Miaka 97 ya Mzee Mwinyi na amani ya moyoni pasipo nongwa na visasi

Miaka 97 ya Mzee Mwinyi na amani ya moyoni pasipo nongwa na visasi

Pia ni somo la ucha Mungu. Kwamba ukimtegemea Mungu siku zote hataweza kukuacha ukatetereka na kuteseka kiafya.
Haupo sawa hapa Mungu ni wetu sote kwa walio wagonjwa na wazima.
Na ni hapa marais wastaafu waislam wanapokuwa ni waalimu wa uungwana unaoambatana na maisha marefu.
Kuishi maisha marefu ni mapenzi ya Mungu ambayo kila binadamu anatamani ayapate,kusema kuwa Marais wa kiislamu wameishi maisha marefu kuzidi wale wakikristo ukimtoa Mzee wetu Mwinyi ni kutudanganya.

Mzee Kikwete ana miaka 71 bado haijui kesho yake.

Rais samia ana miaka 62 Naye bado haijui kesho yake.

Je unajuaje Kama Rais Samia anaweza kufikia miaka aliyoishi Mkapa[81] au Rais Mstaafu Kikwete akafikisha miaka 77 ya baba wa Taifa.Bado ni fumbo.

Maisha ya binadamu kwa yeyote yule ni fumbo Lissu alipigwa risasi zaidi ya kumi yupo hai lakini Magufuli hayupo hayo ni mapenzi ya Mungu sitaki kukufuru.
[
Miaka 27 ya kuishi kama mstaafu ni mingi, wengi wakijitahidi sana wataishi miaka mitano au kumi na kuaga dunia.
Mwalimu aliishi miaka 14 baada ya kustaafu kwake while Mkapa 15 bado ni miaka Mingi tu kwao.
Kheri ya kuzaliwa Mzee Ali Hassan Mwinyi
Nami namtakia heri ya kuzaliwa mzee wetu.
 
Hizo ni akili zinazofikiriwa na watu wavivu, mfumo wa Nyerere alisababisha wengi kuwa mafukara wa hali ya juu sana, watu wazama wanajua kuwa kipindi cha Nyerere watu walivaa makaniki tu na viatu vya magogo ya miti na magome yake, watu walikuwa wanaishi kwenye nyumba ambazo hazikuwa bora, ilikuwa mtu ukijenga nyumba ya bati tu mwaka mzima unakuwa mahabusu kuhojiwa hata kama ulidunduliza kulima ufuta na mbaazi ndipo ukapata hiyo pesa.

Magufuli nae alikuwa mchoyo sana kuliko mlivyokuwa mnafikiria, mapato yote ya serikali asilimia kubwa alipanga yaende kanda ya ziwa. Kwa manufaa ya watu wa kanda hile. Alijawa na nepotism na ukabilarism, na kwa akili ya kawaida tu inaonekana mfumo wa urais angeubadilisha ili aweze kukaa muda mrefu madarakani.

Tupe mfumo wako sahihi. Au ndio huu unaopigania wa SSH.

Pamoja na mapungufu yao. Nyerere, JPM walijali maslahi ya wengi. Walisimama na kusimamia maslahi ya wananchi maskini.
 
Rais Mstaafu wa awamu ya pili leo anatimiza miaka 97, ni mingi kwa kuiandika na kuihisi kichwani ukifanya tafakari ya kina. Ni miongo tisa na miaka saba. Amekula magunia kwa magunia ya chumvi. Ni umri mkubwa sana kuendelea kuwepo hai, akiwaona wajukuu na watoto zao. Mzee Mwinyi kwa sisi tuliokuwepo duniani wakati anaingia na kuondoka ikulu ni heshima na baraka kumuona akiwa hai miaka 27 baada ya kuondoka Ikulu.

Wengi watajiuliza ameweza vipi kuishi miaka mingi namna hii. Wapo watakaosema hana makuu kwa maana ya kutoweka visasi moyoni, wapo watakaosema hanywi pombe akiwa ni muumini mzuri wa dini ya kiislam. Na wapo watakaokwenda mbali zaidi kwa kusema amekuwa akijitunza na siku zote akishiriki matembezi ya hiari na yeye mwenyewe kupenda kutembea. Na anayependa kutembea mazoezi ya asubuhi au kukimbia taratibu (jogging) anakwepa maradhi mengi yakiwepo yale ya moyo yenye kuua haraka na pasipo kutarajiwa.

Mzee Mwinyi ameendelea kuwepo wakati wazee wenzake karibu wote wa miaka ile ya awamu ya kwanza na ya pili wakiwa tayari wameshazikwa. Siku ya msiba wa hayati John Magufuli akasoma pasipo miwani!, na akatembea kwenda na kurudi kwenye kiti chake pasipo msaada wa kushikiliwa na mtu yoyote.

