Miaka, toka kuumbwa kwa adamu hadi kufa kwa Abrahamu. Umeona nini?

Miaka, toka kuumbwa kwa adamu hadi kufa kwa Abrahamu. Umeona nini?

Kwa biblia Dunia haizidi miaka 6000. Kwa uhalisia Dunia ni zaidi ya miaki bilioni 4.5 na binadamu amekuwa muda huo wote ila maafa Kwa njia ya mafuriko, Asteroids, Alien invasion na mengine mengi yamekuwa yakitokea na yataendelea kutokea. We are not the first technologically advanced civilization and neither are we the last.
Nakuunga mkono mkuu,Dunia Ina muda mrefu sana Toka mwanzo wake,Mimi nakazia hapo kwenye Allien invasion ndio chanzo Cha kuibuka Kwa Hizi dini,Kuna watu hua nawaambia hao viumbe wanaoitwa Mungu,Malaika,shetani,jini na jamii zao nyingi ni Aliens walioivamia Dunia na wakazi wake hapo kale na kuwapa ustaarabu wao,

Kutokana na ujuzi wao mkubwa na uwezo wao wa kufanya mambo ya kushangaza kutokana na kua high science advanced watu wakaanza kuwahusudu kama ni miungu,
Angalia zile civilization za kale kama Sumerians, Assyrian,Misri,Aztec,Indus valley nk lazima utaona masimulizi ya viumbe vya ajabu vilivyotenda mambo makuu na wao kuviita miungu ila wale wote ni Alliens wa kale waliopata kuitembelea Dunia!
 
Hivi na wale dinoseria wale wanyama wakubwa kuwahi kutokea waliishi zama gani? Kati ya hizo na hiyo Safina ilikuwa na ukubwa gani?
Pic%20Layer_2021111311215721.jpg


Sent from my TECNO-N2 using JamiiForums mobile app
 
Mzee kumbe unang'aka bure tu hata biblia huijui. Soma Bible Mzee achana na simulizi

5 hapakuwa na mche wa kondeni bado, wala mboga ya kondeni haijachipuka bado, kwa maana Bwana Mungu hajainyeshea nchi mvua, wala hapana mtu wa kuilima ardhi;
Mwanzo 2:5

6 ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi.
Mwanzo 2:6
Ukungu(misty) ndiyo ulikuwa ukilowesha nchi kama umande. Mvua ilikuwa bado kuanza kunyesha.
 
Sasa mzee kwanini usipeleke mada hii kwenye threads za dini!? Sisi hatupo tayari kuletewa uongo tukakaa kimya.
Biblia si kitabu tu cha dini bali pia cha historia, sheria nk. Lakini kama vitabu vingine(vya hesabu, afya nk) unatakiwa ukiamini kwanza ndipo unaweza kwenda mbele. Usipoamini yaliyoandikwa kwenye kitabu cha afya hamuwezi anza kujadili yaliyomo.
 
Adam hakuwa binadamu wa kwanza kuishi duniani,hizi habari sijuwi mnazitoa wapi na mnazisambaza kwa malengo gani.
Hakuna ushahidi wa kihistoria ya kuwa Adam alikuwa binadamu wa kwanza kuishi.
Wakati huyo Adam anaishi miaka 3000-4000bc iliyopita huku Africa Jamii ya Homo ilishaishi miaka million 2-3 iliyopita na walishasambaa hadi maeneo ya mbali sana.
Ukiyachunguza vyema maandiko matakatifu, hasa simulizi kutoka Kitabu cha Mwanzo kama vile kilivyoandikwa na Nabii Musa, hakuna maelezo yoyote yale kuhusu historia ya kuumbwa kwa sayari ya dunia. Bali kimeanza na simulizi kuhusu kazi ya Mungu ya kutengeneza mazingira ambayo yatakuwa ni makazi ya kudumu kwa viumbe ambavyo alipenda kuviumba kwa utashi wake Yeye mwenyewe.

