. Kwamba ukimtegemea Mungu siku zote hataweza kukuacha ukatetereka na kuteseka kiafya. Miaka 97 ni zaidi ya ile miaka 70 ya kwenye Biblia kwa miaka 27. Siku zote jione wa kawaida na jione hufai kitu ukiwa umepiga magoti kanisani au msikitini. Ukiwa mdogo utajifunza kujiona sehemu ya wakosaji hata kama bajeti yako ya ulinzi ni mabilioni ya shilingi kwa siku, hata kama unalindwa na mitambo imara na wanajeshi wanaotumia zana za kisasa.

Na ni hapa marais wastaafu waislam wanapokuwa ni waalimu wa uungwana unaoambatana na maisha marefu. Hawaoni sababu ya kumuonea mtu au watu. Hawaoni sababu ya kuwafanya watu wakajiona ni kwanini wamekuja duniani kupata mateso yote haya!. Wanaweza kuitwa dhaifu kwa kuwa ni watu walio 'too liberal', wakiachia uhuru mwingi wa kuongea na kuandika, lakini hiyo ni sehemu muhimu wa utoaji wa haki ambao umeandikwa katika vitabu vitakatifu. Hivyo kuona marais wastaafu wa kiislam wanaendelea kuzeeka huku nyuso zao zikiwa na tabasamu la kirafiki ni bahati inayokwenda pamoja na kuwa sababu ya tulio wengi kujifunza mambo fulani ya kimaisha.

Kheri ya kuzaliwa Mzee Ali Hassan Mwinyi.
Mzee Mwinyi ameishi miaka mingi kwa vile sera yake ya RUKSA ilimuondolea nafasi ya kufikiri.
Kila mtu alifanya lake.
Economic Hitmen wakamwambia uza na kuua TIPER ili biashara iwe huru, yeye akasema RUKSA!
Matokeo tunayaona miaka mingi baada ya utawala wake na kabla hajafa.
 
Matunzo Mazuri katika Uraisi wake
Matibabu mazuri
Chakula Kizuri
Hewa Nzuri
Nyumba Nzuri
Mtoto wake Ni Raisi
Hana Shida na Pesa

Hata Papa,Mapadri..Askofu..Masista wakubwa wakubwa Wanaishi maisha Marefu.
 
1960 alikuwa Mkuu wa Chuo cha Ualimu Znz cha Lumumba tangu hapo akaanza kuwa na mshahara mkubwa

1966 Balozi, kaja kuwa Waziri wa Jamhuri tangu 1972

kaja kuwa Rais wa Znz

kaja kuwa Rais wa Muungano

binti yake mmoja kaolewa na mtoto wa Mfalme wa Abudhabi

Mtoto wake Rais wa Znz

mtoto wake mwingine Mbunge wa Bunge la Jamhuri

Ma binti zake ni Wafanyabiashara wakubwa wanaoshiriki kwny kandarasi kubwa kubwa za nje na ndani ya nchi

Vijana wake wa kiume ni ma Tycoon kwny biashara ta Utalii Afrika mashariki

wengine ni Wafanyakazi wa Taasisi kubwa kubwa za kimataifa

sasa hapo akiwa na Ukwasi ni jambo la kushangaa kweli ?

mwenzangu na mie kamshara ka TGSD hata shangazi akidondoka kwny bodaboda kijijini lazima utafutwe utume elf 5 ya kumbeba kwny bodaboda utachomokaje kwny lindi la umskini?
Mada ni Mzee Mwinyi na ukosefu wake wa nongwa zenye kuongeza maadui na hasira,Hayo ya watoto na wakwe zake yanamhusu binafsi.
 
Mkuu Asante kwa andiko!
LAKINI
Ili uwe hivyo ulivyo andika inategemea malezi na makuzi uliyokulia!
Vijana wengi kama kina jpm walikulia shida na suluba za utotoni wakiwa wakubwa ile Hali haiwaachi salama kabisa kiakili na kisaikolojia na jpm anawakilisha kundi kubwa la watoto na vijana wengi wa kisasa hapa NCHINI makuzi na malezi DUNI full stress KILA kukicha mtu Huyo akipewa madaraka tu utaziona nyufa nyingi Sana!!malezi ya Mwinyi junior na ridhiwani na baadh yao wanaweza kuyaishi hayo lakini sio kwa WENGINE kama Bashite na wengi Sana!
Kama hiyo unahisi ndio sababu ya mzee Mwinyi kuwa hivyo, wewe ujui kuna watoto wa Mwl na Dr Magufuli walikufa mapema tu ilhali walikulia kwenye maisha ya starehe na raha kuliko wewe.
 