Ni kweli wote tunapita juu ya uso wa dunia, lakini kupita kwa baadhi yetu ni kule kwenye baraka. Unaweza kujiuliza inakuwaje Mzee huyu anazidi kusherehekea siku za kuzaliwa kila mwaka wakati wanasiasa vijana tu wakiaga dunia. Vijana waliozaliwa akiwa tayari ni mwanasiasa wanakufa na kumuacha yeye akiendelea kuishi kwa upole bila ya makuu pale kwake mbele kidogo ya Msasani kwa Mwalimu Nyerere.

Hakuwa na makuu, hakutunza hasira wala visasi. Hakutaka kuibadili dunia (To change the world), hakuamini kuwa kila tatizo anaweza yeye kama yeye akalitatua na hivyo kuumiza walio wengi katika mchakato wa utatuzi wa hilo tatizo. Hata baada ya kukejeliwa na Mwalimu Nyerere pale Kilimanjaro Hotel Simba Grill mwezi March mwaka 1995 aliendelea kuwa mkimya mpaka ilipofika siku akaamua kujibu mapigo.

Na baada ya hapo hakutaka kujikweza au kupandisha mabega, ni kama alisamehe na kuendelea kuwa huru moyoni. Hiyo ni sifa anayotakiwa kuwa nayo kiongozi mkuu wa Taifa. Uwezo wa kunyenyekea kwa kuyaona ni madogo tu baadhi ya mambo yanakukwaza na kukukera ukiwa ofisini. Ni mtihani mgumu sana kwa viongozi wenye madaraka makubwa kwa mujibu wa katiba yetu kuweza kujishusha huku wakiwa na vyombo vyote wanavyoweza kuvitumia katika kumuangamiza mtu anayewakera.

Miaka 27 ya kuishi kama mstaafu ni mingi, wengi wakijitahidi sana wataishi miaka mitano au kumi na kuaga dunia. Amewaona wasaidizi wake watatu wakiingia ikulu na kuondoka akiendelea kula raha pale nyumbani kwake. Huyu ni mwanasiasa ambaye maisha yake ni zaidi ya kitabu alichokizindua mwaka jana. Kwamba ukiwa hai huhitaji kujijazia makorokoro mengi kichwani kwako, yataishia kukuumiza na kukumaliza siku usiyoitarajia.

Pia ni somo la ucha Mungu. Kwamba ukimtegemea Mungu siku zote hataweza kukuacha ukatetereka na kuteseka kiafya. Miaka 97 ni zaidi ya ile miaka 70 ya kwenye Biblia kwa miaka 27. Siku zote jione wa kawaida na jione hufai kitu ukiwa umepiga magoti kanisani au msikitini. Ukiwa mdogo utajifunza kujiona sehemu ya wakosaji hata kama bajeti yako ya ulinzi ni mabilioni ya shilingi kwa siku, hata kama unalindwa na mitambo imara na wanajeshi wanaotumia zana za kisasa.

Na ni hapa marais wastaafu waislam wanapokuwa ni waalimu wa uungwana unaoambatana na maisha marefu. Hawaoni sababu ya kumuonea mtu au watu. Hawaoni sababu ya kuwafanya watu wakajiona ni kwanini wamekuja duniani kupata mateso yote haya!. Wanaweza kuitwa dhaifu kwa kuwa ni watu walio 'too liberal', wakiachia uhuru mwingi wa kuongea na kuandika, lakini hiyo ni sehemu muhimu wa utoaji wa haki ambao umeandikwa katika vitabu vitakatifu. Hivyo kuona marais wastaafu wa kiislam wanaendelea kuzeeka huku nyuso zao zikiwa na tabasamu la kirafiki ni bahati inayokwenda pamoja na kuwa sababu ya tulio wengi kujifunza mambo fulani ya kimaisha.

Kheri ya kuzaliwa Mzee Ali Hassan Mwinyi.
Hata hawa wengine, kama si dhuluma za mtu yule, wangekuwepo hadi leo.
 
Kama hutojali unaweza kutufafanulia para ya tatu?
" Mrema alipambana.............kui- challenge CCM"

Sera yake ilikuwa kila kitu rukhsa. Unaruhusiwa.

Unaruhusìwa kuuza mali zote za serikali, kuuuza kwa washikaji wako kwa bei za sigara moja. kuuza unga mtaaani. Kufanya chochote. Sera hizi ndio zilizoua miundombinu yote muhimu ya kuwasaidia Watz.
 