Nukuu ya maandiko hayo hutupa mazingira ya aina tatu ambayo Mungu aliyafanya. Kwa kuwa dunia ilikuwepo kabla ya uumbaji wa mwanadamu, nayo dunia ilikuwa imezingirwa na sura ya maji, basi Mungu aliyatenga maji hayo ili ikapate kuwepo kwa eneo nchi kavu. Eneo la nchi kavu na maji na eneo la juu akaliita mbingu ambapo aliweka jua na mwezi kwa ajili ya kuwepo kwa usiku na mchana pamoja na majira tofauti ya mwaka.

Kwa hiyo basi maandiko matakatifu hayazungumzii kabisa kuhusu mwanzo halisi wa sayari yetu, "solar system" ama "galaxy" bali huzungumzia kuhusu mwanzo wa viumbe hai vilivyopo juu yake.

Labda ni vyema tupitie kwa pamoja nukuu ya maandiko ili tupate zaidi ufahamu na mantiki ya msimulizi kama ifuatavyo;

Kitabu cha Mwanzo

1 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.
2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.
3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.
4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza.
5 Mungu akaiita nuru Mchana, na giza akaliita Usiku. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku moja.
6 Mungu akasema, Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.
7 Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo.
8 Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili.
9 Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo.
10 Mungu akapaita pale pakavu Nchi; na makusanyiko ya maji akayaita Bahari; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.

Kwa hiyo basi, hakuna ubishi wowote ule kuhusu uwepo wa uhai kabla ya Adam, kwa kuwa malaika wa nuru, shetani na malaika wengine walikuwapo kabla yake, lakini wao walikuwa na miili yenye maumbile ya kiroho, ndiyo maana makazi yao yalikuwa juu ya nchi ama mbinguni. Tofauti yao na Adam, yeye aliumbwa pia kwa roho bali mwili wake uliumbwa kupitia udongo ili aweze kuishi katika nchi kavu.

Kwa kuwa Mungu ni wa milele, basi hata hizo simulizi za mamilioni ya miaka ya uwepo wa dunia huenda zikawa ni za kweli. Lakini zinapatika kutoka katika chanzo kipi cha kuaminika cha habari?

Ni kweli kabisa pengine shetani na malaika wengine waovu waliishi katika sayari ya Mars. Lakini pale walipoasi walitupwa katika sayari yetu ya dunia, na kuwekwa chini ya nchi iliyokuwa imezungukwa na vilindi vya maji.

Na ukweli huu unapatika kuhusu simulizi za uwepo wa kuzimu. Maandiko matakatifu hituambia kuzimu ni chini ya nchi ambapo ni makazi ya muda ya malaika waovu kabla ya hukumu yao ya kutupwa Jehanamu.
Screenshot_20211202-184132.jpg
Screenshot_20211202-184150.jpg


Sent from my Nokia 2.3 using JamiiForums mobile app
 
Hivi na wale dinoseria wale wanyama wakubwa kuwahi kutokea waliishi zama gani? Kati ya hizo na hiyo Safina ilikuwa na ukubwa gani?View attachment 2030614

Sent from my TECNO-N2 using JamiiForums mobile app
Dinosaur waliishi yapata Miaka millions iliyopita na Kuna baadhi ya nadharia ya kwamba walitoweka baada ya Moja ya estoroid kuipiga Dunia na mabadiliko ya kimazingira pia yanachangia!
 
Nakuunga mkono mkuu,Dunia Ina muda mrefu sana Toka mwanzo wake,Mimi nakazia hapo kwenye Allien invasion ndio chanzo Cha kuibuka Kwa Hizi dini,Kuna watu hua nawaambia hao viumbe wanaoitwa Mungu,Malaika,shetani,jini na jamii zao nyingi ni Aliens walioivamia Dunia na wakazi wake hapo kale na kuwapa ustaarabu wao,

Kutokana na ujuzi wao mkubwa na uwezo wao wa kufanya mambo ya kushangaza kutokana na kua high science advanced watu wakaanza kuwahusudu kama ni miungu,
Angalia zile civilization za kale kama Sumerians, Assyrian,Misri,Aztec,Indus valley nk lazima utaona masimulizi ya viumbe vya ajabu vilivyotenda mambo makuu na wao kuviita miungu ila wale wote ni Alliens wa kale waliopata kuitembelea Dunia!
Kina Anunnaki na Igigi Kwa mfano walichimba dhahabu Afrika kusini na walikuwa na teknolojia Kali.
 