1960 alikuwa Mkuu wa Chuo cha Ualimu Znz cha Lumumba tangu hapo akaanza kuwa na mshahara mkubwa

1966 Balozi, kaja kuwa Waziri wa Jamhuri tangu 1972

kaja kuwa Rais wa Znz

kaja kuwa Rais wa Muungano

binti yake mmoja kaolewa na mtoto wa Mfalme wa Abudhabi

Mtoto wake Rais wa Znz

mtoto wake mwingine Mbunge wa Bunge la Jamhuri

Ma binti zake ni Wafanyabiashara wakubwa wanaoshiriki kwny kandarasi kubwa kubwa za nje na ndani ya nchi

Vijana wake wa kiume ni ma Tycoon kwny biashara ta Utalii Afrika mashariki

wengine ni Wafanyakazi wa Taasisi kubwa kubwa za kimataifa

sasa hapo akiwa na Ukwasi ni jambo la kushangaa kweli ?

mwenzangu na mie kamshara ka TGSD hata shangazi akidondoka kwny bodaboda kijijini lazima utafutwe utume elf 5 ya kumbeba kwny bodaboda utachomokaje kwny lindi la umskini?
Hapo wewe ni kula , kuswali na kuuliza…….saa ngapi vile?
 
Nikiri kwamba sijaisoma makala yote ! Lakini Ali Hassan Mwinyi ndio anakula capacity charges za IPTL ! Hana usafi wowote ule babu yule!!

Ni kiri kwamba sijaisoma makala yote ! Lakini Ali Hassan Mwinyi ndio anakula capacity charges za IPTL ! Hana usafi wowote ule babu yule!!

Alimuuzia mwarabu eneo la Loliondo pia, sehemu ambayo ni mapito ya wanyama wanapohama. Waarabu wamehamisha wanyama hai kwenda uarabuni na kutengeneza mbuga ya wanyama.
 
Ukiishi ukiwa unafikiria kuumiza wengine mchana kweupe maana yake na wewe uliumizwa sana utotoni. Kule kuumizwa hakuishi kuwa ni tukio la kivitendo tu, bali kunaingia ndani kabisa ya ubongo wako.
Kwa hiyo unaamaanisha JPM ndio alikuwa ana "nongwa na visasi"! Sawa. Endeleeni kumkana enyi wafuasi uchwara.
 
Alijitahidi chini ya Nyerere. Alipochukua nchi kila kitu alisikiliza Mabeberu, IMF, World Bank.

Aliuza kila kitu, kuviweka vyote sekta binafsi. Walipewa kama bure sekta zote muhimu Mafisadi wote. Matajiri wa sasa. Madhara yake tunapambana nayo hadi leo.

Mrema alipambana akamshinda kwenye uchaguzi. Nyerere alimuunga mkono Mrema kugombea, kui -challenge CCM.

Sababu kubwa ni uhuni kama huu unaondeleo. Unahitaji watu kama JPM, Mrema, Nyerere watu kama hao kuutokomeza.
Hizo ni akili zinazofikiriwa na watu wavivu, mfumo wa Nyerere alisababisha wengi kuwa mafukara wa hali ya juu sana, watu wazama wanajua kuwa kipindi cha Nyerere watu walivaa makaniki tu na viatu vya magogo ya miti na magome yake, watu walikuwa wanaishi kwenye nyumba ambazo hazikuwa bora, ilikuwa mtu ukijenga nyumba ya bati tu mwaka mzima unakuwa mahabusu kuhojiwa hata kama ulidunduliza kulima ufuta na mbaazi ndipo ukapata hiyo pesa.

Magufuli nae alikuwa mchoyo sana kuliko mlivyokuwa mnafikiria, mapato yote ya serikali asilimia kubwa alipanga yaende kanda ya ziwa. Kwa manufaa ya watu wa kanda hile. Alijawa na nepotism na ukabilarism, na kwa akili ya kawaida tu inaonekana mfumo wa urais angeubadilisha ili aweze kukaa muda mrefu madarakani.
 
Wewe mjinga tu wazee wa kislam wanaokufa mapema wote ni waovu? Vipi wakristo wazee wapo wengi tu! Udini ndo shida yenu wavaa madera! Vipi akina warioba huwaoni?Pia akina Butiku, Samwel Marechera!
Unapaniki Bure tu, uwaoni waislamu walio-criticize hilo bandiko, hio ilikuwa fikra zake katika ufahamu wake.
 
Matunzo Mazuri katika Uraisi wake
Matibabu mazuri
Chakula Kizuri
Hewa Nzuri
Nyumba Nzuri
Mtoto wake Ni Raisi
Hana Shida na Pesa

Hata Papa,Mapadri..Askofu..Masista wakubwa wakubwa Wanaishi maisha Marefu.
Na wao wana watoto marais??
 
Back
Top Bottom