Hizo ni akili zinazofikiriwa na watu wavivu, mfumo wa Nyerere alisababisha wengi kuwa mafukara wa hali ya juu sana, watu wazama wanajua kuwa kipindi cha Nyerere watu walivaa makaniki tu na viatu vya magogo ya miti na magome yake, watu walikuwa wanaishi kwenye nyumba ambazo hazikuwa bora, ilikuwa mtu ukijenga nyumba ya bati tu mwaka mzima unakuwa mahabusu kuhojiwa hata kama ulidunduliza kulima ufuta na mbaazi ndipo ukapata hiyo pesa.

Magufuli nae alikuwa mchoyo sana kuliko mlivyokuwa mnafikiria, mapato yote ya serikali asilimia kubwa alipanga yaende kanda ya ziwa. Kwa manufaa ya watu wa kanda hile. Alijawa na nepotism na ukabilarism, na kwa akili ya kawaida tu inaonekana mfumo wa urais angeubadilisha ili aweze kukaa muda mrefu madarakani.

Mvivu wa kufikiri ni wewe, think deep.
 
Rais Mstaafu wa awamu ya pili leo anatimiza miaka 97, ni mingi kwa kuiandika na kuihisi kichwani ukifanya tafakari ya kina. Ni miongo tisa na miaka saba. Amekula magunia kwa magunia ya chumvi. Ni umri mkubwa sana kuendelea kuwepo hai, akiwaona wajukuu na watoto zao. Mzee Mwinyi kwa sisi tuliokuwepo duniani wakati anaingia na kuondoka ikulu ni heshima na baraka kumuona akiwa hai miaka 27 baada ya kuondoka Ikulu.

Wengi watajiuliza ameweza vipi kuishi miaka mingi namna hii. Wapo watakaosema hana makuu kwa maana ya kutoweka visasi moyoni, wapo watakaosema hanywi pombe akiwa ni muumini mzuri wa dini ya kiislam. Na wapo watakaokwenda mbali zaidi kwa kusema amekuwa akijitunza na siku zote akishiriki matembezi ya hiari na yeye mwenyewe kupenda kutembea. Na anayependa kutembea mazoezi ya asubuhi au kukimbia taratibu (jogging) anakwepa maradhi mengi yakiwepo yale ya moyo yenye kuua haraka na pasipo kutarajiwa.

Mzee Mwinyi ameendelea kuwepo wakati wazee wenzake karibu wote wa miaka ile ya awamu ya kwanza na ya pili wakiwa tayari wameshazikwa. Siku ya msiba wa hayati John Magufuli akasoma pasipo miwani!, na akatembea kwenda na kurudi kwenye kiti chake pasipo msaada wa kushikiliwa na mtu yoyote.

Ni kweli wote tunapita juu ya uso wa dunia, lakini kupita kwa baadhi yetu ni kule kwenye baraka. Unaweza kujiuliza inakuwaje Mzee huyu anazidi kusherehekea siku za kuzaliwa kila mwaka wakati wanasiasa vijana tu wakiaga dunia. Vijana waliozaliwa akiwa tayari ni mwanasiasa wanakufa na kumuacha yeye akiendelea kuishi kwa upole bila ya makuu pale kwake mbele kidogo ya Msasani kwa Mwalimu Nyerere.

Hakuwa na makuu, hakutunza hasira wala visasi. Hakutaka kuibadili dunia (To change the world), hakuamini kuwa kila tatizo anaweza yeye kama yeye akalitatua na hivyo kuumiza walio wengi katika mchakato wa utatuzi wa hilo tatizo. Hata baada ya kukejeliwa na Mwalimu Nyerere pale Kilimanjaro Hotel Simba Grill mwezi March mwaka 1995 aliendelea kuwa mkimya mpaka ilipofika siku akaamua kujibu mapigo.

Na baada ya hapo hakutaka kujikweza au kupandisha mabega, ni kama alisamehe na kuendelea kuwa huru moyoni. Hiyo ni sifa anayotakiwa kuwa nayo kiongozi mkuu wa Taifa. Uwezo wa kunyenyekea kwa kuyaona ni madogo tu baadhi ya mambo yanakukwaza na kukukera ukiwa ofisini. Ni mtihani mgumu sana kwa viongozi wenye madaraka makubwa kwa mujibu wa katiba yetu kuweza kujishusha huku wakiwa na vyombo vyote wanavyoweza kuvitumia katika kumuangamiza mtu anayewakera.