Adam hakuwa binadamu wa kwanza kuishi duniani,hizi habari sijuwi mnazitoa wapi na mnazisambaza kwa malengo gani.
Hakuna ushahidi wa kihistoria ya kuwa Adam alikuwa binadamu wa kwanza kuishi.
Wakati huyo Adam anaishi miaka 3000-4000bc iliyopita huku Africa Jamii ya Homo ilishaishi miaka million 2-3 iliyopita na walishasambaa hadi maeneo ya mbali sana.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787].
Ndo wale sokwe?
Akina ndugu zake zinjathropus?
 
Kina Anunnaki na Igigi Kwa mfano walichimba dhahabu Afrika kusini na walikuwa na teknolojia Kali.
Ndio ndio mkuu Hawa viumbe walikua high advanced mfano kule India katika Jimbo la Tamil Nadu Kuna daraja la Rama setu ni Moja kati ya maajabu yanayothibisha kwamba Hawa viumbe walikua na teknolojia kubwa maana Rama setu bridge limejengwa Kwa urefu wa km 40 kukatiza bahari mpaka kisiwa Cha Sri Lanka,
Limejengwa Miaka zaidi 15,000 iliyopita na haijulikani alijenga nani ila ngano za wahindi zinasema walijenga Vanaras hao walikua ni viumbe jamii ya nusu
binadamu nusu nyani waliokua wanaujuzi mkubwa sana
Pia utaona sites kibao mfano ni hayo machimbo ya mwenemutapa Zimbabwe, Stonehenge nk
Annunak walikua ni gold digger ndio maana utaona bronze kibao zilizotengenezwa enzi Hizo kuwaonesha zimenakshiwa na dhahabu kama utambulisho wao!
 
Ukiangalia hiyo chart Kuna watu Wana miss au hawajawekwa je ? Je Hawa watu ni watoto wa nani? Kaini ma Abeli ni watoto wa nani?
Wayahudi walikuwa wanarekodi uzao wao. Bila shaka na wazao wa wengine walirekodi uzao wao.
 
Biblia si kitabu tu cha dini bali pia cha historia, sheria nk. Lakini kama vitabu vingine(vya hesabu, afya nk) unatakiwa ukiamini kwanza ndipo unaweza kwenda mbele. Usipoamini yaliyoandikwa kwenye kitabu cha afya hamuwezi anza kujadili yaliyomo.
Mzee unapo quote comments zangu hakikisha upo open minded. Zaidi ya hapo nitakukera na kukusababisha uniite mpinga kristo.

Unaposema biblia siyo kitabu cha dini unamaana gani!? Ni kitabu cha sayansi, art, music, IT, Cooking au historia!?
Toa ufafanuzi hapa.
 
Mzee unapo quote comments zangu hakikisha upo open minded. Zaidi ya hapo nitakukera na kukusababisha uniite mpinga kristo.

Unaposema biblia siyo kitabu cha dini unamaana gani!? Ni kitabu cha sayansi, art, music, IT, Cooking au historia!?
Toa ufafanuzi hapa.
Nimesema siyo kitabu cha dini tu. Kinaelezea pia masuala ya historia, sheria nk
 
Nimesema siyo kitabu cha dini tu. Kinaelezea pia masuala ya historia, sheria nk
Kwahiyo unakubaliana na suala la Nuhu kuweka wanyama wote ndani ya safina!? Mbona issue hii ni simple tu haihitaji rocket science!?

Maana yake Nuhu aliweka wanyama kwenye safina pamoja na chakula cha chao cha kula siku zote hizo mpaka maji yalipokauka.

Kumbuka baada ya gharika, Nuhu alichinja kondoo, maana yake wanyama walikuwa wanazaliana ndani ya safina.

Use common senses kijana. Acha kulishwa matango pori.
 
Back
Top Bottom