Miaka 27 ya kuishi kama mstaafu ni mingi, wengi wakijitahidi sana wataishi miaka mitano au kumi na kuaga dunia. Amewaona wasaidizi wake watatu wakiingia ikulu na kuondoka akiendelea kula raha pale nyumbani kwake. Huyu ni mwanasiasa ambaye maisha yake ni zaidi ya kitabu alichokizindua mwaka jana. Kwamba ukiwa hai huhitaji kujijazia makorokoro mengi kichwani kwako, yataishia kukuumiza na kukumaliza siku usiyoitarajia.

Pia ni somo la ucha Mungu. Kwamba ukimtegemea Mungu siku zote hataweza kukuacha ukatetereka na kuteseka kiafya. Miaka 97 ni zaidi ya ile miaka 70 ya kwenye Biblia kwa miaka 27. Siku zote jione wa kawaida na jione hufai kitu ukiwa umepiga magoti kanisani au msikitini. Ukiwa mdogo utajifunza kujiona sehemu ya wakosaji hata kama bajeti yako ya ulinzi ni mabilioni ya shilingi kwa siku, hata kama unalindwa na mitambo imara na wanajeshi wanaotumia zana za kisasa.

Na ni hapa marais wastaafu waislam wanapokuwa ni waalimu wa uungwana unaoambatana na maisha marefu. Hawaoni sababu ya kumuonea mtu au watu. Hawaoni sababu ya kuwafanya watu wakajiona ni kwanini wamekuja duniani kupata mateso yote haya!. Wanaweza kuitwa dhaifu kwa kuwa ni watu walio 'too liberal', wakiachia uhuru mwingi wa kuongea na kuandika, lakini hiyo ni sehemu muhimu wa utoaji wa haki ambao umeandikwa katika vitabu vitakatifu. Hivyo kuona marais wastaafu wa kiislam wanaendelea kuzeeka huku nyuso zao zikiwa na tabasamu la kirafiki ni bahati inayokwenda pamoja na kuwa sababu ya tulio wengi kujifunza mambo fulani ya kimaisha.

Kheri ya kuzaliwa Mzee Ali Hassan Mwinyi.
Ni muasisi ya kuwaweka watoto,wake,washikaju serikalini. Kuafinya nchi iwe ya hovyo sana.
 
Alijitahidi kadri ya uwezo wake, aliifanya kilichokuwa ndanii ya mipaka ya uwezo.
Point yangu ni kwamba kama mwenzake Mzee Mwinyi alitawala miaka 10 na amestaafu miaka 27 bado anadunda tu, yule mwingine ameshindwa kutoboa hata 6 tu. Maana yake huyo Magu alikuwa na visasi na roho mbaya ndo maana ameshindwa kutoboa hata miaka 70
 
1960 alikuwa Mkuu wa Chuo cha Ualimu Znz cha Lumumba tangu hapo akaanza kuwa na mshahara mkubwa

1966 Balozi, kaja kuwa Waziri wa Jamhuri tangu 1972

kaja kuwa Rais wa Znz

kaja kuwa Rais wa Muungano

binti yake mmoja kaolewa na mtoto wa Mfalme wa Abudhabi

Mtoto wake Rais wa Znz

mtoto wake mwingine Mbunge wa Bunge la Jamhuri

Ma binti zake ni Wafanyabiashara wakubwa wanaoshiriki kwny kandarasi kubwa kubwa za nje na ndani ya nchi

Vijana wake wa kiume ni ma Tycoon kwny biashara ta Utalii Afrika mashariki

wengine ni Wafanyakazi wa Taasisi kubwa kubwa za kimataifa

sasa hapo akiwa na Ukwasi ni jambo la kushangaa kweli ?

mwenzangu na mie kamshara ka TGSD hata shangazi akidondoka kwny bodaboda kijijini lazima utafutwe utume elf 5 ya kumbeba kwny bodaboda utachomokaje kwny lindi la umskini?
Paragraph ya mwisho sio kweli! Umepuyanga.!
 
Mwinyi ndio Rais ambaye alikuwa anaongoza kwa mawazo ya Nyerere kutokea Butiama.

Alishinikizwa sana ikiwemo hata kuvunja baraza la mawaziri mara mbili kwa oda ya mzee mchonga.

Mwinyi wala hakujali, hata lilipokuja suala la maelekezo ya kuwadili Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wake wa CCM bwana Kolimba bado aliendelea kuwa mtulivu.

Huyu pengine anabakia kuwa Rais ambaye hakutawala kwa matakwa yake, Rais ambaye hakuwa na mamlaka! Lakini hakuwa na chuki wala kinyongo, leo hii ametimiza miaka 97.

Heri ya kuzaliwa kwa mzee Ali Hassan Mwinyi...Mwenyezi Mungu akutunze zaidi!
 
Back
Top Bottom